Categories
Zaburi

Zaburi 80

Maombi Kwa Ajili Ya Kuponywa Kwa Taifa

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu.

1 Ee Mchungaji wa Israeli tusikie,

wewe umwongozaye Yosefu kama kundi;

wewe uketiye katika kiti cha enzi

katikati ya makerubi, angaza

2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase.

Uamshe nguvu zako,

uje utuokoe.

3 Ee Mungu, uturejeshe,

utuangazie uso wako,

ili tuweze kuokolewa.

4 EeBwanaMungu Mwenye Nguvu Zote,

hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi

dhidi ya maombi ya watu wako?

5 Umewalisha kwa mkate wa machozi,

umewafanya wanywe machozi bakuli tele.

6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu,

na adui zetu wanatudhihaki.

7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe;

utuangazie uso wako,

nasi tuweze kuokolewa.

8 Ulileta mzabibu kutoka Misri,

ukawafukuza mataifa, ukaupanda.

9 Uliandaa shamba kwa ajili yake,

mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.

10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake,

matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.

11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini,

machipukizi yake mpaka kwenye Mto.

12 Mbona umebomoa kuta zake

ili wote wapitao karibu

wazichume zabibu zake?

13 Nguruwe mwitu wanauharibu

na wanyama wa kondeni hujilisha humo.

14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote!

Tazama chini kutoka mbinguni na uone!

Linda mzabibu huu,

15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume,

mwana uliyemlea

kwa ajili yako mwenyewe.

16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto,

unapowakemea, watu wako huangamia.

17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume,

mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.

18 Ndipo hatutakuacha tena,

utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.

19 EeBwanaMungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe;

utuangazie uso wako,

ili tuweze kuokolewa.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/80-e66411dc1eba208e8eb0c3030a5e0c2d.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 81

Wimbo Wa Sikukuu

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu.

1 Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu;

mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!

2 Anzeni wimbo, pigeni matari,

pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.

3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume

wakati wa Mwandamo wa Mwezi,

na wakati wa mwezi mpevu,

katika siku ya Sikukuu yetu;

4 hii ni amri kwa Israeli,

agizo la Mungu wa Yakobo.

5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu

alipotoka dhidi ya Misri,

huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.

6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao;

mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.

7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa,

nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo;

nilikujaribu katika maji ya Meriba.

8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya:

laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!

9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu;

msimsujudie mungu wa kigeni.

10 Mimi niBwanaMungu wako,

niliyekutoa nchi ya Misri.

Panua sana kinywa chako

nami nitakijaza.

11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza;

Israeli hakutaka kunitii.

12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao

wafuate mashauri yao wenyewe.

13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza,

kama Israeli wangalifuata njia zangu,

14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka,

na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!

15 Wale wanaomchukiaBwanawangalinyenyekea mbele zake,

na adhabu yao ingedumu milele.

16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora,

na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/81-e87653961eb08b44308f749c8a325e06.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 82

Maombi Kwa Ajili Ya Kutaka Haki

Zaburi ya Asafu.

1 Mungu anaongoza kusanyiko kuu,

anatoa hukumu miongoni mwa “miungu”:

2 “Hata lini utaendelea kuwatetea wasio haki

na kuonyesha upendeleo kwa waovu?

3 Teteeni wanyonge na yatima,

tunzeni haki za maskini na walioonewa.

4 Mwokoeni mnyonge na mhitaji,

wakomboeni kutoka mkononi mwa mwovu.

5 “Hawajui lolote, hawaelewi lolote.

Wanatembea gizani;

misingi yote ya dunia imetikisika.

6 “Nilisema, ‘Ninyi ni “miungu”;

ninyi nyote ni wana wa Aliye Juu Sana.’

7 Lakini mtakufa kama wanadamu wa kawaida;

mtaanguka kama mtawala mwingine yeyote.”

8 Ee Mungu, inuka uihukumu nchi,

kwa kuwa mataifa yote ni urithi wako.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/82-60692687af86ed7e0cf29b48afb24c48.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 83

Maombi Kwa Ajili Ya Kushindwa Kwa Adui Wa Israeli

Wimbo. Zaburi ya Asafu.

1 Ee Mungu, usinyamaze kimya,

usinyamaze, Ee Mungu, usitulie.

2 Tazama watesi wako wanafanya fujo,

jinsi adui zako wanavyoinua vichwa vyao.

3 Kwa hila, wanafanya shauri dhidi ya watu wako,

wanafanya shauri baya dhidi ya wale unaowapenda.

4 Wanasema, “Njooni, tuwaangamize kama taifa,

ili jina la Israeli lisikumbukwe tena.”

5 Kwa nia moja wanapanga mashauri mabaya pamoja,

wanafanya muungano dhidi yako,

6 mahema ya Edomu na Waishmaeli,

ya Wamoabu na Wahagari,

7 Gebali,Amoni na Amaleki,

Ufilisti, pamoja na watu wa Tiro.

8 Hata Ashuru wameungana nao

kuwapa nguvu wazao wa Loti.

9 Uwatendee kama vile ulivyowatendea Midiani,

na kama vile ulivyowatendea Sisera na Yabini

hapo kijito cha Kishoni,

10 ambao waliangamia huko Endori

na wakawa kama takataka juu ya nchi.

11 Wafanye wakuu wao kama Orebu na Zeebu,

watawala wao kama Zeba na Salmuna,

12 ambao walisema, “Na tumiliki nchi

ya malisho ya Mungu.”

13 Ee Mungu wangu, wapeperushe kama mavumbi ya kisulisuli,

kama makapi yapeperushwayo na upepo.

14 Kama vile moto uteketezavyo msitu

au mwali wa moto unavyounguza milima,

15 wafuatilie kwa tufani yako

na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.

16 Funika nyuso zao kwa aibu

ili watu walitafute jina lako, EeBwana.

17 Wao na waaibishwe na kufadhaishwa milele,

na waangamie kwa aibu.

18 Hebu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako niBwana,

kwamba wewe peke yako ndiwe Uliye Juu Sana ya dunia yote.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/83-34518efc42844b96fe74402423a0cd6a.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 84

Kuionea Shauku Nyumba Ya Mungu

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora.

1 EeBwanaMwenye Nguvu Zote,

makao yako yapendeza kama nini!

2 Nafsi yangu inatamani sana,

naam, hata kuona shauku,

kwa ajili ya nyua zaBwana;

moyo wangu na mwili wangu

vinamlilia Mungu Aliye Hai.

3 Hata shomoro amejipatia makao,

mbayuwayu amejipatia kiota

mahali awezapo kuweka makinda yake:

mahali karibu na madhabahu yako,

EeBwanaMwenye Nguvu Zote,

Mfalme wangu na Mungu wangu.

4 Heri wale wanaokaa nyumbani mwako,

wanaokusifu wewe daima.

5 Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako,

na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.

6 Wanapopita katika Bonde la Baka,

hulifanya mahali pa chemchemi,

pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.

7 Huendelea toka nguvu hadi nguvu,

hadi kila mmoja afikapo

mbele za Mungu huko Sayuni.

8 EeBwanaMungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu;

nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.

9 Ee Mungu, uitazame ngao yetu,

mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.

10 Siku moja katika nyua zako ni bora

kuliko siku elfu mahali pengine;

afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu

kuliko kukaa katika mahema ya waovu.

11 Kwa kuwaBwanani jua na ngao,

Bwanahutoa wema na heshima;

hakuna kitu chema anachowanyima

wale ambao hawana hatia.

12 EeBwanaMwenye Nguvu Zote,

heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/84-de9fa6d217312710ae91c4f248286a9d.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 85

Maombi Kwa Ajili Ya Ustawi Wa Taifa

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora.

1 EeBwana, ulionyesha wema kwa nchi yako.

Ulimrejeshea Yakobo baraka zake.

2 Ulisamehe uovu wa watu wako,

na kufunika dhambi zao zote.

3 Uliweka kando ghadhabu yako yote

na umegeuka na kuiacha hasira yako kali.

4 Ee Mungu Mwokozi wetu, uturejeshe tena,

nawe uiondoe chuki yako juu yetu.

5 Je, utatukasirikia milele?

Utaendeleza hasira yako kwa vizazi vyote?

6 Je, hutatuhuisha tena,

ili watu wako wakufurahie?

7 Utuonyeshe upendo wako usiokoma, EeBwana,

utupe wokovu wako.

8 Nitasikiliza lile atakalosema Mungu aliyeBwana;

anaahidi amani kwa watu wake, watakatifu wake:

lakini nao wasirudie upumbavu.

9 Hakika wokovu wake uko karibu na wale wamchao,

ili utukufu wake udumu katika nchi yetu.

10 Upendo na uaminifu hukutana pamoja,

haki na amani hubusiana.

11 Uaminifu huchipua kutoka nchi,

haki hutazama chini kutoka mbinguni.

12 Naam, hakikaBwanaatatoa kilicho chema,

nayo nchi yetu itazaa mavuno yake.

13 Haki itatangulia mbele yake

na kutengeneza njia kwa ajili ya hatua zake.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/85-156429c1a93caa8c13cec7b5208a6cb1.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 86

Kuomba Msaada

Maombi ya Daudi.

1 EeBwana, sikia na unijibu,

kwa maana mimi ni maskini na mhitaji.

2 Linda maisha yangu, kwa maana nimejiweka kwako,

wewe ni Mungu wangu,

mwokoe mtumishi wako anayekutumaini.

3 EeBwana, nihurumie mimi,

kwa maana ninakuita mchana kutwa.

4 Mpe mtumishi wako furaha,

kwa kuwa kwako wewe, EeBwana,

ninainua nafsi yangu.

5 EeBwana, wewe ni mwema na mwenye kusamehe,

umejaa upendo kwa wote wakuitao.

6 EeBwana, sikia maombi yangu,

sikiliza kilio changu unihurumie.

7 Katika siku ya shida yangu nitakuita,

kwa maana wewe utanijibu.

8 EeBwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe,

hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.

9 EeBwana, mataifa yote uliyoyafanya

yatakuja na kuabudu mbele zako;

wataliletea utukufu jina lako.

10 Kwa maana wewe ni mkuu, na unafanya mambo ya ajabu;

wewe peke yako ndiwe Mungu.

11 EeBwana, nifundishe njia yako,

nami nitakwenda katika kweli yako;

nipe moyo usiositasita,

ili niweze kulicha jina lako.

12 EeBwanawangu, nitakusifu kwa moyo wote;

nitaliadhimisha jina lako milele.

13 Kwa maana upendo wako ni mkuu kwangu;

umeniokoa kutoka kwenye vilindi vya kaburi.

14 Ee Mungu, wenye majivuno wananishambulia;

kundi la watu wakatili linatafuta uhai wangu:

watu wasiokuheshimu wewe.

15 Lakini wewe, EeBwana, ni Mungu wa huruma na neema,

si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo na uaminifu.

16 Nigeukie na unihurumie;

mpe mtumishi wako nguvu zako,

mwokoe mwana wa mtumishi wako wa kike.

17 Nipe ishara ya wema wako,

ili adui zangu waione nao waaibishwe,

kwa kuwa wewe, EeBwana,

umenisaidia na kunifariji.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/86-374bffae46feebf1d5ca5d4a064fa2db.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 87

Sifa Za Yerusalemu

Zaburi ya wana wa Kora. Wimbo.

1 Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;

2 Bwanaanayapenda malango ya Sayuni

kuliko makao yote ya Yakobo.

3 Mambo matukufu yanasemwa juu yako,

ee mji wa Mungu:

4 “Nitaweka kumbukumbu ya Rahabuna Babeli

miongoni mwa wale wanaonikubali mimi:

Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi,

nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’ ”

5 Kuhusu Sayuni itasemwa hivi,

“Huyu na yule walizaliwa humo,

naye Aliye Juu Sana mwenyewe

atamwimarisha.”

6 Bwanaataandika katika orodha ya mataifa:

“Huyu alizaliwa Sayuni.”

7 Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba,

“Chemchemi zangu zote ziko kwako.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/87-b58571d086216174f2c1a99235746623.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 88

Kilio Kwa Ajili Ya Kuomba Msaada

Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi.

1 EeBwana, Mungu uniokoaye,

nimelia mbele zako usiku na mchana.

2 Maombi yangu yafike mbele zako,

utegee kilio changu sikio lako.

3 Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu,

na maisha yangu yanakaribia kaburi.

4 Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni,

niko kama mtu asiye na nguvu.

5 Nimetengwa pamoja na wafu,

kama waliochinjwa walalao kaburini,

ambao huwakumbuki tena,

ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.

6 Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana,

katika vina vya giza nene.

7 Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu,

umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.

8 Umenitenga na rafiki zangu wa karibu

na kunifanya chukizo kwao.

Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;

9 nuru ya macho yangu

imefifia kwa ajili ya huzuni.

EeBwana, ninakuita kila siku,

ninakunyooshea wewe mikono yangu.

10 Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako?

Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?

11 Je, upendo wako hutangazwa kaburini,

uaminifu wako katika Uharibifu?

12 Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza,

au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?

13 Lakini ninakulilia wewe, EeBwana, unisaidie;

asubuhi maombi yangu huja mbele zako.

14 EeBwana, kwa nini unanikataa

na kunificha uso wako?

15 Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo;

nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.

16 Ghadhabu yako imepita juu yangu;

hofu zako zimeniangamiza.

17 Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko;

zimenimeza kabisa.

18 Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu;

giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/88-cacc7906f9c2e752d914701be3488263.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 89

Wimbo Wakati Wa Taabu Ya Kitaifa

Utenzi wa Ethani Mwezrahi.

1 Nitaimba juu ya upendo mkuu waBwanamilele;

kwa kinywa changu nitajulisha uaminifu wako

ujulikane kwa vizazi vyote.

2 Nitatangaza kuwa upendo wako unasimama imara milele

na uaminifu wako umeuthibitisha mbinguni.

3 Ulisema, “Nimefanya agano na mteule wangu,

nimemwapia mtumishi wangu Daudi,

4 ‘Nitaimarisha uzao wako milele

na kudumisha ufalme wako kwa vizazi vyote.’ ”

5 EeBwana, mbingu zinayasifu maajabu yako,

uaminifu wako pia katika kusanyiko la watakatifu.

6 Kwa kuwa ni nani katika mbingu

anayeweza kulinganishwa naBwana?

Ni nani miongoni mwa viumbe vya mbinguni

aliye kamaBwana?

7 Katika kusanyiko la watakatifu, Mungu huogopwa sana,

anahofiwa kuliko wote wanaomzunguka.

8 EeBwanaMwenye Nguvu Zote,

ni nani aliye kama wewe?

EeBwana, wewe ni mwenye nguvu,

na uaminifu wako unakuzunguka.

9 Wewe unatawala bahari yenye msukosuko;

wakati mawimbi yake yanapoinuka, wewe unayatuliza.

10 Wewe ulimponda Rahabu

kama mmojawapo wa waliochinjwa;

kwa mkono wako wenye nguvu,

uliwatawanya adui zako.

11 Mbingu ni zako, nayo nchi pia ni yako,

uliuwekea ulimwengu msingi

pamoja na vyote vilivyomo.

12 Uliumba kaskazini na kusini;

Tabori na Hermoni wanaliimbia jina lako kwa furaha.

13 Mkono wako umejaa uwezo;

mkono wako una nguvu,

mkono wako wa kuume umetukuzwa.

14 Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako cha enzi;

upendo na uaminifu vinakutangulia.

15 Heri ni wale ambao wamejifunza kukusifu kwa shangwe,

wanaotembea katika mwanga

wa uwepo wako, EeBwana.

16 Wanashangilia katika jina lako mchana kutwa,

wanafurahi katika haki yako.

17 Kwa kuwa wewe ni utukufu na nguvu yao,

kwa wema wako unatukuza pembeyetu.

18 Naam, ngao yetu ni mali yaBwana,

na mfalme wetu mali ya Aliye Mtakatifu wa Israeli.

19 Ulizungumza wakati fulani katika maono,

kwa watu wako waaminifu, ukasema:

“Nimeweka nguvu kwa shujaa,

nimemwinua kijana miongoni mwa watu.

20 Nimemwona Daudi, mtumishi wangu,

na nimemtia mafuta yangu matakatifu.

21 Kitanga changu kitamtegemeza,

hakika mkono wangu utamtia nguvu.

22 Hakuna adui atakayemtoza ushuru,

hakuna mtu mwovu atakayemwonea.

23 Nitawaponda adui zake mbele zake

na kuwaangamiza watesi wake.

24 Upendo wangu mkamilifu utakuwa pamoja naye,

kwa Jina langu pembe yake itatukuzwa.

25 Nitauweka mkono wake juu ya bahari,

mkono wake wa kuume juu ya mito.

26 Naye ataniita kwa sauti, ‘Wewe ni Baba yangu,

Mungu wangu, Mwamba na Mwokozi wangu.’

27 Nitamteua pia awe mzaliwa wangu wa kwanza,

aliyetukuka kuliko wafalme wote wa dunia.

28 Nitadumisha upendo wangu kwake milele,

na agano langu naye litakuwa imara.

29 Nitaudumisha uzao wake milele,

kiti chake cha enzi kama mbingu zinavyodumu.

30 “Kama wanae wataacha amri yangu

na wasifuate sheria zangu,

31 kama wakihalifu maagizo yangu

na kutoshika amri zangu,

32 nitaadhibu dhambi yao kwa fimbo,

uovu wao kwa kuwapiga,

33 lakini sitauondoa upendo wangu kwake,

wala sitausaliti uaminifu wangu kamwe.

34 Mimi sitavunja agano langu

wala sitabadili lile ambalo midomo yangu imelitamka.

35 Mara moja na kwa milele, nimeapa kwa utakatifu wangu,

nami sitamdanganya Daudi:

36 kwamba uzao wake utaendelea milele,

na kiti chake cha enzi kitadumu mbele zangu kama jua;

37 kitaimarishwa milele kama mwezi,

shahidi mwaminifu angani.”

38 Lakini wewe umemkataa, umemdharau,

umemkasirikia sana mpakwa mafuta wako.

39 Umelikana agano lako na mtumishi wako,

na umeinajisi taji yake mavumbini.

40 Umebomoa kuta zake zote,

na ngome zake zote umezifanya kuwa magofu.

41 Wote wapitao karibu wamemnyangʼanya mali zake;

amekuwa dharau kwa jirani zake.

42 Umeutukuza mkono wa kuume wa adui zake,

umewafanya watesi wake wote washangilie.

43 Umegeuza makali ya upanga wake,

na hukumpa msaada katika vita.

44 Umeikomesha fahari yake,

na kukiangusha kiti chake cha enzi.

45 Umezifupisha siku za ujana wake,

umemfunika kwa vazi la aibu.

46 Hata lini, EeBwana? Utajificha milele?

Ghadhabu yako itawaka kama moto hata lini?

47 Kumbuka jinsi maisha yangu yanavyopita haraka.

Ni kwa ubatili kiasi gani umemuumba mwanadamu!

48 Ni mtu gani awezaye kuishi na asione kifo,

au kujiokoa mwenyewe kutoka nguvu za kaburi?

49 EeBwana, uko wapi upendo wako mkuu wa mwanzoni,

ambao katika uaminifu wako ulimwapia Daudi?

50 Bwana kumbuka jinsi mtumishi wako amesimangwa,

jinsi ninavyovumilia moyoni mwangu dhihaka za mataifa yote,

51 dhihaka ambazo kwazo adui zako

wamenisimanga, EeBwana,

ambazo kwazo wamesimanga

kila hatua ya mpakwa mafuta wako.

52 MsifuniBwanamilele!

Amen na Amen.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/89-837c39996f28e55d2ddacbac4029ab64.mp3?version_id=1627—