Categories
Hosea

Hosea 11

Upendo Wa Mungu Kwa Israeli

1 “Wakati Israeli alipokuwa mtoto, nilimpenda,

nilimwita mwanangu kutoka Misri.

2 Lakini kadiri nilivyomwita Israeli,

ndivyo walivyokwenda mbali nami.

Walitoa dhabihu kwa Mabaali

na kufukiza uvumba kwa vinyago.

3 Mimi ndiye niliyemfundisha Efraimu kutembea,

nikiwashika mikono;

lakini hawakutambua

kuwa ni mimi niliyewaponya.

4 Niliwaongoza kwa kamba za huruma ya kibinadamu,

kwa vifungo vya upendo;

niliondoa nira shingoni mwao

nami nikainama kuwalisha.

5 “Je, hawatarudi Misri,

nayo Ashuru haitawatawala

kwa sababu wamekataa kutubu?

6 Panga zitametameta katika miji yao,

zitaharibu makomeo ya malango yao

na kukomesha mipango yao.

7 Watu wangu wamedhamiria kuniacha.

Hata kama wakimwita Yeye Aliye Juu Sana,

kwa vyovyote hatawainua.

8 “Efraimu, ninawezaje kukuacha?

Ee Israeli, ninawezaje kukutoa?

Nitawezaje kukutendea kama Adma?

Nitawezaje kukufanya kama Seboimu?

Moyo wangu umegeuka ndani yangu,

huruma zangu zote zimeamshwa.

9 Sitatimiza hasira yangu kali,

wala sitageuka na kumharibu Efraimu.

Kwa kuwa mimi ndimi Mungu,

wala si mwanadamu,

Aliye Mtakatifu miongoni mwenu.

Sitakuja kwa ghadhabu.

10 WatamfuataBwana;

atanguruma kama simba.

Wakati angurumapo,

watoto wake watakuja wakitetemeka

kutoka magharibi.

11 Watakuja wakitetemeka

kama ndege wakitoka Misri,

kama hua wakitoka Ashuru.

Nitawakalisha katika nyumba zao,”

asemaBwana.

Dhambi Ya Israeli

12 Efraimu amenizunguka kwa uongo,

nyumba ya Israeli kwa udanganyifu.

Naye Yuda ni mkaidi dhidi ya Mungu,

hata kinyume cha yule mwaminifu Aliye Mtakatifu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/11-000f60637bc045ab5428ac4196071c11.mp3?version_id=1627—

Categories
Hosea

Hosea 12

1 Efraimu anajilisha upepo;

hufukuzia upepo wa mashariki kutwa nzima

na kuzidisha uongo na jeuri.

Anafanya mkataba na Ashuru

na kutuma mafuta ya zeituni Misri.

2 Bwanaanalo shtaka dhidi ya Yuda,

atamwadhibu Yakobo kwa kadiri ya njia zake

na kumlipa kwa kadiri ya matendo yake.

3 Yakobo akiwa tumboni alishika kisigino cha kaka yake;

kama mwanadamu, alishindana na Mungu.

4 Alishindana na malaika na kumshinda;

alilia na kuomba upendeleo wake.

Alimkuta huko Betheli

na kuzungumza naye huko:

5 BwanaMungu Mwenye Nguvu Zote,

Bwanandilo jina lake!

6 Lakini ni lazima urudi kwa Mungu wako;

dumisha upendo na haki,

nawe umngojee Mungu wako siku zote.

7 Mfanyabiashara hutumia vipimo vya udanganyifu;

hupenda kupunja.

8 Efraimu hujisifu akisema,

“Mimi ni tajiri sana; nimetajirika.

Pamoja na utajiri wangu wote hawatakuta ndani yangu

uovu wowote au dhambi.”

9 “Mimi ndimiBwanaMungu wenu

niliyewaleta kutoka Misri;

nitawafanya mkae tena kwenye mahema,

kama vile katika siku

za sikukuu zenu zilizoamriwa.

10 Niliongea na manabii, nikawapa maono mengi

na kusema mifano kupitia wao.”

11 Je, Gileadi si mwovu?

Watu wake hawafai kitu!

Je, hawatoi dhabihu za mafahali huko Gilgali?

Madhabahu zao zitakuwa

kama malundo ya mawe

katika shamba lililolimwa.

12 Yakobo alikimbilia katika nchi ya Aramu;

Israeli alitumika ili apate mke,

ili aweze kulipa kwa ajili yake alichunga kondoo.

13 Bwanaalimtumia nabii

kumpandisha Israeli kutoka Misri,

kwa njia ya nabii alimtunza.

14 Lakini Efraimu amemchochea sana hasira;

Bwana wake ataleta juu yake

hatia yake ya kumwaga damu naye atamlipiza

kwa ajili ya dharau yake.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/12-78dc8f9269267ff93ed97af1852f50f0.mp3?version_id=1627—

Categories
Hosea

Hosea 13

Hasira Ya Bwana Dhidi Ya Israeli

1 Wakati Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka,

alikuwa ametukuzwa katika Israeli.

Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali

naye akafa.

2 Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi;

wanajitengenezea sanamu

kutokana na fedha yao,

vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari,

vyote kazi ya fundi stadi.

Inasemekana kuhusu hawa watu,

“Hutoa dhabihu za binadamu

na kubusu sanamu za ndama.”

3 Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi,

kama umande wa alfajiri utowekao,

kama makapi yapeperushwayo

kutoka sakafu ya kupuria nafaka,

kama moshi utorokao kupitia dirishani.

4 “Bali mimi ndimiBwanaMungu wenu,

niliyewaleta ninyi toka Misri.

Msimkubali Mungu mwingine ila mimi,

hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.

5 Niliwatunza huko jangwani,

katika nchi yenye joto liunguzalo.

6 Nilipowalisha, walishiba,

waliposhiba, wakajivuna,

kisha wakanisahau mimi.

7 Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba,

kama chui nitawavizia kando ya njia.

8 Kama dubu aliyenyangʼanywa watoto wake,

nitawashambulia na kurarua vifua vyenu.

Kama simba nitawala;

mnyama pori atawararua vipande vipande.

9 “Ee Israeli, umeangamizwa,

kwa sababu wewe u kinyume nami,

kinyume na msaidizi wako.

10 Yuko wapi mfalme wako,

ili apate kukuokoa?

Wako wapi watawala wako katika miji yako yote

ambao ulisema kuwahusu,

‘Nipe mfalme na wakuu’?

11 Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme

na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.

12 Kosa la Efraimu limehifadhiwa,

dhambi zake zimewekwa katika kumbukumbu.

13 Utungu kama wa mwanamke anayejifungua mtoto humjia,

lakini yeye ni mtoto asiyekuwa na hekima;

wakati utakapowadia hatatoka

katika tumbo la mama yake.

14 “Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi,

nitawakomboa kutoka mautini.

Yako wapi, ee mauti, mateso yako?

Uko wapi, ee kuzimu, uharibifu wako?

“Sitakuwa na huruma,

15 hata ingawa Efraimu atastawi

miongoni mwa ndugu zake.

Upepo wa mashariki kutoka kwaBwanautakuja,

ukivuma kutoka jangwani,

chemchemi yake haitatoa maji

na kisima chake kitakauka.

Ghala lake litatekwa

hazina zake zote.

16 Watu wa Samaria ni lazima wabebe hatia yao,

kwa sababu wameasi dhidi ya Mungu wao.

Wataanguka kwa upanga;

watoto wao wadogo watatupwa kwa nguvu ardhini,

wanawake wao walio na mimba watatumbuliwa.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/13-4d260f4230ffca6f074e731e55a03566.mp3?version_id=1627—

Categories
Hosea

Hosea 14

Toba Iletayo Baraka

1 Rudi, ee Israeli, kwaBwanaMungu wako.

Dhambi zako zimekuwa

ndilo anguko lako!

2 Chukueni maneno pamoja nanyi,

mkamrudieBwana.

Mwambieni:

“Samehe dhambi zetu zote

na utupokee kwa neema,

ili tuweze kutoa matunda yetu

kama sadaka za mafahali.

3 Ashuru hawezi kutuokoa,

hatutapanda farasi wa vita.

Kamwe hatutasema tena ‘Miungu yetu’

kwa kile ambacho mikono yetu wenyewe imetengeneza,

kwa kuwa kwako wewe yatima hupata huruma.”

4 “Nitaponya ukaidi wao

na kuwapenda kwa hiari yangu,

kwa kuwa hasira yangu imeondoka kwao.

5 Nitakuwa kama umande kwa Israeli;

atachanua kama yungiyungi.

Kama mwerezi wa Lebanoni

atashusha mizizi yake chini;

6 matawi yake yatatanda.

Fahari yake itakuwa kama mti wa mzeituni,

harufu yake nzuri kama mwerezi wa Lebanoni.

7 Watu wataishi tena kwenye kivuli chake.

Atastawi kama nafaka.

Atachanua kama mzabibu,

nao umaarufu wake utakuwa

kama divai itokayo Lebanoni.

8 Ee Efraimu, nina shughuli gani tena na sanamu?

Nitamjibu na kumtunza.

Mimi ni kama msunobari wenye majani mabichi;

kuzaa kwako matunda kunatoka kwangu.”

9 Ni nani mwenye hekima? Atayatambua mambo haya.

Ni nani mwenye ufahamu? Huyu atayaelewa.

Njia zaBwanani adili;

wenye haki huenda katika njia hizo,

lakini waasi watajikwaa ndani yake.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/14-521fc4943468d9e6135356aa63b8d720.mp3?version_id=1627—

Categories
Yoeli

Yoeli Utangulizi

Utangulizi

Yoeli mwana wa Pethueli maana ya jina lake ni “Bwana ni Mungu.” Nyingi ya kumbukumbu zake katika hiki kitabu na huduma yake hekaluni zinaonyesha kwamba alikuwa nabii aliyetumwa kwa Yuda na Yerusalemu. Kutokana na huduma yake, wengi wamemdhania kuwa nabii wa “kikuhani” (linganisha

Yer 28:1

5

) aliyenena neno la kweli la Bwana.

Tukio la unabii wa Yoeli lilikuwa pigo kubwa la nzige waliokula kila jani bichi na hata magome ya miti na mizizi. Akiwaonya watu wamgeukie

Bwana

kwa njia ya toba, Yoeli anatangaza kwamba “siku ya

Bwana

” inakuja na italeta hukumu kubwa. Kabla hiyo hukumu haijakuja, Mungu atatuma Roho wake ili kuleta baraka. Yoeli anaelezea kwa undani kuhusu kundi la nzige walioshambulia Palestina. Katika tukio hili aliona ishara ya hukumu ya mwisho na akawaonya watu watubu na kumrudia Mungu.

Mwandishi

Yoeli mwana wa Pethueli.

Kusudi

Kuionya Yuda juu ya hukumu ya Mungu iliyokuwa karibu kwa sababu ya dhambi zake, na kuwahimiza watu wamrudie Mungu.

Mahali

Yerusalemu.

Tarehe

Miaka 835–796 K.K.

Wahusika Wakuu

Yoeli na watu wa Yuda.

Wazo Kuu

Toba husababisha Mungu kughairi mabaya aliyoyakusudia, na badala yake kuleta baraka.

Mambo Muhimu

Pigo la nzige, kuwaonya watu watubu, na tumaini kwa watu wa Mungu.

Mgawanyo

Kuvamiwa na nzige (

1:1-12

)

Wito wa kutubu (

1:12-20

)

Maonyo na baraka za Mungu (

2:1-32

)

Hukumu ya Mungu ya mwisho, na sheria (

3:1-12

).

Categories
Yoeli

Yoeli 1

1 Neno laBwanaambalo lilimjia Yoeli mwana wa Pethueli.

Uvamizi Wa Nzige

2 Sikilizeni hili, enyi wazee;

sikilizeni, ninyi nyote mnaoishi katika nchi.

Je, jambo kama hili lilishawahi kutokea

katika siku zenu au katika siku za babu zenu?

3 Waelezeni watoto wenu,

na watoto wenu wawaambie watoto wao,

na watoto wao kwa kizazi kitakachofuata.

4 Kilichosazwa na kundi la tunutu

nzige wakubwa wamekula,

kilichosazwa na nzige wakubwa

parare wamekula,

kilichosazwa na parare

madumadu wamekula.

5 Amkeni, enyi walevi, mlie!

Pigeni yowe enyi wanywaji wote wa mvinyo,

pigeni yowe kwa sababu ya mvinyo mpya,

kwa kuwa mmenyangʼanywa

kutoka midomoni mwenu.

6 Taifa limevamia nchi yangu,

lenye nguvu tena lisilo na idadi;

lina meno ya simba,

magego ya simba jike.

7 Limeharibu mizabibu yangu

na kuangamiza mitini yangu.

Limebambua magome yake

na kuyatupilia mbali,

likayaacha matawi yake yakiwa meupe.

8 Omboleza kama bikira aliyevaa nguo ya gunia

anayehuzunika kwa ajili ya mume wa ujana wake.

9 Sadaka za nafaka na sadaka za kinywaji

zimekatiliwa mbali kutoka nyumba yaBwana.

Makuhani wanaomboleza,

wale wanaohudumu mbele zaBwana.

10 Mashamba yameharibiwa,

ardhi imekauka;

nafaka imeharibiwa,

mvinyo mpya umekauka,

mafuta yamekoma.

11 Kateni tamaa, enyi wakulima,

lieni, enyi mlimao mizabibu;

huzunikeni kwa ajili ya ngano na shayiri,

kwa sababu mavuno ya shambani yameharibiwa.

12 Mzabibu umekauka

na mtini umenyauka;

mkomamanga, mtende na mtofaa,

miti yote shambani, imekauka.

Hakika furaha yote ya mwanadamu

imeondoka.

Wito Wa Toba

13 Vaeni nguo ya gunia, enyi makuhani, muomboleze;

pigeni yowe, enyi mnaohudumu madhabahuni.

Njooni, vaeni nguo ya gunia usiku kucha,

enyi mnaohudumu mbele za Mungu wangu;

kwa kuwa sadaka za nafaka na sadaka za kinywaji

zimezuiliwa kufika katika nyumba ya Mungu wenu.

14 Tangazeni saumu takatifu;

liiteni kusanyiko takatifu.

Iteni wazee

na wote waishio katika nchi

waende katika nyumba yaBwanaMungu wenu,

wakamlilieBwana.

15 Ole kwa siku hiyo!

Kwa kuwa siku yaBwanaiko karibu;

itakuja kama uharibifu

kutoka kwa Mwenyezi.

16 Je, chakula hakikukatiliwa mbali

mbele ya macho yetu:

furaha na shangwe

kutoka nyumba ya Mungu wetu?

17 Mbegu zinakauka

chini ya mabonge ya udongo.

Ghala zimeachwa katika uharibifu,

ghala za nafaka zimebomolewa,

kwa maana hakuna nafaka.

18 Jinsi gani ngʼombe wanavyolia!

Makundi ya mifugo yanahangaika

kwa sababu hawana malisho;

hata makundi ya kondoo yanateseka.

19 Kwako, EeBwana, naita,

kwa kuwa moto umeteketeza

malisho ya mbugani

na miali ya moto imeunguza

miti yote shambani.

20 Hata wanyama wa porini wanakuonea shauku;

vijito vya maji vimekauka,

na moto umeteketeza

malisho yote ya mbugani.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOL/1-c143eaab6d0d73e6f8727b9d2499d297.mp3?version_id=1627—

Categories
Yoeli

Yoeli 2

Jeshi La Nzige

1 Pigeni tarumbeta katika Sayuni;

pigeni mbiu katika mlima wangu mtakatifu.

Wote waishio katika nchi na watetemeke,

kwa kuwa siku yaBwanainakuja. Iko karibu,

2 siku ya giza na huzuni,

siku ya mawingu na utusitusi.

Kama mapambazuko yasambaavyo

toka upande huu wa milima

hata upande mwingine

jeshi kubwa na lenye nguvu linakuja.

Jambo kama hili halijakuwepo tangu zamani

wala halitakuwepo tena kamwe

kwa vizazi vijavyo.

3 Mbele yao moto unateketeza,

nyuma yao miali ya moto

inawaka kwa nguvu.

Mbele yao nchi iko kama bustani ya Edeni,

nyuma yao ni jangwa lisilofaa:

hakuna kitu kinachowaepuka.

4 Wanaonekana kama farasi;

wanakwenda mbio

kama askari wapanda farasi.

5 Wanatoa sauti kama magari ya vita,

wanaporukaruka juu ya vilele vya milima,

kama mlio wa miali ya moto ilayo mabua,

kama jeshi kubwa lililojipanga kwa ajili ya vita.

6 Wanapoonekana, mataifa yanakuwa katika maumivu makuu;

kila uso unabadilika rangi.

7 Wanashambulia kama wapiganaji wa vita;

wanapanda kuta kama askari.

Wote wanatembea katika safu,

hawapotoshi safu zao.

8 Hakuna anayemsukuma mwenzake;

kila mmoja anakwenda mbele moja kwa moja.

Wanapita katika vizuizi

bila kuharibu safu zao.

9 Wanaenda kasi kuingia mjini;

wanakimbia ukutani.

Wanaingia ndani ya nyumba;

kwa kuingilia madirishani kama wevi.

10 Mbele yao dunia inatikisika,

anga linatetemeka,

jua na mwezi vinatiwa giza,

na nyota hazitoi mwanga wake tena.

11 Bwanaanatoa mshindo wa ngurumo

mbele ya jeshi lake;

majeshi yake hayana idadi,

ni wenye nguvu nyingi

wale ambao hutii agizo lake.

Siku yaBwanani kuu,

ni ya kutisha.

Ni nani anayeweza kuistahimili?

Rarueni Mioyo Yenu

12 “Hata sasa,” asemaBwana,

“nirudieni kwa mioyo yenu yote,

kwa kufunga, kwa kulia na kuomboleza.”

13 Rarueni mioyo yenu

na siyo mavazi yenu.

MrudieniBwana, Mungu wenu,

kwa maana yeye ndiye mwenye neema

na mwingi wa huruma,

si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo,

huona huruma, hujizuia kuleta maafa.

14 Ni nani ajuaye? Yeye aweza kugeuka na kuwa na huruma

na kuacha baraka nyuma yake:

sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji

kwa ajili yaBwanaMungu wenu.

15 Pigeni tarumbeta katika Sayuni,

tangazeni saumu takatifu,

liiteni kusanyiko takatifu.

16 Wakusanyeni watu,

wekeni wakfu kusanyiko;

waleteni pamoja wazee,

wakusanyeni watoto,

wale wanyonyao maziwa.

Bwana arusi na atoke chumbani mwake

na bibi arusi naye atoke katika chumba chake.

17 Makuhani, ambao wanahudumu mbele zaBwana,

na walie katikati ya ukumbi

wa Hekalu na madhabahu.

Waseme, “Wahurumie watu wako, EeBwana.

Usifanye urithi wako kitu cha kudharauliwa,

neno la dhihaka kati ya mataifa.

Kwa nini wasemezane miongoni mwao,

‘Yuko wapi Mungu wao?’ ”

Jibu La Bwana

18 KishaBwanaatakuwa na wivu kwa ajili ya nchi yake

na kuwa na huruma juu ya watu wake.

19 Bwanaatawajibu:

“Ninawapelekea nafaka,

mvinyo mpya na mafuta,

vya kuwatosha ninyi

hadi mridhike kabisa;

kamwe sitawafanya tena

kitu cha kudharauliwa na mataifa.

20 “Nitafukuza jeshi la kaskazini likae mbali nanyi,

nikilisukuma ndani ya jangwa,

askari wa safu za mbele wakienda

ndani ya bahari ya mashariki

na wale wa safu za nyuma

katika bahari ya magharibi.

Uvundo wake utapaa juu;

harufu yake itapanda juu.”

Hakika ametenda mambo makubwa.

21 Usiogope, ee nchi;

furahi na kushangilia.

HakikaBwanaametenda mambo makubwa.

22 Msiogope, enyi wanyama pori,

kwa kuwa mbuga za malisho yenu

zinarudia ubichi.

Miti nayo inazaa matunda,

mtini na mzabibu inatoa utajiri wake.

23 Furahini, enyi watu wa Sayuni,

shangilieni katikaBwanaMungu wenu,

kwa kuwa amewapa mvua za vuli

kwa kipimo cha haki.

Anawapelekea mvua nyingi,

mvua ya vuli na ya masika, kama mwanzoni.

24 Sakafu za kupuria zitajaa nafaka,

mapipa yatafurika mvinyo mpya na mafuta.

25 “Nitawalipa kwa ajili ya miaka ile iliyoliwa na nzige:

parare, madumadu na tunutu,

jeshi langu kubwa ambalo

nililituma katikati yenu.

26 Mtakuwa na wingi wa vyakula mpaka mshibe,

na mtalisifu jina laBwanaMungu wenu,

ambaye amefanya maajabu kwa ajili yenu;

kamwe watu wangu hawataaibishwa tena.

27 Ndipo mtakapojua kwamba mimi niko katika Israeli

kwamba mimi ndimiBwanaMungu wenu,

na kwamba hakuna mwingine;

kamwe watu wangu hawataaibika tena.

Siku Ya Bwana

28 “Hata itakuwa, baada ya hayo,

nitamimina Roho wangu juu ya wote wenye mwili.

Wana wenu na binti zenu watatabiri,

wazee wenu wataota ndoto,

na vijana wenu wataona maono.

29 Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake,

katika siku zile nitamimina Roho wangu.

30 Nami nitaonyesha maajabu katika mbingu

na duniani:

damu, moto na mawimbi ya moshi.

31 Jua litageuzwa kuwa giza

na mwezi kuwa mwekundu kama damu,

kabla ya kuja siku yaBwana

ile kuu na ya kutisha.

32 Na kila mtu atakayeliitia

jina laBwanaataokolewa.

Kwa maana juu ya Mlima Sayuni na katika Yerusalemu

kutakuwepo wokovu,

kamaBwanaalivyosema,

miongoni mwa walionusurika

ambaoBwanaawaita.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOL/2-834e1ac8d2542f5b1a07a9f9571d5538.mp3?version_id=1627—

Categories
Yoeli

Yoeli 3

Mataifa Yahukumiwa

1 “Katika siku hizo na wakati huo,

nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,

2 nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta

katika Bonde la Yehoshafati

Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao

kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli,

kwa kuwa waliwatawanya watu wangu

miongoni mwa mataifa

na kuigawa nchi yangu.

3 Wanawapigia kura watu wangu

na kuwauza wavulana ili kupata makahaba;

waliwauza wasichana

ili wapate kunywa mvinyo.

4 “Sasa una nini dhidi yangu, ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda.

5 Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu.

6 Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.

7 “Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya.

8 Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Waseba, taifa lililo mbali.”Bwanaamesema.

9 Tangazeni hili miongoni mwa mataifa:

Jiandaeni kwa vita!

Amsha askari!

Wanaume wote wapiganaji

wasogee karibu na kushambulia.

10 Majembe yenu yafueni yawe panga

na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki.

Aliye dhaifu na aseme,

“Mimi nina nguvu!”

11 Njooni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote,

kusanyikeni huko.

Shusha wapiganaji wako, EeBwana!

12 “Mataifa na yaamshwe;

na yasonge mbele kuelekea Bonde la Yehoshafati,

kwa kuwa nitaketi mahali pale

kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.

13 Tia mundu,

kwa kuwa mavuno yamekomaa.

Njooni, mkanyage zabibu,

kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa

na mapipa yanafurika:

kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”

14 Umati mkubwa, umati mkubwa

katika bonde la uamuzi!

Kwa kuwa siku yaBwanani karibu

katika bonde la uamuzi.

15 Jua na mwezi vitatiwa giza,

na nyota hazitatoa mwanga wake tena.

16 Bwanaatanguruma kutoka Sayuni

na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu;

dunia na mbingu vitatikisika.

LakiniBwanaatakuwa kimbilio la watu wake,

ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.

Baraka Kwa Watu Wa Mungu

17 “Ndipo mtakapojua kwamba Mimi,BwanaMungu wenu,

nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.

Yerusalemu utakuwa mtakatifu;

kamwe wageni hawatavamia tena.

18 “Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya,

na vilima vitatiririka maziwa;

mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji.

Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba yaBwana

na kunywesha Bonde la Shitimu.

19 Lakini Misri itakuwa ukiwa,

Edomu itakuwa jangwa tupu,

kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda,

ambao katika nchi yao

walimwaga damu isiyo na hatia.

20 Yuda itakaliwa na watu milele

na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.

21 Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe,

nitasamehe.”

Bwanaanakaa Sayuni!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOL/3-8663e10b8d72a40fd5193aeae4bf422a.mp3?version_id=1627—

Categories
Amosi

Amosi Utangulizi

Utangulizi

Amosi maana yake ni “Mchukua mzigo.” Yeye alikuwa mchunga wanyama na pia mtunza mikuyu kutoka Tekoa, kijiji kilicho karibu na Bethlehemu na kilomita 16 kutoka Yerusalemu. Mungu alimwita kuwa nabii katika Ufalme wa Kaskazini (Israeli). Wakati huo ufalme ulikuwa na utajiri mwingi. Ujumbe wa Amosi unaonyesha kwamba wakati huo ulikuwa wa mafanikio mengi kiuchumi na kisiasa katika Israeli kuliko nyakati zingine zote, isipokuwa zile za enzi ya Solomoni.

Amosi aliwalaumu watu vikali kwa kuliacha neno la Mungu, kukosa haki katika jamii na kwa maskini, kuwa wakatili, kutawaliwa na ubinafsi, na kufuata anasa na kuabudu sanamu. Uwajibikaji wa Israeli ulikuwa mkubwa kuliko wa mataifa mengine yaliyowazunguka kwa sababu walikuwa wamepewa upendeleo mkubwa zaidi. Katika maono matano mfululizo, Amosi aliona kuwa siku ya maangamizi ilikuwa karibu. Aliwaonya watu kwamba iliwapasa kujiandaa kukutana na Mungu. Kwa wale waliokuwa wanampenda Mungu, Amosi alikuwa na neno la kuwapa matumaini. Siku ilikuwa inakuja ambapo ufalme wa Daudi ungekomeshwa ghafula lakini wacha Mungu wangeishi salama.

Mwandishi

Amosi.

Kusudi

Kutangaza hukumu ya Mungu dhidi ya Israeli kwa kuishi katika hali ya kutosheka na kuridhika, kuabudu sanamu na kuwadhulumu maskini.

Mahali

Samaria, Betheli, Gilgali.

Tarehe

760–750 K.K.

Wahusika Wakuu

Amosi, Amazia, na Yeroboamu wa Pili.

Wazo Kuu

Amosi aliwashutumu watu vikali kwa kuwagandamiza maskini. Kutokana na haya, alitangaza hukumu ya Mungu dhidi yao kwa sababu walikuwa wamemwacha Mungu.

Mambo Muhimu

Amosi ametumia mifano ya maneno ya kusisimua kutokana na uzoefu wake wa ukulima na uchungaji wa wanyama: Simba angurumaye, kipande cha kondoo kilichopokonywa kinywani mwa simba, ngʼombe walioshiba, kapu la matunda, n.k.

Mgawanyo

Hukumu kwa majirani wa Israeli (

1:1–2:5

)

Hukumu kwa Israeli (

2:6-16

)

Uovu wa Israeli (

3:1–6:14

)

Maono matano (

7:1–9:10

)

Matengenezo ya Israeli (

9:11-15

).

Categories
Amosi

Amosi 1

1 Maneno ya Amosi, mmoja wa wachunga wanyama wa Tekoa: yale aliyoyaona kuhusu Israeli miaka miwili kabla ya tetemeko la ardhi, wakati Uzia alikuwa mfalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yehoashi alikuwa mfalme wa Israeli.

2 Alisema:

“Bwanaananguruma toka Sayuni,

pia ananguruma kutoka Yerusalemu;

malisho ya wachunga wanyama yanakauka,

kilele cha Karmeli kinanyauka.”

Hukumu Juu Ya Majirani Wa Israeli

3 Hili ndilo asemaloBwana:

“Kwa dhambi tatu za Dameski,

hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu.

Kwa sababu aliipura Gileadi

kwa vyombo vya chuma vyenye meno.

4 Nitatuma moto juu ya nyumba ya Hazaeli

ambao utateketeza ngome za Ben-Hadadi.

5 Nitalivunja lango la Dameski;

nitamwangamiza mfalme aliyeko katika Bonde la Aveni,

na yeye ambaye anaishika fimbo ya utawala katika Beth-Edeni.

Watu wote wa Aramu watakwenda uhamishoni huko Kiri,”

asemaBwana.

6 Hili ndilo asemaloBwana:

“Kwa dhambi tatu za Gaza,

hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu.

Kwa sababu walichukua mateka jumuiya nzima

na kuwauza kwa Edomu,

7 nitatuma moto juu ya kuta za Gaza

ambao utateketeza ngome zake.

8 Nitamwangamiza mfalme wa Ashdodi

na yeye aishikaye fimbo ya utawala katika Ashkeloni.

Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni,

hadi Mfilisti wa mwisho atakapokufa,”

asemaBwanaMwenyezi.

9 Hili ndilo asemaloBwana:

“Kwa dhambi tatu za Tiro,

hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu.

Kwa sababu ameuza jumuiya nzima ya mateka kwa Edomu,

na kutokujali mapatano ya undugu,

10 Nitatuma moto kwenye kuta za Tiro

ambao utateketeza ngome zake.”

11 Hili ndiloBwanaasemalo:

“Kwa dhambi tatu za Edomu,

hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu.

Kwa sababu alimfuatia ndugu yake kwa upanga,

alikataa kuonyesha huruma yoyote,

kwa sababu hasira yake kali iliendelea kupanda wakati wote

na ghadhabu iliwaka bila kuzuiliwa.

12 Nitatuma moto juu ya Temani

ambao utateketeza ngome za Bosra.”

13 Hili ndilo asemaloBwana:

“Kwa dhambi tatu za Amoni,

hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu.

Kwa sababu aliwatumbua wanawake wajawazito wa Gileadi

ili kuongeza mipaka yake.

14 Nitatuma moto kwenye kuta za Raba

ambao utateketeza ngome zake

katikati ya vilio vya vita katika siku ya mapigano,

katikati ya upepo mkali katika siku ya dhoruba.

15 Mfalme wake atakwenda uhamishoni,

yeye pamoja na maafisa wake,”

asemaBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/AMO/1-bd20a9f8d7c7ee7f62bebeb1022c5061.mp3?version_id=1627—