Categories
Isaya

Isaya 10

1 Ole wao wawekao sheria zisizo za haki,

kwa wale watoao amri za kuonea,

2 kuwanyima maskini haki zao

na kuzuilia haki za watu wangu walioonewa,

kuwafanya wajane mawindo yao

na kuwanyangʼanya yatima.

3 Mtafanya nini siku ya kutoa hesabu,

wakati maafa yatakapokuja kutoka mbali?

Mtamkimbilia nani awape msaada?

Mtaacha wapi mali zenu?

4 Hakutasalia kitu chochote,

isipokuwa kujikunyata miongoni mwa mateka,

au kuanguka miongoni mwa waliouawa.

Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali,

mkono wake bado umeinuliwa juu.

Hukumu Ya Mungu Juu Ya Ashuru

5 “Ole kwa Ashuru, fimbo ya hasira yangu,

ambaye mkononi mwake ana rungu ya ghadhabu yangu!

6 Ninamtuma dhidi ya taifa lisilomjua Mungu,

ninamtuma dhidi ya taifa linalonikasirisha,

kukamata mateka na kunyakua nyara,

pia kuwakanyaga chini kama matope ya barabarani.

7 Lakini hili silo analokusudia,

hili silo alilo nalo akilini;

kusudi lake ni kuangamiza,

kuyakomesha mataifa mengi.

8 Maana asema, ‘Je, wafalme wote

si majemadari wangu?

9 Je, Kalno hakutendwa kama Karkemishi?

Hamathi si kama Arpadi,

nayo Samaria si kama Dameski?

10 Kama vile mkono wangu ulivyotwaa falme za sanamu,

falme ambazo vinyago vyao vilizidi vile vya Yerusalemu na Samaria:

11 je, nisiishughulikie Yerusalemu na sanamu zake

kama nilivyoshughulikia Samaria na vinyago vyake?’ ”

12 Bwana atakapokuwa amemaliza kazi yake yote dhidi ya Mlima Sayuni na Yerusalemu, atasema, “Nitamwadhibu mfalme wa Ashuru kwa ajili ya majivuno ya ukaidi wa moyo wake na kutazama kwa macho yenye dharau.”

13 Kwa kuwa anasema:

“ ‘Kwa nguvu za mkono wangu nimefanya hili,

kwa hekima yangu, kwa sababu nina ufahamu.

Niliondoa mipaka ya mataifa,

niliteka nyara hazina zao,

kama yeye aliye shujaa

niliwatiisha wafalme wao.

14 Kama mtu atiavyo mkono kwenye kiota,

ndivyo mkono wangu ulivyochukua utajiri wa mataifa;

kama watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa,

ndivyo nilivyokusanya nchi zote;

wala hakuna hata mmoja aliyepiga bawa

au kufungua kinywa chake kutoa mlio.’ ”

15 Je, shoka laweza kujigamba kuwa na nguvu zaidi

kuliko yule anayelitumia,

au msumeno kujisifu

dhidi ya yule anayeutumia?

Ni kana kwamba fimbo ingeweza kumwinua yeye aichukuaye,

au mkongojo ungemwinua mwenye kuutumia!

16 Kwa hiyo Bwana,BwanaMwenye Nguvu Zote,

atatuma ugonjwa wa kudhoofisha kwa askari wake walio hodari,

katika fahari yake moto utawaka

kama mwali wa moto.

17 Nuru ya Israeli itakuwa moto,

Aliye Mtakatifu wao mwali wa moto;

katika siku moja utaunguza na kuteketeza miiba

na michongoma yake.

18 Fahari ya misitu yake na mashamba yenye rutuba

utateketeza kabisa,

kama vile mtu mgonjwa adhoofikavyo.

19 Nayo miti inayobaki katika misitu yake itakuwa michache sana

hata mtoto mdogo angeweza kuihesabu.

Mabaki Ya Israeli

20 Katika siku ile, mabaki ya Israeli,

walionusurika wa nyumba ya Yakobo,

hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga,

lakini watamtegemea kwa kweli

BwanaAliye Mtakatifu wa Israeli.

21 Mabaki watarudi,mabaki wa Yakobo

watamrudia Mungu Mwenye Nguvu.

22 Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani,

ni mabaki yao tu watakaorudi.

Maangamizi yamekwisha amriwa,

ni mengi tena ni haki.

23 Bwana,BwanaMwenye Nguvu Zote, atatekeleza

maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote.

24 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana,BwanaMwenye Nguvu Zote asemalo:

“Enyi watu wangu mkaao Sayuni,

msiwaogope Waashuru,

wanaowapiga ninyi kwa fimbo

na kuinua rungu dhidi yenu, kama Misri ilivyofanya.

25 Bado kitambo kidogo sana hasira yangu dhidi yenu itakoma,

na ghadhabu yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.”

26 BwanaMwenye Nguvu Zote atawachapa kwa mjeledi,

kama alivyowapiga Wamidiani katika mwamba wa Orebu,

naye atainua fimbo yake juu ya maji,

kama alivyofanya huko Misri.

27 Katika siku hiyo mzigo wao utainuliwa kutoka mabegani mwenu,

na nira yao kutoka shingoni mwenu;

nira itavunjwa

kwa sababu ya kutiwa mafuta.

28 Wanaingia Ayathi,

wanapita katikati ya Migroni,

wanahifadhi mahitaji huko Mikmashi.

29 Wanavuka kivukoni, nao wanasema,

“Tutapiga kambi huko Geba usiku kucha.”

Rama inatetemeka;

Gibea ya Sauli inakimbia.

30 Piga kelele, ee Binti Galimu!

Sikiliza, ee Laisha!

Maskini Anathothi!

31 Madmena inakimbia;

watu wa Gebimu wanajificha.

32 Siku hii ya leo watasimama Nobu;

watatikisa ngumi zao

kwa mlima wa Binti Sayuni,

kwa kilima cha Yerusalemu.

33 Tazama, Bwana,BwanaMwenye Nguvu Zote,

atayakata matawi kwa nguvu kuu.

Miti mirefu sana itaangushwa,

ile mirefu itashushwa chini.

34 Atakata vichaka vya msitu kwa shoka;

Lebanoni itaanguka mbele zake yeye Mwenye Nguvu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ISA/10-534bef37fc072b5a69f674d40031757a.mp3?version_id=1627—

Categories
Isaya

Isaya 11

Tawi Kutoka Kwa Yese

1 Chipukizi litatokea kutoka shina la Yese,

kutoka mizizi yake Tawi litazaa tunda.

2 Roho waBwanaatakaa juu yake,

Roho wa hekima na wa ufahamu,

Roho wa shauri na wa uweza,

Roho wa maarifa na wa kumchaBwana

3 naye atafurahia kumchaBwana.

Hatahukumu kwa yale ayaonayo kwa macho yake,

wala kuamua kwa yale ayasikiayo kwa masikio yake,

4 bali kwa uadilifu atahukumu wahitaji,

kwa haki ataamua wanyenyekevu wa dunia.

Ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake,

kwa pumzi ya midomo yake atawaua waovu.

5 Haki itakuwa mkanda wake

na uaminifu utakuwa mshipi kiunoni mwake.

6 Mbwa mwitu ataishi pamoja na mwana-kondoo,

naye chui atalala pamoja na mbuzi,

ndama, mwana simba na ngʼombe wa mwaka mmoja watakaa pamoja,

naye mtoto mdogo atawaongoza.

7 Ngʼombe na dubu watalisha pamoja,

watoto wao watalala pamoja,

na simba atakula majani makavu kama maksai.

8 Mtoto mchanga atacheza karibu na shimo la nyoka,

naye mtoto mdogo ataweka mkono wake

kwenye kiota cha fira.

9 Hawatadhuru wala kuharibu

juu ya mlima wangu mtakatifu wote,

kwa kuwa dunia itajawa na kumjuaBwana

kama maji yajazavyo bahari.

10 Katika siku hiyo, Shina la Yese atasimama kama bendera kwa ajili ya mataifa. Mataifa yatakusanyika kwake, na mahali pake pa kupumzikia patakuwa utukufu.

11 Katika siku hiyo Bwana atanyoosha mkono wake mara ya pili kurudisha mabaki ya watu wake waliosalia kutoka Ashuru, Misri, Pathrosi,Kushi, Elamu, Babeli, Hamathi na kutoka visiwa vya baharini.

12 Atainua bendera kwa mataifa

na kuwakusanya Waisraeli walioko uhamishoni;

atawakusanya watu wa Yuda waliotawanyika

kutoka pembe nne za dunia.

13 Wivu wa Efraimu utatoweka,

na adui wa Yuda watakatiliwa mbali;

Efraimu hatamwonea Yuda wivu,

wala Yuda hatakuwa na uadui na Efraimu.

14 Watawashukia katika miteremko ya Wafilisti

hadi upande wa magharibi,

kwa pamoja watawateka watu nyara

hadi upande wa mashariki.

Watawapiga Edomu na Moabu,

na Waamoni watatawaliwa nao.

15 Bwanaatakausha

ghuba ya bahari ya Misri;

kwa upepo mkavu ataupeleka mkono wake

juu ya Mto Frati.

Ataugawanya katika vijito saba

ili watu waweze kuuvuka wakiwa wamevaa viatu.

16 Itakuwepo njia kuu kwa mabaki ya watu wake

wale waliosalia kutoka Ashuru,

kama ilivyokuwa kwa Israeli

walipopanda kutoka Misri.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ISA/11-2d0bea8c3d526964595a3f81ddac2594.mp3?version_id=1627—

Categories
Isaya

Isaya 12

Kushukuru Na Kusifu

1 Katika siku ile utasema:

“Nitakusifu wewe, EeBwana.

Ingawa ulinikasirikia,

hasira yako imegeukia mbali

nawe umenifariji.

2 Hakika Mungu ni wokovu wangu;

nitamtumaini wala sitaogopa.

Bwana,Bwana, ni nguvu zangu na wimbo wangu;

amekuwa wokovu wangu.”

3 Kwa furaha mtachota maji

kutoka visima vya wokovu.

4 Katika siku hiyo mtasema:

“MshukuruniBwana, mliitie jina lake;

julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya,

tangazeni kuwa jina lake limetukuka.

5 MwimbieniBwana, kwa kuwa ametenda mambo makuu,

hili na lijulikane duniani kote.

6 Pazeni sauti mwimbe kwa furaha, watu wa Sayuni,

kwa maana mkuu ni yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli miongoni mwenu.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ISA/12-3cb1715dd81e8f1610a2b4da0e31be68.mp3?version_id=1627—

Categories
Isaya

Isaya 13

Unabii Dhidi Ya Babeli

1 Neno kuhusu Babeli ambalo Isaya mwana wa Amozi aliliona:

2 Twekeni bendera juu ya mlima usio na kitu,

wapazieni sauti,

wapungieni mkono waingie

katika malango ya wenye heshima.

3 Nimewaamuru watakatifu wangu;

nimewaita mashujaa wangu waitimize hasira yangu:

wale wanaoshangilia ushindi wangu.

4 Sikilizeni kelele juu ya milima,

kama ile ya umati mkubwa wa watu!

Sikilizeni, makelele katikati ya falme,

kama mataifa yanayokusanyika pamoja!

BwanaMwenye Nguvu Zote anakusanya

jeshi kwa ajili ya vita.

5 Wanakuja kutoka nchi za mbali sana,

kutoka miisho ya mbingu,

Bwanana silaha za ghadhabu yake,

kuangamiza nchi yote.

6 Ombolezeni, kwa maana siku yaBwanai karibu,

itakuja kama uharibifu kutoka kwa Mwenyezi.

7 Kwa sababu ya hili, mikono yote italegea,

moyo wa kila mtu utayeyuka.

8 Hofu itawakamata,

uchungu na maumivu makali yatawashika,

watagaagaa kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa.

Watatazamana kwa hofu kila mtu na mwenzake,

nyuso zao zikiwaka kama moto.

9 Tazameni, siku yaBwanainakuja,

siku katili, yenye ghadhabu na hasira kali,

kuifanya nchi kuwa ukiwa

na kuwaangamiza wenye dhambi waliomo ndani yake.

10 Nyota za mbinguni na makundi ya nyota

havitatoa mwanga wake.

Jua linalochomoza litatiwa giza

na mwezi hautatoa nuru yake.

11 Nitauadhibu ulimwengu kwa ajili ya uovu wake,

waovu kwa ajili ya dhambi zao.

Nitakomesha majivuno ya wenye kiburi,

na nitakishusha kiburi cha watu wakatili.

12 Nitawafanya wanadamu kuwa adimu kuliko dhahabu safi,

watakuwa wachache sana kuliko dhahabu ya Ofiri.

13 Kwa hiyo nitazifanya mbingu zitetemeke,

nayo dunia itatikisika kutoka mahali pake

katika ghadhabu yaBwanaMwenye Nguvu Zote,

katika siku ya hasira yake iwakayo.

14 Kama swala awindwaye,

kama kondoo wasio na mchungaji,

kila mmoja atarudi kwa watu wake mwenyewe,

kila mmoja atakimbilia nchi yake ya kuzaliwa.

15 Yeyote atakayetekwa atapasuliwa tumbo,

wote watakaokamatwa watauawa kwa upanga.

16 Watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande

mbele ya macho yao;

nyumba zao zitatekwa

na wake zao watatendwa jeuri.

17 Tazama, nitawachochea Wamedi dhidi yao,

ambao hawajali fedha

wala hawafurahii dhahabu.

18 Mishale yao itawaangusha vijana,

hawatakuwa na huruma kwa watoto wachanga

wala hawataangalia watoto kwa huruma.

19 Babeli, johari ya falme,

utukufu wa kiburi cha Wababeli,

itaangushwa na Mungu

kama Sodoma na Gomora.

20 Hautakaliwa na watu kamwe

wala watu hawataishi humo kwa vizazi vyote.

Hakuna Mwarabu atakayepiga hema lake huko,

hakuna mchungaji atakayepumzisha makundi yake huko.

21 Lakini viumbe wa jangwani watalala huko,

mbweha watajaza nyumba zake,

bundi wataishi humo

nao mbuzi-mwitu watarukaruka humo.

22 Fisi watalia ndani ya ngome zake,

mbweha ndani ya majumba yake ya kifahari.

Wakati wake umewadia,

na siku zake hazitaongezwa.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ISA/13-151cf828900c0ae989de041b08c49078.mp3?version_id=1627—

Categories
Isaya

Isaya 14

Yuda Kufanywa Upya

1 Bwanaatamhurumia Yakobo,

atamchagua Israeli tena,

na kuwakalisha katika nchi yao wenyewe.

Wageni wataungana nao

na kujiunga na nyumba ya Yakobo.

2 Mataifa watawachukua

na kuwaleta mahali pao wenyewe.

Nayo nyumba ya Israeli itamiliki mataifa

kama watumishi na wajakazi katika nchi yaBwana.

Watawafanya watekaji wao kuwa mateka,

na kutawala juu ya wale waliowaonea.

3 Katika sikuBwanaatakapokuondolea mateso, udhia na utumwa wa kikatili,

4 utaichukua dhihaka hii dhidi ya mfalme wa Babeli:

Tazama jinsi mtesi alivyofikia mwisho!

Tazama jinsi ghadhabu yake kali ilivyokoma!

5 Bwanaamevunja fimbo ya mwovu,

fimbo ya utawala ya watawala,

6 ambayo kwa hasira waliyapiga mataifa

kwa mapigo yasiyo na kikomo,

nao kwa ghadhabu kali waliwatiisha mataifa

kwa jeuri pasipo huruma.

7 Nchi zote ziko kwenye mapumziko na kwenye amani,

wanabubujika kwa kuimba.

8 Hata misunobari na mierezi ya Lebanoni

inashangilia mbele yako na kusema,

“Basi kwa sababu umeangushwa chini,

hakuna mkata miti atakayekuja kutukata.”

9 Kuzimu kote kumetaharuki

kukulaki unapokuja,

kunaamsha roho za waliokufa ili kukupokea,

wote waliokuwa viongozi katika ulimwengu,

kunawafanya wainuke kwenye viti vyao vya kifalme:

wale wote waliokuwa wafalme juu ya mataifa.

10 Wote wataitikia,

watakuambia,

“Wewe pia umekuwa dhaifu, kama sisi tulivyo;

wewe umekuwa kama sisi.”

11 Majivuno yako yote yameshushwa mpaka kuzimu,

pamoja na kelele ya vinubi vyako,

mafunza yametanda chini yako,

na minyoo imekufunika.

12 Tazama jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni,

ewe nyota ya asubuhi, mwana wa mapambazuko!

Umetupwa chini duniani,

wewe uliyepata kuangusha mataifa!

13 Ulisema moyoni mwako,

“Nitapanda juu hadi mbinguni,

nitakiinua kiti changu cha enzi

juu ya nyota za Mungu,

nitaketi nimetawazwa

juu ya mlima wa kusanyiko,

kwenye vimo vya juu sana vya Mlima Mtakatifu.

14 Nitapaa juu kupita mawingu,

nitajifanya kama Yeye Aliye Juu Sana.”

15 Lakini umeshushwa chini hadi kuzimu,

hadi kwenye vina vya shimo.

16 Wale wanaokuona wanakukazia macho,

wanatafakari hatima yako:

“Je, huyu ndiye yule aliyetikisa dunia

na kufanya falme zitetemeke,

17 yule aliyeifanya dunia kuwa jangwa,

aliyeipindua miji yake,

na ambaye hakuwaachia mateka wake

waende nyumbani?”

18 Wafalme wote wa mataifa wamelala kwa heshima

kila mmoja katika kaburi lake.

19 Lakini wewe umetupwa nje ya kaburi lako

kama tawi lililokataliwa,

umefunikwa na waliouawa

pamoja na wale waliochomwa kwa upanga,

wale washukao mpaka

kwenye mawe ya shimo.

Kama mzoga uliokanyagwa chini ya nyayo,

20 Hutajumuika nao kwenye mazishi,

kwa kuwa umeharibu nchi yako

na kuwaua watu wako.

Mzao wa mwovu

hatatajwa tena kamwe.

21 Andaa mahali pa kuwachinjia wanawe

kwa ajili ya dhambi za baba zao,

wasije wakainuka ili kuirithi nchi

na kuijaza dunia kwa miji yao.

22 BwanaMwenye Nguvu Zote asema,

“Nitainuka dhidi yao,

nitalikatilia mbali jina lake kutoka Babeli pamoja na watu wake walionusurika,

watoto wake na wazao wake,”

asemaBwana.

23 “Nitaifanya kuwa mahali pa bundi,

na kuwa nchi ya matope;

nitaifagia kwa ufagio wa maangamizi,”

asemaBwanaMwenye Nguvu Zote.

Unabii Dhidi Ya Ashuru

24 BwanaMwenye Nguvu Zote ameapa,

“Hakika, kama vile nilivyopanga, ndivyo itakavyokuwa,

nami kama nilivyokusudia, ndivyo itakavyosimama.

25 Nitamponda Mwashuru katika nchi yangu,

juu ya milima yangu nitawakanyagia chini.

Nira yake itaondolewa kutoka kwa watu wangu,

nao mzigo wake utaondolewa kutoka mabegani mwao.”

26 Huu ndio mpango uliokusudiwa kwa ajili ya ulimwengu wote,

huu ni mkono ulionyooshwa juu ya mataifa yote.

27 Kwa kuwaBwanaMwenye Nguvu Zote amekusudia,

ni nani awezaye kumzuia?

Mkono wake umenyooshwa,

ni nani awezaye kuurudisha?

Unabii Dhidi Ya Wafilisti

28 Neno hili lilikuja mwaka ule Mfalme Ahazi alipofariki:

29 Msifurahi, enyi Wafilisti wote,

kwamba fimbo iliyowapiga imevunjika;

kutoka mzizi wa huyo nyoka

atachipuka nyoka mwenye sumu kali,

uzao wake utakuwa joka lirukalo,

lenye sumu kali.

30 Maskini kuliko maskini wote watapata malisho,

nao wahitaji watalala salama.

Lakini mzizi wako nitauangamiza kwa njaa,

nayo njaa itawaua walionusurika.

31 Piga yowe, ee lango! Bweka, ee mji!

Yeyukeni, enyi Wafilisti wote!

Wingu la moshi linakuja toka kaskazini,

wala hakuna atakayechelewa katika safu zake.

32 Ni jibu gani litakalotolewa

kwa wajumbe wa taifa hilo?

“Bwanaameifanya imara Sayuni,

nako ndani yake watu wake walioonewa watapata kimbilio.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ISA/14-eae0592fce4bc6b4c99ed9ef6670f182.mp3?version_id=1627—

Categories
Isaya

Isaya 15

Unabii Dhidi Ya Moabu

1 Neno kuhusu Moabu:

Ari iliyo Moabu imeangamizwa:

imeharibiwa kwa usiku mmoja!

Kiri iliyo Moabu imeangamizwa,

imeharibiwa kwa usiku mmoja!

2 Diboni anakwea hadi kwenye hekalu lake,

mpaka mahali pake pa juu ili walie,

Moabu anaombolezea Nebo na Medeba.

Kila kichwa kimenyolewa

na kila ndevu limeondolewa.

3 Wamevaa nguo za magunia barabarani,

juu ya mapaa na kwenye viwanja

wote wanaomboleza,

wamelala kifudifudi kwa kulia.

4 Heshboni na Eleale wanalia,

sauti zao zinasikika hadi Yahazi.

Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu wanapiga kelele,

nayo mioyo yao imezimia.

5 Moyo wangu unamlilia Moabu;

wakimbizi wake wanakimbilia Soari,

hadi Eglath-Shelishiya.

Wanapanda njia ya kwenda Luhithi,

wanakwenda huku wanalia;

barabarani iendayo Horonaimu

wanaombolezea maangamizi yao.

6 Maji ya Nimrimu yamekauka

na majani yamenyauka;

mimea imekauka wala hakuna

kitu chochote kibichi kilichobaki.

7 Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba

wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi.

8 Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu,

kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu,

maombolezo yao hadi Beer-Elimu.

9 Maji ya Dimoni yamejaa damu,

lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni:

simba juu ya wakimbizi wa Moabu

na juu ya wale wanaobaki katika nchi.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ISA/15-f1ae431bfd5abb13adc60051601fe9a6.mp3?version_id=1627—

Categories
Isaya

Isaya 16

Hali Ya Kukata Tamaa Ya Moabu

1 Pelekeni wana-kondoo kama ushuru

kwa mtawala wa nchi,

Kutoka Sela, kupitia jangwani,

hadi mlima wa Binti Sayuni.

2 Kama ndege wanaopapatika

waliofukuzwa kutoka kwenye kiota,

ndivyo walivyo wanawake wa Moabu

kwenye vivuko vya Arnoni.

3 “Tupeni shauri,

toeni uamuzi.

Wakati wa adhuhuri,

fanyeni kivuli chenu kama usiku.

Waficheni watoro,

msisaliti wakimbizi.

4 Waacheni watoro wa Moabu wakae pamoja nanyi;

kuweni mahali pao pa salama ili kuepuka mharabu.”

Mtesi atafikia mwisho na maangamizi yatakoma,

aletaye vita atatoweka kutoka nchi.

5 Kwa upendo kiti cha enzi kitaimarishwa,

kwa uaminifu mtu ataketi juu yake,

yeye atokaye nyumba ya Daudi:

yeye ambaye katika kuhukumu hutafuta haki,

na huhimiza njia ya haki.

6 Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu:

kiburi chake cha kujivuna na udanganyifu,

kiburi chake na ufidhuli wake,

lakini majivuno yake si kitu.

7 Kwa hiyo Wamoabu wanaomboleza,

wanaiombolezea Moabu kwa pamoja.

Wanaomboleza na kuhuzunika

kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.

8 Mashamba ya Heshboni yananyauka,

pia na mizabibu ya Sibma.

Watawala wa mataifa

wamekanyaga mizabibu iliyo mizuri sana,

ambayo ilipata kufika Yazeri

na kuenea kuelekea jangwani.

Machipukizi yake yalienea

yakafika hadi baharini.

9 Hivyo ninalia kama Yazeri aliavyo,

kwa ajili ya mizabibu ya Sibma.

Ee Heshboni, ee Eleale,

ninakulowesha kwa machozi!

Kelele za furaha kwa ajili ya tunda lako lililoiva

na kwa ajili ya mavuno zimekomeshwa.

10 Furaha na shangwe zimeondolewa

kutoka mashamba ya matunda;

hakuna yeyote aimbaye wala apazaye sauti

katika mashamba ya mizabibu;

hakuna yeyote akanyagaye zabibu shinikizoni,

kwa kuwa nimekomesha makelele.

11 Moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama kinubi,

nafsi yangu yote kwa ajili ya Kir-Haresethi.

12 Wakati Moabu anapojitokeza mahali pake pa juu,

anajichosha mwenyewe tu;

anapokwenda mahali pake pa kuabudia miungu ili kuomba,

haitamfaidi lolote.

13 Hili ndilo neno ambaloBwanaameshasema kuhusu Moabu.

14 Lakini sasaBwanaanasema: “Katika miaka mitatu, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, fahari ya Moabu na watu wake wengi watadharauliwa, nao walionusurika watakuwa wachache sana, tena wanyonge.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ISA/16-d91df6bdb9aa60c24594b248f5d7ef31.mp3?version_id=1627—

Categories
Isaya

Isaya 17

Neno Dhidi Ya Dameski

1 Neno kuhusu Dameski:

“Tazama, Dameski haitakuwa tena mji

bali itakuwa lundo la magofu.

2 Miji ya Aroeri itaachwa

na itaachiwa mifugo ambayo italala huko,

bila yeyote wa kuyaogopesha.

3 Mji wenye ngome utatoweka kutoka Efraimu,

nao uweza wa ufalme kutoka Dameski;

mabaki ya Aramu yatakuwa

kama utukufu wa Waisraeli,”

asemaBwanaMwenye Nguvu Zote.

4 “Katika siku ile utukufu wa Yakobo utafifia,

unono wa mwili wake utadhoofika.

5 Itakuwa kama mvunaji akusanyavyo nafaka

na kuvuna nafaka kwa mikono yake,

kama wakati mtu aokotapo masazo ya masuke

katika Bonde la Warefai.

6 Hata hivyo baadhi ya masazo yatabaki,

kama vile mti wa mzeituni unavyopigwa,

kukiachwa zeituni mbili au tatu juu ya matawi kileleni,

nne au tano katika matawi yazaayo sana,”

asemaBwana, Mungu wa Israeli.

7 Katika siku ile watu watamwangalia Muumba wao,

na kuelekeza macho yao kwa yule Aliye Mtakatifu wa Israeli.

8 Hawataziangalia tena madhabahu,

kazi za mikono yao,

nao hawataheshimu nguzo za Ashera,

na madhabahu za kufukizia uvumba zilizofanywa kwa mikono yao.

9 Katika siku ile miji yao iliyo imara, ambayo waliihama kwa sababu ya Waisraeli, itakuwa kama mahali palipoachwa pa vichaka na magugu. Nayo yote itakuwa ukiwa.

10 Mmemsahau Mungu Mwokozi wenu,

hamkumkumbuka Mwamba aliye ngome yenu.

Kwa hiyo, hata ingawa mlipandikiza mimea iliyo mizuri sana

na kuotesha mizabibu ya kigeni,

11 hata kama siku ile unapoipandikiza, unaifanya iote

na asubuhi ile ile unayoipanda, unaifanya ichipue,

hata hivyo mavuno yatakuwa kama si kitu

katika siku ile ya ugonjwa na maumivu yasiyoponyeka.

12 Lo! Ghadhabu ya mataifa mengi,

wanaghadhibika kama bahari iliyochafuka!

Lo! Makelele ya mataifa

wanavuma kama ngurumo za maji mengi!

13 Ingawa mataifa yanavuma kama ngurumo za maji yanayofanya mawimbi,

wakati anapoyakemea yanakimbia mbali,

yanafukuzwa mbele ya upepo kama makapi juu ya milima,

kama jani livingirishwapo na dhoruba.

14 Wakati wa jioni, hofu ya ghafula!

Kabla ya asubuhi, wametoweka!

Hili ndilo fungu la wale wanaotupora,

fungu la wale wanaotunyangʼanya mali zetu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ISA/17-04b51c536a0dc3a1618bb7b3188095e8.mp3?version_id=1627—

Categories
Isaya

Isaya 18

Unabii Dhidi Ya Kushi

1 Ole kwa nchi ya mvumo wa mabawa,

kando ya mito ya Kushi,

2 iwapelekayo wajumbe wake kwa njia ya bahari

kwa mashua za mafunjo juu ya maji.

Nendeni, wajumbe wepesi,

kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo,

kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu,

taifa gomvi lenye lugha ngeni,

ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito.

3 Enyi mataifa yote ya ulimwengu,

ninyi mnaoishi duniani

wakati bendera itakapoinuliwa milimani,

mtaiona,

nayo tarumbeta itakapolia,

mtaisikia.

4 Hili ndiloBwanaaliloniambia:

“Nitatulia kimya na kutazama

kutoka maskani yangu,

kama joto linalometameta katika mwanga wa jua,

kama wingu la umande

katika joto la wakati wa mavuno.”

5 Kwa maana, kabla ya mavuno,

wakati wa kuchanua ukishapita

na maua yakawa zabibu zinazoiva,

atayakata machipukizi kwa mundu wa kupogolea matawi,

naye atakata na kuyaondoa matawi yaliyopanuka.

6 Yote yataachwa kwa ajili ya ndege wawindao wa mlimani

na wanyama pori,

ndege watajilisha juu yake wakati wote wa kiangazi,

nao wanyama pori wakati wote wa masika.

7 Wakati huo matoleo yataletwa kwaBwanaMwenye Nguvu Zote

kutoka kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo,

kutoka kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu,

kutoka taifa gomvi lenye lugha ngeni,

ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito,

matoleo yataletwa katika Mlima Sayuni, mahali pa Jina laBwanaMwenye Nguvu Zote.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ISA/18-57ad4b41e9dfa662f5ab0789c6356fd2.mp3?version_id=1627—

Categories
Isaya

Isaya 19

Unabii Kuhusu Misri

1 Neno kuhusu Misri:

Tazama,Bwanaamepanda juu ya wingu liendalo kwa haraka

naye anakuja Misri.

Sanamu za Misri zinatetemeka mbele yake,

nayo mioyo ya Wamisri inayeyuka ndani yao.

2 “Nitamchochea Mmisri dhidi ya Mmisri,

ndugu atapigana dhidi ya ndugu,

jirani dhidi ya jirani,

mji dhidi ya mji,

ufalme dhidi ya ufalme.

3 Wamisri watakufa moyo,

na nitaibatilisha mipango yao.

Watatafuta ushauri kwa sanamu na kwa roho za waliokufa,

kwa waaguzi na kwa wale waongeao na mizimu.

4 Nitawatia Wamisri

mikononi mwa bwana mkatili

na mfalme mkali atatawala juu yao,”

asema Bwana,BwanaMwenye Nguvu Zote.

5 Maji ya mito yatakauka,

chini ya mto kutakauka kwa jua.

6 Mifereji itanuka;

vijito vya Misri vitapungua

na kukauka.

Mafunjo na nyasi vitanyauka,

7 pia mimea iliyoko kando ya Mto Naili,

pale mto unapomwaga maji baharini.

Kila shamba lililopandwa kando ya Mto Naili litakauka,

litapeperushwa na kutoweka kabisa.

8 Wavuvi watalia na kuomboleza,

wale wote watupao ndoano katika Mto Naili,

watadhoofika kwa majonzi.

9 Wale watu wafanyao kazi ya kitani kilichochambuliwa watakata tamaa,

wafumaji wa kitani safi watavunjika moyo.

10 Wafanyao kazi ya kufuma nguo watahuzunishwa,

nao vibarua wataugua moyoni.

11 Maafisa wa Soani ni wapumbavu kabisa,

washauri wa Farao wenye busara wanatoa ushauri wa kijinga.

Unawezaje kumwambia Farao,

“Mimi ni mmojawapo wa watu wenye hekima,

mwanafunzi wa wafalme wa zamani”?

12 Wako wapi sasa watu wako wenye hekima?

Wao wakuonyeshe na kukufahamisha

ni niniBwanaMwenye Nguvu Zote

amepanga dhidi ya Misri.

13 Maafisa wa Soani wamekuwa wapumbavu,

viongozi wa Memfisiwamedanganyika,

walio mawe ya pembe ya taifa lake

wameipotosha Misri.

14 Bwanaamewamwagia

roho ya kizunguzungu;

wanaifanya Misri iyumbayumbe

katika yale yote inayoyafanya,

kama vile mlevi ayumbayumbavyo

katika kutapika kwake.

15 Misri haiwezi kufanya kitu chochote,

cha kichwa wala cha mkia,

cha tawi la mtende wala cha tete.

16 Katika siku ile Wamisri watakuwa kama wanawake. Watatetemeka kwa hofu mbele ya mkono waBwanaMwenye Nguvu Zote anaoinua dhidi yao.

17 Nayo nchi ya Yuda itawatia hofu Wamisri, kila mmoja atakayetajiwa Yuda ataingiwa na hofu, kwa sababu ya kile ambachoBwanaMwenye Nguvu Zote anapanga dhidi yao.

18 Katika siku hiyo miji mitano ya Misri, itazungumza lugha ya Kanaani, na kuapa kumtiiBwanaMwenye Nguvu Zote. Mji mmojawapo utaitwa Mji wa Uharibifu.

19 Katika siku hiyo patakuwepo madhabahu yaBwanakatikati ya Misri na mnara wa kumbukumbu kwaBwanakwenye mpaka wa Misri.

20 Itakuwa alama na ushahidi kwa ajili yaBwanaMwenye Nguvu Zote katika nchi ya Misri. WatakapomliliaBwanakwa sababu ya watesi wao, Mungu atawapelekea mwokozi na mtetezi, naye atawaokoa.

21 HivyoBwanaatajijulisha mwenyewe kwa Wamisri, nao katika siku hiyo watamkubaliBwana. Wataabudu kwa kumtolea dhabihu na sadaka za nafaka, watamwekeaBwananadhiri na kuzitimiza.

22 Bwanaataipiga Misri kwa tauni; atawapiga na kuwaponya. WatamgeukiaBwana, naye atayasikia maombi yao na kuwaponya.

23 Katika siku hiyo kutakuwepo na njia kuu kutoka Misri hadi Ashuru. Waashuru watakwenda Misri, na Wamisri watakwenda Ashuru. Wamisri na Waashuru wataabudu pamoja.

24 Katika siku hiyo Israeli itakuwa ya tatu, pamoja na Misri na Ashuru, nao watakuwa baraka kwa dunia.

25 BwanaMwenye Nguvu Zote atawabariki, akisema, “Baraka iwe kwa Misri watu wangu, kwa Ashuru kazi ya mikono yangu, na kwa Israeli urithi wangu.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/ISA/19-7e69346dd835d2fc7178455831747681.mp3?version_id=1627—