Categories
Yeremia

Yeremia 52

Anguko La Yerusalemu

1 Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.

2 Alifanya maovu machoni paBwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.

3 Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira yaBwanahaya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake.

Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.

4 Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Wakapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote.

5 Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.

6 Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu.

7 Kisha ukuta wa mji ukavunjwa na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba.

8 Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia Mfalme Sedekia na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika,

9 naye akakamatwa.

Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.

10 Huko Ribla mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Pia akawaua maafisa wote wa Yuda.

11 Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia, akamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli, alipomweka gerezani mpaka siku ya kifo chake.

12 Mnamo siku ya kumi ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, aliyemtumikia mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu.

13 Alichoma moto Hekalu laBwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu.

14 Jeshi lote la Wakaldayo chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme walivunja kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu.

15 Nebuzaradani, jemadari wa askari walinzi, akawapeleka uhamishoni baadhi ya watu maskini sana na wale waliobaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli.

16 Lakini Nebuzaradani akawaacha mabaki ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.

17 Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu laBwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba yote na kuipeleka Babeli.

18 Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu.

19 Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua yale masinia, vile vyetezo, yale mabakuli ya kunyunyizia, zile sufuria, vile vinara vya taa, zile sahani na yale mabakuli yaliyotumika kwa sadaka za vinywaji, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.

20 Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na wale mafahali kumi na mawili wa shaba waliokuwa chini yake, pamoja na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Mfalme Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu laBwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika.

21 Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane, kimo chake na mzunguko dhiraa kumi na mbili, na unene wa nyanda nne, na zote zilikuwa wazi ndani.

22 Sehemu ya shaba juu ya ile nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tano, na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na makomamanga yake ilifanana na hiyo ya kwanza.

23 Kulikuwa na makomamanga tisini na sita pembeni; jumla ya makomamanga juu ya wavu uliokuwa umezunguka yalikuwa mia moja.

24 Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu.

25 Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri saba wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji.

26 Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.

27 Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe.

Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao.

28 Hii ndiyo hesabu ya watu ambao Nebukadneza aliwachukua kwenda uhamishoni:

katika mwaka wa saba,

Wayahudi 3,023;

29 katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Nebukadneza,

watu 832 kutoka Yerusalemu;

30 katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake,

Wayahudi 745 walichukuliwa kwenda uhamishoni na Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme.

Jumla ya watu wote walikuwa 4,600.

Yehoyakini Anaachiwa Huru

31 Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodakialifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini mfalme wa Yuda, na kumfungua kutoka gerezani siku ya ishirini na tano ya mwezi wa kumi na mbili.

32 Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli.

33 Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme.

34 Siku kwa siku mfalme wa Babeli alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake, hadi siku ya kifo chake.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JER/52-c2b86b923a92dc454bdb791d63c04e8c.mp3?version_id=1627—

Categories
Maombolezo

Maombolezo Utangulizi

Utangulizi

Jina la kitabu hiki ni “Ekah” kwa Kiebrania, maana yake “Jinsi gani.” Maombolezo ni wimbo wa maziko wa kuomboleza Yerusalemu na kuharibiwa kwa Hekalu. Nchi iliachwa bila mfalme, na watu walikuwa wamepelekwa utumwani. Mungu alikuwa amewaonya kuwa wangeenda utumwani wakimwacha.

Yeremia aliandika maombolezo haya kuonyesha huzuni yake kubwa na kuchomwa moyo kwa sababu ya uharibifu wa kutisha wa Yerusalemu. Maafa haya yalihusisha anguko la kuaibisha la utawala wa ukoo wa Daudi, kuangamizwa kabisa kwa kuta za mji na Hekalu, jumba la mfalme na mji kwa ujumla, na mwishowe kupelekwa mbali sana kwa mateka wengi huko Babeli.

Mwandishi

Mapokeo na maandishi ya Kiyahudi na ya Kikristo husema ni Yeremia.

Kusudi

Kuwafundisha watu kwamba kutomtii Mungu huleta maangamizi.

Mahali

Yerusalemu.

Tarehe

586–585 K.K.

Wahusika Wakuu

Yeremia, na watu wa Yerusalemu.

Wazo Kuu

Kutafakari mateso na matumaini kwa Mungu.

Mambo Muhimu

Yeremia auomboleza mji wa Yerusalemu, Mungu kugadhibishwa na dhambi, na hali ya kuwa na tumaini katika mateso.

Mgawanyo

Kuangamizwa kabisa kwa Yerusalemu (

1:1-22

)

Hasira ya Mungu, na kutafuta faraja (

2:1-22

)

Kutafakari mateso, na kuweka matumaini kwa Mungu (

3:1-66

)

Utukufu wa awali wa Yerusalemu, na hali ya sasa ya ukiwa (

4:1-22

)

Kumwomba Mungu aonyeshe huruma (

5:1-22

).

Categories
Maombolezo

Maombolezo 1

1 Tazama jinsi mji ulivyoachwa ukiwa,

mji ambao zamani ulikuwa umejaa watu!

Jinsi ambavyo umekuwa kama mama mjane,

ambaye wakati fulani alikuwa maarufu miongoni mwa mataifa!

Yule ambaye alikuwa malkia miongoni mwa majimbo

sasa amekuwa mtumwa.

2 Kwa uchungu, hulia sana usiku,

machozi yapo kwenye mashavu yake.

Miongoni mwa wapenzi wake wote

hakuna yeyote wa kumfariji.

Rafiki zake wote wamemsaliti,

wamekuwa adui zake.

3 Baada ya mateso na kufanyishwa kazi kikatili,

Yuda amekwenda uhamishoni.

Anakaa miongoni mwa mataifa,

hapati mahali pa kupumzika.

Wote ambao wanamsaka wamemkamata

katikati ya dhiki yake.

4 Barabara zielekeazo Sayuni zaomboleza,

kwa kuwa hakuna yeyote anayekuja

kwenye sikukuu zake zilizoamriwa.

Malango yake yote yamekuwa ukiwa,

makuhani wake wanalia kwa uchungu,

wanawali wake wanahuzunika,

naye yuko katika uchungu wa maumivu makuu.

5 Adui zake wamekuwa mabwana zake,

watesi wake wana raha.

Bwanaamemletea huzuni

kwa sababu ya dhambi zake nyingi.

Watoto wake wamekwenda uhamishoni,

mateka mbele ya adui.

6 Fahari yote imeondoka

kutoka kwa Binti Sayuni.

Wakuu wake wako kama ayala

ambaye hapati malisho,

katika udhaifu wamekimbia

mbele ya anayewasaka.

7 Katika siku za mateso yake na kutangatanga,

Yerusalemu hukumbuka hazina zote

ambazo zilikuwa zake siku za kale.

Wakati watu wake walipoanguka katika mikono ya adui,

hapakuwepo na yeyote wa kumsaidia.

Watesi wake walimtazama

na kumcheka katika maangamizi yake.

8 Yerusalemu ametenda dhambi sana

kwa hiyo amekuwa najisi.

Wote waliomheshimu wanamdharau,

kwa maana wameuona uchi wake.

Yeye mwenyewe anapiga kite

na kugeukia mbali.

9 Uchafu wake umegandamana na nguo zake;

hakuwaza juu ya maisha yake ya baadaye.

Anguko lake lilikuwa la kushangaza,

hapakuwepo na yeyote wa kumfariji.

“Tazama, EeBwana, teso langu,

kwa maana adui ameshinda.”

10 Adui ametia mikono

juu ya hazina zake zote,

aliona mataifa ya kipagani

wakiingia mahali patakatifu pake,

wale uliowakataza kuingia

kwenye kusanyiko lako.

11 Watu wake wote wanalia kwa uchungu

watafutapo chakula;

wanabadilisha hazina zao kwa chakula

ili waweze kuendelea kuishi.

“Tazama, EeBwana, ufikiri,

kwa maana nimedharauliwa.”

12 “Je, si kitu kwenu, ninyi nyote mpitao kando?

Angalieni kote mwone.

Je, kuna maumivu kama maumivu yangu

yale yaliyotiwa juu yangu,

yaleBwanaaliyoyaleta juu yangu

katika siku ya hasira yake kali?

13 “Kutoka juu alipeleka moto,

akaushusha katika mifupa yangu.

Aliitandia wavu miguu yangu

na akanirudisha nyuma.

Akanifanya mkiwa,

na mdhaifu mchana kutwa.

14 “Dhambi zangu zimefungwa kwenye nira,

kwa mikono yake zilifumwa pamoja.

Zimefika shingoni mwangu

na Bwana ameziondoa nguvu zangu.

Amenitia mikononi mwa wale

ambao siwezi kushindana nao.

15 “Bwana amewakataa wapiganaji wa vita

wote walio kati yangu,

ameagiza jeshi dhidi yangu

kuwaponda vijana wangu wa kiume.

Katika shinikizo lake la divai Bwana amemkanyaga

Bikira Binti Yuda.

16 “Hii ndiyo sababu ninalia

na macho yangu yanafurika machozi.

Hakuna yeyote aliye karibu kunifariji,

hakuna yeyote wa kuhuisha roho yangu.

Watoto wangu ni wakiwa

kwa sababu adui ameshinda.”

17 Sayuni ananyoosha mikono yake,

lakini hakuna yeyote wa kumfariji.

Bwanaametoa amri kwa ajili ya Yakobo

kwamba majirani zake wawe adui zake;

Yerusalemu umekuwa

kitu najisi miongoni mwao.

18 “Bwanani mwenye haki,

hata hivyo niliasi dhidi ya amri yake.

Sikilizeni, enyi mataifa yote,

tazameni maumivu yangu.

Wavulana wangu na wasichana wangu

wamekwenda uhamishoni.

19 “Niliita washirika wangu

lakini walinisaliti.

Makuhani wangu na wazee wangu

waliangamia mjini

walipokuwa wakitafuta chakula

ili waweze kuishi.

20 “Angalia, EeBwana, jinsi nilivyo katika dhiki!

Nina maumivu makali ndani yangu,

nami ninahangaika moyoni mwangu,

kwa kuwa nimekuwa mwasi sana.

Huko nje, upanga unaua watu,

ndani, kipo kifo tu.

21 “Watu wamesikia ninavyolia kwa uchungu,

lakini hakuna yeyote wa kunifariji.

Adui zangu wote wamesikia juu ya dhiki yangu,

wanafurahia lile ulilolitenda.

Naomba uilete siku uliyoitangaza

ili wawe kama mimi.

22 “Uovu wao wote na uje mbele zako;

uwashughulikie wao

kama vile ulivyonishughulikia mimi

kwa sababu ya dhambi zangu zote.

Kulia kwangu kwa uchungu ni kwingi

na moyo wangu umedhoofika.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/LAM/1-fe84efa99093d520960c29d74e38ee5e.mp3?version_id=1627—

Categories
Maombolezo

Maombolezo 2

1 Tazama jinsi Bwana alivyomfunika Binti Sayuni

kwa wingu la hasira yake!

Ameitupa chini fahari ya Israeli

kutoka mbinguni mpaka duniani,

hakukumbuka kiti chake cha kuwekea miguu

katika siku ya hasira yake.

2 Bila huruma Bwana ameyameza

makao yote ya Yakobo;

katika ghadhabu yake amebomoa

ngome za Binti Yuda.

Ameuangusha ufalme wake na wakuu wake

chini kwa aibu.

3 Katika hasira kali amevunja

kila pembeya Israeli.

Ameuondoa mkono wake wa kuume

alipokaribia adui.

Amemteketeza Yakobo kama moto uwakao

ule uteketezao kila kitu kinachouzunguka.

4 Ameupinda upinde wake kama adui,

mkono wake wa kuume uko tayari.

Kama vile adui amewachinja

wote waliokuwa wanapendeza jicho,

amemwaga ghadhabu yake kama moto

juu ya hema la Binti Sayuni.

5 Bwana ni kama adui;

amemmeza Israeli.

Amemeza majumba yake yote ya kifalme

na kuangamiza ngome zake.

Ameongeza huzuni na maombolezo

kwa ajili ya Binti Yuda.

6 Ameharibu maskani yake kama bustani,

ameharibu mahali pake pa mkutano.

Bwanaamemfanya Sayuni kusahau

sikukuu zake zilizoamriwa na Sabato zake;

katika hasira yake kali amewadharau

mfalme na kuhani.

7 Bwana amekataa madhabahu yake

na kuacha mahali patakatifu pake.

Amemkabidhi adui kuta

za majumba yake ya kifalme;

wamepiga kelele katika nyumba yaBwana

kama katika siku ya sikukuu iliyoamriwa.

8 Bwanaalikusudia kuangusha

ukuta uliomzunguka Binti Sayuni.

Ameinyoosha kamba ya kupimia

na hakuuzuia mkono wake usiangamize.

Alifanya maboma na kuta ziomboleze,

vyote vikaharibika pamoja.

9 Malango yake yamezama ardhini,

makomeo yake ameyavunja na kuyaharibu.

Mfalme wake na wakuu wake wamepelekwa uhamishoni

miongoni mwa mataifa,

sheria haipo tena,

na manabii wake hawapati tena

maono kutoka kwaBwana.

10 Wazee wa Binti Sayuni

wanaketi chini kimya,

wamenyunyiza mavumbi kwenye vichwa vyao

na kuvaa nguo za gunia.

Wanawali wa Yerusalemu

wamesujudu hadi ardhini.

11 Macho yangu yamedhoofika kwa kulia,

nina maumivu makali ndani,

moyo wangu umemiminwa ardhini

kwa sababu watu wangu wameangamizwa,

kwa sababu watoto na wanyonyao wanazimia

kwenye barabara za mji.

12 Wanawaambia mama zao,

“Wapi mkate na divai?”

wazimiapo kama watu waliojeruhiwa

katika barabara za mji,

maisha yao yadhoofikavyo

mikononi mwa mama zao.

13 Ninaweza kusema nini kwa ajili yako?

Nikulinganishe na nini,

ee Binti Yerusalemu?

Nitakufananisha na nini,

ili nipate kukufariji,

ee Bikira Binti Sayuni?

Jeraha lako lina kina kama bahari.

Ni nani awezaye kukuponya?

14 Maono ya manabii wako

yalikuwa ya uongo na yasiyofaa kitu,

hawakuifunua dhambi yako

ili kukuzuilia kwenda utumwani.

Maneno waliyokupa

yalikuwa ya uongo na ya kupotosha.

15 Wote wapitiao njia yako

wanakupigia makofi,

wanakudhihaki na kutikisa vichwa vyao

kwa Binti Yerusalemu:

“Huu ndio ule mji ulioitwa

mkamilifu wa uzuri,

furaha ya dunia yote?”

16 Adui zako wote wanapanua

vinywa vyao dhidi yako,

wanadhihaki na kusaga meno yao

na kusema, “Tumemmeza.

Hii ndiyo siku tuliyoingojea,

tumeishi na kuiona.”

17 Bwanaamefanya lile alilolipanga;

ametimiza neno lake

aliloliamuru siku za kale.

Amekuangusha bila huruma,

amewaacha adui wakusimange,

ametukuza pembe ya adui yako.

18 Mioyo ya watu

inamlilia Bwana.

Ee ukuta wa Binti Sayuni,

machozi yako na yatiririke kama mto

usiku na mchana;

usijipe nafuu,

macho yako yasipumzike.

19 Inuka, lia usiku,

zamu za usiku zianzapo;

mimina moyo wako kama maji

mbele za Bwana.

Mwinulie yeye mikono yako

kwa ajili ya maisha ya watoto wako,

ambao wanazimia kwa njaa

kwenye kila mwanzo wa barabara.

20 “Tazama, EeBwana, ufikirie:

Ni nani ambaye umepata

kumtendea namna hii?

Je, wanawake wakule wazao wao,

watoto waliowalea?

Je, kuhani na nabii auawe

mahali patakatifu pa Bwana?

21 “Vijana na wazee hujilaza pamoja

katika mavumbi ya barabarani,

wavulana wangu na wasichana

wameanguka kwa upanga.

Umewaua katika siku ya hasira yako,

umewachinja bila huruma.

22 “Kama ulivyoita siku ya karamu,

ndivyo ulivyoagiza hofu kuu

dhidi yangu kila upande.

Katika siku ya hasira yaBwana

hakuna yeyote aliyekwepa au kupona;

wale niliowatunza na kuwalea,

adui yangu amewaangamiza.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/LAM/2-cb20a5aaf59c8cada0cbd201bf7e3125.mp3?version_id=1627—

Categories
Maombolezo

Maombolezo 3

1 Mimi ndiye mtu aliyeona mateso

kwa fimbo ya ghadhabu yake.

2 Amenifukuzia mbali na kunifanya nitembee

gizani wala si katika nuru;

3 hakika, amegeuza mkono wake dhidi yangu

tena na tena, mchana kutwa.

4 Amefanya ngozi yangu na nyama yangu kuchakaa

na ameivunja mifupa yangu.

5 Amenizingira na kunizunguka

kwa uchungu na taabu.

6 Amenifanya niishi gizani

kama wale waliokufa.

7 Amenizungushia ukuta ili nisiweze kutoroka,

amenifunga kwa minyororo mizito.

8 Hata ninapoita au kulia ili kuomba msaada,

anakataa kupokea maombi yangu.

9 Ameizuia njia yangu kwa mapande ya mawe,

amepotosha njia zangu.

10 Kama dubu aviziaye,

kama simba mafichoni,

11 ameniburuta kutoka njia,

akanirarua na kuniacha bila msaada.

12 Amevuta upinde wake

na kunifanya mimi niwe lengo

kwa ajili ya mishale yake.

13 Alinichoma moyo wangu kwa mishale

iliyotoka kwenye podo lake.

14 Nimekuwa kichekesho kwa watu wangu wote,

wananidhihaki kwa wimbo mchana kutwa.

15 Amenijaza kwa majani machungu

na kunishibisha kwa nyongo.

16 Amevunja meno yangu kwa changarawe,

amenikanyagia mavumbini.

17 Amani yangu imeondolewa,

nimesahau kufanikiwa ni nini.

18 Kwa hiyo nasema, “Fahari yangu imeondoka

na yale yote niliyokuwa nimetarajia kutoka kwaBwana.”

19 Nayakumbuka mateso yangu na kutangatanga kwangu,

uchungu na nyongo.

20 Ninayakumbuka vyema,

nayo nafsi yangu imezimia ndani yangu.

21 Hata hivyo najikumbusha neno hili

na kwa hiyo ninalo tumaini.

22 Kwa sababu ya upendo mkuu waBwana, hatuangamii,

kwa kuwa huruma zake hazikomi kamwe.

23 Ni mpya kila asubuhi,

uaminifu wako ni mkuu.

24 Nimeiambia nafsi yangu, “Bwanani fungu langu,

kwa hiyo nitamngojea.”

25 Bwanani mwema kwa wale ambao tumaini lao ni kwake,

kwa yule ambaye humtafuta;

26 ni vyema kungojea kwa utulivu

kwa ajili ya wokovu waBwana.

27 Ni vyema mtu kuchukua nira

bado angali kijana.

28 Na akae peke yake awe kimya,

kwa maanaBwanaameiweka juu yake.

29 Na azike uso wake mavumbini

bado panawezekana kuwa na matumaini.

30 Na atoe shavu lake kwa yule ampigaye,

na ajazwe na aibu.

31 Kwa kuwa watu hawakatiliwi mbali

na Bwana milele.

32 Ingawa huleta huzuni, ataonyesha huruma,

kwa kuwa upendo wake usiokoma ni mkuu.

33 Kwa maana hapendi kuwaletea mateso

au huzuni watoto wa wanadamu.

34 Kuwaponda chini ya nyayo

wafungwa wote katika nchi,

35 Kumnyima mtu haki zake

mbele za Aliye Juu Sana,

36 kumnyima mtu haki:

Je, Bwana asione mambo kama haya?

37 Nani awezaye kusema nalo likatendeka

kama Bwana hajaamuru?

38 Je, si ni kwenye kinywa cha Aliye Juu Sana

ndiko yatokako maafa na mambo mema?

39 Mwanadamu yeyote aliye hai aweza kulalamika

wakati anapoadhibiwa kwa ajili ya dhambi zake?

40 Tuzichunguze njia zetu na kuzijaribu,

na tumrudieBwanaMungu.

41 Tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu

kwa Mungu mbinguni, na tuseme:

42 “Tumetenda dhambi na kuasi

nawe hujasamehe.

43 “Umejifunika mwenyewe kwa hasira na kutufuatilia;

umetuchinja bila huruma.

44 Unajifunika mwenyewe kwa wingu,

ili pasiwe na ombi

litakaloweza kupenya.

45 Umetufanya takataka na uchafu

miongoni mwa mataifa.

46 “Adui zetu wote wamefumbua vinywa vyao

wazi dhidi yetu.

47 Tumeteseka kwa hofu kuu na shida ya ghafula,

uharibifu na maangamizi.”

48 Vijito vya machozi vinatiririka kutoka machoni mwangu,

kwa sababu watu wangu wameangamizwa.

49 Macho yangu yatatiririka machozi bila kukoma,

bila kupata nafuu,

50 hadiBwanaatazame chini

kutoka mbinguni na kuona.

51 Lile ninaloliona huniletea huzuni nafsini

kwa sababu ya wanawake wote wa mji wangu.

52 Wale waliokuwa adui zangu bila sababu

wameniwinda kama ndege.

53 Walijaribu kukomesha maisha yangu ndani ya shimo

na kunitupia mawe;

54 maji yalifunika juu ya kichwa changu,

nami nikafikiri nilikuwa karibu

kukatiliwa mbali.

55 Nililiitia jina lako, EeBwana,

kutoka vina vya shimo.

56 Ulisikia ombi langu: “Usikizibie masikio yako

kilio changu nikuombapo msaada.”

57 Ulikuja karibu nilipokuita,

nawe ukasema, “Usiogope.”

58 Ee Bwana, ulichukua shauri langu,

ukaukomboa uhai wangu.

59 Umeona, EeBwana, ubaya niliotendewa.

Tetea shauri langu!

60 Umeona kina cha kisasi chao,

mashauri yao yote mabaya dhidi yangu.

61 EeBwana, umesikia matukano yao,

mashauri yao yote mabaya dhidi yangu:

62 kile adui zangu wanachonongʼona na kunungʼunikia

dhidi yangu mchana kutwa.

63 Watazame! Wakiwa wameketi au wamesimama,

wananidhihaki katika nyimbo zao.

64 Uwalipe kile wanachostahili, EeBwana,

kwa yale ambayo mikono yao imetenda.

65 Weka pazia juu ya mioyo yao,

laana yako na iwe juu yao!

66 Wafuatilie katika hasira na uwaangamize

kutoka chini ya mbingu zaBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/LAM/3-b873e8351240c387c9da090573d487e9.mp3?version_id=1627—

Categories
Maombolezo

Maombolezo 4

1 Jinsi dhahabu ilivyopoteza mngʼao wake,

dhahabu iliyo safi haingʼai!

Vito vya thamani vimetawanywa

kwenye mwanzo wa kila barabara.

2 Wana wa Sayuni wenye thamani,

ambao mwanzo uzito wa thamani yao

ulikuwa wa dhahabu,

sasa wanaangaliwa kama vyungu vya udongo,

kazi ya mikono ya mfinyanzi!

3 Hata mbweha hutoa matiti yao

kunyonyesha watoto wao,

lakini watu wangu wamekuwa wasio na huruma

kama mbuni jangwani.

4 Kwa sababu ya kiu ulimi wa mtoto mchanga

umegandamana na kaakaa la kinywa chake,

watoto huomba mkate,

lakini hakuna yeyote awapaye.

5 Wale waliokula vyakula vya kifahari

ni maskini barabarani.

Wale waliokuzwa wakivaa nguo za zambarau

sasa wanalalia majivu.

6 Adhabu ya watu wangu

ni kubwa kuliko ile ya Sodoma,

ambayo ilipinduliwa ghafula

bila kuwepo mkono wa msaada.

7 Wakuu wao walikuwa wamengʼaa kuliko theluji

na weupe kuliko maziwa,

miili yao ilikuwa myekundu kuliko marijani,

kuonekana kwao kama yakuti samawi.

8 Lakini sasa ni weusi kuliko masizi;

hawatambulikani barabarani.

Ngozi yao imeshikamana juu ya mifupa yao,

imekuwa mikavu kama fimbo.

9 Wale waliouawa kwa upanga ni bora

kuliko wale wanaokufa njaa;

wanateseka kwa njaa, wanatokomea

kwa kukosa chakula kutoka shambani.

10 Kwa mikono yao wenyewe wanawake wenye huruma

wanapika watoto wao wenyewe,

waliokuwa chakula chao

watu wangu walipoangamizwa.

11 Bwanaametoa nafasi kamilifu ya ghadhabu yake;

ameimwaga hasira yake kali.

Amewasha moto katika Sayuni

ambao umeteketeza misingi yake.

12 Wafalme wa dunia hawakuamini,

wala mtu yeyote wa duniani,

kwamba adui na watesi wangeweza kuingia

kwenye malango ya Yerusalemu.

13 Lakini hili lilitokea kwa sababu ya dhambi za manabii wake,

na maovu ya makuhani wake,

waliomwaga ndani yake

damu ya wenye haki.

14 Sasa wanapapasa papasa barabarani

kama watu ambao ni vipofu.

Wamenajisiwa kabisa kwa damu,

hata hakuna anayethubutu kugusa mavazi yao.

15 Watu wanawapigia kelele, “Ondokeni! Ninyi ni najisi!

Ondokeni! Ondokeni! Msituguse!”

Wanapokimbia na kutangatanga huku na huko,

watu miongoni mwa mataifa wanasema,

“Hawawezi kukaa hapa zaidi.”

16 Bwanamwenyewe amewatawanya;

hawaangalii tena.

Makuhani hawaonyeshwi heshima,

wazee hawakubaliki.

17 Zaidi ya hayo, macho yetu yalichoka,

kwa kutazamia bure msaada;

tuliangalia kutoka minara yetu

kwa taifa lisiloweza kutuokoa.

18 Watu walituvizia katika kila hatua

hata hatukuweza kutembea katika barabara zetu.

Mwisho wetu ulikuwa karibu, siku zetu zilikuwa zimetimia,

kwa maana mwisho wetu ulikuwa umefika.

19 Waliotufuatia walikuwa wepesi

kuliko tai angani;

walitusaka juu milimani

na kutuvizia jangwani.

20 Mpakwa mafuta waBwana, pumzi ya uhai wetu hasa,

alinaswa katika mitego yao.

Tulifikiri kwamba chini ya kivuli chake

tungeliweza kuishi miongoni mwa mataifa.

21 Shangilia na ufurahi, ee Binti Edomu,

wewe unayeishi nchi ya Usi.

Lakini kwako pia kikombe kitapitishwa,

Utalewa na kuvuliwa nguo ubaki uchi.

22 Ee Binti Sayuni, adhabu yako itaisha,

hatarefusha muda wako wa kukaa uhamishoni.

Lakini, ee Binti Edomu, ataadhibu dhambi yako,

na atafunua uovu wako.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/LAM/4-933953c0cd481067c2446f7585721e18.mp3?version_id=1627—

Categories
Maombolezo

Maombolezo 5

1 Kumbuka, EeBwana, yaliyotupata,

tazama, nawe uione aibu yetu.

2 Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni,

na nyumba zetu kwa wageni.

3 Tumekuwa yatima wasio na baba,

mama zetu wamekuwa kama wajane.

4 Ni lazima tununue maji tunayokunywa,

kuni zetu zapatikana tu kwa kununua.

5 Wanaotufuatilia wapo kwenye visigino vyetu,

tumechoka na hakuna pumziko.

6 Tumejitolea kwa Misri na Ashuru

tupate chakula cha kutosha.

7 Baba zetu walitenda dhambi na hawapo tena,

na sisi tunachukua adhabu yao.

8 Watumwa wanatutawala

na hakuna wa kutuokoa mikononi yao.

9 Tunapata chakula chetu kwa kuhatarisha maisha yetu

kwa sababu ya upanga jangwani.

10 Ngozi yetu ina joto kama tanuru,

kwa sababu ya fadhaa itokanayo na njaa.

11 Wanawake wametendwa jeuri katika Sayuni,

na mabikira katika miji ya Yuda.

12 Wakuu wametungikwa juu kwa mikono yao,

wazee hawapewi heshima.

13 Vijana wanataabika kwenye mawe ya kusagia,

wavulana wanayumbayumba chini ya mizigo ya kuni.

14 Wazee wameondoka langoni la mji,

vijana wameacha kuimba nyimbo zao.

15 Furaha imeondoka mioyoni mwetu,

kucheza kwetu kumegeuka maombolezo.

16 Taji imeanguka kutoka kichwani petu.

Ole wetu, kwa maana tumetenda dhambi!

17 Kwa sababu hiyo, mioyo yetu inazimia,

kwa sababu ya hayo, macho yetu yamefifia,

18 kwa ajili ya Mlima Sayuni, ambao unakaa ukiwa,

nao mbweha wanatembea juu yake.

19 Wewe, EeBwanaunatawala milele,

kiti chako cha enzi chadumu kizazi hadi kizazi.

20 Kwa nini watusahau siku zote?

Kwa nini umetuacha kwa muda mrefu?

21 Turudishe kwako mwenyewe, EeBwana,

ili tupate kurudi.

Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale,

22 isipokuwa uwe umetukataa kabisa

na umetukasirikia pasipo kipimo.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/LAM/5-39cf2feb8cdceb81c0778397c80b0acc.mp3?version_id=1627—

Categories
Ezekieli

Ezekieli Utangulizi

Utangulizi

Kitabu hiki kimepewa jina la nabii Ezekieli ambaye maana yake ni “Mungu ni Mwenye Nguvu.” Alizaliwa katika jamii ya kikuhani na kulelewa katika mazingira ya hekalu huko Yerusalemu. Mnamo mwaka wa 597 K.K. Ezekieli alikuwa mmoja wa mateka 10,000 waliopelekwa uhamishoni Babeli. Mungu alimwita katika huduma mwaka wa 593 K.K. kwa njia ya ufunuo.

Katika sehemu ya kwanza ya huduma yake alitoa ujumbe ule ule ambao Yeremia aliutangaza kwamba mji wa Yerusalemu na Hekalu vingeliharibiwa. Wingi wa dhambi na kuabudu sanamu kulikokuwa kunaendelea huko Yerusalemu kungelisababisha Mungu kuliacha Hekalu na Yerusalemu pia, kukifuatiwa na hukumu. Kuja kwa Babeli kuteka na kuharibu kulikuwa ni uhakikisho.

Baada ya habari kufika Babeli mwaka wa 586 K.K. kwamba Yerusalemu ilikuwa imeangamizwa, Ezekieli alitangaza ujumbe mpya wa matumaini ya kurudishwa kwa Waisraeli. Kama Mchungaji Mkuu, Mungu angewakusanya tena Waisraeli kutoka miisho ya dunia na kuwaimarisha tena katika nchi yao wenyewe. Mataifa ambayo yangeleta upinzani kuhusu kurudi kwa Waisraeli wangeshindwa na kuhukumiwa.

Mwandishi

Ezekieli mwana wa Buzi.

Kusudi

Kutangaza hukumu ya Mungu dhidi ya Wayahudi na mataifa mengine, na kuelezea wokovu wa watu wa Mungu.

Mahali

Babeli.

Tarehe

Kama mwaka wa 571 K.K.

Wahusika Wakuu

Ezekieli, viongozi wa Israeli, mke wa Ezekieli, Nebukadneza.

Wazo Kuu

Kuwaonya watu juu ya dhambi zao na kutokutii. Kuonyesha pia wema wa Mungu kwa watu wake na kuweka wazi rehema za Mungu endapo watu wangetubu.

Mambo Muhimu

Ujumbe wa Mungu kwa taifa la Israeli kuhusu hukumu ya dhambi zao, hukumu ya watu wa mataifa, na tumaini kwa watu wa Israeli kwa siku za mwisho.

Mgawanyo

Mwito wa Ezekieli (

1:1–3:27

)

Hali ya dhambi ya Yerusalemu na maangamizi (

4:1–24:27

)

Unabii dhidi ya mataifa ya kigeni (

25:1–32:32

)

Matumaini ya kurudishwa upya (

33:1–39:29

)

Israeli kurudishwa kwenye nchi yao (

40:1–48:35

).

Categories
Ezekieli

Ezekieli 1

Viumbe Hai Na Utukufu Wa Bwana

1 Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, wakati nilipokuwa miongoni mwa hao waliokuwa uhamishoni kando ya Mto Kebari, mbingu zilifunguka nami nikaona maono ya Mungu.

2 Katika siku ya tano ya mwezi, ilikuwa mwaka wa tano wa kuhamishwa kwa Mfalme Yehayakini,

3 neno laBwanalilimjia Ezekieli kuhani, mwana wa Buzi, kando ya Mto Kebari, katika nchi ya Wakaldayo. Huko mkono waBwanaulikuwa juu yake.

4 Nilitazama, nikaona dhoruba kubwa ikitoka kaskazini, wingu kubwa sana pamoja likiwa na umeme wa radi likiwa limezungukwa na mwanga mkali. Katikati ya huo moto kulikuwa kama rangi ya manjano ya chuma kinapokuwa ndani ya moto.

5 Katika ule moto kulikuwa na kitu kinachofanana na viumbe vinne vyenye uhai. Katika kuonekana kwake vilikuwa na umbo mfano wa mwanadamu,

6 lakini kila kimoja kilikuwa na nyuso nne na mabawa manne.

7 Miguu yao ilikuwa imenyooka, nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za miguu ya ndama, nazo zilimetameta kama shaba iliyosuguliwa.

8 Chini ya mabawa yao katika pande zao nne walikuwa na mikono ya mwanadamu. Wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa,

9 nayo mabawa yao yaligusana. Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja, hawakugeuka walipokuwa wanatembea.

10 Kuonekana kwa nyuso zao kulikuwa hivi: Kila mmoja wa wale wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na kwa upande wa kulia kila mmoja alikuwa na uso wa simba, upande wa kushoto alikuwa na uso wa ngʼombe pia kila mmoja alikuwa na uso wa tai.

11 Hivyo ndivyo zilivyokuwa nyuso zao. Mabawa yao yalikunjuliwa kuelekea juu, kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ambayo kila moja liligusa bawa la mwenzake kila upande na mabawa mengine mawili yakifunika mwili wake.

12 Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja. Popote roho alipotaka kwenda, ndipo walipokwenda pasipo kugeuka.

13 Kuonekana kwa vile viumbe hai katikati kulikuwa kama makaa ya mawe yanayowaka au kama mienge. Moto ule ulikuwa ukienda mbele na nyuma katikati ya vile viumbe, ulikuwa na mwangaza mkali na katikati ya ule moto kulitoka kimulimuli kama umeme wa radi.

14 Vile viumbe vilipiga mbio kwenda na kurudi, kama vimulimuli vya umeme wa radi.

15 Nilipokuwa nikitazama vile viumbe hai, niliona gurudumu moja juu ya ardhi kando ya kila kiumbe kikiwa na nyuso zake nne.

16 Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa hayo magurudumu na muundo wake: yalingʼaa kama zabarajadi, nayo yote manne yalifanana. Kila gurudumu lilikuwa na gurudumu jingine ndani yake.

17 Yalipokwenda yalielekea upande wowote wa pande nne walipoelekea wale viumbe, magurudumu hayakuzunguka wakati viumbe vile vilipokwenda.

18 Kingo zake zilikuwa ndefu kwenda juu na za kutisha, nazo zote nne zilijawa na macho pande zote.

19 Vile viumbe hai vilipokwenda, magurudumu yaliyokuwa kando yao yalisogea na wakati hivyo viumbe hai vilipoinuka kutoka ardhini magurudumu nayo yaliinuka.

20 Mahali popote roho alipokwenda wale viumbe nao walikwenda, nayo magurudumu yaliinuka pamoja navyo, kwa sababu roho ya vile viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.

21 Wakati viumbe vile viliposogea, nayo magurudumu yalisogea, viumbe viliposimama kimya, nayo pia yalisimama kimya, viumbe vilipoinuka juu ya nchi magurudumu yaliinuliwa pamoja navyo kwa kuwa roho ya hivyo viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.

22 Juu ya vichwa vya hao viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa eneo lililokuwa wazi, lililokuwa angavu kabisa na lenye kutisha.

23 Chini ya hiyo nafasi mabawa yao yalitanda moja kuelekea jingine, kila mmoja alikuwa na mabawa mengine mawili yaliyofunika mwili wake.

24 Viumbe wale waliposogea nilisikia sauti ya mabawa yao, kama ngurumo ya maji yaendayo kasi, kama sauti ya Mwenyezi,kama makelele ya jeshi. Waliposimama kimya walishusha mabawa yao.

25 Ndipo ikaja sauti toka juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao, waliposimama mabawa yao yakiwa yameshushwa.

26 Juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. Na juu ya kile kiti cha enzi kulikuwa na umbo mfano wa mwanadamu.

27 Nikaona kwamba kutokana na kile nilichoona kama kiuno chake kuelekea juu alionekana kama chuma inayowaka kana kwamba imejaa moto na kuanzia kiuno kwenda chini alionekana kama moto na mwanga mkali ulimzunguka.

28 Kama vile kuonekana kwa upinde wa mvua mawinguni siku ya mvua, ndivyo ulivyokuwa ule mngʼao uliomzunguka.

Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa utukufu waBwana. Nilipouona, nikaanguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mtu anaongea.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/EZK/1-641cb6f6c2bbe5248b2f6c79869990b7.mp3?version_id=1627—

Categories
Ezekieli

Ezekieli 2

Wito Wa Ezekieli

1 Akaniambia, “Mwanadamu, simama kwa miguu yako nami nitasema nawe.”

2 Alipokuwa akiongea nami, Roho akanijia na kunisimamisha wima, nikamsikia akisema nami.

3 Akaniambia: “Mwanadamu, ninakutuma kwa Waisraeli, kwa taifa asi ambalo limeniasi mimi, wao na baba zao wananikosea mimi hadi leo.

4 Watu ambao ninakutuma kwao ni wapotovu na wakaidi. Waambie, ‘Hivi ndivyo anavyosemaBwanaMwenyezi.’

5 Kama watasikiliza au hawatasikiliza, kwa kuwa wao ni nyumba ya kuasi, watajua nabii amekuwa miongoni mwao.

6 Nawe mwanadamu, usiwaogope wao wala maneno yao, usiogope, ingawa michongoma na miiba vinakuzunguka na unaishi katikati ya nge. Usiogope yale wasemayo wala usitishwe nao, ingawa wao ni nyumba ya uasi.

7 Wewe lazima uwaambie maneno yangu, ikiwa wanasikiliza au hawasikilizi, kwa kuwa wao ni watu waasi.

8 Lakini wewe mwanadamu, sikiliza ninalokuambia. Usiwe mwenye kuasi kama hiyo nyumba ya kuasi. Fungua kinywa chako na ule nikupacho.”

9 Ndipo nikatazama, nami nikaona mkono ulionyooshwa kunielekea. Nao ulikuwa na ukurasa wa kitabu,

10 ambao aliukunjua mbele yangu. Pande zote mbili ulikuwa umeandikwa maneno ya maombolezo, vilio na ole.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/EZK/2-b246d5e9a25f410b94cd34685873fd63.mp3?version_id=1627—