Msifuni Bwana Kwa Ukuu Wake
1 MsifuniBwana.
Msifuni Mungu katika patakatifu pake,
msifuni katika mbingu zake kuu.
2 Msifuni kwa matendo yake makuu,
msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
3 Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta,
msifuni kwa kinubi na zeze,
4 msifuni kwa matari na kucheza,
msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,
5 msifuni kwa matoazi yaliayo,
msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
6 Kila chenye pumzi na kimsifuBwana.
MsifuniBwana!
—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/150-cc95c5b1e920e3320c0de853056acb58.mp3?version_id=1627—