Categories
Zaburi

Zaburi 140

Kuomba Ulinzi Wa Mungu

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu;

nilinde na watu wenye jeuri,

2 ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao,

na kuchochea vita siku zote.

3 Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka,

sumu ya nyoka iko midomoni mwao.

4 EeBwana, niepushe na mikono ya waovu;

nilinde na watu wenye jeuri

wanaopanga kunikwaza miguu yangu.

5 Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa,

wametandaza kamba za wavu wao,

wametega mitego kwenye njia yangu.

6 EeBwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.”

EeBwana, usikie kilio changu na kunihurumia.

7 EeBwanaMwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu,

unikingaye kichwa changu siku ya vita:

8 EeBwana, usiwape waovu matakwa yao,

usiache mipango yao ikafanikiwa,

wasije wakajisifu.

9 Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe

na shida zinazosababishwa na midomo yao.

10 Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie!

Na watupwe motoni,

katika mashimo ya matope,

wasiinuke tena kamwe.

11 Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi;

maafa na yawawinde watu wenye jeuri.

12 Najua kwambaBwanahuwapatia maskini haki,

na kuitegemeza njia ya mhitaji.

13 Hakika wenye haki watalisifu jina lako,

na waadilifu wataishi mbele zako.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/140-c7abfd880fe0c293fccb9cebb7d5d1a7.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 141

Maombi Ya Kuhifadhiwa Dhidi Ya Uovu

Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima.

Sikia sauti yangu ninapokuita.

2 Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba;

kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.

3 EeBwana, weka mlinzi kinywani mwangu,

weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.

4 Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya,

nisije nikashiriki katika matendo maovu

pamoja na watu watendao mabaya,

wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.

5 Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma;

na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu.

Kichwa changu hakitalikataa.

Hata hivyo, maombi yangu daima

ni kinyume cha watenda mabaya,

6 watawala wao watatupwa chini

kutoka kwenye majabali,

waovu watajifunza kwamba maneno yangu

yalikuwa kweli.

7 Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi,

ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.”

8 Lakini nimekaza macho yangu kwako, EeBwanaMwenyezi,

ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.

9 Niepushe na mitego waliyonitegea,

kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya.

10 Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe,

wakati mimi ninapita salama.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/141-2e78f72da3c85efe3c132cabfafda772.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 142

Maombi Ya Kuokolewa Dhidi Ya Watesi

Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi.

1 NamliliaBwanakwa sauti,

nainua sauti yangu kwaBwanaanihurumie.

2 Namimina malalamiko yangu mbele zake,

mbele zake naeleza shida zangu.

3 Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu,

wewe ndiwe unajua njia zangu.

Katika njia ninayopita

watu wameniwekea mtego.

4 Tazama kuume kwangu na uone,

hakuna hata mmoja anayejihusisha nami.

Sina kimbilio,

hakuna anayejali maisha yangu.

5 EeBwana, nakulilia wewe,

nasema, “Wewe ni kimbilio langu,

fungu langu katika nchi ya walio hai.”

6 Sikiliza kilio changu,

kwa sababu mimi ni mhitaji sana;

niokoe na wale wanaonifuatilia,

kwa kuwa wamenizidi nguvu.

7 Nifungue kutoka kifungo changu,

ili niweze kulisifu jina lako.

Ndipo wenye haki watanizunguka,

kwa sababu ya wema wako kwangu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/142-016a7e0786320f3f02f0ea5ebd0aba8f.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 143

Maombi Ya Kuokolewa Dhidi Ya Adui

Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, sikia sala yangu,

sikiliza kilio changu unihurumie;

katika uaminifu na haki yako

njoo unisaidie.

2 Usimhukumu mtumishi wako,

kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako.

3 Adui hunifuatilia,

hunipondaponda chini;

hunifanya niishi gizani

kama wale waliokufa zamani.

4 Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu,

moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.

5 Nakumbuka siku za zamani;

natafakari juu ya kazi zako zote,

naangalia juu ya kazi

ambazo mikono yako imezifanya.

6 Nanyoosha mikono yangu kwako,

nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame.

7 EeBwana, unijibu haraka,

roho yangu inazimia.

Usinifiche uso wako,

ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni.

8 Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma,

kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako.

Nionyeshe njia nitakayoiendea,

kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.

9 EeBwana, uniokoe na adui zangu,

kwa kuwa nimejificha kwako.

10 Nifundishe kufanya mapenzi yako,

kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu,

Roho wako mwema na aniongoze

katika nchi tambarare.

11 EeBwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu,

kwa haki yako nitoe katika taabu.

12 Kwa upendo wako usiokoma,

nyamazisha adui zangu;

waangamize watesi wangu wote,

kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/143-cd2153934e693222771bbe87b6f52c43.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 144

Mfalme Amshukuru Mungu Kwa Ushindi

Zaburi ya Daudi.

1 Sifa ni kwaBwanaMwamba wangu,

aifundishaye mikono yangu vita,

na vidole vyangu kupigana.

2 Yeye ni Mungu wangu wa upendo na boma langu,

ngome yangu na mwokozi wangu,

ngao yangu ninayemkimbilia,

ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.

3 EeBwana, mwanadamu ni nini hata umjali,

Binadamu ni nini hata umfikirie?

4 Mwanadamu ni kama pumzi,

siku zake ni kama kivuli kinachopita.

5 EeBwana, pasua mbingu zako, ushuke,

gusa milima ili itoe moshi.

6 Peleka umeme uwatawanye adui,

lenga mishale yako uwashinde.

7 Nyoosha mkono wako kutoka juu,

nikomboe na kuniokoa

kutoka maji makuu,

kutoka mikononi mwa wageni

8 ambao vinywa vyao vimejaa uongo,

na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.

9 Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya,

kwa zeze yenye nyuzi kumi nitakuimbia,

10 kwa Yule awapaye wafalme ushindi,

ambaye humwokoa Daudi, mtumishi wake kutokana na upanga hatari.

11 Nikomboe na uniokoe

kutoka mikononi mwa wageni

ambao vinywa vyao vimejaa uongo,

na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.

12 Kisha wana wetu wakati wa ujana wao

watakuwa kama mimea iliyotunzwa vizuri,

binti zetu watakuwa kama nguzo zilizoviringwa

kurembesha jumba la kifalme.

13 Ghala zetu zitajazwa

aina zote za mahitaji.

Kondoo zetu watazaa kwa maelfu,

kwa makumi ya maelfu katika mashamba yetu;

14 maksai wetu watakokota

mizigo mizito.

Hakutakuwa na kubomoka kuta,

hakuna kuchukuliwa mateka,

wala kilio cha taabu

katika barabara zetu.

15 Heri watu ambao hili ni kweli;

heri wale ambaoBwanani Mungu wao.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/144-86d8063c5d30fe1a92aca97c91b2c345.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 145

Wimbo Wa Kusifu Ukuu Na Wema Wa Mungu

Wimbo wa Sifa. Wa Daudi.

1 Nitakutukuza wewe, Mungu wangu Mfalme,

nitalisifu jina lako milele na milele.

2 Kila siku nitakusifu

na kulitukuza jina lako milele na milele.

3 Bwanani mkuu, anayestahili kusifiwa sana,

ukuu wake haupimiki.

4 Kizazi kimoja kitasifia kazi zako kwa kizazi kingine,

watasimulia matendo yako makuu.

5 Watasema juu ya utukufu wa fahari ya ukuu wako,

nami nitatafakari juu ya kazi zako za ajabu.

6 Watasimulia uwezo wa kazi zako za kutisha,

nami nitatangaza matendo yako makuu.

7 Wataadhimisha wema wako mwingi,

na wataimba kwa shangwe juu ya haki yako.

8 Bwanani mwenye neema na mwingi wa huruma,

si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo.

9 Bwanani mwema kwa wote,

ana huruma kwa vyote alivyovifanya.

10 EeBwana, vyote ulivyovifanya vitakusifu,

watakatifu wako watakutukuza.

11 Watasimulia utukufu wa ufalme wako

na kusema juu ya ukuu wako,

12 ili watu wote wajue matendo yako makuu

na utukufu wa fahari ya ufalme wako.

13 Ufalme wako ni ufalme wa milele,

mamlaka yako hudumu vizazi vyote.

Bwanani mwaminifu kwa ahadi zake zote

na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.

14 Bwanahuwategemeza wote waangukao,

na huwainua wote waliolemewa na mizigo yao.

15 Macho yao wote yanakutazama wewe,

nawe huwapa chakula chao wakati wake.

16 Waufumbua mkono wako,

watosheleza haja ya kila kitu kilicho hai.

17 Bwanani mwenye haki katika njia zake zote,

na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.

18 Bwanayu karibu na wote wamwitao,

karibu na wote wamwitao kwa uaminifu.

19 Huwatimizia wamchao matakwa yao,

husikia kilio chao na kuwaokoa.

20 Bwanahuwalinda wote wampendao,

bali waovu wote atawaangamiza.

21 Kinywa changu kitazinena sifa zaBwana.

Kila kiumbe na kilisifu jina lake takatifu

milele na milele.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/145-926e00a6b42abbd14c4a202c1b1131c0.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 146

Kumsifu Mungu Mwokozi

1 MsifuniBwana!

Ee nafsi yangu, umsifuBwana,

2 NitamsifuBwanamaisha yangu yote;

nitamwimbia Mungu wangu sifa

wakati wote niishipo.

3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu,

kwa wanadamu ambao hufa,

ambao hawawezi kuokoa.

4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini,

siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.

5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake,

ambaye tumaini lake ni katikaBwana, Mungu wake,

6 Muumba wa mbingu na nchi,

na bahari na vyote vilivyomo ndani yake:

Bwanaanayedumu kuwa mwaminifu

milele na milele.

7 Naye huwapatia haki walioonewa

na kuwapa wenye njaa chakula.

Bwanahuwaweka wafungwa huru,

8 Bwanahuwafumbua vipofu macho,

Bwanahuwainua waliolemewa na mizigo yao,

Bwanahuwapenda wenye haki.

9 Bwanahuwalinda wageni

na kuwategemeza yatima na wajane,

lakini hupinga njia za waovu.

10 Bwanaatamiliki milele,

Mungu wako, ee Sayuni,

kwa vizazi vyote.

MsifuniBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/146-95c39d5fcce9e781a19eaaf806aab6ef.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 147

Kumsifu Mungu Mwenye Nguvu Zote

1 MsifuniBwana.

Tazama jinsi ilivyo vyema kumwimbia Mungu wetu sifa,

jinsi inavyopendeza na kustahili kumsifu yeye!

2 Bwanahujenga Yerusalemu,

huwakusanya Israeli walio uhamishoni.

3 Anawaponya waliovunjika mioyo

na kuvifunga vidonda vyao.

4 Huzihesabu nyota

na huipa kila moja jina lake.

5 Bwana wetu ni mkuu na mwenye uwezo mwingi,

ufahamu wake hauna kikomo.

6 Bwanahuwahifadhi wanyenyekevu

lakini huwashusha waovu mpaka mavumbini.

7 MwimbieniBwanakwa shukrani,

mpigieni Mungu wetu kinubi.

8 Yeye huzifunika anga kwa mawingu,

huinyeshea ardhi mvua,

na kuzifanya nyasi kuota juu ya vilima.

9 Huwapa chakula mifugo

na pia makinda ya kunguru yanapolia.

10 Furaha yake haipo katika nguvu za farasi,

wala furaha yake kwenye miguu ya mwanadamu.

11 Bwanahupendezwa na wale wamchao,

wale wanaoweka tumaini lao katika upendo wake usiokoma.

12 MtukuzeBwana, ee Yerusalemu,

msifu Mungu wako, ee Sayuni,

13 kwa maana huimarisha makomeo ya malango yako

na huwabariki watu wako walio ndani yako.

14 Huwapa amani mipakani mwenu

na kukushibisha kwa ngano safi kabisa.

15 Hutuma amri yake duniani,

neno lake hukimbia kasi.

16 Anatandaza theluji kama sufu

na kutawanya umande kama majivu.

17 Huvurumisha mvua yake ya mawe kama changarawe.

Ni nani awezaye kustahimili ukali wa baridi yake?

18 Hutuma neno lake na kuviyeyusha,

huvumisha upepo wake, nayo maji hutiririka.

19 Amemfunulia Yakobo neno lake,

sheria zake na maagizo yake kwa Israeli.

20 Hajafanya hivyo kwa taifa lingine lolote,

hawazijui sheria zake.

MsifuniBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/147-6ec7e09cc3e3b2da07364666932b199b.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 148

Mwito Kwa Ulimwengu Kumsifu Mungu

1 MsifuniBwana.

MsifuniBwanakutoka mbinguni,

msifuni juu vileleni.

2 Msifuni, enyi malaika wake wote,

msifuni yeye, enyi jeshi lake lote la mbinguni.

3 Msifuni yeye, enyi jua na mwezi,

msifuni yeye, enyi nyota zote zingʼaazo.

4 Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu sana,

na ninyi maji juu ya anga.

5 Vilisifu jina laBwana

kwa maana aliamuru navyo vikaumbwa.

6 Aliviweka mahali pake milele na milele,

alitoa amri ambayo haibadiliki milele.

7 MtukuzeniBwanakutoka duniani,

ninyi viumbe vikubwa vya baharini na vilindi vyote vya bahari,

8 umeme wa radi na mvua ya mawe, theluji na mawingu,

pepo za dhoruba zinazofanya amri zake,

9 ninyi milima na vilima vyote,

miti ya matunda na mierezi yote,

10 wanyama wa mwituni na mifugo yote,

viumbe vidogo na ndege warukao,

11 wafalme wa dunia na mataifa yote,

ninyi wakuu na watawala wote wa dunia,

12 wanaume vijana na wanawali,

wazee na watoto.

13 Wote na walisifu jina laBwana,

kwa maana jina lake pekee limetukuka,

utukufu wake uko juu ya nchi na mbingu.

14 Amewainulia watu wake pembe,

sifa ya watakatifu wake wote,

ya Israeli, watu walio karibu na moyo wake.

MsifuniBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/148-41b131ad3ce27044f048b5cc8f4781ee.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 149

Wimbo Wa Kumsifu Mungu Kwa Wema Wake

1 MsifuniBwana.

MwimbieniBwanawimbo mpya,

sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.

2 Israeli na washangilie katika Muumba wao,

watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.

3 Na walisifu jina lake kwa kucheza

na wampigie muziki kwa matari na kinubi.

4 Kwa maanaBwanaanapendezwa na watu wake,

anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.

5 Watakatifu washangilie katika heshima hii,

na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.

6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao

na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,

7 ili walipize mataifa kisasi

na adhabu juu ya mataifa,

8 wawafunge wafalme wao kwa minyororo,

wakuu wao kwa pingu za chuma,

9 ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao.

Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote.

MsifuniBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/149-61e7d4fbad63268e796907d56d248b66.mp3?version_id=1627—