Categories
Mika

Mika 5

Mtawala Aliyeahidiwa Kutoka Bethlehemu

1 Panga majeshi yako, ee mji wa majeshi,

kwa kuwa kuzingirwa kumepangwa dhidi yetu.

Watampiga mtawala wa Israeli

shavuni kwa fimbo.

2 “Lakini wewe, Bethlehemu Efrathi,

ingawa u mdogo miongoni mwa koo za Yuda,

kutoka kwako atatokea kwa ajili yangu

yeye atakayekuwa mtawala katika Israeli,

ambaye asili yake ni kutoka zamani,

kutoka milele.”

3 Kwa hiyo Israeli utaachwa mpaka wakati

mwanamke aliye na utungu atakapozaa

na ndugu zake wengine warudi

kujiunga na Waisraeli.

4 Atasimama na kulichunga kundi lake

katika nguvu yaBwana,

katika utukufu wa jina laBwanaMungu wake.

Nao wataishi kwa usalama, kwa kuwa wakati huo

ukuu wake utaenea hadi miisho ya dunia.

5 Naye atakuwa amani yao.

Ukombozi Na Uharibifu

Wakati Mwashuru atakapovamia nchi yetu

na kupita katika ngome zetu,

tutawainua wachungaji saba dhidi yake,

hata viongozi wanane wa watu.

6 Wataitawala nchi ya Ashuru kwa upanga,

nchi ya Nimrodi kwa upanga.

Atatuokoa kutoka kwa Mwashuru

atakapoivamia nchi yetu

na kuingia katika mipaka yetu.

7 Mabaki ya Yakobo yatakuwa

katikati ya mataifa mengi

kama umande kutoka kwaBwana,

kama manyunyu juu ya majani,

ambayo hayamngoji mtu

wala kukawia kwa mwanadamu.

8 Mabaki ya Yakobo yatakuwa miongoni mwa mataifa,

katikati ya mataifa mengi,

kama simba miongoni mwa wanyama wa msituni,

kama mwana simba miongoni

mwa makundi ya kondoo,

ambaye anaumiza vibaya na kuwararua

kila anapopita katikati yao,

wala hakuna awezaye kuokoa.

9 Mkono wako utainuliwa juu kwa ushindi juu ya watesi wako,

nao adui zako wote wataangamizwa.

10 “Katika siku ile,” asemaBwana,

“nitaangamiza farasi zenu katikati yenu

na kubomoa magari yenu ya vita.

11 Nitaiangamiza miji ya nchi yenu

na kuziangusha chini ngome zenu zote.

12 Nitaangamiza uchawi wenu

na hamtapiga tena ramli.

13 Nitaangamiza vinyago vyenu vya kuchonga

na mawe yenu ya ibada yatoke katikati yenu;

hamtasujudia tena

kazi ya mikono yenu.

14 Nitangʼoa nguzo za Ashera katikati yenu

na kubomoa miji yenu.

15 Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu

juu ya mataifa ambayo hayajanitii.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/MIC/5-89f2f5314d9cbc53b197da6836b87709.mp3?version_id=1627—

Categories
Mika

Mika 6

Shauri La Bwana Dhidi Ya Israeli

1 Sikiliza asemaloBwana:

“Simama, tetea shauri lako mbele ya milima;

vilima na visikie lile unalotaka kusema.

2 Sikilizeni, ee milima, mashtaka yaBwana,

sikilizeni, enyi misingi ya milele ya dunia.

Kwa kuwaBwanaana shauri dhidi ya watu wake;

anatoa mashtaka dhidi ya Israeli.

3 “Watu wangu, nimewatendea nini?

Nimewalemea kwa jinsi gani? Mnijibu.

4 Nimewatoa kutoka Misri na kuwakomboa

kutoka nchi ya utumwa.

Nilimtuma Mose awaongoze,

pia Aroni na Miriamu.

5 Watu wangu, kumbukeni jinsi Balaki mfalme wa Moabu

alivyofanya shauri

na kile Balaamu mwana wa Beori alichojibu.

Kumbukeni safari yenu kutoka Shitimu mpaka Gilgali,

ili mfahamu matendo ya haki yaBwana.”

6 NimjieBwanana kitu gani na kusujudu

mbele za Mungu aliyetukuka?

Je, nije mbele zake na sadaka za kuteketezwa,

nije na ndama za mwaka mmoja?

7 Je,Bwanaatafurahishwa na kondoo dume elfu,

au mito elfu kumi ya mafuta?

Je, nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa ajili ya kosa langu,

mtoto wangu mwenyewe

kwa ajili ya dhambi ya nafsi yangu?

8 Amekuonyesha yaliyo mema, ee mwanadamu.

Bwanaanataka nini kwako?

Ila kutenda kwa haki na kupenda rehema,

na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako.

Hatia Na Adhabu Ya Israeli

9 Sikiliza!Bwanaanauita mji:

kulicha jina lako ni hekima:

“Tii hiyo fimbo na yeye aliyeiamuru.

10 Je, bado nisahau, ee nyumba ya uovu,

hazina yako uliyopata kwa udanganyifu

na vipimo vilivyopunguka,

ambavyo vimelaaniwa?

11 Je, naweza kuhukumu kuwa

mtu mwenye mizani ya udanganyifu hana hatia,

aliye na mfuko wa mawe ya kupimia ya uongo?

12 Matajiri wake ni wajeuri;

watu wake ni waongo

na ndimi zao zinazungumza

kwa udanganyifu.

13 Kwa hiyo, nimeanza kukuharibu,

kuwaangamiza kwa sababu ya dhambi zenu.

14 Mtakula lakini hamtashiba;

matumbo yenu bado yatakuwa matupu.

Mtaweka akiba lakini hamtaokoa chochote,

kwa sababu mtakachoweka akiba

nitatoa kwa upanga.

15 Mtapanda lakini hamtavuna;

mtakamua zeituni lakini

hamtatumia mafuta yake.

Mtakamua zabibu

lakini hamtakunywa hiyo divai.

16 Mmezishika sheria za Omri

na matendo yote ya nyumba ya Ahabu,

tena umefuata desturi zao.

Kwa hiyo nitakutoa kwa maangamizi

na watu wako kuwa dhihaka;

mtachukua dharau za mataifa.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/MIC/6-ff861ca39e31ef65682dde44fedc0dd1.mp3?version_id=1627—

Categories
Mika

Mika 7

Taabu Ya Israeli

1 Taabu gani hii niliyo nayo!

Nimefanana na yule akusanyaye

matunda ya kiangazi,

aokotaye masazo baada ya kuvunwa

shamba la mizabibu;

hakuna kishada chenye matunda ya kula,

hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.

2 Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi;

hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki.

Watu wote wanavizia kumwaga damu,

kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.

3 Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya,

mtawala anadai zawadi,

hakimu anapokea rushwa,

wenye nguvu wanaamuru wanachotaka:

wote wanafanya shauri baya pamoja.

4 Aliye mwema kupita wote kati yao

ni kama mchongoma,

anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao

ni mbaya kuliko uzio wa miiba.

Siku ya walinzi wako imewadia,

siku atakayokutembelea Mungu.

Sasa ni wakati wao

wa kuchanganyikiwa.

5 Usimtumaini jirani;

usiweke matumaini kwa rafiki.

Hata kwa yule alalaye kifuani mwako

uwe mwangalifu kwa maneno yako.

6 Kwa kuwa mwana humdharau baba yake,

naye binti huinuka dhidi ya mama yake,

mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake:

adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.

7 Lakini mimi, namtazamaBwanakwa matumaini,

namngoja Mungu Mwokozi wangu;

Mungu wangu atanisikia mimi.

Israeli Atainuka

8 Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu!

Ingawa nimeanguka, nitainuka.

Japo ninaketi gizani,

Bwanaatakuwa nuru yangu.

9 Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake,

nitabeba ghadhabu yaBwana,

mpaka atakaponitetea shauri langu

na kuithibitisha haki yangu.

Atanileta nje kwenye mwanga,

nami nitaiona haki yake.

10 Kisha adui yangu ataliona

naye atafunikwa na aibu,

yule aliyeniambia,

“Yu wapiBwanaMungu wako?”

Macho yangu yataona kuanguka kwake,

hata sasa atakanyagwa chini ya mguu

kama tope barabarani.

11 Siku ya kujenga kuta zako itawadia,

siku ya kupanua mipaka yako.

12 Siku hiyo watu watakuja kwako

kutoka Ashuru na miji ya Misri,

hata kutoka Misri hadi Frati

na kutoka bahari hadi bahari

na kutoka mlima hadi mlima.

13 Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake,

kwa sababu ya matunda ya matendo yao.

Sala Na Sifa

14 Wachunge watu wako kwa fimbo yako,

kundi la urithi wako,

ambalo linaishi peke yake msituni,

katika nchi ya malisho yenye rutuba.

Waache walishe katika Bashani na Gileadi

kama ilivyokuwa siku za kale.

15 “Kama siku zile mlipotoka Misri,

nitawaonyesha maajabu yangu.”

16 Mataifa yataona na kuaibika,

waliondolewa nguvu zao zote.

Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao

na masikio yao yatakuwa na uziwi.

17 Wataramba mavumbi kama nyoka,

kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi.

Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka;

watamgeukiaBwanaMungu wetu kwa hofu

nao watakuogopa.

18 Ni nani Mungu kama wewe,

ambaye anaachilia dhambi

na kusamehe makosa

ya mabaki ya urithi wake?

Wewe huwi na hasira milele,

bali unafurahia kuonyesha rehema.

19 Utatuhurumia tena,

utazikanyaga dhambi zetu

chini ya nyayo zako,

na kutupa maovu yetu yote

katika vilindi vya bahari.

20 Utakuwa wa kweli kwa Yakobo,

nawe utamwonyesha Abrahamu rehema,

kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu

siku za kale.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/MIC/7-ca45d233b469bf8ef7c59311f5f4c08e.mp3?version_id=1627—

Categories
Nahumu

Nahumu Utangulizi

Utangulizi

Nahumu ambaye jina lake linamaanisha “Faraja” alikuwa mwenyeji wa Elikoshi. Alihudumu wakati mmoja na Sefania, Yeremia na Habakuki. Katika ujumbe wake alizungumzia kuanguka kwa Thebesi mwaka wa 663 K.K. na kuanguka kwa Ninawi mnamo mwaka wa 612 K.K. Nahumu anaeleza kwa wazi juu ya uonevu na udhalimu wa kikatili wa Ashuru, na jinsi walivyosonga mbele na kushinda taifa moja baada ya lingine.

Ukatili huo usiokuwa na chembe cha huruma usingeweza kuvumiliwa na Mungu mwenye haki aliye mtakatifu pasipo kikomo. Katika unabii huu Nahumu anaelezea vizuri na kuonyesha kuzingirwa na kuanguka kwa Ninawi kuwa ndio mwisho wa huu ufalme wenye nguvu wa Ashuru, ambao ndio ulikuwa unakalia sehemu zenye rutuba kwa zaidi ya karne nzima. Kwa nasaha fupi kwa watu wa Yuda, Nahumu anawashauri watu wake kuzitii sikukuu zao za kidini, kwa kuwa Waashuru wasingeliishambulia tena Yerusalemu.

Mwandishi

Nahumu.

Kusudi

Kutamka hukumu ya Mungu dhidi ya Waashuru na kuwafariji Yuda.

Tarehe

Kati ya 663–612 K.K.

Mahali

Ninawi.

Wahusika Wakuu

Waninawi.

Wazo Kuu

Yehova ni Mungu mwenye wivu ambaye mapatilizo yake kwa hakika lazima yawapate adui zake, lakini yeye ni ngome kwa wale wanaomtumaini.

Mambo Muhimu

Nahumu anaeleza kukaribia kwa hukumu ya Ninawi na jinsi itakavyokuwa kwa lugha ya wazi. Anaorodhesha kwa kifupi dhambi za Ninawi na kutamka kwamba Mungu ni mwenye haki katika hukumu zake. Anamalizia kwa kuiona hukumu iliyokamilika. Hiki ndicho kitabu cha Agano la Kale kinachotoa unabii wake waziwazi juu ya ukatili wa Waashuru.

Mgawanyo

Hasira ya Mungu dhidi ya Ninawi (

1:1-15

)

Kuanguka kwa Ninawi (

2:1-13

)

Ukiwa kwa Ninawi (

3:1-19

).

Categories
Nahumu

Nahumu 1

1 Neno alilosema Mungu kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono cha Nahumu, Mwelkoshi.

Hasira Ya Mungu Dhidi Ya Ninawi

2 Bwanani mwenye wivu na Mungu mlipiza kisasi;

Bwanahulipiza kisasi na amejaa ghadhabu.

Bwanahulipiza kisasi juu ya watesi wake,

naye anadumisha ghadhabu yake dhidi ya adui zake.

3 Bwanasi mwepesi wa hasira naye ni mwenye nguvu,

Bwanahataacha kuadhibu wenye hatia.

Njia yake ipo katika kisulisuli na tufani,

na mawingu ni vumbi la miguu yake.

4 Anakemea bahari na kuikausha,

anafanya mito yote kukauka.

Bashani na Karmeli zinanyauka

na maua ya Lebanoni hukauka.

5 Milima hutikisika mbele yake

na vilima huyeyuka.

Nchi hutetemeka mbele yake,

dunia na wote waishio ndani yake.

6 Ni nani awezaye kuzuia hasira yake yenye uchungu?

Nani awezaye kuvumilia hasira yake kali?

Ghadhabu yake imemiminwa kama moto,

na miamba inapasuka mbele zake.

7 Bwanani Mwema,

kimbilio wakati wa taabu.

Huwatunza wale wanaomtegemea,

8 lakini kwa mafuriko makubwa,

ataangamiza Ninawi;

atafuatilia adui zake hadi gizani.

9 Shauri baya lolote wapangalo dhidi yaBwana

yeye atalikomesha;

taabu haitatokea mara ya pili.

10 Watasongwa katikati ya miiba

na kulewa kwa mvinyo wao.

Watateketezwa kama mabua makavu.

11 Ee Ninawi, kutoka kwako amejitokeza mmoja,

ambaye anapanga shauri baya

dhidi yaBwana

na kushauri uovu.

12 Hili ndilo asemaloBwana:

“Ingawa wana muungano nao ni wengi sana,

watakatiliwa mbali na kuangamia.

Ingawa nimekutesa wewe, ee Yuda,

sitakutesa tena.

13 Sasa nitavunja nira zao kutoka shingo yako,

nami nitazivunjilia mbali pingu zako.”

14 Hii ndiyo amriBwanaaliyoitoa kukuhusu wewe, Ninawi:

“Hutakuwa na wazao

watakaoendeleza jina lako.

Nitaharibu sanamu za kuchonga na sanamu za kuyeyusha

ambazo zipo katika hekalu la miungu yenu.

Nitaandaa kaburi lako,

kwa maana wewe ni mwovu kabisa.”

15 Tazama, huko juu milimani,

miguu ya huyo mmoja aletaye habari njema,

ambaye anatangaza amani!

Ee Yuda, sherehekea sikukuu zako,

nawe utimize nadhiri zako.

Waovu hawatakuvamia tena;

wataangamizwa kabisa.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/NAM/1-e7b3a0bd3e138a8d3423ddb036387da5.mp3?version_id=1627—

Categories
Nahumu

Nahumu 2

Ninawi Kuanguka

1 Mshambuliaji anasogea dhidi yako, Ninawi.

Linda ngome,

chunga barabara,

jitieni nguvu wenyewe,

kusanya nguvu zako zote!

2 Bwanaatarudisha fahari ya Yakobo,

kama fahari ya Israeli,

ingawa waangamizi wamewaacha ukiwa

na wameharibu mizabibu yao.

3 Ngao za askari wake ni nyekundu,

mashujaa wamevaa nguo nyekundu.

Chuma kwenye magari ya vita chametameta,

katika siku aliyoyaweka tayari,

mikuki ya mierezi inametameta.

4 Magari ya vita yanafanya msukosuko barabarani,

yakikimbia nyuma na mbele uwanjani.

Yanaonekana kama mienge ya moto;

yanakwenda kasi kama umeme.

5 Anaita vikosi vilivyochaguliwa,

lakini bado wanajikwaa njiani.

Wanakimbilia haraka kwenye ukuta wa mji,

ile ngao ya kuwakinga imetayarishwa.

6 Malango ya mto yamefunguliwa wazi,

na jumba la kifalme limeanguka.

7 Imeagizwa kwamba mji uchukuliwe

na upelekwe uhamishoni.

Vijakazi wake wanaomboleza kama hua

na kupigapiga vifua vyao.

8 Ninawi ni kama dimbwi,

nayo maji yake yanakauka.

Wanalia, “Simama! Simama!”

Lakini hakuna anayegeuka nyuma.

9 Chukueni nyara za fedha!

Chukueni nyara za dhahabu!

Wingi wake hauna mwisho,

utajiri kutoka hazina zake zote!

10 Ameharibiwa, ametekwa nyara, ameachwa uchi!

Mioyo inayeyuka, magoti yanalegea,

miili inatetemeka,

na kila uso umebadilika rangi.

11 Liko wapi sasa pango la simba,

mahali ambapo waliwalisha watoto wao,

ambapo simba dume na simba jike walikwenda

na ambapo wana simba walikwenda

bila kuogopa chochote?

12 Simba aliua mawindo ya kutosha watoto wake,

alinyonga mawindo kwa ajili ya mwenzi wake,

akijaza makao yake kwa alivyoua

na mapango yake kwa mawindo.

13 BwanaMwenye Nguvu Zote anatangaza,

“Mimi ni kinyume na ninyi.

Magari yenu ya vita nitayateketeza kwa moto,

na upanga utakula wana simba wako.

Sitawaachia mawindo juu ya nchi.

Sauti za wajumbe wako

hazitasikika tena.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/NAM/2-a38be8b5316b20df831b93932f1e5efe.mp3?version_id=1627—

Categories
Nahumu

Nahumu 3

Ole Wa Ninawi

1 Ole wa mji umwagao damu,

uliojaa uongo,

umejaa nyara,

usiokosa kuwa na vitu vya kuteka nyara.

2 Kelele za mijeledi,

vishindo vya magurudumu,

farasi waendao mbio

na mshtuo wa magari ya vita!

3 Wapanda farasi wanaenda mbio,

panga zinameremeta,

na mikuki inangʼaa!

Majeruhi wengi,

malundo ya maiti,

idadi kubwa ya miili isiyohesabika,

watu wanajikwaa juu ya mizoga:

4 yote haya kwa sababu ya wingi wa tamaa za kahaba,

anayeshawishi, bibi wa mambo ya uchawi,

anayewatia utumwani mataifa kwa ukahaba wake

na pia jamaa za watu kwa ulozi wake.

5 BwanaMwenye Nguvu Zote anasema,

“Mimi ni kinyume na ninyi.

Nitafunika uso wako kwa gauni lako.

Nitaonyesha mataifa uchi wako

na falme aibu yako.

6 Nitakutupia uchafu,

nitakufanyia dharau

na kukufanya kioja.

7 Wote wanaokuona watakukimbia na kusema,

‘Ninawi ipo katika kuangamia:

ni nani atakayeomboleza kwa ajili yake?’

Nitampata wapi yeyote wa kukufariji?”

8 Je, wewe ni bora kuliko No-Amoni,

uliopo katika Mto Naili,

uliozungukwa na maji?

Mto ulikuwa kinga yake,

nayo maji yalikuwa ukuta wake.

9 Kushina Misri walikuwa nguvu zake zisizo na mpaka;

Putu na Libia walikuwa miongoni mwa wale walioungana naye.

10 Hata hivyo alichukuliwa mateka

na kwenda uhamishoni.

Watoto wake wachanga walivunjwa vunjwa vipande

kwenye mwanzo wa kila barabara.

Kura zilipigwa kwa watu wake wenye heshima,

na watu wake wote wakuu walifungwa kwa minyororo.

11 Wewe pia utalewa;

utakwenda mafichoni

na kutafuta kimbilio kutoka kwa adui.

12 Ngome zako zote ni kama mitini

yenye matunda yake ya kwanza yaliyoiva;

wakati inapotikiswa,

tini huanguka kwenye kinywa chake alaye.

13 Tazama vikosi vyako:

wote ni wanawake!

Malango ya nchi yako

yamekuwa wazi kwa adui zako;

moto umeteketeza mapingo yake.

14 Teka maji kwa ajili ya kuzingirwa kwako,

imarisha ulinzi wako,

Ufanyie udongo wa mfinyanzi kazi,

yakanyage matope,

karabati tanuru la kuchomea matofali!

15 Huko moto utakuteketeza,

huko upanga utakuangusha chini

na kama vile panzi, watakumaliza.

Ongezeka kama panzi,

ongezeka kama nzige!

16 Umeongeza idadi ya wafanyabiashara wako

mpaka wamekuwa wengi kuliko nyota za angani,

lakini kama nzige wanaacha nchi tupu

kisha huruka na kwenda zake.

17 Walinzi wako ni kama nzige,

maafisa wako ni kama makundi ya nzige

watuao kwenye kuta wakati wa siku ya baridi:

lakini wakati jua linapotokea wanaruka kwenda zao,

na hakuna ajuaye waendako.

18 Ee mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wanasinzia;

wakuu wako wanalala chini mavumbini kupumzika.

Watu wako wametawanyika juu ya milima

bila kuwa na mtu yeyote wa kuwakusanya.

19 Hakuna kitu kinachoweza kuponya jeraha lako;

jeraha lako ni la kukuua.

Kila anayesikia habari zako,

hupiga makofi kwa kuanguka kwako,

kwa kuwa ni nani ambaye hajaguswa

na ukatili wako usio na mwisho?

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/NAM/3-042fb57d52bd9f9110981ba6bbb7d98c.mp3?version_id=1627—

Categories
Habakuki

Habakuki Utangulizi

Utangulizi

Habakuki maana yake ni “Kumbatia.” Alikuwa nabii wa Yuda wa kabila la Lawi, mmoja wa waimbaji katika Hekalu. Kitabu hiki kimeandikwa kwa mtindo wa mazungumzo kati ya Mungu na nabii. Habakuki hakuelewa jinsi gani Mungu angeweza kuwatumia Wakaldayo, waliokuwa waovu kuliko Wayahudi, kutekeleza hukumu dhidi ya watu waliokuwa wamechaguliwa na Mungu. Jibu la Mungu lilikuwa kwamba wenye haki wangeishi kwa imani kwa Mungu, na kwamba walikuwa na uhakika kwamba Mungu alikuwa anafanya lililo sahihi. Mungu alimwambia Habakuki kwamba punde si punde Wakaldayo wangehukumiwa, na kwamba hatimaye haki ingeshinda kwa ajili ya watu wa Mungu.

Mwandishi

Habakuki.

Kusudi

Kuonyesha kwamba bado Mungu anaitawala dunia. Hata kama tunaona uovu ukishamiri, kuna siku Mungu atahukumu na kuadhibu huo uovu, na hatimaye kuuangamiza kabisa, usiwepo tena.

Mahali

Yuda.

Tarehe

Kati ya 612–589 K.K.

Wahusika Wakuu

Habakuki, na Wakaldayo.

Wazo Kuu

Mungu anaweza kuwatumia waovu kuadhibu watu wake wanapotenda dhambi kwa nia ya kuwarudisha kwake. Lakini hao waovu wakiisha kutimiza kusudi la Mungu, wao nao huadhibiwa zaidi.

Mambo Muhimu

Mungu hutumia watu waovu kuwaadhibu watu wake wanapokosea. Imani na mamlaka ya Mungu ni uhakika kwamba Mungu ana haki katika njia zake zote.

Mgawanyo

Swali la Habakuki na jibu la Mungu (

1:1-11

)

Swali la pili la Habakuki na jibu la Mungu (

1:12–2:20

)

Maombi ya Habakuki (

3:1-19

).

Categories
Habakuki

Habakuki 1

1 Neno alilopokea nabii Habakuki.

Lalamiko La Habakuki

2 EeBwana, hata lini nitakuomba msaada,

lakini wewe husikilizi?

Au kukulilia, “Udhalimu!”

Lakini hutaki kuokoa?

3 Kwa nini unanifanya nitazame dhuluma?

Kwa nini unavumilia makosa?

Uharibifu na udhalimu viko mbele yangu;

kuna mabishano na mapambano kwa wingi.

4 Kwa hiyo sheria imepotoshwa,

nayo haki haipo kabisa.

Waovu wanawazunguka wenye haki,

kwa hiyo haki imepotoshwa.

Jibu La Bwana

5 “Yatazame mataifa,

uangalie na ushangae kabisa.

Kwa sababu katika siku zako nitafanya kitu

ambacho hungeamini,

hata kama ungeambiwa.

6 Nitawainua Wakaldayo,

watu hao wakatili na wenye haraka,

ambao hupita dunia yote

kuteka mahali pa kuishi pasipo pao wenyewe.

7 Ni watu wanoogopwa na wanaotisha;

wenyewe ndio sheria yao,

na huinua heshima yao wenyewe.

8 Farasi wao ni wepesi kuliko chui,

na wakali kuliko mbwa mwitu wakati wa machweo.

Askari wapanda farasi wao huenda mbio;

waendesha farasi wao wanatoka mbali.

Wanaruka kasi kama tai ili kurarua;

9 wote wanakuja tayari kwa fujo.

Makundi yao ya wajeuri yanasonga mbele

kama upepo wa jangwani,

na kukusanya wafungwa

kama mchanga.

10 Wanawabeza wafalme,

na kuwadhihaki watawala.

Wanaicheka miji yote iliyozungushiwa maboma;

wanafanya malundo ya udongo na kuiteka hiyo miji.

11 Kisha wanapita kasi kama upepo na kusonga mbele:

watu wenye hatia, ambao nguvu zao ndio mungu wao.”

Lalamiko La Pili La Habakuki

12 EeBwana, je, wewe sio wa tangu milele?

Mungu wangu, Uliye Mtakatifu wangu, hatutakufa.

EeBwana, umewachagua wao ili watekeleze hukumu;

Ee Mwamba, umewaamuru watuadhibu.

13 Macho yako ni safi mno hata yasiweze kuutazama uovu,

wala huwezi kuvumilia makosa.

Kwa nini basi unawavumilia wadanganyifu?

Kwa nini unakuwa kimya wakati waovu

wanawameza wale wenye haki

kuliko wao wenyewe?

14 Umewafanya watu kama samaki baharini,

kama viumbe wa bahari wasio na mtawala.

15 Adui mwovu anawavuta wote kwa ndoana,

anawakamata katika wavu wake,

anawakusanya katika juya lake;

kwa hiyo anashangilia na anafurahi.

16 Kwa hiyo anatoa kafara kwa wavu wake,

na kuchoma uvumba kwa juya lake,

kwa kuwa kwa wavu wake anaishi kwa starehe,

na anafurahia chakula kizuri.

17 Je, aendelee kuwatoa walio katika wavu wake,

akiangamiza mataifa bila huruma?

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HAB/1-2499ca2309f069f88b812cf56b5f222e.mp3?version_id=1627—

Categories
Habakuki

Habakuki 2

1 Nitasimama katika zamu yangu,

na kujiweka mwenyewe juu ya maboma;

nitatazama nione atakaloniambia,

na ni jibu gani nitakalotoa kuhusu lalamiko hili.

Jibu La Bwana

2 KishaBwanaakajibu:

“Andika ufunuo huu,

na ukaufanye wazi juu ya vibao,

ili mpiga mbiu akimbie nao.

3 Kwa kuwa ufunuo huu unasubiri wakati uliokubalika;

unazungumzia mambo ya mwisho,

na kamwe hautakosea.

Iwapo utakawia, wewe usubiri;

kwa hakika utakuja na hautachelewa.

4 “Tazama, amejaa majivuno;

anavyovitamani si vya unyofu:

lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake:

5 hakika mvinyo humsaliti;

ni mwenye kiburi na hana amani.

Kwa sababu ni mlafi kama kuzimu

na kama kifo kamwe hatosheki;

anajikusanyia mataifa yote

na kuchukua watu wote mateka.

6 “Je, watu wote hawatamsuta kwa dhihaka na kumbeza, wakisema,

“ ‘Ole wake yeye akusanyaye bidhaa zilizoibwa

na kujifanyia utajiri kwa kutoza kwa nguvu!

Ataendelea hivi kwa muda gani?’

7 Je, wadai wako hawatainuka ghafula?

Je, hawataamka na kukufanya utetemeke?

Kisha utakuwa mhanga kwao.

8 Kwa kuwa umeteka nyara mataifa mengi,

watu waliobaki watakuteka nyara wewe.

Kwa kuwa umemwaga damu ya mtu;

umeharibu nchi na miji, na kila mmoja ndani yake.

9 “Ole wake yeye ajengaye milki yake kwa mapato ya udhalimu,

awekaye kiota chake juu,

ili kukimbia makucha ya uharibifu!

10 Umefanya shauri la maangamizi ya watu wengi,

ukiaibisha nyumba yako mwenyewe, na kupotewa na maisha yako.

11 Mawe ya kuta yatapiga kelele,

na mihimili ya kazi ya mbao itarudisha mwangwi wake.

12 “Ole wake yeye ajengaye mji kwa kumwaga

damu na kuusimamisha mji kwa uhalifu!

13 Je,BwanaMwenye Nguvu Zote hakuonyesha

kwamba kazi ya wanadamu ni mafuta tu kwa ajili ya moto,

na kwamba mataifa

yanajichosha bure?

14 Kwa kuwa dunia itajazwa na maarifa ya utukufu waBwana,

kama maji yaifunikavyo bahari.

15 “Ole wake yeye awapaye jirani zake kileo,

akiimimina kutoka kwenye kiriba

cha mvinyo mpaka wamelewa,

ili apate kutazama miili yao iliyo uchi.

16 Utajazwa na aibu badala ya utukufu.

Sasa ni zamu yako! Kunywa na ujifunue!

Kikombe kutoka kwenye mkono wa kuume waBwanakinakujia,

na aibu itafunika utukufu wako.

17 Ukatili ulioifanyia Lebanoni utakufunika,

na uharibifu uliowafanyia wanyama utakutisha.

Kwa sababu umemwaga damu ya mtu;

umeharibu nchi na miji na kila mmoja aliyeko ndani yake.

18 “Sanamu ina thamani gani,

kwani mwanadamu ndiye alichonga?

Ama kinyago kinachofundisha uongo?

Kwa kuwa yeye aliyekitengeneza

hutegemea kazi ya mikono yake mwenyewe;

hutengeneza sanamu zisizoweza kuzungumza.

19 Ole wake yeye auambiaye mti, ‘Uwe hai!’

Ama asemaye na jiwe lisilo na uhai, ‘Amka!’

Je, linaweza kuongoza?

Limefunikwa kwa dhahabu na fedha;

hakuna pumzi ndani yake.

20 LakiniBwanayuko katika Hekalu lake takatifu;

dunia yote na inyamaze mbele yake.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HAB/2-04979c73066568b41ab1d6b764839675.mp3?version_id=1627—