Categories
Zaburi

Zaburi 150

Msifuni Bwana Kwa Ukuu Wake

1 MsifuniBwana.

Msifuni Mungu katika patakatifu pake,

msifuni katika mbingu zake kuu.

2 Msifuni kwa matendo yake makuu,

msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

3 Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta,

msifuni kwa kinubi na zeze,

4 msifuni kwa matari na kucheza,

msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,

5 msifuni kwa matoazi yaliayo,

msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6 Kila chenye pumzi na kimsifuBwana.

MsifuniBwana!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/150-cc95c5b1e920e3320c0de853056acb58.mp3?version_id=1627—