Categories
Zaburi

Zaburi Utangulizi

Utangulizi

Jina la kitabu hiki kwa Kiebrania ni “Sepher Tehillim,” maana yake “Nyimbo za Sifa.” Jina la Kiyunani ni “Psalmoi,” yaani “Nyimbo zinazoandamana na ala za uimbaji za nyuzi,” na ndiyo kiini cha kitabu hiki. Kila sura ya 150 za kitabu hiki ni ya kipekee tena imekamilika, isipokuwa chache tu.

Zaburi zinaleta hisia mbalimbali kama vile misisimko, hali na mivuto mikubwa tofauti. Kwa kuwa Zaburi zinatokana na uzoefu wa kibinafsi kutoka asili pana hivyo, bado zimekuwa na mvuto mkubwa ulimwenguni wote kwa miaka mingi hivi tangu ziandikwe.

Mara kwa mara Zaburi zimeainishwa kwa kufuata namna fulani za maelezeo au mafundisho. Baadhi ya mapendekezo ya aina zenyewe, na mifano yake ambayo inaweza kuwa msaada mkubwa katika kujifunza zaidi ni kama ifuatavyo:

Kawaida ya ibada na sala

120–130

Kuhusu Masiya

2

16

22

25

69

110

Kuomba toba

6

32

51

Kumkaribia Mungu binafsi

23

27

37

Historia

78

105–106

Kumsifu Mungu

95

100

146–150

Maombi ya mwenye haki

17

20

40

55

Kuna uwezekano mkubwa kwamba makusanyo ya awali yalifanywa na Daudi. Nyongeza nyingine na mpangilio inawezekana vilifanywa na Solomoni, Yehoshafati, Hezekia, Yosia na wengine.

Mwandishi

Daudi: 73, Asafu: 12, Wana wa Kora: 10, Mose: 1, Hemani: 1, Ethani: 1, Solomoni: 2, Hazijulikani: 50.

Kusudi

Kuelezea umuhimu wa mashairi katika sifa, kuabudu na kukiri dhambi mbele za Mungu.

Mahali

Palestina na Babeli.

Tarehe

Kati ya wakati wa Mose (1440 K.K.) na wakati wa utumwa wa Babeli (586 K.K.).

Wahusika Wakuu

Daudi, Asafu, Wana wa Kora, Mose, Hemani na Solomoni.

Wazo Kuu

Kusifu ni kutambua na kutangaza ukuu wa Mungu, kufurahia na kudhihirisha wema wake.

Mambo Muhimu

Zaburi zimeelezea ufunuo wa Mungu, uumbaji, hali ya mwanadamu, wokovu, dhambi na uovu, toba, haki na uadilifu, kuabudu na kusifu, maombi na hukumu.

Mgawanyo

Kitabu I:

1–41

Kitabu II:

42–72

Kitabu III:

73–89

Kitabu IV:

90–106

Kitabu V:

107–150

.

Categories
Zaburi

Zaburi 1

Furaha Ya Kweli

1 Heri mtu yule ambaye

haendi katika shauri la watu waovu,

wala hasimami katika njia ya wenye dhambi,

au kuketi katika baraza la wenye mizaha.

2 Bali huifurahia sheria yaBwana,

naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.

3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa

kando ya vijito vya maji,

ambao huzaa matunda kwa majira yake

na majani yake hayanyauki.

Lolote afanyalo hufanikiwa.

Huzuni Ya Waovu

4 Sivyo walivyo waovu!

Wao ni kama makapi

yapeperushwayo na upepo.

5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu,

wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.

6 Kwa maanaBwanahuziangalia njia za mwenye haki,

bali njia ya waovu itaangamia.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/1-461588185b7df957126ca69dd341074d.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 2

Mfalme Aliyechaguliwa Na Mungu

1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya,

na kabila za watu kula njama bure?

2 Wafalme wa dunia wanajipanga

na watawala wanajikusanya pamoja

dhidi yaBwana

na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.

3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao

na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”

4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka,

Bwana huwadharau.

5 Kisha huwakemea katika hasira yake

na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,

6 “Nimemtawaza Mfalme wangu

juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”

Ushindi Wa Mfalme

7 Nitatangaza amri yaBwana:

Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu,

leo mimi nimekuzaa.

8 Niombe, nami nitayafanya mataifa

kuwa urithi wako,

miisho ya dunia kuwa milki yako.

9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma

na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”

10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima;

mwonyeke, enyi watawala wa dunia.

11 MtumikieniBwanakwa hofu

na mshangilie kwa kutetemeka.

12 Mbusu Mwana, asije akakasirika

nawe ukaangamizwa katika njia yako,

kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula.

Heri wote wanaomkimbilia.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/2-a11c6bc14963afae6c73d8884c7251e0.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 3

Sala Ya Asubuhi Ya Kuomba Msaada

Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu.

1 EeBwana, tazama adui zangu walivyo wengi!

Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!

2 Wengi wanasema juu yangu,

“Mungu hatamwokoa.”

3 Lakini wewe, EeBwana, ni ngao pande zote;

umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.

4 NinamliliaBwanakwa sauti kuu,

naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.

5 Ninajilaza na kupata usingizi;

naamka tena, kwa maanaBwanahunitegemeza.

6 Sitaogopa makumi elfu ya adui,

wanaojipanga dhidi yangu kila upande.

7 EeBwana, amka!

Niokoe, Ee Mungu wangu!

Wapige adui zangu wote kwenye taya,

vunja meno ya waovu.

8 Kwa maana wokovu watoka kwaBwana.

Baraka yako na iwe juu ya watu wako.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/3-02ebf1108eb4cf43d48b6134dc9a3fcb.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 4

Sala Ya Jioni Ya Kuomba Msaada

Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi.

1 Nijibu nikuitapo,

Ee Mungu wangu mwenye haki!

Nipumzishe katika shida zangu;

nirehemu, usikie ombi langu.

2 Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu

kuwa aibu mpaka lini?

Mtapenda udanganyifu

na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?

3 Fahamuni hakika kwambaBwanaamewatenga

wale wamchao kwa ajili yake;

Bwanaatanisikia nimwitapo.

4 Katika hasira yako, usitende dhambi.

Mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya

mkiichunguza mioyo yenu.

5 Toeni dhabihu zilizo haki;

mtegemeeniBwana.

6 Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye

kutuonyesha jema lolote?”

EeBwana, tuangazie nuru ya uso wako.

7 Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa

kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.

8 Nitajilaza chini na kulala kwa amani,

kwa kuwa wewe peke yako, EeBwana,

waniwezesha kukaa kwa salama.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/4-d29771b2637e4953932c84584e8c7c0e.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 5

Sala Kwa Ajili Ya Ulinzi Wakati Wa Hatari

Kwa mwimbishaji. Kwa filimbi. Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, tegea sikio maneno yangu,

uangalie kupiga kite kwangu.

2 Sikiliza kilio changu ili unisaidie,

Mfalme wangu na Mungu wangu,

kwa maana kwako ninaomba.

3 Asubuhi, unasikia sauti yangu, EeBwana;

asubuhi naleta haja zangu mbele zako,

na kusubiri kwa matumaini.

4 Wewe si Mungu unayefurahia uovu,

kwako mtu mwovu hataishi.

5 Wenye kiburi hawawezi kusimama mbele yako,

unawachukia wote watendao mabaya.

6 Unawaangamiza wasemao uongo.

Bwanahuwachukia

wamwagao damu na wadanganyifu.

7 Lakini mimi, kwa rehema zako kuu,

nitakuja katika nyumba yako,

kwa unyenyekevu, nitasujudu

kuelekea Hekalu lako takatifu.

8 Niongoze katika haki yako, EeBwana,

kwa sababu ya adui zangu,

nyoosha njia yako mbele yangu.

9 Hakuna neno kinywani mwao linaloweza kuaminika,

mioyo yao imejaa maangamizi.

Koo lao ni kaburi lililo wazi,

kwa ndimi zao, wao hunena udanganyifu.

10 Uwatangaze kuwa wenye hatia, Ee Mungu!

Hila zao ziwe anguko lao wenyewe.

Wafukuzie mbali kwa sababu ya dhambi zao nyingi,

kwa kuwa wamekuasi wewe.

11 Lakini wote wakimbiliao kwako na wafurahi,

waimbe kwa shangwe daima.

Ueneze ulinzi wako juu yao,

ili wale wapendao jina lako

wapate kukushangilia.

12 Kwa hakika, EeBwana, unawabariki wenye haki,

unawazunguka kwa wema wako kama ngao.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/5-2a517cdb34986fc621a99e3f7cba50d4.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 6

Sala Kwa Ajili Ya Msaada Wakati Wa Taabu

Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa sheminithi.

Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, usinikemee katika hasira yako,

wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.

2 UnirehemuBwana,

kwa maana nimedhoofika;

EeBwana, uniponye,

kwa maana mifupa yangu

ina maumivu makali.

3 Nafsi yangu ina uchungu mwingi.

Mpaka lini, EeBwana, mpaka lini?

4 Geuka EeBwana, unikomboe,

uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.

5 Hakuna mtu anayekukumbuka

akiwa amekufa.

Ni nani awezaye kukusifu

akiwa kuzimu?

6 Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni;

usiku kucha nafurikisha

kitanda changu kwa machozi;

nimelowesha viti vyangu vya fahari

kwa machozi.

7 Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika,

yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.

8 Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya,

kwa maanaBwanaamesikia kulia kwangu.

9 Bwanaamesikia kilio changu kwa huruma,

Bwanaamekubali sala yangu.

10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika,

watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/6-a9a79421fa300ef0aa37e5024d36f37d.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 7

Sala Ya Mtu Anayedhulumiwa

Ombolezo la Daudi kwa

Bwana

kwa sababu ya Kushi, Mbenyamini.

1 EeBwana, Mungu wangu, ninakukimbilia wewe,

uniokoe na kunikomboa na wote wanaonifuatia,

2 la sivyo watanirarua kama simba

na kunichana vipande vipande, asiwepo wa kuniokoa.

3 EeBwana, Mungu wangu, kama nimetenda haya

na kuna hatia mikononi mwangu,

4 au ikiwa nimemtenda uovu aliye na amani nami,

au nimemnyangʼanya adui yangu pasipo sababu,

5 basi adui anifuatie na kunipata,

auponde uhai wangu ardhini

na kunilaza mavumbini.

6 Amka kwa hasira yako, EeBwana,

inuka dhidi ya ghadhabu ya adui zangu.

Amka, Mungu wangu, uamue haki.

7 Kusanyiko la watu na likuzunguke.

Watawale kutoka juu.

8 Bwanana awahukumu kabila za watu.

Nihukumu EeBwana,

kwa kadiri ya haki yangu,

kwa kadiri ya uadilifu wangu,

Ewe Uliye Juu Sana.

9 Ee Mungu mwenye haki,

uchunguzaye mawazo na mioyo,

komesha ghasia za waovu

na ufanye wenye haki waishi kwa amani.

10 Ngao langu ni Mungu Aliye Juu Sana,

awaokoaye wanyofu wa moyo.

11 Mungu ni mwamuzi mwenye haki,

Mungu aghadhibikaye kila siku.

12 Kama hakutuhurumia,

atanoa upanga wake,

ataupinda na kuufunga uzi upinde wake.

13 Ameandaa silaha zake kali,

ameweka tayari mishale yake ya moto.

14 Yeye aliye na mimba ya uovu

na achukuaye mimba ya ghasia huzaa uongo.

15 Yeye achimbaye shimo na kulifukua

hutumbukia katika shimo alilochimba mwenyewe.

16 Ghasia azianzishazo humrudia mwenyewe,

ukatili wake humrudia kichwani.

17 NitamshukuruBwanakwa ajili ya haki yake,

na nitaliimbia sifa jina laBwanaAliye Juu Sana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/7-9e53f9c428c3200c087bbe4527cde841.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 8

Utukufu Wa Mungu Na Heshima Ya Mwanadamu

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, Bwana wetu,

tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

Umeuweka utukufu wako

juu ya mbingu.

2 Midomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao

umeamuru sifa,

kwa sababu ya watesi wako,

kumnyamazisha adui na mlipiza kisasi.

3 Nikiziangalia mbingu zako,

kazi ya vidole vyako,

mwezi na nyota,

ulizoziratibisha,

4 mwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria,

binadamu ni nani hata unamjali?

5 Umemfanya chini kidogo kuliko viumbe wa mbinguni,

ukamvika taji ya utukufu na heshima.

6 Umemfanya mtawala juu ya kazi za mikono yako;

umeweka vitu vyote chini ya miguu yake.

7 Mifugo na makundi yote pia,

naam, na wanyama wa kondeni,

8 ndege wa angani na samaki wa baharini,

naam, kila kiogeleacho katika njia za bahari.

9 EeBwana, Bwana wetu,

tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/8-9b9688e20a06c6dd7f5a4839406532c4.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 9

Shukrani Kwa Mungu Kwa Ajili Ya Haki Yake

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa muth-labeni.

Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, nitakutukuza kwa moyo wangu wote,

nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.

2 Nitafurahi na kushangilia ndani yako.

Nitaliimbia sifa jina lako, Ewe Uliye Juu Sana.

3 Adui zangu wamerudi nyuma,

wamejikwaa na kuangamia mbele zako.

4 Kwa maana umetetea haki yangu na msimamo wangu;

umeketi kwenye kiti chako cha enzi,

ukihukumu kwa haki.

5 Umekemea mataifa na kuwaangamiza waovu;

umeyafuta majina yao milele na milele.

6 Uharibifu usiokoma umempata adui,

umeingʼoa miji yao;

hata kumbukumbu lao limetoweka.

7 Bwanaanatawala milele,

ameweka kiti chake cha enzi apate kuhukumu.

8 Mungu atahukumu ulimwengu kwa haki,

atatawala mataifa kwa haki.

9 Bwanani kimbilio la watu wanaoonewa,

ni ngome imara wakati wa shida.

10 Wote wanaolijua jina lako watakutumaini wewe,

kwa maana weweBwana,

hujawaacha kamwe wakutafutao.

11 MwimbieniBwanasifa, amefanywa mtawala Sayuni,

tangazeni miongoni mwa mataifa, yale aliyoyatenda.

12 Kwa maana yeye alipizaye kisasi cha damu hukumbuka,

hapuuzi kilio cha wanaoonewa.

13 EeBwana, tazama jinsi walivyo wengi adui zangu wanaonitesa!

Nihurumie, uniinue kutoka malango ya mauti,

14 ili niweze kutangaza sifa zako

katika malango ya Binti Sayuni

na huko niushangilie wokovu wako.

15 Mataifa wameanguka kwenye shimo walilolichimba,

miguu yao imenaswa kwenye wavu waliouficha.

16 Bwanaanajulikana kwa haki yake,

waovu wamenaswa katika kazi za mikono yao.

17 Waovu wataishia kuzimu,

naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu.

18 Lakini mhitaji hatasahaulika siku zote,

wala matumaini ya walioonewa hayatapotea.

19 EeBwana, inuka, usimwache binadamu ashinde.

Mataifa na yahukumiwe mbele zako.

20 EeBwana, wapige kwa hofu,

mataifa na yajue kuwa wao ni watu tu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/9-0f5efef9c3685c2abd60fe6eb0bef333.mp3?version_id=1627—