Categories
Zaburi

Zaburi 20

Maombi Kwa Ajili Ya Ushindi

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 Bwanana akujibu unapokuwa katika dhiki,

jina la Mungu wa Yakobo na liwe kinga yako.

2 Na akutumie msaada kutoka patakatifu

na akupatie msaada kutoka Sayuni.

3 Na azikumbuke dhabihu zako zote,

na azikubali sadaka zako za kuteketezwa.

4 Na akujalie haja ya moyo wako,

na aifanikishe mipango yako yote.

5 Tutashangilia kwa furaha utakaposhinda,

tutainua bendera zetu kwa jina la Mungu wetu.

Bwanana akupe haja zako zote.

6 Sasa nafahamu kuwaBwana

humwokoa mpakwa mafuta wake,

humjibu kutoka mbingu yake takatifu

kwa nguvu za wokovu wa mkono wake wa kuume.

7 Wengine wanatumaini magari ya vita, na wengine farasi,

bali sisi tutalitumainia jina laBwana, Mungu wetu.

8 Wao wameshushwa chini na kuanguka,

bali sisi tunainuka na kusimama imara.

9 EeBwana, mwokoe mfalme!

Tujibu tunapokuita!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/20-577ad76d017b4bd9d7e850b41c9fe1d4.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 21

Shukrani Kwa Mungu Kwa Ajili Ya Ushindi

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, mfalme huzifurahia nguvu zako.

Tazama jinsi ilivyo kuu furaha yake

kwa ushindi unaompa!

2 Umempa haja ya moyo wake

na hukumzuilia maombi ya midomo yake.

3 Ulimkaribisha kwa baraka tele

na kumvika taji ya dhahabu safi kichwani pake.

4 Alikuomba maisha, nawe ukampa,

wingi wa siku milele na milele.

5 Kutokana na ushindi uliompa, utukufu wake ni mkubwa,

umeweka juu yake fahari na utukufu.

6 Hakika umempa baraka za milele,

umemfanya awe na furaha

kwa shangwe ya uwepo wako.

7 Kwa kuwa mfalme anamtumainiBwana;

kwa upendo usiokoma wa Aliye Juu Sana hatatikiswa.

8 Mkono wako utawashika adui zako wote,

mkono wako wa kuume utawakamata adui zako.

9 Wakati utakapojitokeza

utawafanya kama tanuru ya moto.

Katika ghadhabu yakeBwanaatawameza,

moto wake utawateketeza.

10 Utawaangamiza wazao wao kutoka duniani,

uzao wao kutoka wanadamu.

11 Ingawa watapanga mabaya dhidi yako

na kutunga hila, hawawezi kufanikiwa,

12 kwa kuwa utawafanya wakimbie

utakapowalenga usoni pao

kwa mshale kutoka kwenye upinde wako.

13 EeBwana, utukuzwe katika nguvu zako,

tutaimba na kusifu nguvu zako.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/21-d146c2180055da91be31c243779ac087.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 22

Kilio Cha Uchungu Na Wimbo Wa Sifa

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi.

1 Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?

Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa?

Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?

2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu,

hata usiku, sinyamazi.

3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu;

wewe ni sifa ya Israeli.

4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao,

walikutumaini nawe ukawaokoa.

5 Walikulilia wewe na ukawaokoa,

walikutegemea wewe nao hawakuaibika.

6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu,

wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.

7 Wote wanionao hunidhihaki,

hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:

8 Husema, “AnamtegemeaBwana,

basiBwanana amwokoe.

Amkomboe basi, kwa maana

anapendezwa naye.”

9 Hata hivyo ulinitoa tumboni,

ukanifanya nikutegemee,

hata nilipokuwa ninanyonya

matiti ya mama yangu.

10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa,

toka tumboni mwa mama yangu

umekuwa Mungu wangu.

11 Usiwe mbali nami,

kwa maana shida iko karibu

na hakuna wa kunisaidia.

12 Mafahali wengi wamenizunguka,

mafahali wa Bashani wenye nguvu

wamenizingira.

13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo

yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.

14 Nimemiminwa kama maji,

mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake.

Moyo wangu umegeuka kuwa nta,

umeyeyuka ndani yangu.

15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae,

ulimi wangu umegandamana

na kaakaa la kinywa changu,

kwa sababu umenilaza

katika mavumbi ya kifo.

16 Mbwa wamenizunguka,

kundi la watu waovu limenizingira,

wametoboa mikono yangu na miguu yangu.

17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote,

watu wananikodolea macho na kunisimanga.

18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao,

na vazi langu wanalipigia kura.

19 Lakini wewe, EeBwana,

usiwe mbali.

Ee Nguvu yangu,

uje haraka unisaidie.

20 Okoa maisha yangu na upanga,

uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.

21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba,

niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.

22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu,

katika kusanyiko nitakusifu wewe.

23 Ninyi ambao mnamchaBwana, msifuni!

Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye!

Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!

24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau

mateso ya aliyeonewa;

hakumficha uso wake

bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.

25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa,

nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.

26 Maskini watakula na kushiba,

wale wamtafutaoBwanawatamsifu:

mioyo yenu na iishi milele!

27 Miisho yote ya dunia itakumbuka

na kumgeukiaBwana,

nazo jamaa zote za mataifa

watasujudu mbele zake,

28 kwa maana ufalme ni waBwana

naye hutawala juu ya mataifa.

29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu.

Wote waendao mavumbini

watapiga magoti mbele yake,

wote ambao hawawezi

kudumisha uhai wao.

30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye;

vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.

31 Watatangaza haki yake kwa watu

ambao hawajazaliwa bado,

kwa maana yeye ametenda hili.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/22-c4299ee39d33f726a920e2bded588c50.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 23

Bwana Mchungaji Wetu

Zaburi ya Daudi.

1 Bwanandiye mchungaji wangu,

sitapungukiwa na kitu.

2 Hunilaza katika malisho

ya majani mabichi,

kando ya maji matulivu huniongoza,

3 hunihuisha nafsi yangu.

Huniongoza katika njia za haki

kwa ajili ya jina lake.

4 Hata kama nikipita katikati

ya bonde la uvuli wa mauti,

sitaogopa mabaya,

kwa maana wewe upo pamoja nami;

fimbo yako na mkongojo wako

vyanifariji.

5 Waandaa meza mbele yangu

machoni pa adui zangu.

Umenipaka mafuta kichwani pangu,

kikombe changu kinafurika.

6 Hakika wema na upendo vitanifuata

siku zote za maisha yangu,

nami nitakaa nyumbani mwaBwana

milele.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/23-dc391d02f87b42fe58b081c51d280890.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 24

Mfalme Mkuu

Zaburi ya Daudi.

1 Dunia ni mali yaBwana, na vyote vilivyomo ndani yake,

ulimwengu, na wote waishio ndani yake,

2 maana aliiwekea misingi yake baharini

na kuifanya imara juu ya maji.

3 Nani awezaye kuupanda mlima waBwana?

Ni nani awezaye kusimama patakatifu pake?

4 Ni yule mwenye mikono safi na moyo mweupe,

yule ambaye hakuinulia sanamu nafsi yake

au kuapa kwa kitu cha uongo.

5 Huyo atapokea baraka kutoka kwaBwana,

na hukumu ya haki kutoka kwa Mungu Mwokozi wake.

6 Hiki ndicho kizazi cha wale wamtafutao,

wale wautafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.

7 Inueni vichwa vyenu, enyi malango,

inukeni enyi milango ya kale,

ili mfalme wa utukufu apate kuingia.

8 Ni nani huyu Mfalme wa utukufu?

NiBwanaaliye na nguvu na uweza,

niBwanaaliye hodari katika vita.

9 Inueni vichwa vyenu, enyi malango,

viinueni juu enyi milango ya kale,

ili Mfalme wa utukufu apate kuingia.

10 Ni nani yeye, huyu Mfalme wa utukufu?

NiBwanaMwenye Nguvu Zote;

yeye ndiye Mfalme wa utukufu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/24-91c40c17d34778b02a40e9bd38202f5a.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 25

Kumwomba Mungu Uongozi Na Ulinzi

Zaburi ya Daudi.

1 Kwako wewe, EeBwana,

nainua nafsi yangu,

2 ni wewe ninayekutumainia,

Ee Mungu wangu.

Usiniache niaibike,

wala usiache adui zangu wakanishinda.

3 Kamwe hakuna hata mmoja anayekutegemea

atakayeaibishwa,

bali wataaibishwa

wafanyao hila bila sababu.

4 Nionyeshe njia zako, EeBwana,

nifundishe mapito yako,

5 niongoze katika kweli yako na kunifundisha,

kwa maana wewe ni Mungu Mwokozi wangu,

nalo tumaini langu liko kwako wakati wote.

6 Kumbuka, EeBwana, rehema zako kuu na upendo,

kwa maana zimekuwepo tangu zamani.

7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu

wala njia zangu za uasi,

sawasawa na upendo wako unikumbuke,

kwa maana wewe ni mwema, EeBwana.

8 Bwanani mwema na mwenye adili,

kwa hiyo huwafundisha wenye dhambi njia zake.

9 Huwaongoza wanyenyekevu katika haki,

naye huwafundisha njia yake.

10 Njia zote zaBwanani za upendo na uaminifu

kwa wale wanaoshika shuhuda za agano lake.

11 EeBwana, kwa ajili ya jina lako,

unisamehe uovu wangu, ijapokuwa ni mwingi.

12 Ni nani basi, mtu yule anayemchaBwana?

Atamfundisha katika njia

atakayoichagua kwa ajili yake.

13 Mtu huyo atafanikiwa maishani mwake,

nao wazao wake watairithi nchi.

14 Siri yaBwanaiko kwa wale wamchao,

yeye huwajulisha agano lake.

15 Macho yangu humwelekeaBwanadaima,

kwa kuwa yeye peke yake ndiye ataitoa

miguu yangu kutoka mtego.

16 Nigeukie na unihurumie,

kwa maana mimi ni mpweke na mwenye kuteseka.

17 Shida za moyo wangu zimeongezeka,

niokoe katika dhiki yangu.

18 Uangalie mateso na shida zangu

na uniondolee dhambi zangu zote.

19 Tazama adui zangu walivyo wengi,

pia uone jinsi wanavyonichukia vikali!

20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe,

usiniache niaibike,

kwa maana nimekukimbilia wewe.

21 Uadilifu na uaminifu vinilinde,

kwa sababu tumaini langu ni kwako.

22 Ee Mungu, wakomboe Israeli,

katika shida zao zote!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/25-d574a817dbd54a3e276411792368f1c6.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 26

Maombi Ya Mtu Mwema

Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, nithibitishe katika haki,

maana nimeishi maisha yasiyo na lawama;

nimemtumainiaBwana

bila kusitasita.

2 EeBwana, unijaribu, unipime,

uuchunguze moyo wangu

na mawazo yangu;

3 kwa maana upendo wako

uko mbele yangu daima,

nami natembea siku zote

katika kweli yako.

4 Siketi pamoja na watu wadanganyifu,

wala siandamani na wanafiki,

5 ninachukia kusanyiko la watenda mabaya

na ninakataa kuketi pamoja na waovu.

6 Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia,

naikaribia madhabahu yako, EeBwana,

7 nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa,

huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.

8 EeBwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi,

mahali ambapo utukufu wako hukaa.

9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi,

wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,

10 ambao mikononi mwao kuna mipango miovu,

ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.

11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama;

nikomboe na unihurumie.

12 Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare;

katika kusanyiko kuu nitamsifuBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/26-7419f63c65255b42ade02f98cd34b3ef.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 27

Sala Ya Kusifu

Zaburi ya Daudi.

1 Bwanani nuru yangu na wokovu wangu,

nimwogope nani?

Bwanani ngome ya uzima wangu,

nimhofu nani?

2 Waovu watakaposogea dhidi yangu

ili wanile nyama yangu,

adui zangu na watesi wangu watakaponishambulia,

watajikwaa na kuanguka.

3 Hata jeshi linizunguke pande zote,

moyo wangu hautaogopa;

hata vita vitokee dhidi yangu,

hata hapo nitakuwa na ujasiri.

4 Jambo moja ninamwombaBwana,

hili ndilo ninalolitafuta:

niweze kukaa nyumbani mwaBwana

siku zote za maisha yangu,

niutazame uzuri waBwana

na kumtafuta hekaluni mwake.

5 Kwa kuwa siku ya shida,

atanihifadhi salama katika maskani yake,

atanificha uvulini mwa hema yake

na kuniweka juu kwenye mwamba.

6 Kisha kichwa changu kitainuliwa

juu ya adui zangu wanaonizunguka.

Katika maskani yake nitatoa dhabihu kwa kelele za shangwe;

nitamwimbiaBwanana kumsifu.

7 Isikie sauti yangu nikuitapo, EeBwana,

unihurumie na unijibu.

8 Moyo wangu unasema kuhusu wewe,

“Utafute uso wake!”

Uso wako,Bwana“Nitautafuta.”

9 Usinifiche uso wako,

usimkatae mtumishi wako kwa hasira;

wewe umekuwa msaada wangu.

Usinikatae wala usiniache,

Ee Mungu Mwokozi wangu.

10 Hata kama baba yangu na mama wakiniacha,

Bwanaatanipokea.

11 Nifundishe njia yako, EeBwana,

niongoze katika njia iliyonyooka

kwa sababu ya watesi wangu.

12 Usiniachilie kwa nia za adui zangu,

kwa maana mashahidi wa uongo

wameinuka dhidi yangu,

wakipumua ujeuri.

13 Nami bado nina tumaini hili:

nitauona wema waBwana

katika nchi ya walio hai.

14 MngojeeBwana,

uwe hodari na mwenye moyo mkuu,

nawe, umngojeeBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/27-9152c2d2d9cc93af54e1c71054b93235.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 28

Kuomba Msaada

Zaburi ya Daudi.

1 Ninakuita wewe, EeBwana, Mwamba wangu;

usiwe kwangu kama kiziwi.

Kwa sababu ukinyamaza

nitafanana na walioshuka shimoni.

2 Sikia kilio changu unihurumie

ninapokuita kwa ajili ya msaada,

niinuapo mikono yangu kuelekea

Patakatifu pa Patakatifu pako.

3 Usiniburute pamoja na waovu,

pamoja na hao watendao mabaya,

ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri,

lakini mioyoni mwao wameficha chuki.

4 Walipe sawasawa na matendo yao,

sawasawa na matendo yao maovu;

walipe sawasawa na kazi za mikono yao,

uwalipe wanavyostahili.

5 Kwa kuwa hawaheshimu kazi zaBwana,

na yale ambayo mikono yake imetenda,

atawabomoa na kamwe

hatawajenga tena.

6 Bwanaasifiwe,

kwa maana amesikia kilio changu

nikimwomba anihurumie.

7 Bwanani nguvu zangu na ngao yangu,

moyo wangu umemtumaini yeye,

nami nimesaidiwa.

Moyo wangu unarukaruka kwa furaha

nami nitamshukuru kwa wimbo.

8 Bwanani nguvu ya watu wake,

ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.

9 Waokoe watu wako na uubariki urithi wako;

uwe mchungaji wao na uwabebe milele.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/28-ccdd4c1f15c10ab12f79c0f60d9b93a3.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 29

Sauti Ya Bwana Wakati Wa Dhoruba

Zaburi ya Daudi.

1 MpeniBwana, enyi mashujaa,

mpeniBwanautukufu na nguvu.

2 MpeniBwanautukufu unaostahili jina lake;

mwabuduniBwanakatika uzuri wa utakatifu wake.

3 Sauti yaBwanaiko juu ya maji;

Mungu wa utukufu hupiga radi,

Bwanahupiga radi juu ya maji makuu.

4 Sauti yaBwanaina nguvu;

sauti yaBwanani tukufu.

5 Sauti yaBwanahuvunja mierezi;

Bwanahuvunja vipande vipande

mierezi ya Lebanoni.

6 Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama,

Sirioniurukaruke kama mwana nyati.

7 Sauti yaBwanahupiga kwa miali

ya umeme wa radi.

8 Sauti yaBwanahutikisa jangwa;

Bwanahutikisa Jangwa la Kadeshi.

9 Sauti yaBwanahuzalisha ayala,

na huuacha msitu wazi.

Hekaluni mwake wote wasema,

“Utukufu!”

10 Bwanahuketi akiwa ametawazwa juu ya gharika;

Bwanaametawazwa kuwa Mfalme milele.

11 Bwanahuwapa watu wake nguvu;

Bwanahuwabariki watu wake kwa kuwapa amani.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/29-a77bafb769001fb1643ac0ddcb064950.mp3?version_id=1627—