Categories
Mithali

Mithali 3

Faida Nyingine Za Hekima

1 Mwanangu, usisahau mafundisho yangu,

bali zitunze amri zangu moyoni mwako,

2 kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako

na kukuletea mafanikio.

3 Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe;

vifunge shingoni mwako,

viandike katika ubao wa moyo wako.

4 Ndipo utapata kibali na jina zuri

mbele za Mungu na mwanadamu.

5 MtumainiBwanakwa moyo wako wote

wala usizitegemee akili zako mwenyewe;

6 katika njia zako zote mkiri yeye,

naye atayanyoosha mapito yako.

7 Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe;

mcheBwanaukajiepushe na uovu.

8 Hii itakuletea afya mwilini mwako,

na mafuta kwenye mifupa yako.

9 MheshimuBwanakwa mali zako na

kwa malimbuko ya mazao yako yote;

10 ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika,

viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.

11 Mwanangu, usiidharau adhabu yaBwana

na usichukie kukaripiwa naye,

12 kwa sababuBwanahuwaadibisha wale awapendao,

kama vile baba afanyavyo

kwa mwana apendezwaye naye.

13 Heri mtu yule aonaye hekima,

mtu yule apataye ufahamu,

14 kwa maana hekima ana faida kuliko fedha

na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.

15 Hekima ana thamani kuliko marijani;

hakuna chochote unachokitamani

kinachoweza kulinganishwa naye.

16 Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume;

katika mkono wake wa kushoto

kuna utajiri na heshima.

17 Njia zake zinapendeza,

mapito yake yote ni amani.

18 Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia;

wale wamshikao watabarikiwa.

19 Kwa hekimaBwanaaliiweka misingi ya dunia,

kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;

20 kwa maarifa yake vilindi viligawanywa,

nayo mawingu yanadondosha umande.

21 Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara,

usiache vitoke machoni pako;

22 ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako

na pambo la neema shingoni mwako.

23 Kisha utaenda katika njia yako salama,

wala mguu wako hautajikwaa;

24 ulalapo, hautaogopa;

ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.

25 Usiogope maafa ya ghafula

au maangamizi yanayowapata waovu,

26 kwa kuwaBwanaatakuwa tumaini lako

na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.

27 Usizuie wema kwa wale wanaostahili

ikiwa katika uwezo wako kutenda.

28 Usimwambie jirani yako,

“Njoo baadaye, nitakupa kesho”:

wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.

29 Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako,

ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.

30 Usimshtaki mtu bila sababu,

wakati hajakutenda dhara lolote.

31 Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri

wala kuchagua njia yake iwayo yote,

32 kwa kuwaBwanahumchukia mtu mpotovu,

lakini siri yake iko kwa mwenye haki.

33 Laana yaBwanai juu ya nyumba ya mwovu,

lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.

34 Huwadhihaki wale wanaodhihaki,

lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.

35 Wenye hekima hurithi heshima,

bali huwaaibisha wapumbavu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PRO/3-0d7d31ecef474efe5f9e52c71d027fe1.mp3?version_id=1627—

Categories
Mithali

Mithali 4

Hekima Ni Bora Kupita Vitu Vyote

1 Sikilizeni wanangu, mafundisho ya baba yenu;

sikilizeni kwa makini na mpate ufahamu.

2 Ninawapa mafundisho ya maana,

kwa hiyo msiyaache mafundisho yangu.

3 Nilipokuwa mvulana mdogo katika nyumba ya baba yangu,

ningali mchanga na mtoto pekee kwa mama yangu,

4 baba alinifundisha akisema,

“Yashike maneno yangu yote kwa moyo wako wote;

yashike maagizo yangu na wewe utaishi.

5 Pata hekima, pata ufahamu;

usiyasahau maneno yangu wala usiyaache.

6 Usimwache hekima naye atakuweka salama;

mpende, naye atakulinda.

7 Hekima ni bora kuliko vitu vyote; kwa hiyo jipe hekima.

Hata ikikugharimu vyote ulivyo navyo, pata ufahamu.

8 Mstahi, naye atakukweza;

mkumbatie, naye atakuheshimu.

9 Atakuvika shada la neema kichwani mwako

na kukupa taji ya utukufu.”

10 Sikiliza mwanangu, kubali ninachokuambia,

nayo miaka ya maisha yako itakuwa mingi.

11 Ninakuongoza katika njia ya hekima

na kukuongoza katika mapito yaliyonyooka.

12 Utembeapo, hatua zako hazitazuiliwa;

ukimbiapo, hutajikwaa.

13 Mkamate sana elimu, usimwache aende zake;

mshike, maana yeye ni uzima wako.

14 Usiuweke mguu wako katika njia ya waovu

wala usitembee katika njia ya watu wabaya.

15 Epukana nayo, usisafiri katika njia hiyo;

achana nayo, na uelekee njia yako.

16 Kwa kuwa hawawezi kulala mpaka watende uovu;

wanashindwa hata kusinzia mpaka wamwangushe mtu.

17 Wanakula mkate wa uovu,

na kunywa mvinyo wa jeuri.

18 Njia ya wenye haki ni kama nuru ya kwanza ya mapambazuko,

ambayo hungʼaa zaidi na zaidi mpaka mchana mkamilifu.

19 Lakini njia ya waovu ni kama giza nene;

hawajui kinachowafanya wajikwae.

20 Mwanangu, yasikilize kwa makini yale ninayokuambia;

sikiliza kwa makini maneno yangu.

21 Usiruhusu yaondoke machoni pako,

yahifadhi ndani ya moyo wako;

22 kwa sababu ni uzima kwa wale wanaoyapata

na afya kwa mwili wote wa mwanadamu.

23 Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo,

maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.

24 Epusha kinywa chako na ukaidi;

weka mazungumzo machafu mbali na midomo yako.

25 Macho yako na yatazame mbele,

kaza macho yako moja kwa moja mbele yako.

26 Sawazisha mapito ya miguu yako

na njia zako zote ziwe zimethibitika.

27 Usigeuke kulia wala kushoto;

epusha mguu wako na ubaya.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PRO/4-b76a8a3d6bf6eda8ca51a36517ab8650.mp3?version_id=1627—

Categories
Mithali

Mithali 5

Onyo Dhidi Ya Uzinzi

1 Mwanangu, sikiliza kwa makini hekima yangu,

sikiliza vizuri maneno yangu ya busara,

2 ili uweze kutunza busara

na midomo yako ihifadhi maarifa.

3 Kwa maana midomo ya mwanamke kahaba

hudondoza asali,

na maneno ya kinywa chake

ni laini kuliko mafuta;

4 lakini mwisho wake ni mchungu kama nyongo,

mkali kama upanga ukatao kuwili.

5 Miguu yake hushuka kuelekea kwenye kifo;

hatua zake huelekea moja kwa moja kaburini.

6 Yeye hafikiri juu ya njia ya uzima;

njia zake zimepotoka, lakini yeye hajui.

7 Sasa basi wanangu, nisikilizeni;

msiache ninalowaambia.

8 Njia zenu ziwe mbali naye,

msiende karibu na mlango wa nyumba yake,

9 usije ukatoa nguvu zako nzuri kwa wengine

na miaka yako kwa aliye mkatili,

10 wageni wasije wakasherehekea utajiri wako

na jitihada yako ikatajirisha

nyumba ya mwanaume mwingine.

11 Mwishoni mwa maisha yako utalia kwa uchungu,

wakati nyama na mwili wako vimechakaa.

12 Utasema, “Tazama jinsi gani nilivyochukia adhabu!

Tazama jinsi moyo wangu ulivyodharau maonyo!

13 Sikuwatii walimu wangu

wala kuwasikiliza wakufunzi wangu.

14 Nimefika ukingoni mwa maangamizi kabisa

katikati ya kusanyiko lote.”

15 Kunywa maji kutoka kwenye kisima chako mwenyewe,

maji yanayotiririka kutoka kwenye kisima chako mwenyewe.

16 Je, chemchemi zako zifurike katika barabara za mji

na vijito vyako vya maji viwanjani?

17 Na viwe vyako mwenyewe,

kamwe visishirikishwe wageni.

18 Chemchemi yako na ibarikiwe

na umfurahie mke wa ujana wako.

19 Kulungu jike apendaye, kulungu mzuri:

matiti yake na yakutosheleze siku zote,

nawe utekwe daima na upendo wake.

20 Kwa nini mwanangu, utekwe na mwanamke kahaba?

Kwa nini ukumbatie kifua cha mke wa mwanaume mwingine?

21 Kwa maana njia za mtu ni wazi kabisa mbele zaBwana,

naye huyapima mapito yake yote.

22 Matendo mabaya ya mtu mwovu humnasa yeye mwenyewe;

kamba za dhambi yake humkamata kwa nguvu.

23 Atakufa kwa kukosa nidhamu,

akipotoshwa kwa upumbavu wake mwenyewe.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PRO/5-ec7bece217996f84309c7493d7146286.mp3?version_id=1627—

Categories
Mithali

Mithali 6

Maonyo Dhidi Ya Upumbavu

1 Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako,

ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi

kwa ajili ya mwingine,

2 kama umetegwa na ulichosema,

umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,

3 basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru,

kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako:

Nenda ukajinyenyekeshe kwake;

msihi jirani yako!

4 Usiruhusu usingizi machoni pako,

usiruhusu kope zako zisinzie.

5 Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji,

kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.

6 Ewe mvivu, mwendee mchwa;

zitafakari njia zake ukapate hekima!

7 Kwa maana yeye hana msimamizi,

wala mwangalizi, au mtawala,

8 lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi

na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.

9 Ewe mvivu, utalala hata lini?

Utaamka lini kutoka usingizi wako?

10 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo,

bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:

11 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi,

na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.

12 Mtu mbaya sana na mlaghai,

ambaye huzungukazunguka

na maneno ya upotovu,

13 ambaye anakonyeza kwa jicho lake,

anayetoa ishara kwa miguu yake

na kuashiria kwa vidole vyake,

14 ambaye hupanga ubaya

kwa udanganyifu moyoni mwake:

daima huchochea fitina.

15 Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula;

ataangamizwa mara, pasipo msaada.

16 Kuna vitu sita anavyovichukiaBwana,

naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:

17 macho ya kiburi,

ulimi udanganyao,

mikono imwagayo damu isiyo na hatia,

18 moyo uwazao mipango miovu,

miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,

19 shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo,

na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.

Onyo Dhidi Ya Uasherati

20 Mwanangu, zishike amri za baba yako,

wala usiyaache mafundisho ya mama yako.

21 Yafunge katika moyo wako daima,

yakaze kuizunguka shingo yako.

22 Wakati utembeapo, yatakuongoza;

wakati ulalapo, yatakulinda;

wakati uamkapo, yatazungumza nawe.

23 Kwa maana amri hizi ni taa,

mafundisho haya ni mwanga

na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,

24 yakikulinda na mwanamke aliyepotoka,

kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.

25 Moyo wako usitamani uzuri wake

wala macho yake yasikuteke,

26 kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini,

hata ukose kipande cha mkate,

naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.

27 Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake

bila nguo zake kuungua?

28 Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka

bila miguu yake kuungua?

29 Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine;

hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.

30 Watu hawamdharau mwizi kama akiiba

kukidhi njaa yake wakati ana njaa.

31 Pamoja na hayo, kama akikamatwa,

lazima alipe mara saba,

ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.

32 Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa;

yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.

33 Mapigo na aibu ni fungu lake

na aibu yake haitafutika kamwe;

34 kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume,

naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.

35 Hatakubali fidia yoyote;

atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PRO/6-a4b3c022120d52ef14e70a88c5e20644.mp3?version_id=1627—

Categories
Mithali

Mithali 7

Onyo Dhidi Ya Mwanamke Mzinzi

1 Mwanangu, shika maneno yangu

na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.

2 Shika amri zangu nawe utaishi;

linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.

3 Yafunge katika vidole vyako;

yaandike katika kibao cha moyo wako.

4 Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,”

uite ufahamu jamaa yako;

5 watakuepusha na mwanamke mzinzi,

kutokana na mwanamke mpotovu

na maneno yake ya kubembeleza.

6 Kwenye dirisha la nyumba yangu

nilitazama nje kupitia upenyo

kwenye mwimo wa dirisha.

7 Niliona miongoni mwa wajinga,

nikagundua miongoni mwa wanaume vijana,

kijana asiye na akili.

8 Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake,

akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke

9 wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake,

giza la usiku lilipokuwa likiingia.

10 Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki,

hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.

11 (Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi,

miguu yake haitulii nyumbani;

12 mara kwenye barabara za mji,

mara kwenye viwanja vikubwa,

kwenye kila pembe huvizia.)

13 Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu,

na kwa uso usio na haya akamwambia:

14 “Nina sadaka za amani nyumbani;

leo nimetimiza nadhiri zangu.

15 Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki;

nimekutafuta na nimekupata!

16 Nimetandika kitanda changu

kwa kitani za rangi kutoka Misri.

17 Nimetia manukato kitanda changu

kwa manemane, udi na mdalasini.

18 Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi;

tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!

19 Mume wangu hayupo nyumbani;

amekwenda safari ya mbali.

20 Amechukua mkoba uliojazwa fedha

na hatakuwepo nyumbani karibuni.”

21 Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha;

alimshawishi kwa maneno yake laini.

22 Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke

kama fahali aendaye machinjoni,

kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,

23 mpaka mshale umchome ini lake,

kama ndege anayenaswa kwenye mtego,

bila kujua itamgharimu maisha yake.

24 Sasa basi wanangu, nisikilizeni;

sikilizeni kwa makini nisemalo.

25 Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke,

wala usitangetange katika mapito yake.

26 Aliowaangusha ni wengi;

aliowachinja ni kundi kubwa.

27 Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini,

ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PRO/7-462699024114165a2f98ded840077133.mp3?version_id=1627—

Categories
Mithali

Mithali 8

Wito Wa Hekima

1 Je, hekima haitani?

Je, ufahamu hapazi sauti?

2 Juu ya miinuko karibu na njia,

penye njia panda, ndipo asimamapo;

3 kando ya malango yaelekeayo mjini,

kwenye maingilio, hulia kwa sauti kubwa, akisema:

4 “Ni ninyi wanaume, ninaowaita;

ninapaza sauti yangu kwa wanadamu wote.

5 Ninyi ambao ni wajinga, pateni akili;

ninyi mlio wapumbavu, pateni ufahamu.

6 Sikilizeni, kwa maana nina mambo muhimu ya kusema;

ninafungua midomo yangu kusema lililo sawa.

7 Kinywa changu husema lililo kweli,

kwa maana midomo yangu huchukia uovu.

8 Maneno yote ya kinywa changu ni haki;

hakuna mojawapo lililopotoka wala ukaidi.

9 Kwa wenye kupambanua yote ni sahihi;

hayana kasoro kwa wale wenye maarifa.

10 Chagua mafundisho yangu badala ya fedha,

maarifa badala ya dhahabu safi,

11 kwa maana hekima ina thamani kuliko marijani

na hakuna chochote unachohitaji kinacholingana naye.

12 “Mimi hekima, nakaa pamoja na busara;

ninamiliki maarifa na busara.

13 KumchaBwanani kuchukia uovu;

ninachukia kiburi na majivuno,

tabia mbaya na mazungumzo potovu.

14 Ushauri na hukumu sahihi ni vyangu;

nina ufahamu na nina nguvu.

15 Kwa msaada wangu wafalme hutawala

na watawala hutunga sheria zilizo za haki,

16 kwa msaada wangu wakuu hutawala,

na wenye vyeo wote watawalao dunia.

17 Nawapenda wale wanipendao,

na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.

18 Utajiri na heshima viko kwangu,

utajiri udumuo na mafanikio.

19 Tunda langu ni bora kuliko dhahabu safi;

kile nitoacho hupita fedha iliyo bora.

20 Natembea katika njia ya unyofu

katika mapito ya haki,

21 nawapa utajiri wale wanipendao

na kuzijaza hazina zao.

22 “Bwanaaliniumba mwanzoni mwa kazi yake,

kabla ya matendo yake ya zamani;

23 niliteuliwa tangu milele,

tangu mwanzoni, kabla ya dunia kuumbwa.

24 Wakati hazijakuwepo bahari, nilikwishazaliwa,

wakati hazijakuwepo chemchemi zilizojaa maji;

25 kabla milima haijawekwa mahali pake,

kabla vilima havijakuwepo, nilikwishazaliwa,

26 kabla hajaumba dunia wala mashamba yake

au vumbi lolote la dunia.

27 Nilikuwepo alipoziweka mbingu mahali pake,

wakati alichora mstari wa upeo wa macho

juu ya uso wa kilindi,

28 wakati aliweka mawingu juu

na kuziweka imara chemchemi za bahari,

29 wakati aliiwekea bahari mpaka wake

ili maji yasivunje agizo lake,

na wakati aliweka misingi ya dunia.

30 Wakati huo nilikuwa fundi stadi kando yake.

Nilijazwa na furaha siku baada ya siku,

nikifurahi daima mbele zake,

31 nikifurahi katika dunia yake yote

nami nikiwafurahia wanadamu.

32 “Basi sasa wanangu, nisikilizeni;

heri wale wanaozishika njia zangu.

33 Sikilizeni mafundisho yangu mwe na hekima;

msiyapuuze.

34 Heri mtu yule anisikilizaye mimi,

akisubiri siku zote malangoni mwangu,

akingoja kwenye vizingiti vya mlango wangu.

35 Kwa maana yeyote anipataye mimi amepata uzima

na kujipatia kibali kutoka kwaBwana.

36 Lakini yeyote ashindwaye kunipata

hujiumiza mwenyewe;

na wote wanichukiao mimi hupenda mauti.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PRO/8-d4c99cb9aea433eb7256382a216b2dca.mp3?version_id=1627—

Categories
Mithali

Mithali 9

Makaribisho Ya Hekima Na Ya Upumbavu

1 Hekima amejenga nyumba yake;

amechonga nguzo zake saba.

2 Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake;

pia ameandaa meza yake.

3 Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita

kutoka mahali pa juu sana pa mji.

4 Anawaambia wale wasio na akili,

“Wote ambao ni wajinga na waje hapa!

5 Njooni, mle chakula changu

na mnywe divai niliyoichanganya.

6 Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi;

tembeeni katika njia ya ufahamu.

7 “Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha

hukaribisha matukano;

yeyote anayekemea mtu mwovu

hupatwa na matusi.

8 Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia;

mkemee mwenye hekima naye atakupenda.

9 Mfundishe mtu mwenye hekima

naye atakuwa na hekima zaidi;

mfundishe mtu mwadilifu

naye atazidi kufundishika.

10 “KumchaBwanandicho chanzo cha hekima,

na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.

11 Kwa maana kwa msaada wangu

siku zako zitakuwa nyingi,

na miaka itaongezwa katika maisha yako.

12 Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo;

kama wewe ni mtu wa mzaha,

wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”

13 Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele;

hana adabu na hana maarifa.

14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake,

juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,

15 akiita wale wapitao karibu,

waendao moja kwa moja kwenye njia yao.

16 Anawaambia wale wasio na akili,

“Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”

17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu;

chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”

18 Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo,

kwamba wageni wake huyo mwanamke

wako katika vilindi vya kuzimu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PRO/9-c3a87b1a9f5e783705bc603cfc14739d.mp3?version_id=1627—

Categories
Mithali

Mithali 10

Mithali Za Solomoni

1 Mithali za Solomoni:

Mwana mwenye hekima

huleta furaha kwa baba yake,

lakini mwana mpumbavu

huleta huzuni kwa mama yake.

2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai,

lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.

3 Bwanahawaachi waadilifu kukaa njaa,

lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.

4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini

lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.

5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi

ni mwana mwenye hekima,

lakini yeye alalaye wakati wa mavuno

ni mwana mwenye kuaibisha.

6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki,

lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.

7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka,

lakini jina la mwovu litaoza.

8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo,

lakini mpumbavu apayukaye huangamia.

9 Mtu mwadilifu hutembea salama,

lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.

10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni,

naye mpumbavu apayukaye huangamia.

11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima,

lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.

12 Chuki huchochea faraka,

lakini upendo husitiri mabaya yote.

13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua,

lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.

14 Wenye hekima huhifadhi maarifa,

bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.

15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome,

bali ufukara ni maangamizi ya maskini.

16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima,

lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.

17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima,

lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.

18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo,

na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.

19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani,

lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.

20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora,

bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.

21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi,

lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.

22 Baraka yaBwanahutajirisha,

wala haichanganyi huzuni.

23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya,

lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.

24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata;

kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.

25 Tufani inapopita, waovu hutoweka,

lakini wenye haki husimama imara milele.

26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho,

ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.

27 KumchaBwanahuongeza urefu wa maisha,

lakini miaka ya mwovu inafupishwa.

28 Tarajio la mwenye haki ni furaha,

bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.

29 Njia yaBwanani kimbilio kwa wenye haki,

lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.

30 Kamwe wenye haki hawataondolewa,

bali waovu hawatasalia katika nchi.

31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima,

bali ulimi wa upotovu utakatwa.

32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa,

bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PRO/10-5250544be7804d87ab7f98988d8167e9.mp3?version_id=1627—

Categories
Mithali

Mithali 11

1 Bwanahuchukia sana mizani za udanganyifu,

bali vipimo sahihi ni furaha yake.

2 Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu,

bali unyenyekevu huja na hekima.

3 Uadilifu wa wenye haki huwaongoza,

bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.

4 Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu,

bali haki huokoa kutoka mautini.

5 Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka,

bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.

6 Haki ya wanyofu huwaokoa,

bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.

7 Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka;

yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.

8 Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu,

naye mtu mwovu huingia humo badala yake.

9 Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu

humwangamiza jirani yake,

bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.

10 Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi;

mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.

11 Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa,

bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.

12 Mtu asiye na akili humdharau jirani yake,

bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.

13 Masengenyo husaliti tumaini,

bali mtu mwaminifu hutunza siri.

14 Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka,

bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.

15 Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka,

bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.

16 Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima,

bali wanaume wakorofi hupata mali tu.

17 Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe,

bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.

18 Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu,

bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.

19 Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima,

bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.

20 Bwanahuwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu,

bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.

21 Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa,

bali wenye haki watakuwa huru.

22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe

ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.

23 Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema,

bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.

24 Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi,

mwingine huzuia, lakini huwa maskini.

25 Mtu mkarimu atastawi;

yeye awaburudishaye wengine

ataburudishwa mwenyewe.

26 Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka,

bali baraka itamkalia kichwani kama taji

yeye aliye radhi kuiuza.

27 Yeye atafutaye mema hupata ukarimu,

bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.

28 Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka,

bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.

29 Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo,

naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.

30 Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima,

naye mwenye hekima huvuta roho za watu.

31 Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani,

si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PRO/11-81584545fab6ddaa41d75fc3209ba4c1.mp3?version_id=1627—

Categories
Mithali

Mithali 12

Mafundisho Ya Kifamilia Na Ya Kijamii

1 Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa,

bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.

2 Mtu mwema hupata kibali kutoka kwaBwana,

baliBwanahumhukumu mwenye hila.

3 Mtu hathibitiki kutokana na uovu,

bali mwenye haki hataondolewa.

4 Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe,

bali aaibishaye ni kama uozo

katika mifupa ya mumewe.

5 Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki,

bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.

6 Maneno ya waovu huotea kumwaga damu,

bali maneno ya waadilifu huwaokoa.

7 Watu waovu huondolewa na kutoweka,

bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.

8 Mtu husifiwa kulingana na hekima yake,

bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.

9 Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi,

kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.

10 Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake,

bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.

11 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele,

bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.

12 Waovu hutamani mateka ya watu wabaya,

bali shina la mwenye haki hustawi.

13 Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi,

bali mwenye haki huepuka taabu.

14 Kutokana na tunda la midomo yake

mtu hujazwa na mambo mema,

hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.

15 Njia ya mpumbavu huonekana sawa

machoni pake mwenyewe,

bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.

16 Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja,

bali mtu wa busara hupuuza matukano.

17 Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika,

bali shahidi wa uongo husema uongo.

18 Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga,

bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.

19 Midomo isemayo kweli hudumu milele,

bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.

20 Upo udanganyifu katika mioyo

ya wale ambao hupanga mabaya,

bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.

21 Hakuna dhara linalompata mwenye haki,

bali waovu wana taabu nyingi.

22 Bwanaanachukia sana midomo idanganyayo,

bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.

23 Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe,

bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.

24 Mikono yenye bidii itatawala,

bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.

25 Moyo wa wasiwasi humlemea mtu,

bali neno la huruma humfurahisha.

26 Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki,

bali njia ya waovu huwapotosha.

27 Mtu mvivu haoki mawindo yake,

bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.

28 Katika njia ya haki kuna uzima;

katika mapito hayo kuna maisha ya milele.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PRO/12-c450a442ab8087f82a1232c137345f3a.mp3?version_id=1627—