Categories
Mhubiri

Mhubiri 11

Mkate Juu Ya Maji

1 Tupa mkate wako juu ya maji,

kwa maana baada ya siku nyingi

utaupata tena.

2 Wape sehemu watu saba, naam hata wanane,

kwa maana hujui ni baa gani

litakalokuwa juu ya nchi.

3 Kama mawingu yamejaa maji,

hunyesha mvua juu ya nchi.

Kama mti ukianguka kuelekea kusini

au kuelekea kaskazini,

mahali ulipoangukia,

hapo ndipo utakapolala.

4 Yeyote atazamaye upepo hatapanda,

yeyote aangaliaye mawingu hatavuna.

5 Kama vile usivyofahamu njia ya upepo,

au jinsi mwili uumbwavyo

ndani ya tumbo la mama,

vivyo hivyo huwezi kufahamu kazi ya Mungu,

Muumba wa vitu vyote.

6 Panda mbegu yako asubuhi,

nako jioni usiruhusu mikono yako ilegee,

kwa maana hujui ni ipi itakayofanikiwa,

kwamba ni hii au ni ile,

au kwamba zote zitafanikiwa sawasawa.

Mkumbuke Muumba Wako Ukiwa Bado Kijana

7 Nuru ni tamu,

tena inafurahisha macho kuona jua.

8 Hata kama mtu ataishi miaka mingi kiasi gani,

na aifurahie yote.

Lakini na akumbuke siku za giza,

kwa maana zitakuwa nyingi.

Kila kitu kitakachokuja ni ubatili.

9 Furahi ewe kijana, wakati ungali kijana,

moyo wako na ukupe furaha

katika siku za ujana wako.

Fuata njia za moyo wako

na chochote macho yako yaonayo,

lakini ujue kwamba kwa ajili ya haya yote

Mungu atakuleta hukumuni.

10 Kwa hiyo basi, ondoa wasiwasi moyoni mwako

na utupilie mbali masumbufu ya mwili wako,

kwa kuwa ujana na nguvu ni ubatili.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ECC/11-08c8b8fb2bf4ebf3529b7a786c3319fb.mp3?version_id=1627—

Categories
Mhubiri

Mhubiri 12

1 Mkumbuke Muumba wako

siku za ujana wako,

kabla hazijaja siku za taabu,

wala haijakaribia miaka utakaposema,

“Mimi sifurahii hiyo”:

2 kabla jua na nuru,

nao mwezi na nyota havijatiwa giza,

kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;

3 siku ile walinzi wa nyumba watakapotetemeka,

nao watu wenye nguvu watakapojiinamisha,

wakati wasagao watakapokoma kwa sababu ya uchache,

nao wachunguliao madirishani kutiwa giza;

4 wakati milango ya kuingia barabarani itakapofungwa

na sauti ya kusaga kufifia;

wakati watu wataamshwa kwa sauti ya ndege,

lakini nyimbo zao zote zikififia;

5 wakati watu watakapoogopa kilichoinuka juu

na hatari zitakazokuwepo barabarani;

wakati mlozi utakapochanua maua

na panzi kujikokota

nawe usiwe na shauku ya kitu chochote.

Ndipo mwanadamu aiendea nyumba yake ya milele

nao waombolezaji wakizunguka barabarani.

6 Mkumbuke Muumba wako: kabla haijakatika kamba ya fedha,

au bakuli la dhahabu halijavunjika;

kabla mtungi kuvunjika kwenye chemchemi,

au gurudumu kuvunjika kisimani,

7 nayo mavumbi kurudi ardhini yalikotoka,

na roho kurudi kwa Mungu aliyeitoa.

8 Mhubiri asema, “Ubatili! Ubatili!

Kila kitu ni ubatili!”

Hitimisho La Mambo

9 Mhubiri hakuwa tu na hekima, bali aliwagawia watu maarifa pia. Alitafakari na kutafiti na akaweka katika utaratibu mithali nyingi.

10 Mhubiri alitafiti ili kupata maneno sahihi na kila alichoandika kilikuwa sawa na kweli.

11 Maneno ya wenye hekima ni kama mchokoro, mithali zao zilizokusanywa pamoja ni kama misumari iliyogongomewa ikawa imara, yaliyotolewa na Mchungaji mmoja.

12 Tena zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo, hakuna mwisho wa kutunga vitabu vingi, nako kusoma sana huuchosha mwili.

13 Hii ndiyo jumla ya maneno;

yote yamekwisha sikiwa:

Mche Mungu, nawe uzishike amri zake,

maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.

14 Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi,

pamoja na kila neno la siri,

likiwa jema au baya.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ECC/12-994a2f19195380145c3a7bd900bc563b.mp3?version_id=1627—

Categories
Wimbo

Wimbo Utangulizi

Utangulizi

Kitabu hiki huitwa “Wimbo wa Nyimbo” yaani “Wimbo Mzuri Kupita Zote,” na ni tafsiri ya moja kwa moja kutoka kwa Kiebrania “Shir Hash-Shirim,” na Kiyunani “Asma Asmaton.” Nyongeza “Asher li-Shelomoth,” ambayo imetafsiriwa “Wimbo wa Solomoni,” ndiyo chimbuko ya jina linalotumika kwa kawaida katika Kiingereza.

Mwandishi

Inadhaniwa kuwa mwandishi wa kitabu hiki ni Solomoni.

Kusudi

Kusudi la kitabu hiki ni kuthibitisha utakatifu wa ndoa, na kuonyesha picha ya upendo wa Mungu kwa watu wake.

Mahali

Bustani ya mwanamke Mshulami na jumba la kifalme.

Tarehe

Hakuna uhakika wa tarehe ya kuandikwa kwa kitabu hiki.

Wahusika Wakuu

Mfalme Solomoni, Mwanamke Mshulami, na marafiki.

Wazo Kuu

Watu wengine wanafananishia Wimbo Ulio Bora na upendo wa Kristo kwa kanisa lake. Lakini vinavyokubalika zaidi ni kwamba Wimbo Ulio Bora ni mkusanyo wa mashairi kati ya wawili wapendanao. Ni picha nzuri ya upendo wa mume na mke katika ndoa.

Mambo Muhimu

Mambo yanayohusu upendo na ndoa.

Mgawanyo

Bibi arusi na bwana arusi (

1:1–2:7

)

Sifa za mpenzi wake (

2:8–3:5

)

Kumsifu bibi arusi (

3:6–5:1

)

Upendo wenye msukosuko (

5:2–7:9

)

Urafiki ambao haujavunjika (

7:10–8:14

).

Categories
Wimbo

Wimbo 1

1 Wimbo ulio bora wa Solomoni.

Shairi La Kwanza

2 Unibusu kwa busu la kinywa chako,

kwa maana upendo wako unafurahisha kuliko divai.

3 Manukato yako yananukia vizuri,

jina lako ni kama manukato yaliyomiminwa.

Ndiyo sababu wanawali wanakupenda!

4 Nichukue twende nawe, na tufanye haraka!

Mfalme na anilete ndani ya vyumba vyake.

Tunakushangilia na kukufurahia,

tutasifu upendo wako zaidi kuliko divai.

Tazama jinsi ilivyo bora wakupende!

5 Mimi ni mweusi, lakini napendeza,

enyi binti za Yerusalemu,

mweusi kama mahema ya Kedari,

kama mapazia ya hema la Solomoni.

6 Usinikazie macho kwa sababu mimi ni mweusi,

kwa sababu nimefanywa mweusi na jua.

Wana wa mama yangu walinikasirikia

na kunifanya niwe mtunza mashamba ya mizabibu.

Shamba langu mwenyewe la mizabibu nimeliacha.

7 Niambie, wewe ambaye ninakupenda,

unalisha wapi kundi lako la kondoo

na ni wapi unapowapumzisha kondoo wako adhuhuri.

Kwa nini niwe kama mwanamke aliyefunikwa shela

karibu na makundi ya rafiki zako?

8 Kama hujui, ewe mwanamke mzuri kuliko wote,

fuata nyayo za kondoo,

na kulisha wana-mbuzi wako

karibu na hema za wachungaji.

9 Mpenzi wangu, ninakufananisha na farasi jike

aliyefungwa katika mojawapo ya magari ya vita ya Farao.

10 Mashavu yako yanapendeza yakiwa na vipuli,

shingo yako ikiwa na mikufu ya vito.

11 Tutakufanyia vipuli vya dhahabu,

vyenye kupambwa kwa fedha.

12 Wakati mfalme alipokuwa mezani pake,

manukato yangu yalisambaza harufu yake nzuri.

13 Mpenzi wangu kwangu mimi ni kifuko cha manemane

kati ya matiti yangu.

14 Mpenzi wangu kwangu mimi ni kama kishada cha maua ya mhina

kutoka mashamba ya mizabibu ya En-Gedi.

15 Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu!

Tazama jinsi ulivyo mzuri!

Macho yako ni kama ya hua.

16 Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu!

Ee, tazama jinsi unavyopendeza!

Na kitanda chetu ni cha majani mazuri.

17 Nguzo za nyumba yetu ni mierezi,

na mapao yetu ni miberoshi.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/SNG/1-aa5542e6a01defc4e02688125b839d1d.mp3?version_id=1627—

Categories
Wimbo

Wimbo 2

1 Mimi ni ua la Sharoni,

yungiyungi ya bondeni.

2 Kama yungiyungi katikati ya miiba

ndivyo alivyo mpenzi wangu katikati ya wanawali.

3 Kama mti wa mtofaa miongoni mwa miti ya msituni

ndivyo alivyo mpenzi wangu

miongoni mwa wanaume vijana.

Ninafurahia kuketi kivulini mwa mwanaume huyu,

na tunda lake ni tamu kwangu.

4 Amenichukua mpaka kwenye ukumbi wa karamu,

na bendera ya huyu mwanaume

juu yangu ni upendo.

5 Nitie nguvu kwa zabibu kavu,

niburudishe kwa matofaa,

kwa maana ninazimia kwa mapenzi.

6 Mkono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu,

na mkono wake wa kuume unanikumbatia.

7 Binti za Yerusalemu, ninawaagiza

kwa paa na kwa ayala wa shambani:

Msichochee wala kuamsha mapenzi

hata yatakapotaka yenyewe.

Shairi La Pili

8 Sikiliza! Mpenzi wangu!

Tazama! Huyu hapa anakuja,

akirukaruka juu milimani

akizunguka juu ya vilima.

9 Mpenzi wangu ni kama paa au ayala kijana.

Tazama! Anasimama nyuma ya ukuta wetu,

akitazama kupitia madirishani,

akichungulia kimiani.

10 Mpenzi wangu alizungumza na kuniambia,

“Inuka, mpenzi wangu,

mrembo wangu, tufuatane.

11 Tazama! Wakati wa masika umepita,

mvua imekwisha na ikapita.

12 Maua yanatokea juu ya nchi;

majira ya kuimba yamewadia,

sauti za njiwa zinasikika

katika nchi yetu.

13 Mtini unatunga matunda yake ya mwanzoni,

zabibu zinazochanua zaeneza harufu nzuri.

Inuka, njoo mpenzi wangu.

Mrembo wangu, tufuatane.”

14 Hua wangu penye nyufa za majabali,

mafichoni pembezoni mwa mlima,

nionyeshe uso wako,

na niisikie sauti yako,

kwa maana sauti yako ni tamu,

na uso wako unapendeza.

15 Tukamatie mbweha,

mbweha wale wadogo

wanaoharibu mashamba ya mizabibu,

mashamba yetu ya mizabibu yaliyochanua.

16 Mpenzi wangu ni wangu, nami ni wake,

yeye hujilisha katikati ya yungiyungi.

17 Mpaka jua linapochomoza,

na vivuli vikimbie,

rudi, mpenzi wangu,

na uwe kama paa,

au kama ayala kijana

juu ya vilima vya Betheri.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/SNG/2-e8bb73f313408f6ed2c4314bc12546ae.mp3?version_id=1627—

Categories
Wimbo

Wimbo 3

1 Usiku kucha kwenye kitanda changu

nilimtafuta yule moyo wangu umpendaye;

nilimtafuta, lakini sikumpata.

2 Sasa nitaondoka na kuzunguka mjini,

katika barabara zake na viwanja;

nitamtafuta yule moyo wangu umpendaye.

Kwa hiyo nilimtafuta lakini sikumpata.

3 Walinzi walinikuta

walipokuwa wakizunguka mji.

Nikawauliza, “Je, mmemwona

yule moyo wangu umpendaye?”

4 Kitambo kidogo tu baada ya kuwapita

nilimpata yule moyo wangu umpendaye.

Nilimshika na sikumwachia aende

mpaka nilipomleta katika nyumba ya mama yangu,

katika chumba cha yule aliyenichukua mimba.

5 Binti za Yerusalemu, ninawaagiza

kwa paa na kwa ayala wa shambani:

Msichochee wala kuamsha mapenzi

hata yatakapotaka yenyewe.

Shairi La Tatu

6 Ni nani huyu anayekuja kutoka jangwani

kama nguzo ya moshi,

anayenukia manemane na uvumba

iliyotengenezwa kwa vikolezo vyote

vya mfanyabiashara?

7 Tazama! Ni gari la Solomoni

lisindikizwalo na mashujaa sitini,

walio wakuu sana wa Israeli,

8 wote wamevaa panga,

wote wazoefu katika vita,

kila mmoja na upanga wake pajani,

wamejiandaa kwa ajili ya hofu za usiku.

9 Mfalme Solomoni alijitengenezea gari;

alilitengeneza kwa mbao kutoka Lebanoni.

10 Nguzo zake alizitengeneza kwa fedha,

kitako chake kwa dhahabu.

Kiti chake kilipambwa kwa zambarau,

gari lake likanakshiwa njumu kwa upendo

na binti za Yerusalemu.

11 Tokeni nje, ninyi binti za Sayuni,

mkamtazame Mfalme Solomoni akiwa amevaa taji,

taji ambalo mama yake alimvika

siku ya arusi yake,

siku ambayo moyo wake ulishangilia.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/SNG/3-92b9f3c5a11759d9568a6fa395eeeddb.mp3?version_id=1627—

Categories
Wimbo

Wimbo 4

1 Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu!

Ee, jinsi ulivyo mzuri!

Macho yako nyuma ya shela yako

ni kama ya hua.

Nywele zako ni kama kundi la mbuzi

zikishuka kutoka Mlima Gileadi.

2 Meno yako ni kama kundi la kondoo waliokatwa manyoya sasa hivi,

watokao kuogeshwa.

Kila mmoja ana pacha lake,

hakuna hata mmoja aliye peke yake.

3 Midomo yako ni kama uzi mwekundu,

kinywa chako kinapendeza.

Mashavu yako nyuma ya shela yako

ni kama vipande viwili vya komamanga.

4 Shingo yako ni kama mnara wa Daudi,

uliojengwa kwa madaha,

juu yake zimetundikwa ngao elfu,

zote ni ngao za mashujaa.

5 Matiti yako mawili ni kama wana-paa wawili,

kama wana-paa mapacha

wajilishao katikati ya yungiyungi.

6 Hata kupambazuke na vivuli vikimbie,

nitakwenda kwenye mlima wa manemane

na kwenye kilima cha uvumba.

7 Wewe ni mzuri kote, mpenzi wangu,

hakuna hitilafu ndani yako.

8 Enda nami kutoka Lebanoni, bibi arusi wangu,

enda nami kutoka Lebanoni.

Shuka kutoka ncha ya Amana,

kutoka juu ya Seniri, kilele cha Hermoni,

kutoka mapango ya simba

na kutoka mlima wapendapo kukaa chui.

9 Umeiba moyo wangu, dada yangu, bibi arusi wangu;

umeiba moyo wangu

kwa mtazamo mmoja wa macho yako,

kwa kito kimoja cha mkufu wako.

10 Tazama jinsi pendo lako linavyofurahisha,

dada yangu, bibi arusi wangu!

Pendo lako linafurahisha aje zaidi ya divai,

na harufu ya manukato yako zaidi ya kikolezo chochote!

11 Midomo yako inadondosha utamu kama sega la asali,

bibi arusi wangu;

maziwa na asali viko chini ya ulimi wako.

Harufu nzuri ya mavazi yako ni kama ile ya Lebanoni.

12 Wewe ni bustani iliyofungwa, dada yangu,

bibi arusi wangu;

wewe ni chanzo cha maji kilichozungushiwa kabisa,

chemchemi yangu peke yangu.

13 Mimea yako ni bustani ya mikomamanga

yenye matunda mazuri sana,

yenye hina na nardo,

14 nardo na zafarani,

mchai na mdalasini,

pamoja na kila aina ya mti wa uvumba,

manemane na udi,

na aina zote za vikolezo bora kuliko vyote.

15 Wewe ni chemchemi ya bustani,

kisima cha maji yatiririkayo,

yakitiririka kutoka Lebanoni.

16 Amka, upepo wa kaskazini,

na uje, upepo wa kusini!

Vuma juu ya bustani yangu,

ili harufu yake nzuri iweze kuenea mpaka ngʼambo.

Mpendwa wangu na aje bustanini mwake

na kuonja matunda mazuri sana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/SNG/4-b7bfa511541d24823c02d513c04318ac.mp3?version_id=1627—

Categories
Wimbo

Wimbo 5

1 Nimekuja kwenye bustani yangu, dada yangu,

bibi arusi wangu;

nimekusanya manemane yangu pamoja

na kikolezo changu.

Nimekula sega langu la asali na asali yangu;

nimekunywa divai yangu na maziwa yangu.

Kuleni, enyi marafiki, mnywe;

kunyweni ya kutosha, ee wapenzi.

Shairi La Nne

2 Nililala lakini moyo wangu ulikuwa macho.

Sikiliza! Mpenzi wangu anabisha:

“Nifungulie, dada yangu, mpenzi wangu,

hua wangu, asiye na hitilafu.

Kichwa changu kimeloa umande,

na nywele zangu manyunyu ya usiku.”

3 Nimevua joho langu:

je, ni lazima nivae tena?

Nimenawa miguu yangu:

je, ni lazima niichafue tena?

4 Mpenzi wangu aliweka mkono wake kwenye tundu la komeo;

moyo wangu ulianza kugonga kwa ajili yake.

5 Niliinuka kumfungulia mpenzi wangu,

mikono yangu ikidondosha manemane,

vidole vyangu vikitiririka manemane,

penye vipini vya komeo.

6 Nilimfungulia mpenzi wangu,

lakini mpenzi wangu alishaondoka;

alikuwa amekwenda zake.

Moyo wangu ulishuka kwa kuondoka kwake.

Nilimtafuta lakini sikumpata.

Nilimwita lakini hakunijibu.

7 Walinzi walinikuta

walipokuwa wakifanya zamu za ulinzi mjini.

Walinipiga, wakanijeruhi,

wakaninyangʼanya joho langu,

hao walinzi wa kuta!

8 Enyi binti za Yerusalemu, ninawaagiza:

kama mkimpata mpenzi wangu,

mtamwambia nini?

Mwambieni ninazimia kwa mapenzi.

9 Je, mpendwa wako ni bora kuliko wengine namna gani,

wewe uliye mzuri kupita wanawake wote?

Je, mpendwa wako ni mzuri kuliko wengine, namna gani,

hata unatuagiza hivyo?

10 Mpenzi wangu anangʼaa, tena ni mwekundu,

wa kuvutia miongoni mwa wanaume kumi elfu.

11 Kichwa chake ni dhahabu safi kuliko zote,

nywele zake ni za mawimbi

na ni nyeusi kama kunguru.

12 Macho yake ni kama ya hua

kandokando ya vijito vya maji,

aliyeogeshwa kwenye maziwa,

yaliyopangwa kama vito vya thamani.

13 Mashavu yake ni kama matuta ya vikolezo

yakitoa manukato.

Midomo yake ni kama yungiyungi

inayodondosha manemane.

14 Mikono yake ni fimbo za dhahabu

iliyopambwa kwa krisolitho.

Mwili wake ni kama pembe ya ndovu iliyongʼarishwa

iliyopambwa na yakuti samawi.

15 Miguu yake ni nguzo za marmar

zilizosimikwa katika vitako vya dhahabu safi.

Sura yake ni kama Lebanoni,

bora kama miti yake ya mierezi.

16 Kinywa chake chenyewe ni utamu,

kwa ujumla yeye ni wa kupendeza.

Huyu ndiye mpenzi wangu, huyu ndiye rafiki yangu,

ee binti za Yerusalemu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/SNG/5-ecc48cc679f9d87d8ca6243ded71bc45.mp3?version_id=1627—

Categories
Wimbo

Wimbo 6

1 Mpenzi wako amekwenda wapi,

ewe mzuri kupita wanawake wote?

Mpenzi wako amegeukia njia ipi,

tupate kumtafuta pamoja nawe?

2 Mpenzi wangu amekwenda bustanini mwake,

kwenye vitalu vya vikolezo,

kujilisha bustanini

na kukusanya yungiyungi.

3 Mimi ni wake mpenzi wangu,

na mpenzi wangu ni wangu;

yeye hujilisha katikati ya yungiyungi.

Shairi La Tano

4 Wewe ni mzuri, mpenzi wangu, kama Tirsa,

upendezaye kama Yerusalemu,

umetukuka kama jeshi lenye bendera.

5 Uyageuze macho yako mbali nami,

yananigharikisha.

Nywele zako ni kama kundi la mbuzi

wanaoteremka kutoka Gileadi.

6 Meno yako ni kama kundi la kondoo

watokao kuogeshwa.

Kila mmoja ana pacha lake,

hakuna hata mmoja aliye peke yake.

7 Mashavu yako nyuma ya shela yako

ni kama vipande viwili vya komamanga.

8 Panaweza kuwepo malkia sitini,

masuria themanini

na mabikira wasiohesabika;

9 lakini hua wangu, mkamilifu wangu,

ni wa namna ya pekee,

binti pekee kwa mama yake,

kipenzi cha yeye aliyemzaa.

Wanawali walimwona na kumwita aliyebarikiwa;

malkia na masuria walimsifu.

10 Ni nani huyu atokeaye kama mapambazuko,

mzuri kama mwezi, mwangavu kama jua,

ametukuka kama nyota zifuatanazo?

11 Niliteremka kwenye bustani ya miti ya milozi

ili kutazama machipuko ya bondeni,

kuona kama mizabibu imechipua

au kama mikomamanga imechanua maua.

12 Kabla sijangʼamua,

shauku yangu iliniweka

katikati ya magari ya kifalme ya kukokotwa na farasi ya watu wangu.

13 Rudi, rudi, ee Mshulami;

rudi, rudi ili tupate kukutazama!

Kwa nini kumtazama Mshulami,

kama kutazama ngoma ya Mahanaimu?

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/SNG/6-6e5ca2b6b3f2cbc660fcf8246dd18bce.mp3?version_id=1627—

Categories
Wimbo

Wimbo 7

1 Ee binti wa mwana wa mfalme,

tazama jinsi inavyopendeza miguu yako katika viatu!

Miguu yako yenye madaha ni kama vito vya thamani,

kazi ya mikono ya fundi stadi.

2 Kitovu chako ni kama bilauri ya mviringo

ambayo kamwe haikosi divai iliyochanganywa.

Kiuno chako ni kichuguu cha ngano

kilichozungukwa kwa yungiyungi.

3 Matiti yako ni kama wana-paa wawili,

mapacha wa paa.

4 Shingo yako ni kama mnara wa pembe ya ndovu.

Macho yako ni vidimbwi vya Heshboni

karibu na lango la Beth-Rabi.

Pua lako ni kama mnara wa Lebanoni

ukitazama kuelekea Dameski.

5 Kichwa chako kinakuvika taji kama mlima Karmeli.

Nywele zako ni kama zulia la urujuani;

mfalme ametekwa na mashungi yake.

6 Tazama jinsi ulivyo mzuri na unavyopendeza,

ee pendo, kwa uzuri wako!

7 Umbo lako ni kama la mtende,

nayo matiti yako kama vishada vya matunda.

8 Nilisema, “Nitakwea mtende,

nami nitayashika matunda yake.”

Matiti yako na yawe kama vishada vya mzabibu,

harufu nzuri ya pumzi yako kama matofaa,

9 na kinywa chako kama divai

bora kuliko zote.

Divai na iende moja kwa moja hadi kwa mpenzi wangu,

ikitiririka polepole juu ya midomo na meno.

10 Mimi ni mali ya mpenzi wangu,

nayo shauku yake ni juu yangu.

11 Njoo, mpenzi wangu, twende mashambani,

twende tukalale huko vijijini.

12 Hebu na twende mapema

katika mashamba ya mizabibu

tuone kama mizabibu imechipua,

kama maua yake yamefunguka,

na kama mikomamanga imetoa maua:

huko nitakupa penzi langu.

13 Mitunguja hutoa harufu zake nzuri,

kwenye milango yetu kuna matunda mazuri,

mapya na ya zamani,

ambayo nimekuhifadhia wewe,

mpenzi wangu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/SNG/7-5c3cefdcb92e234defb3e7eb7ef32ca3.mp3?version_id=1627—