Categories
Ayubu

Ayubu 37

1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka,

nao unaruka kutoka mahali pake.

2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake,

sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.

3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote

na kuupeleka hata miisho ya dunia.

4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake;

Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari.

Wakati sauti yake ingurumapo tena,

huuachilia umeme wake wa radi.

5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu;

yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.

6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’

nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’

7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake,

yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.

8 Wanyama hujificha;

hubakia kwenye mapango yao.

9 Dhoruba hutoka katika chumba chake,

baridi hutoka katika upepo uendao kasi.

10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu,

eneo kubwa la maji huganda.

11 Huyasheheneza mawingu kwa maji,

naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.

12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake,

juu ya uso wa dunia yote,

kufanya lolote ayaamuruyo.

13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu,

au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.

14 “Ayubu, sikiliza hili;

nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.

15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu,

na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?

16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia,

hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?

17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako

wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,

18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga,

zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?

19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia;

hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.

20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea?

Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?

21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua,

jinsi linavyongʼaa angani,

upepo ukishafagia mawingu.

22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu;

Mungu huja katika utukufu wa kutisha.

23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza;

katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.

24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni,

kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOB/37-1ce551230e0e6b77be709801a1c6dde5.mp3?version_id=1627—

Categories
Ayubu

Ayubu 38

Bwana Anamjibu Ayubu

1 KishaBwanaakamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:

2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza

kwa maneno yasiyo na maarifa?

3 Jikaze kama mwanaume;

nitakuuliza swali,

nawe unijibu.

4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia?

Niambie, kama unafahamu.

5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake?

Hakika wewe unajua!

Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?

6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini,

au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,

7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja,

na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?

8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango

ilipopasuka kutoka tumbo,

9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake,

na kuyafungia katika giza nene,

10 nilipoamuru mipaka yake,

na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,

11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi;

hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?

12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke,

au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,

13 yapate kushika miisho ya dunia,

na kuwakungʼuta waovu waliomo?

14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri;

sura yake hukaa kama ile ya vazi.

15 Waovu huzuiliwa nuru yao,

nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.

16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari?

Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?

17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti?

Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?

18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia?

Niambie kama unajua haya yote.

19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi?

Nako maskani mwa giza ni wapi?

20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake?

Unajua njia za kufika maskani mwake?

21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa!

Kwani umeishi miaka mingi!

22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji,

au kuona ghala za mvua ya mawe,

23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu,

na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?

24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa,

au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?

25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi

na njia ya umeme wa radi,

26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu,

jangwa lisilo na yeyote ndani yake,

27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa,

na majani yaanze kumea ndani yake?

28 Je, mvua ina baba?

Ni nani baba azaaye matone ya umande?

29 Barafu inatoka tumbo la nani?

Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,

30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe,

wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?

31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia?

Waweza kulegeza kamba za Orioni?

32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake,

au kuongoza Dubu na watoto wake?

33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu?

Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?

34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni,

na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?

35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake?

Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?

36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima

au kuzipa akili ufahamu?

37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu?

Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni

38 wakati mavumbi yawapo magumu,

na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?

39 “Je, utamwindia simba jike mawindo,

na kuwashibisha simba wenye njaa

40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao,

au wakivizia kichakani?

41 Ni nani ampaye kunguru chakula

wakati makinda yake yanamlilia Mungu,

yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOB/38-7c604a5e83e01c6fdafe8560184cbdb2.mp3?version_id=1627—

Categories
Ayubu

Ayubu 39

1 “Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa?

Je, watambua ni wakati gani kulungu jike azaapo mtoto wake?

2 Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo?

Je, unajua majira yao ya kuzaa?

3 Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao;

utungu wa kuzaa unakoma.

4 Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani;

huenda zao wala hawarudi tena.

5 “Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru?

Ni nani aliyezifungua kamba zake?

6 Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake,

nchi ya chumvi kuwa makao yake.

7 Huzicheka ghasia za mji,

wala hasikii kelele za mwendesha gari.

8 Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho

na kutafuta kila kitu kibichi.

9 “Je, nyati atakubali kukutumikia?

Atakaa karibu na hori lako usiku?

10 Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba?

Je, atalima mabonde nyuma yako?

11 Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi?

Utamwachia yeye kazi zako nzito?

12 Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani

kutoka shambani na kuikusanya kwenye sakafu yako ya kupuria?

13 “Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha,

lakini hayawezi kulinganishwa

na mabawa na manyoya ya korongo.

14 Huyataga mayai yake juu ya ardhi,

na kuyaacha yapate joto mchangani,

15 bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda,

kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.

16 Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake;

hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,

17 kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima,

wala hakumpa fungu la akili njema.

18 Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia,

humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.

19 “Je, wewe humpa farasi nguvu

au kuivika shingo yake manyoya marefu?

20 Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige,

akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?

21 Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake,

husonga mbele kukabiliana na silaha.

22 Huicheka hofu, haogopi chochote,

wala haukimbii upanga.

23 Podo hutoa sauti kando yake,

pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.

24 Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi,

wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.

25 Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’

Hunusa harufu ya vita toka mbali,

sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.

26 “Je, mwewe huruka kwa hekima yako

na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?

27 Je, tai hupaa juu kwa amri yako

na kujenga kiota chake mahali pa juu?

28 Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku;

majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.

29 Kutoka huko hutafuta chakula chake;

macho yake hukiona kutoka mbali.

30 Makinda yake hujilisha damu,

na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOB/39-3de4d0f9a36a733ce63a94621bf3cc7a.mp3?version_id=1627—

Categories
Ayubu

Ayubu 40

1 Bwanaakamwambia Ayubu:

2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha?

Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”

3 Ndipo Ayubu akamjibuBwana:

4 “Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe?

Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.

5 Nimesema mara moja, lakini sina jibu;

naam, nimesema mara mbili,

lakini sitasema tena.”

6 NdipoBwanaakasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:

7 “Jikaze kama mwanaume;

nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.

8 “Je, utabatilisha hukumu yangu?

Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?

9 Je, una mkono kama wa Mungu,

nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?

10 Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari,

nawe uvae heshima na enzi.

11 Fungulia ukali wa ghadhabu yako,

mtafute kila mwenye kiburi umshushe,

12 mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze,

waponde waovu mahali wasimamapo.

13 Wazike wote mavumbini pamoja;

wafunge nyuso zao kaburini.

14 Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia

kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.

15 “Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi,

niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe,

anayekula majani kama ngʼombe.

16 Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake,

uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!

17 Mkia wake hutikisika kama mwerezi;

mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.

18 Mifupa yake ni bomba za shaba,

maungo yake ni kama fito za chuma.

19 Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu,

lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.

20 Vilima humletea yeye mazao yake,

nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.

21 Hulala chini ya mimea ya yungiyungi,

katika maficho ya matete kwenye matope.

22 Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake;

miti mirefu karibu na kijito humzunguka.

23 Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu;

yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.

24 Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho,

au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOB/40-9a82a235af97c35ef4e9bdfbd9bb1399.mp3?version_id=1627—

Categories
Ayubu

Ayubu 41

1 “Je, waweza kumvua Lewiathanikwa ndoano ya samaki,

au kufunga ulimi wake kwa kamba?

2 Waweza kupitisha kamba puani mwake,

au kutoboa taya lake kwa kulabu?

3 Je, ataendelea kukuomba umhurumie?

Atasema nawe maneno ya upole?

4 Je, atafanya agano nawe ili umtwae

awe mtumishi wako maisha yake yote?

5 Je, utamfuga na kumfanya rafiki kama ndege,

au kumfunga kamba kwa ajili ya wasichana wako?

6 Je, wafanyabiashara watabadilishana bidhaa kwa ajili yake?

Watamgawanya miongoni mwa wafanyao biashara?

7 Je, waweza kuijaza ngozi yake kwa vyuma vyenye ncha kali,

au kichwa chake kwa mkuki wa kuvulia samaki?

8 Kama ukiweka mkono wako juu yake,

utavikumbuka hivyo vita na kamwe hutarudia tena!

9 Tumaini lolote la kumtiisha ni kujidanganya;

kule kumwona tu kunamwangusha mtu chini.

10 Hakuna yeyote aliye mkali athubutuye kumchokoza.

Ni nani basi awezaye kusimama dhidi yangu?

11 Ni nani mwenye madai dhidi yangu ili nipate kumlipa?

Kila kitu kilicho chini ya mbingu ni mali yangu.

12 “Sitashindwa kunena juu ya maungo yake,

nguvu zake na umbo lake zuri.

13 Ni nani awezaye kumvua gamba lake la nje?

Ni nani awezaye kumsogelea na lijamu?

14 Nani athubutuye kuufungua mlango wa kinywa chake,

kilichozungukwa na meno yake ya kutisha pande zote?

15 Mgongo wake una safu za ngao

zilizoshikamanishwa imara pamoja;

16 kila moja iko karibu sana na mwenzake,

wala hakuna hewa iwezayo kupita kati yake.

17 Zimeunganishwa imara kila moja na nyingine;

zimengʼangʼaniana pamoja wala haziwezi kutenganishwa.

18 Akipiga chafya mwanga humetameta;

macho yake ni kama mionzi ya mapambazuko.

19 Mienge iwakayo humiminika kutoka kinywani mwake;

cheche za moto huruka nje.

20 Moshi hufuka kutoka puani mwake,

kama kutoka kwenye chungu kinachotokota kwa moto wa matete.

21 Pumzi yake huwasha makaa ya mawe,

nayo miali ya moto huruka kutoka kinywani mwake.

22 Nguvu hukaa katika shingo yake;

utisho hutangulia mbele yake.

23 Mikunjo ya nyama yake imeshikamana imara pamoja;

iko imara na haiwezi kuondolewa.

24 Kifua chake ni kigumu kama mwamba,

kigumu kama jiwe la chini la kusagia.

25 Ainukapo, mashujaa wanaogopa;

hurudi nyuma mbele yake anapokwenda kwa kishindo.

26 Upanga unaomfikia haumdhuru,

wala mkuki au mshale wala fumo.

27 Chuma hukiona kama unyasi,

na shaba kama mti uliooza.

28 Mishale haimfanyi yeye akimbie;

mawe ya kombeo kwake ni kama makapi.

29 Rungu kwake huwa kama kipande cha jani kavu;

hucheka sauti za kugongana kwa mkuki.

30 Sehemu zake za chini kwenye tumbo

zina menomeno na mapengo kama vigae vya chungu,

zikiacha mburuzo kwenye matope

kama chombo chenye meno cha kupuria.

31 Huvisukasuka vilindi kama sufuria kubwa ichemkayo,

na kukoroga bahari kama chungu cha marhamu.

32 Anapopita nyuma yake huacha mkondo unaometameta;

mtu angedhani vilindi vilikuwa na mvi.

33 Hakuna chochote duniani kinacholingana naye:

yeye ni kiumbe kisicho na woga.

34 Yeye huwatazama chini wale wote wenye kujivuna;

yeye ni mfalme juu ya wote wenye kiburi.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOB/41-b80ee188812911100ed0a7552396d5a7.mp3?version_id=1627—

Categories
Ayubu

Ayubu 42

Ayubu Anamjibu Bwana

1 Ndipo Ayubu akamjibuBwana:

2 “Ninajua ya kuwa unaweza kufanya mambo yote,

wala hakuna mpango wako unaoweza kuzuilika.

3 Uliuliza, ‘Ni nani huyu afichaye mashauri yangu bila maarifa?’

Hakika nilisema juu ya mambo niliyokuwa siyaelewi,

mambo ya ajabu mno kwangu mimi kuyajua.

4 “Ulisema, ‘Sikiliza sasa, nami nitanena;

nitakuuliza swali, nawe yakupasa kunijibu.’

5 Masikio yangu yalikuwa yamesikia habari zako,

lakini sasa macho yangu yamekuona.

6 Kwa hiyo najidharau mwenyewe,

na kutubu katika mavumbi na majivu.”

Mwisho: Marafiki Wa Ayubu Wanafedheheshwa

7 Baada yaBwanakusema mambo haya yote na Ayubu, akamwambia Elifazi Mtemani, “Nina hasira juu yako na juu ya rafiki zako wawili, kwa sababu hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.

8 Basi sasa chukueni mafahali saba na kondoo dume saba mkamwendee mtumishi wangu Ayubu nanyi mkatoe sadaka za kuteketezwa kwa ajili yenu wenyewe. Mtumishi wangu Ayubu ataomba kwa ajili yenu, nami nitayakubali maombi yake ili nisiwatendee sawasawa na upumbavu wenu. Ninyi hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.”

9 Kwa hiyo Elifazi Mtemani, Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi wakafanya kamaBwanaalivyowaambia; nayeBwanaakayakubali maombi ya Ayubu.

10 Baada ya Ayubu kuwaombea rafiki zake,Bwanaakamwondoa kwenye uteka, akamfanikisha tena naye akampa mara mbili ya vile alivyokuwa navyo hapo mwanzoni.

11 Ndipo ndugu zake wote waume kwa wake na kila mtu aliyemfahamu mwanzoni, wakaja wakala pamoja naye katika nyumba yake. Wakamfariji na kumtuliza moyo juu ya taabu yoteBwanaaliyoileta juu yake, nao kila mmoja akampa kipande cha fedha na pete ya dhahabu.

12 Bwanaakaibariki sehemu ya mwisho ya maisha ya Ayubu kuliko ile ya kwanza. Alikuwa na kondoo elfu kumi na nne, ngamia elfu sita, jozi za mafahali elfu moja, na punda wa kike elfu moja.

13 Tena alikuwa na wana saba na binti watatu.

14 Binti wa kwanza aliitwa Yemima, wa pili Kesia na wa tatu Keren-Hapuki.

15 Hapakuwepo mahali popote katika nchi ile yote palipopatikana wanawake wazuri kama binti za Ayubu; naye baba yao akawapa urithi pamoja na ndugu zao.

16 Baada ya hili Ayubu akaishi miaka 140; akawaona wanawe na wana wa wanawe hata kizazi cha nne.

17 Hivyo Ayubu akafa, akiwa mzee aliyekuwa ameshiba siku.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOB/42-f4f15620604b73cc5f955b360bb8d163.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi Utangulizi

Utangulizi

Jina la kitabu hiki kwa Kiebrania ni “Sepher Tehillim,” maana yake “Nyimbo za Sifa.” Jina la Kiyunani ni “Psalmoi,” yaani “Nyimbo zinazoandamana na ala za uimbaji za nyuzi,” na ndiyo kiini cha kitabu hiki. Kila sura ya 150 za kitabu hiki ni ya kipekee tena imekamilika, isipokuwa chache tu.

Zaburi zinaleta hisia mbalimbali kama vile misisimko, hali na mivuto mikubwa tofauti. Kwa kuwa Zaburi zinatokana na uzoefu wa kibinafsi kutoka asili pana hivyo, bado zimekuwa na mvuto mkubwa ulimwenguni wote kwa miaka mingi hivi tangu ziandikwe.

Mara kwa mara Zaburi zimeainishwa kwa kufuata namna fulani za maelezeo au mafundisho. Baadhi ya mapendekezo ya aina zenyewe, na mifano yake ambayo inaweza kuwa msaada mkubwa katika kujifunza zaidi ni kama ifuatavyo:

Kawaida ya ibada na sala

120–130

Kuhusu Masiya

2

16

22

25

69

110

Kuomba toba

6

32

51

Kumkaribia Mungu binafsi

23

27

37

Historia

78

105–106

Kumsifu Mungu

95

100

146–150

Maombi ya mwenye haki

17

20

40

55

Kuna uwezekano mkubwa kwamba makusanyo ya awali yalifanywa na Daudi. Nyongeza nyingine na mpangilio inawezekana vilifanywa na Solomoni, Yehoshafati, Hezekia, Yosia na wengine.

Mwandishi

Daudi: 73, Asafu: 12, Wana wa Kora: 10, Mose: 1, Hemani: 1, Ethani: 1, Solomoni: 2, Hazijulikani: 50.

Kusudi

Kuelezea umuhimu wa mashairi katika sifa, kuabudu na kukiri dhambi mbele za Mungu.

Mahali

Palestina na Babeli.

Tarehe

Kati ya wakati wa Mose (1440 K.K.) na wakati wa utumwa wa Babeli (586 K.K.).

Wahusika Wakuu

Daudi, Asafu, Wana wa Kora, Mose, Hemani na Solomoni.

Wazo Kuu

Kusifu ni kutambua na kutangaza ukuu wa Mungu, kufurahia na kudhihirisha wema wake.

Mambo Muhimu

Zaburi zimeelezea ufunuo wa Mungu, uumbaji, hali ya mwanadamu, wokovu, dhambi na uovu, toba, haki na uadilifu, kuabudu na kusifu, maombi na hukumu.

Mgawanyo

Kitabu I:

1–41

Kitabu II:

42–72

Kitabu III:

73–89

Kitabu IV:

90–106

Kitabu V:

107–150

.

Categories
Zaburi

Zaburi 1

Furaha Ya Kweli

1 Heri mtu yule ambaye

haendi katika shauri la watu waovu,

wala hasimami katika njia ya wenye dhambi,

au kuketi katika baraza la wenye mizaha.

2 Bali huifurahia sheria yaBwana,

naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.

3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa

kando ya vijito vya maji,

ambao huzaa matunda kwa majira yake

na majani yake hayanyauki.

Lolote afanyalo hufanikiwa.

Huzuni Ya Waovu

4 Sivyo walivyo waovu!

Wao ni kama makapi

yapeperushwayo na upepo.

5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu,

wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.

6 Kwa maanaBwanahuziangalia njia za mwenye haki,

bali njia ya waovu itaangamia.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/1-461588185b7df957126ca69dd341074d.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 2

Mfalme Aliyechaguliwa Na Mungu

1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya,

na kabila za watu kula njama bure?

2 Wafalme wa dunia wanajipanga

na watawala wanajikusanya pamoja

dhidi yaBwana

na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.

3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao

na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”

4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka,

Bwana huwadharau.

5 Kisha huwakemea katika hasira yake

na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,

6 “Nimemtawaza Mfalme wangu

juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”

Ushindi Wa Mfalme

7 Nitatangaza amri yaBwana:

Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu,

leo mimi nimekuzaa.

8 Niombe, nami nitayafanya mataifa

kuwa urithi wako,

miisho ya dunia kuwa milki yako.

9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma

na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”

10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima;

mwonyeke, enyi watawala wa dunia.

11 MtumikieniBwanakwa hofu

na mshangilie kwa kutetemeka.

12 Mbusu Mwana, asije akakasirika

nawe ukaangamizwa katika njia yako,

kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula.

Heri wote wanaomkimbilia.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/2-a11c6bc14963afae6c73d8884c7251e0.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 3

Sala Ya Asubuhi Ya Kuomba Msaada

Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu.

1 EeBwana, tazama adui zangu walivyo wengi!

Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!

2 Wengi wanasema juu yangu,

“Mungu hatamwokoa.”

3 Lakini wewe, EeBwana, ni ngao pande zote;

umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.

4 NinamliliaBwanakwa sauti kuu,

naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.

5 Ninajilaza na kupata usingizi;

naamka tena, kwa maanaBwanahunitegemeza.

6 Sitaogopa makumi elfu ya adui,

wanaojipanga dhidi yangu kila upande.

7 EeBwana, amka!

Niokoe, Ee Mungu wangu!

Wapige adui zangu wote kwenye taya,

vunja meno ya waovu.

8 Kwa maana wokovu watoka kwaBwana.

Baraka yako na iwe juu ya watu wako.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/3-02ebf1108eb4cf43d48b6134dc9a3fcb.mp3?version_id=1627—