Categories
Zaburi

Zaburi 144

Mfalme Amshukuru Mungu Kwa Ushindi

Zaburi ya Daudi.

1 Sifa ni kwaBwanaMwamba wangu,

aifundishaye mikono yangu vita,

na vidole vyangu kupigana.

2 Yeye ni Mungu wangu wa upendo na boma langu,

ngome yangu na mwokozi wangu,

ngao yangu ninayemkimbilia,

ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.

3 EeBwana, mwanadamu ni nini hata umjali,

Binadamu ni nini hata umfikirie?

4 Mwanadamu ni kama pumzi,

siku zake ni kama kivuli kinachopita.

5 EeBwana, pasua mbingu zako, ushuke,

gusa milima ili itoe moshi.

6 Peleka umeme uwatawanye adui,

lenga mishale yako uwashinde.

7 Nyoosha mkono wako kutoka juu,

nikomboe na kuniokoa

kutoka maji makuu,

kutoka mikononi mwa wageni

8 ambao vinywa vyao vimejaa uongo,

na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.

9 Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya,

kwa zeze yenye nyuzi kumi nitakuimbia,

10 kwa Yule awapaye wafalme ushindi,

ambaye humwokoa Daudi, mtumishi wake kutokana na upanga hatari.

11 Nikomboe na uniokoe

kutoka mikononi mwa wageni

ambao vinywa vyao vimejaa uongo,

na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.

12 Kisha wana wetu wakati wa ujana wao

watakuwa kama mimea iliyotunzwa vizuri,

binti zetu watakuwa kama nguzo zilizoviringwa

kurembesha jumba la kifalme.

13 Ghala zetu zitajazwa

aina zote za mahitaji.

Kondoo zetu watazaa kwa maelfu,

kwa makumi ya maelfu katika mashamba yetu;

14 maksai wetu watakokota

mizigo mizito.

Hakutakuwa na kubomoka kuta,

hakuna kuchukuliwa mateka,

wala kilio cha taabu

katika barabara zetu.

15 Heri watu ambao hili ni kweli;

heri wale ambaoBwanani Mungu wao.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/144-86d8063c5d30fe1a92aca97c91b2c345.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 145

Wimbo Wa Kusifu Ukuu Na Wema Wa Mungu

Wimbo wa Sifa. Wa Daudi.

1 Nitakutukuza wewe, Mungu wangu Mfalme,

nitalisifu jina lako milele na milele.

2 Kila siku nitakusifu

na kulitukuza jina lako milele na milele.

3 Bwanani mkuu, anayestahili kusifiwa sana,

ukuu wake haupimiki.

4 Kizazi kimoja kitasifia kazi zako kwa kizazi kingine,

watasimulia matendo yako makuu.

5 Watasema juu ya utukufu wa fahari ya ukuu wako,

nami nitatafakari juu ya kazi zako za ajabu.

6 Watasimulia uwezo wa kazi zako za kutisha,

nami nitatangaza matendo yako makuu.

7 Wataadhimisha wema wako mwingi,

na wataimba kwa shangwe juu ya haki yako.

8 Bwanani mwenye neema na mwingi wa huruma,

si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo.

9 Bwanani mwema kwa wote,

ana huruma kwa vyote alivyovifanya.

10 EeBwana, vyote ulivyovifanya vitakusifu,

watakatifu wako watakutukuza.

11 Watasimulia utukufu wa ufalme wako

na kusema juu ya ukuu wako,

12 ili watu wote wajue matendo yako makuu

na utukufu wa fahari ya ufalme wako.

13 Ufalme wako ni ufalme wa milele,

mamlaka yako hudumu vizazi vyote.

Bwanani mwaminifu kwa ahadi zake zote

na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.

14 Bwanahuwategemeza wote waangukao,

na huwainua wote waliolemewa na mizigo yao.

15 Macho yao wote yanakutazama wewe,

nawe huwapa chakula chao wakati wake.

16 Waufumbua mkono wako,

watosheleza haja ya kila kitu kilicho hai.

17 Bwanani mwenye haki katika njia zake zote,

na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.

18 Bwanayu karibu na wote wamwitao,

karibu na wote wamwitao kwa uaminifu.

19 Huwatimizia wamchao matakwa yao,

husikia kilio chao na kuwaokoa.

20 Bwanahuwalinda wote wampendao,

bali waovu wote atawaangamiza.

21 Kinywa changu kitazinena sifa zaBwana.

Kila kiumbe na kilisifu jina lake takatifu

milele na milele.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/145-926e00a6b42abbd14c4a202c1b1131c0.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 146

Kumsifu Mungu Mwokozi

1 MsifuniBwana!

Ee nafsi yangu, umsifuBwana,

2 NitamsifuBwanamaisha yangu yote;

nitamwimbia Mungu wangu sifa

wakati wote niishipo.

3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu,

kwa wanadamu ambao hufa,

ambao hawawezi kuokoa.

4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini,

siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.

5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake,

ambaye tumaini lake ni katikaBwana, Mungu wake,

6 Muumba wa mbingu na nchi,

na bahari na vyote vilivyomo ndani yake:

Bwanaanayedumu kuwa mwaminifu

milele na milele.

7 Naye huwapatia haki walioonewa

na kuwapa wenye njaa chakula.

Bwanahuwaweka wafungwa huru,

8 Bwanahuwafumbua vipofu macho,

Bwanahuwainua waliolemewa na mizigo yao,

Bwanahuwapenda wenye haki.

9 Bwanahuwalinda wageni

na kuwategemeza yatima na wajane,

lakini hupinga njia za waovu.

10 Bwanaatamiliki milele,

Mungu wako, ee Sayuni,

kwa vizazi vyote.

MsifuniBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/146-95c39d5fcce9e781a19eaaf806aab6ef.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 147

Kumsifu Mungu Mwenye Nguvu Zote

1 MsifuniBwana.

Tazama jinsi ilivyo vyema kumwimbia Mungu wetu sifa,

jinsi inavyopendeza na kustahili kumsifu yeye!

2 Bwanahujenga Yerusalemu,

huwakusanya Israeli walio uhamishoni.

3 Anawaponya waliovunjika mioyo

na kuvifunga vidonda vyao.

4 Huzihesabu nyota

na huipa kila moja jina lake.

5 Bwana wetu ni mkuu na mwenye uwezo mwingi,

ufahamu wake hauna kikomo.

6 Bwanahuwahifadhi wanyenyekevu

lakini huwashusha waovu mpaka mavumbini.

7 MwimbieniBwanakwa shukrani,

mpigieni Mungu wetu kinubi.

8 Yeye huzifunika anga kwa mawingu,

huinyeshea ardhi mvua,

na kuzifanya nyasi kuota juu ya vilima.

9 Huwapa chakula mifugo

na pia makinda ya kunguru yanapolia.

10 Furaha yake haipo katika nguvu za farasi,

wala furaha yake kwenye miguu ya mwanadamu.

11 Bwanahupendezwa na wale wamchao,

wale wanaoweka tumaini lao katika upendo wake usiokoma.

12 MtukuzeBwana, ee Yerusalemu,

msifu Mungu wako, ee Sayuni,

13 kwa maana huimarisha makomeo ya malango yako

na huwabariki watu wako walio ndani yako.

14 Huwapa amani mipakani mwenu

na kukushibisha kwa ngano safi kabisa.

15 Hutuma amri yake duniani,

neno lake hukimbia kasi.

16 Anatandaza theluji kama sufu

na kutawanya umande kama majivu.

17 Huvurumisha mvua yake ya mawe kama changarawe.

Ni nani awezaye kustahimili ukali wa baridi yake?

18 Hutuma neno lake na kuviyeyusha,

huvumisha upepo wake, nayo maji hutiririka.

19 Amemfunulia Yakobo neno lake,

sheria zake na maagizo yake kwa Israeli.

20 Hajafanya hivyo kwa taifa lingine lolote,

hawazijui sheria zake.

MsifuniBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/147-6ec7e09cc3e3b2da07364666932b199b.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 148

Mwito Kwa Ulimwengu Kumsifu Mungu

1 MsifuniBwana.

MsifuniBwanakutoka mbinguni,

msifuni juu vileleni.

2 Msifuni, enyi malaika wake wote,

msifuni yeye, enyi jeshi lake lote la mbinguni.

3 Msifuni yeye, enyi jua na mwezi,

msifuni yeye, enyi nyota zote zingʼaazo.

4 Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu sana,

na ninyi maji juu ya anga.

5 Vilisifu jina laBwana

kwa maana aliamuru navyo vikaumbwa.

6 Aliviweka mahali pake milele na milele,

alitoa amri ambayo haibadiliki milele.

7 MtukuzeniBwanakutoka duniani,

ninyi viumbe vikubwa vya baharini na vilindi vyote vya bahari,

8 umeme wa radi na mvua ya mawe, theluji na mawingu,

pepo za dhoruba zinazofanya amri zake,

9 ninyi milima na vilima vyote,

miti ya matunda na mierezi yote,

10 wanyama wa mwituni na mifugo yote,

viumbe vidogo na ndege warukao,

11 wafalme wa dunia na mataifa yote,

ninyi wakuu na watawala wote wa dunia,

12 wanaume vijana na wanawali,

wazee na watoto.

13 Wote na walisifu jina laBwana,

kwa maana jina lake pekee limetukuka,

utukufu wake uko juu ya nchi na mbingu.

14 Amewainulia watu wake pembe,

sifa ya watakatifu wake wote,

ya Israeli, watu walio karibu na moyo wake.

MsifuniBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/148-41b131ad3ce27044f048b5cc8f4781ee.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 149

Wimbo Wa Kumsifu Mungu Kwa Wema Wake

1 MsifuniBwana.

MwimbieniBwanawimbo mpya,

sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.

2 Israeli na washangilie katika Muumba wao,

watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.

3 Na walisifu jina lake kwa kucheza

na wampigie muziki kwa matari na kinubi.

4 Kwa maanaBwanaanapendezwa na watu wake,

anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.

5 Watakatifu washangilie katika heshima hii,

na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.

6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao

na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,

7 ili walipize mataifa kisasi

na adhabu juu ya mataifa,

8 wawafunge wafalme wao kwa minyororo,

wakuu wao kwa pingu za chuma,

9 ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao.

Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote.

MsifuniBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/149-61e7d4fbad63268e796907d56d248b66.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 150

Msifuni Bwana Kwa Ukuu Wake

1 MsifuniBwana.

Msifuni Mungu katika patakatifu pake,

msifuni katika mbingu zake kuu.

2 Msifuni kwa matendo yake makuu,

msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

3 Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta,

msifuni kwa kinubi na zeze,

4 msifuni kwa matari na kucheza,

msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,

5 msifuni kwa matoazi yaliayo,

msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6 Kila chenye pumzi na kimsifuBwana.

MsifuniBwana!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/150-cc95c5b1e920e3320c0de853056acb58.mp3?version_id=1627—

Categories
Mithali

Mithali Utangulizi

Utangulizi

Neno la Kiebrania ni “Mashal”; ndilo lililotafsiriwa “Mithali” na lina maana nyingine zaidi, yaani “Mapokeo,” “Mafumbo,” au “Semi za hekima.” Hivyo Mithali ni mkusanyiko wa semi nyingi za hekima, na mambo kuhusu maisha ya busara na haki ya kila siku. Kitabu hiki kinatoa mafundisho yenye mafumbo ambayo yalikuwa ya kawaida katika eneo la Mashariki ya Kati ya zamani. Hekima yake ni ya kipekee kwa sababu imeelezwa katika mtazamo wa Mungu na viegezo vyake vya haki kwa ajili ya watu wake wa Agano. Kama vile Daudi alivyo chimbuko la Zaburi katika Israeli, ndivyo Solomoni alivyo chimbuko la hekima katika Israeli (

1:1

10:1

25:1

).

Mwandishi

Solomoni, Aguri mwana wa Yake, Mfalme Lemueli, na wenye hekima ambao majina yao hayakutajwa; zilikusanywa pamoja na Mfalme Hezekia.

Kusudi

Kusudi la kitabu hiki ni kuwafundisha watu jinsi ya kupata hekima, adabu njema na maisha ya uadilifu, jinsi ya kufanya vitu katika njia sahihi na ya haki, na njia inayompendeza Mungu.

Mahali

Yerusalemu.

Tarehe

Zilikusanywa pamoja na Mfalme Hezekia kati ya 715–686 K.K.

Wahusika Wakuu

Solomoni, Aguri na Lemueli.

Wazo Kuu

Kumjua Mungu ndio mwanzo wa hekima.

Mambo Muhimu

Kati ya mambo muhimu ambayo yameorodheshwa katika kitabu hiki ni: Vijana na nidhamu, familia, kumjua Mungu, ndoa, kufahamu ukweli na hekima.

Mgawanyo

Maelezo juu ya hekima na upumbavu (

1:1–9:18

)

Mithali za Solomoni (

10:1–22:16

)

Mithali za wengine wenye hekima (

22:17–24:34

)

Mithali nyingine za Solomoni (

25:1–29:27

)

Mithali za Aguri na Lemueli (

30:1–31:31

).

Categories
Mithali

Mithali 1

Utangulizi: Kusudi Na Kiini

1 Mithali za Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:

2 Kwa kupata hekima na nidhamu;

kwa kufahamu maneno ya busara;

3 kwa kujipatia nidhamu na busara,

kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;

4 huwapa busara wajinga,

maarifa na akili kwa vijana;

5 wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao,

wenye kupambanua na wapate mwongozo;

6 kwa kufahamu mithali na mifano,

misemo na vitendawili vya wenye hekima.

7 KumchaBwanandicho chanzo cha maarifa,

lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.

Onyo Dhidi Ya Ushawishi Wa Marafiki Waovu

8 Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako,

wala usiyaache mafundisho ya mama yako.

9 Hayo yatakuwa taji la maua la neema kichwani pako,

na mkufu wa kuipamba shingo yako.

10 Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi,

usikubaliane nao.

11 Kama wakisema, “Twende tufuatane;

tukamvizie mtu na kumwaga damu,

njoo tukavizie nafsi isiyo na hatia;

12 tuwameze wakiwa hai kama kaburi,

wakiwa wazima kama wale wanaotumbukia shimoni.

13 Tutapata aina zote za vitu vya thamani

na kujaza nyumba zetu kwa nyara.

14 Njoo ushirikiane nasi,

vitu vyote tutakavyopata tutagawana.”

15 Mwanangu, usiandamane nao.

Usiweke mguu wako katika njia zao,

16 kwa kuwa miguu yao hukimbilia kwenye dhambi,

ni wepesi kumwaga damu.

17 Tazama ni jinsi gani ilivyo kazi bure kutandaza wavu

wakati ndege wote wanakuona!

18 Watu hawa huvizia kumwaga damu yao wenyewe;

hujivizia tu wenyewe!

19 Huu ndio mwisho wa wote ambao wanajipatia mali kwa hila;

huuondoa uhai wa wale wenye mali.

Onyo Dhidi Ya Kukataa Hekima

20 Hekima huita kwa sauti kuu barabarani,

hupaza sauti yake kwenye viwanja vikubwa;

21 kwenye makutano ya barabara za mji

zenye makelele mengi hupaza sauti,

kwenye malango ya mji hutoa hotuba yake:

22 “Enyi wajinga, mtangʼangʼania ujinga wenu hadi lini?

Mpaka lini wenye mizaha watafurahia mizaha,

na wapumbavu kuchukia maarifa?

23 Kama mngekuwa mmeitikia karipio langu,

ningekuwa nimemimina roho yangu kwenu

na kuwafahamisha maneno yangu.

24 Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita

na hakuna yeyote aliyekubali

niliponyoosha mkono wangu,

25 kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote

na hamkukubali karipio langu,

26 mimi nami nitawacheka katika maafa yenu,

nitawadhihaki wakati janga litawapata:

27 wakati janga litawapata kama tufani,

wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli,

wakati dhiki na taabu zitawalemea.

28 “Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu;

watanitafuta lakini hawatanipata.

29 Kwa kuwa walichukia maarifa,

wala hawakuchagua kumchaBwana,

30 kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu,

na kukataa maonyo yangu,

31 watakula matunda ya njia zao,

na watashibishwa matunda ya hila zao.

32 Kwa kuwa ukaidi wa wajinga utawaua,

nako kuridhika kwa wajinga kutawaangamiza.

33 Lakini yeyote anisikilizaye ataishi kwa usalama,

atatulia, bila kuwa na hofu ya madhara.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PRO/1-0b5742ff8c29a4403f401e70ecd2823c.mp3?version_id=1627—

Categories
Mithali

Mithali 2

Faida Za Hekima

1 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu

na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,

2 kutega sikio lako kwenye hekima

na kuweka moyo wako katika ufahamu,

3 na kama ukiita busara

na kuita kwa sauti ufahamu,

4 na kama utaitafuta kama fedha

na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,

5 ndipo utakapoelewa kumchaBwana

na kupata maarifa ya Mungu.

6 Kwa maanaBwanahutoa hekima,

na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.

7 Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu,

yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,

8 kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki

na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.

9 Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki

na sawa: yaani kila njia nzuri.

10 Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako,

nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.

11 Busara itakuhifadhi

na ufahamu utakulinda.

12 Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu,

kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,

13 wale waachao mapito yaliyonyooka

wakatembea katika njia za giza,

14 wale wapendao kutenda mabaya

na kufurahia upotovu wa ubaya,

15 ambao mapito yao yamepotoka

na ambao ni wapotovu katika njia zao.

16 Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba,

kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno

ya kushawishi kutenda ubaya,

17 aliyemwacha mwenzi wa ujana wake

na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.

18 Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo

na mapito yake kwenye roho za waliokufa.

19 Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi,

au kufikia mapito ya uzima.

20 Hivyo utatembea katika njia za watu wema

na kushikamana na mapito ya wenye haki.

21 Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi,

nao wasio na lawama watabakia ndani yake.

22 Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi,

nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PRO/2-ea08cd3b924427c425c645de0f3f04e9.mp3?version_id=1627—