Categories
Habakuki

Habakuki 3

Maombi Ya Habakuki

1 Sala ya nabii Habakuki iliyoimbwa kwa shigionothi.

2 Bwana, nimezisikia sifa zako;

nami naogopa kwa matendo yako, EeBwana.

Fufua kazi yako katikati ya miaka,

katikati ya miaka tangaza habari yako;

katika ghadhabu kumbuka rehema.

3 Mungu alitoka Temani,

yeye Aliye Mtakatifu kutoka Mlima Parani.

Utukufu wake ulifunika mbingu,

na sifa zake zikaifunika dunia.

4 Mngʼao wake ulikuwa kama jua lichomozalo;

mionzi ilimulika kutoka mkononi mwake,

ambako nguvu zake zilifichwa.

5 Tauni ilimtangulia;

maradhi ya kuambukiza yalifuata nyayo zake.

6 Alisimama, akaitikisa dunia;

alitazama, na kuyafanya mataifa yatetemeke.

Milima ya zamani iligeuka mavumbi

na vilima vilivyozeeka vikaanguka.

Njia zake ni za milele.

7 Niliona watu wa Kushani katika dhiki,

na makazi ya Midiani katika maumivu makali.

8 EeBwana, uliikasirikia mito?

Je, ghadhabu yako ilikuwa dhidi ya vijito?

Je, ulighadhibikia bahari

ulipoendesha farasi wako

na magari yako ya ushindi?

9 Uliufunua upinde wako

na kuita mishale mingi.

Uliigawa dunia kwa mito;

10 milima ilikuona ikatetemeka.

Mafuriko ya maji yakapita huko;

vilindi vilinguruma

na kuinua mawimbi yake juu.

11 Jua na mwezi vilisimama kimya mbinguni

katika mngʼao wa mishale yako inayoruka,

na katika mngʼao wa mkuki wako umeremetao.

12 Kwa ghadhabu ulipita juu ya dunia,

na katika hasira ulikanyaga mataifa.

13 Ulikuja kuwaokoa watu wako,

kumwokoa uliyemtia mafuta.

Ulimponda kiongozi wa nchi ya uovu,

ukamvua toka kichwani hadi wayo.

14 Kwa mkuki wake mwenyewe ulitoboa kichwa chake

wakati mashujaa wake walifurika nje kwa kishindo kututawanya,

wakifurahi kama walio karibu kutafuna

wale wanyonge waliokuwa mafichoni.

15 Ulikanyaga bahari kwa farasi wako,

ukisukasuka maji makuu.

16 Nilisikia na moyo wangu ukagonga kwa nguvu,

midomo yangu ikatetemeka kwa hofu niliposikia sauti;

uchakavu ukanyemelea mifupa yangu,

na miguu yangu ikatetemeka.

Hata hivyo nitasubiri kwa uvumilivu siku ya maafa

kuyajilia mataifa yaliyotuvamia.

17 Ingawa mtini hauchanui maua

na hakuna zabibu juu ya mizabibu,

ingawaje mzeituni hauzai,

na hata mashamba hayatoi chakula,

iwapo hakuna kondoo katika banda,

wala ngʼombe katika zizi,

18 hata hivyo nitashangilia katikaBwana,

nitamfurahia Mungu Mwokozi wangu.

19 BwanaMwenyezi ni nguvu yangu;

huifanya miguu yangu kama miguu ya ayala,

huniwezesha kupita juu ya vilima.

Kwa kiongozi wa uimbaji. Kwa vinanda vyangu vya nyuzi.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HAB/3-bec1d4175c363e1dfe8d2d3391793194.mp3?version_id=1627—

Categories
Sefania

Sefania Utangulizi

Utangulizi

Maana ya Sefania ni “Aliyefichwa na Yehova.” Alikuwa wa ukoo wa Hezekia, mfalme wa Yuda. Nabii Sefania alihudumu wakati wa utawala wa Mfalme Yosia. Sefania alionya kwamba siku ya Bwana ingeleta hukumu kwa Yuda pamoja na Yerusalemu, hivyo akawashauri Wayahudi kumrudia Mungu. Uvamizi wa kuteka Yuda ulikuwa unakuja kutoka kaskazini, nao ungekumba pia mataifa yaliyowazunguka. Ingawa hukumu ya Yuda imeainishwa, ahadi ya kufanywa upya ni yakini. Mataifa yatahukumiwa na kutiishwa na mfalme wa Israeli, atakayetawala kutoka Sayuni.

Mwandishi

Sefania.

Kusudi

Kuwaonya watu wa Yuda waepukane na kuabudu sanamu na wamrudie Mungu wao.

Mahali

Yerusalemu.

Tarehe

Kati ya 640–621 K.K.

Wahusika Wakuu

Sefania, na watu wa Yuda.

Wazo Kuu

Sefania aliwapa watu matumaini kwamba Mungu angewarudisha watu wake nyumbani.

Mambo Muhimu

Hukumu juu ya Yuda na mataifa ya Wafilisti, Amoni na Moabu. Yerusalemu pia inatajwa kwa siku zijazo.

Mgawanyo

Kutangazwa kwa hukumu ya Mungu (

1:1–2:3

)

Hukumu dhidi ya mataifa (

2:4-15

)

Maisha ya baadaye ya Yerusalemu (

3:1-20

).

Categories
Sefania

Sefania 1

1 Neno laBwanalililomjia Sefania mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria, mwana wa Hezekia, wakati wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda:

Onyo La Maangamizi Yanayokuja

2 Bwanaasema,

“Nitafagia kila kitu

kutoka kwenye uso wa dunia.”

3 “Nitafagilia mbali watu na wanyama;

nitafagilia mbali ndege wa angani

na samaki wa baharini.

Wafanyao maovu watapata tu kokoto,

nami nitamkatilia mbali mwanadamu atoke katika dunia,”

asemaBwana.

Dhidi Ya Yuda

4 “Nitaiadhibu Yuda

na wote wakaao Yerusalemu.

Kutoka mahali hapa nitakatilia mbali

kila mabaki ya Baali,

majina ya wapagani na makuhani

waabuduo sanamu:

5 wale ambao husujudu juu ya mapaa

kuabudu jeshi la vitu vya angani,

wale ambao husujudu na kuapa kwaBwana

na ambao pia huapa kwa Malkamu,

6 wale wanaoacha kumfuataBwana,

wala hawamtafutiBwana

wala kutaka shauri lake.

7 Nyamazeni mbele zaBwanaMwenyezi,

kwa maana siku yaBwanaiko karibu.

Bwanaameandaa dhabihu,

amewaweka wakfu wale aliowaalika.

8 Katika siku ya dhabihu yaBwana

nitawaadhibu wakuu

na wana wa mfalme

na wale wote wanaovaa

nguo za kigeni.

9 Katika siku hiyo nitaadhibu wote ambao

hukwepa kukanyaga kizingiti,

ambao hujaza hekalu la miungu yao

kwa dhuluma na udanganyifu.”

10 Bwanaasema, “Katika siku hiyo

kilio kitapanda juu kutoka lango la Samaki,

maombolezo kutoka mtaa wa pili,

na mshindo mkubwa kutoka vilimani.

11 Ombolezeni, ninyi mnaoishi katika eneo la sokoni;

wafanyabiashara wenu wote wameangamizwa,

wote ambao wanafanya biashara ya fedha

wataangamizwa.

12 Wakati huo nitasaka mji wa Yerusalemu kwa taa,

na kuwaadhibu wale ambao

wanakaa katika hali ya kuridhika,

ambao ni kama divai

iliyobaki kwenye machicha,

ambao hudhani, ‘Bwanahatafanya lolote,

jema au baya.’

13 Utajiri wao utatekwa nyara,

nyumba zao zitabomolewa.

Watajenga nyumba,

lakini hawataishi ndani yake;

watapanda mizabibu

lakini hawatakunywa divai yake.

Siku Kubwa Ya Bwana

14 “Siku kubwa yaBwanaiko karibu:

iko karibu na inakuja haraka.

Sikilizeni! Kilio katika siku yaBwana

kitakuwa kichungu,

hata shujaa atapiga kelele.

15 Siku ile ni siku ya ghadhabu,

siku ya fadhaa na dhiki,

siku ya uharibifu na ukiwa,

siku ya giza na utusitusi,

siku ya mawingu na giza nene,

16 siku ya tarumbeta na mlio wa vita

dhidi ya miji yenye ngome

na dhidi ya minara mirefu.

17 Nitawaletea watu dhiki,

nao watatembea kama vipofu,

kwa sababu wametenda dhambi

dhidi yaBwana.

Damu yao itamwagwa kama vumbi

na matumbo yao kama taka.

18 Fedha yao wala dhahabu yao

hazitaweza kuwaokoa

katika siku hiyo ya ghadhabu yaBwana.

Katika moto wa wivu wake

dunia yote itateketezwa,

kwa maana ataleta mwisho

wa wote wanaoishi katika dunia ghafula.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ZEP/1-7b0933800ffffe34ebb9fa5dcbd54cdb.mp3?version_id=1627—

Categories
Sefania

Sefania 2

1 Kusanyikeni pamoja, kusanyikeni pamoja,

enyi taifa lisilo na aibu,

2 kabla ya wakati ulioamriwa haujafika

na siku ile inayopeperusha kama makapi,

kabla hasira kali yaBwanahaijaja juu yenu,

kabla siku ya ghadhabu yaBwana

haijaja juu yenu.

3 MtafuteniBwana, enyi nyote wanyenyekevu wa nchi,

ninyi ambao hufanya lile analoamuru.

Tafuteni haki, tafuteni unyenyekevu;

labda mtahifadhiwa

siku ya hasira yaBwana.

Dhidi Ya Ufilisti

4 Gaza utaachwa

na Ashkeloni utaachwa magofu.

Wakati wa adhuhuri Ashdodi utaachwa mtupu

na Ekroni utangʼolewa.

5 Ole wenu ninyi ambao mnaishi kando ya bahari,

enyi Wakerethi;

neno laBwanaliko dhidi yenu,

ee Kanaani, nchi ya Wafilisti.

“Mimi nitawaangamiza,

na hakuna atakayebaki.”

6 Nchi kando ya bahari, mahali ambapo wanaishi Wakerethi,

patakuwa mahali pa wachungaji

na mazizi ya kondoo.

7 Itakuwa mali ya mabaki ya nyumba ya Yuda,

hapo watapata malisho.

Wakati wa jioni watajilaza chini

katika nyumba za Ashkeloni.

BwanaMungu wao atawatunza,

naye atawarudishia wafungwa wao.

Dhidi Ya Moabu Na Amoni

8 “Nimeyasikia matukano ya Moabu

nazo dhihaka za Waamoni,

ambao waliwatukana watu wangu

na kutoa vitisho dhidi ya nchi yao.

9 Hakika, kama niishivyo,”

asemaBwanaMwenye Nguvu Zote,

Mungu wa Israeli,

“hakika Moabu itakuwa kama Sodoma,

Waamoni kama Gomora:

mahali pa magugu na mashimo ya chumvi,

nchi ya ukiwa milele.

Mabaki ya watu wangu watawateka nyara;

mabaki ya taifa langu watarithi nchi yao.”

10 Hiki ndicho watarudishiwa kwa ajili ya kiburi chao,

kwa kutukana na kudhihaki

watu waBwanaMwenye Nguvu Zote.

11 Bwanaatakuwa wa kuhofisha kwao

atakapoangamiza miungu yote ya nchi.

Mataifa katika kila pwani yatamwabudu,

kila moja katika nchi yake.

Dhidi Ya Kushi

12 “Ninyi pia, ee Wakushi,

mtauawa kwa upanga wangu.”

Dhidi Ya Ashuru

13 Mungu atanyoosha mkono wake dhidi ya kaskazini

na kuangamiza Waashuru,

akiiacha Ninawi ukiwa

na pakame kama jangwa.

14 Makundi ya kondoo na ngʼombe yatajilaza pale,

viumbe vya kila aina.

Bundi wa jangwani na bundi waliao kwa sauti nyembamba

wataishi juu ya nguzo zake.

Mwangwi wa kuita kwao utapita madirishani,

kifusi kitakuwa milangoni,

boriti za mierezi zitaachwa wazi.

15 Huu ndio mji uliotukuka na kuishi kwa furaha

wakijisikia salama.

Ulisema moyoni mwako,

“Mimi ndimi, na wala hapana mwingine ila mimi.”

Jinsi gani umekuwa gofu,

mahali pa kulala wanyama pori!

Wote wanaopita kando yake wanauzomea

na kutikisa mkono kwa dharau.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ZEP/2-1b18ca38d2ccf242c0429323ed47e58d.mp3?version_id=1627—

Categories
Sefania

Sefania 3

Hatima Ya Yerusalemu

1 Ole mji wa wadhalimu,

waasi na waliotiwa unajisi!

2 Hautii mtu yeyote,

haukubali maonyo.

HaumtumainiBwana,

haukaribii karibu na Mungu wake.

3 Maafisa wake ni simba wangurumao,

watawala wake ni mbwa mwitu wa jioni,

ambao hawabakizi chochote

kwa ajili ya asubuhi.

4 Manabii wake ni wenye kiburi,

ni wadanganyifu.

Makuhani wake hunajisi patakatifu

na kuihalifu sheria.

5 Bwanaaliye ndani yake ni mwenye haki,

hafanyi kosa.

Asubuhi kwa asubuhi hutoa haki yake,

kila kukipambazuka huitimiza,

bali mtu dhalimu hana aibu.

6 “Nimeyafutilia mbali mataifa,

ngome zao zimebomolewa.

Nimeziacha barabara ukiwa,

hakuna anayepita humo.

Miji yao imeharibiwa;

hakuna mmoja atakayeachwa:

hakuna hata mmoja.

7 Niliuambia huo mji,

‘Hakika utaniogopa na kukubali maonyo!’

Ndipo makao yake hayatafutiliwa mbali,

wala adhabu zangu zote hazitakuja juu yake.

Lakini walikuwa bado na shauku

kutenda kwa upotovu katika yote waliyofanya.”

8 Bwanaanasema,

“Kwa hiyo ningojee mimi,

siku nitakayosimama kuteka nyara.

Nimeamua kukusanya mataifa,

kukusanya falme

na kumimina ghadhabu yangu juu yao,

hasira yangu kali yote.

Dunia yote itateketezwa

kwa moto wa wivu wa hasira yangu.

9 “Ndipo nitatakasa midomo ya mataifa,

kwamba wote waweze kuliitia jina laBwana

na kumtumikia kwa pamoja.

10 Kutoka ngʼambo ya mito ya Kushi

watu wangu wanaoniabudu,

watu wangu waliotawanyika,

wataniletea sadaka.

11 Siku hiyo hutaaibishwa

kwa ajili ya makosa yote ulionitendea,

kwa sababu nitawaondoa kutoka mji huu

wale wote wanaoshangilia

katika kiburi chao.

Kamwe hutajivuna tena

katika kilima changu kitakatifu.

12 Lakini nitakuachia ndani yako

wapole na wanyenyekevu,

ambao wanatumaini jina laBwana.

13 Mabaki ya Israeli hayatafanya kosa;

hawatasema uongo,

wala udanganyifu hautakuwa

katika vinywa vyao.

Watakula na kulala

wala hakuna yeyote

atakayewaogopesha.”

14 Imba, ee Binti Sayuni;

paza sauti, ee Israeli!

Furahi na kushangilia kwa moyo wako wote,

ee Binti Yerusalemu!

15 Bwanaamekuondolea adhabu yako,

amewarudisha nyuma adui zako.

Bwana, Mfalme wa Israeli, yu pamoja nawe;

kamwe hutaogopa tena madhara yoyote.

16 Katika siku hiyo watauambia Yerusalemu,

“Usiogope, ee Sayuni;

usiiache mikono yako ilegee.

17 BwanaMungu wako yu pamoja nawe,

yeye ni mwenye nguvu kuokoa.

Atakufurahia kwa furaha kubwa,

atakutuliza kwa pendo lake,

atakufurahia kwa kuimba.”

18 “Huzuni katika sikukuu zilizoamriwa

nitaziondoa kwenu;

hizo ni mzigo na fedheha kwenu.

19 Wakati huo nitawashughulikia

wote waliokudhulumu;

nitaokoa vilema na kukusanya

wale ambao wametawanywa.

Nitawapa sifa na heshima

katika kila nchi ambayo waliaibishwa.

20 Wakati huo nitawakusanya;

wakati huo nitawaleta nyumbani.

Nitawapa sifa na heshima

miongoni mwa mataifa yote ya dunia

wakati nitakapowarudishia mateka yenu

mbele ya macho yenu hasa,”

asemaBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ZEP/3-f093c4ce0bcf69b438670c034e31a7bd.mp3?version_id=1627—

Categories
Hagai

Hagai Utangulizi

Utangulizi

Hagai ni moja ya vitabu vitatu vya kinabii vya Agano la Kale vilivyoandikwa baada ya uhamisho. Hagai na Zekaria ndio waliowatia moyo watu waliorudi kutoka uhamishoni kujenga upya Hekalu baada ya Mfalme Dario kupitisha amri kuwaruhusu Wayahudi kurudi Yerusalemu.

Kundi la kwanza la Wayahudi liliporudi Yerusalemu liliweka msingi wa Hekalu jipya wakiwa na furaha na matumaini makubwa. Hata hivyo, Wasamaria na majirani wengine walipinga ujenzi huo kwa nguvu nyingi na kuwakatisha tamaa wafanyakazi, na hata kuufanya ujenzi huo usimame. Watu wakageukia ujenzi wa nyumba zao wenyewe. Ujumbe wa Hagai ulikuwa kwamba ni wakati wa kujenga nyumba ya Mungu.

Mwandishi

Hagai.

Kusudi

Kuwahimiza watu kujenga upya Hekalu la

Bwana

, na kuwahamasisha kuyatengeneza maisha yao upya na Mungu ili waweze kupata baraka zake.

Mahali

Yerusalemu.

Tarehe

520 K.K.

Wahusika Wakuu

Hagai, Zerubabeli, Yoshua.

Wazo Kuu

Hagai aliwaambia watu kwamba utukufu wa Hekalu walilokuwa wanajenga ungekuwa mkubwa kuliko ule wa Hekalu lililotangulia, ingawaje halingekuwa imara kama la kwanza. Hili Hekalu lingekuwa bora zaidi kwa sababu Mungu angelijaza utukufu wake ndani yake.

Mambo Muhimu

Kuwaita watu kujenga upya Hekalu la Yerusalemu lililobomolewa, na ahadi ya Mungu ya kuwabariki kama wangemtii.

Mgawanyo

Wito wa kujenga Hekalu (

1:1-15

)

Matumaini ya Hekalu jipya (

2:1-9

)

Baraka zilizoahidiwa (

2:10-19

)

Ushindi wa mwisho wa Mungu (

2:20-23

).

Categories
Hagai

Hagai 1

Wito Wa Kuijenga Nyumba Ya Bwana

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi, katika siku ya kwanza ya mwezi wa sita, neno laBwanalilikuja kupitia kwa nabii Hagai kwenda kwa Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda na kwa Yoshuamwana wa kuhani mkuu Yehosadaki:

2 Hivi ndivyo asemavyoBwanaMwenye Nguvu Zote: “Hawa watu husema, ‘Wakati haujawadia wa kujenga nyumba yaBwana.’ ”

3 Kisha neno laBwanalikaja kupitia kwa nabii Hagai:

4 “Je, ni wakati wenu ninyi wa kuishi katika nyumba zenu zilizojengwa vizuri, wakati hii nyumba ikibaki, gofu?”

5 Sasa hili ndilo asemaloBwanaMwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.

6 Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotobokatoboka.”

7 Hili ndilo asemaloBwanaMwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.

8 Pandeni milimani mkalete miti na kujenga nyumba, ili nipate kuifurahia, na nitukuzwe,” asemaBwana.

9 “Mlitarajia mengi, kumbe, yametokea kidogo. Ulichokileta nyumbani nilikipeperusha. Kwa nini?” asemaBwanaMwenye Nguvu Zote. “Ni kwa sababu ya nyumba yangu, inayobaki katika hali ya magofu, wakati kila mmoja wenu anajishughulisha na nyumba yake mwenyewe.

10 Kwa hiyo, kwa sababu yenu mbingu zimezuia umande wake na ardhi mavuno yake.

11 Niliita ukame mashambani na milimani, kwenye nafaka, mvinyo mpya, mafuta pamoja na chochote kinachozalishwa na ardhi, juu ya watu na ngʼombe, pamoja na kazi za mikono yenu.”

12 Kisha Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yoshua kuhani mkuu mwana wa Yehosadaki, pamoja na mabaki yote ya watu wakaitii sauti yaBwanaMungu wao pamoja na ujumbe wa nabii Hagai, kwa sababu alikuwa ametumwa naBwanaMungu wao. Watu walimwogopaBwana.

13 Kisha Hagai, mjumbe waBwana, akawapa watu ujumbe huu waBwana: “Mimi niko pamoja nanyi,” asemaBwana.

14 Kwa hiyoBwanaakachochea roho ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, na roho ya kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, pamoja na roho za mabaki yote ya watu. Walikuja wakaanza kufanya kazi katika nyumba yaBwanaMwenye Nguvu Zote, Mungu wao,

15 katika siku ya ishirini na nne mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HAG/1-69a75d53ced7552db5a3c2fe4a8597fc.mp3?version_id=1627—

Categories
Hagai

Hagai 2

Utukufu Ulioahidiwa Wa Nyumba Mpya

1 Katika siku ya ishirini na moja ya mwezi wa saba, neno laBwanalilikuja kupitia nabii Hagai, kusema:

2 “Sema na Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, na mabaki ya watu. Uwaulize,

3 ‘Ni nani miongoni mwenu aliyebaki ambaye aliiona hii nyumba katika utukufu wake wa mwanzo? Sasa inaonekanaje kwenu? Je, haionekani kwenu kama si kitu?

4 Lakini sasa uwe imara, ee Zerubabeli,’ asemaBwana. ‘Kuwa imara, ee kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki. Mwe imara, enyi watu wote wa nchi,’ asemaBwana, ‘na mfanye kazi. Kwa kuwa mimi nipo pamoja nanyi,’ asemaBwanaMwenye Nguvu Zote.

5 ‘Hili ndilo nililoagana nanyi mlipotoka katika nchi ya Misri. Pia Roho wangu anadumu katikati yenu. Msiogope.’

6 “Hili ndilo asemaloBwanaMwenye Nguvu Zote: ‘Baada ya muda kidogo kwa mara nyingine nitazitikisa mbingu na nchi, bahari na nchi kavu.

7 Nitatikisa mataifa yote, nacho kile kinachotamaniwa na mataifa yote kitakuja, nami nitaujaza utukufu katika nyumba hii,’ asemaBwanaMwenye Nguvu Zote.

8 ‘Fedha ni mali yangu na dhahabu ni mali yangu,’ asemaBwanaMwenye Nguvu Zote.

9 ‘Utukufu wa nyumba hii ya sasa utakuwa mkubwa kuliko utukufu wa ile nyumba ya mwanzoni,’ asemaBwanaMwenye Nguvu Zote. ‘Na mahali hapa nitawapa amani,’ asemaBwanaMwenye Nguvu Zote.”

Baraka Kwa Watu Waliotiwa Unajisi

10 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno laBwanalilikuja kwa nabii Hagai:

11 “Hili ndilo asemaloBwanaMwenye Nguvu Zote: ‘Ulizeni makuhani jinsi sheria inavyosema:

12 Kama mtu akibeba nyama iliyowekwa wakfu katika pindo la vazi lake, kisha lile pindo likagusa mkate au mchuzi, divai, mafuta au chakula kingine, je, kitu hicho kitakuwa kimewekwa wakfu?’ ”

Makuhani wakajibu, “La hasha.”

13 Kisha Hagai akasema, “Je, kama mtu aliyetiwa unajisi kwa kugusa maiti akigusa mojawapo ya vitu hivi, kitu hicho kitakuwa kimetiwa unajisi?”

Makuhani wakajibu, “Ndiyo, huwa kimenajisiwa.”

14 Kisha Hagai akasema, “ ‘Basi ndivyo walivyo machoni pangu hawa watu na taifa hili,’ asemaBwana. ‘Lolote wafanyalo na chochote watoacho hapo ni najisi.

15 “ ‘Sasa fikirini kwa uangalifu kuanzia leo na kuendelea: tafakarini jinsi mambo yalivyokuwa kabla halijawekwa jiwe moja juu ya lingine katika Hekalu laBwana.

16 Wakati mtu alipoendea lundo la nafaka la vipimo ishirini, kulikuwa na vipimo kumi tu. Wakati mtu alipoendea pipa la mvinyo ili kuchota vipimo hamsini, kulikuwa na vipimo ishirini tu.

17 Kazi zenu zote za mikono nilizipiga kwa ukame, ukungu na mvua ya mawe, lakini hata hivyo, hamkunigeukia mimi,’ asemaBwana.

18 ‘Tangu leo na kuendelea, kuanzia siku hii ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, tafakarini siku ambayo msingi wa Hekalu laBwanauliwekwa. Tafakarini:

19 Je, bado kuna mbegu iliyobakia ghalani? Mpaka sasa, hakuna mzabibu au mtini, mkomamanga wala mzeituni uliozaa tunda.

“ ‘Kuanzia leo na kuendelea, nitawabariki.’ ”

Zerubabeli Pete Ya Muhuri Ya Bwana

20 Neno laBwanalikamjia Hagai kwa mara ya pili katika siku ya ishirini na nne ya mwezi kusema:

21 “Mwambie Zerubabeli mtawala wa Yuda kwamba nitazitikisa mbingu na nchi.

22 Nitapindua viti vya enzi vya falme, na kuziharibu kabisa nguvu za falme za kigeni. Nitapindua magari ya vita pamoja na waendeshaji wake; farasi na wapanda farasi wataanguka, kila mmoja kwa upanga wa ndugu yake.

23 “ ‘Katika siku ile,’ asemaBwanaMwenye Nguvu Zote, ‘nitakuchukua wewe, mtumishi wangu Zerubabeli mwana wa Shealtieli,’ asemaBwana. ‘Nitakufanya kama pete yangu ya muhuri, kwa kuwa nimekuchagua,’ asemaBwanaMwenye Nguvu Zote.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HAG/2-26cce82c34d9eebd11892eb101f1a27b.mp3?version_id=1627—

Categories
Zekaria

Zekaria Utangulizi

Utangulizi

Maana ya jina Zekaria ni “

Bwana

amekumbuka.” Yaonekana kama alikuwa kijana wakati alipoanza huduma yake. Zekaria aliwaonya watu waliokuwa wameanza kujenga upya Hekalu kwamba iliwapasa kusikiliza ujumbe wa Mungu kupitia kwa manabii. Aliwahimiza kudumisha uhusiano wa muhimu na Mungu ili wasiiharakishe hukumu ya Mungu. Mfululizo wa maono yalikuwa ya kuwatia moyo wajenzi katika wakati mgumu. Mtazamo wa jumla wa mafunzo wa maono haya manane yaliwahakikishia wajenzi kwamba Mungu alikuwa na mpango wa muda mrefu kwa ajili ya Israeli.

Sehemu ya mwisho wa huduma yake, Zekaria alikazia mpango wa maendeleo wa muda mrefu akionyesha kusimamishwa kwa ufalme wa mwisho. Mfalme anatambulishwa kama anayekuja kwa unyenyekevu akileta wokovu lakini akikataliwa na watu wake mwenyewe, yaani, Waisraeli, ambao baadaye wanaachwa kwenye hukumu ya mataifa. Mataifa yatakapokusanyika kwa ajili ya vita dhidi ya Yerusalemu, Waisraeli watamtambua Masiya na wataibuka na ushindi, nayo mataifa yote yatakuja Yerusalemu kumwabudu Mfalme.

Mwandishi

Zekaria.

Kusudi

Kuwapa watu wa Mungu matumaini kwa kuwajulisha watu mpango wa Mungu wa baadaye wa ukombozi kupitia kwa Masiya.

Mahali

Yerusalemu.

Tarehe

Sura 1-8 kati ya 520–518 K.K.; sura 9-14 mwaka wa 480 K.K.

Wahusika Wakuu

Zekaria, Zerubabeli, Yoshua na waliorudi kutoka uhamishoni.

Wazo Kuu

Zekaria anaonyesha kwamba Mungu ana mpango wa muda mrefu na Israeli, hivyo anaita watu kwa mwito wa utii. Anaonyesha jinsi watu wanaweza kufanya mambo kwa Roho wa Mungu.

Mambo Muhimu

Zekaria alieleza juu ya hukumu ya Mungu dhidi ya maadui wa Israeli, baraka kwa ajili ya Yerusalemu, na umuhimu wa watu wa Mungu kudumu katika utakatifu. Mungu atawahukumu adui wa Israeli na Mfalme (Masiya) atakuja.

Mgawanyo

Utangulizi (

1:1-6

)

Maono nane ya kinabii (

1:7–6:8

)

Kutawazwa kwa Yoshua kinabii (

6:9-15

)

Jumbe mbali mbali za hukumu na matumaini (

7:1–10:12

)

Kuja kwa Masiya na kukataliwa kwake (

11:1–13:9

)

Ushindi mwishowe wa Masiya (

14:1-21

).

Categories
Zekaria

Zekaria 1

Wito Wa Kumrudia Bwana

1 Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno laBwanalilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:

2 “Bwanaaliwakasirikia sana baba zako wa zamani.

3 Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyoBwanaMwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asemaBwanaMwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asemaBwanaMwenye Nguvu Zote.

4 Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyoBwanaMwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asemaBwana.

5 Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele?

6 Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?”

“Kisha walitubu na kusema, ‘BwanaMwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’ ”

Maono Ya Kwanza: Mtu Katikati Ya Miti Ya Mihadasi

7 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno laBwanalilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.

8 Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.

9 Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?”

Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”

10 Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambaoBwanaamewatuma waende duniani kote.”

11 Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika waBwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”

12 Kisha malaika waBwanaakasema, “BwanaMwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?”

13 Kwa hiyoBwanaakazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.

14 Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndiloBwanaMwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni,

15 lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’

16 “Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyoBwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asemaBwanaMwenye Nguvu Zote.

17 “Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyoBwanaMwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi naBwanaatamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’ ”

Maono Ya Pili: Pembe Nne Na Mafundi Wanne

18 Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne!

19 Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?”

Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”

20 KishaBwanaakanionyesha mafundi wanne.

21 Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?”

Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ZEC/1-820ed10f4b850a2f4b472d51dc147d9d.mp3?version_id=1627—