Categories
Hosea

Hosea 10

1 Israeli alikuwa mzabibu uliostawi sana,

alijizalia matunda mwenyewe.

Kadiri matunda yake yalivyoongezeka,

alijenga madhabahu zaidi;

kadiri nchi yake ilivyostawi,

alipamba mawe yake ya ibada.

2 Moyo wao ni mdanganyifu,

nao sasa lazima wachukue hatia yao.

Bwanaatabomoa madhabahu zao

na kuharibu mawe yao ya ibada.

3 Kisha watasema, “Hatuna mfalme

kwa sababu hatukumheshimuBwana.

Lakini hata kama tungelikuwa na mfalme,

angeweza kutufanyia nini?”

4 Wanaweka ahadi nyingi,

huapa viapo vya uongo

wanapofanya mapatano;

kwa hiyo mashtaka huchipuka

kama magugu ya sumu

katika shamba lililolimwa.

5 Watu wanaoishi Samaria huogopa

kwa ajili ya sanamu ya ndama ya Beth-Aveni.

Watu wake wataiombolezea,

vivyo hivyo kuhani wake wa kuabudu sanamu,

wale waliokuwa wamefurahia fahari yake,

kwa sababu itaondolewa kutoka kwao

kwenda uhamishoni.

6 Itachukuliwa kwenda Ashuru

kama ushuru kwa mfalme mkuu.

Efraimu atafedheheshwa;

Israeli ataaibika kwa ajili ya sanamu zake za mti.

7 Samaria na mfalme wake wataelea

kama kijiti juu ya uso wa maji.

8 Mahali pa kuabudia sanamu pa uovupataharibiwa:

ndiyo dhambi ya Israeli.

Miiba na mibaruti itaota

na kufunika madhabahu zao.

Kisha wataiambia milima, “Tufunikeni!”

na vilima, “Tuangukieni!”

9 “Tangu siku za Gibea, mmetenda dhambi, ee Israeli,

huko ndiko mlikobaki.

Je, vita havikuwapata

watenda mabaya huko Gibea?

10 Wakati nitakapopenda, nitawaadhibu;

mataifa yatakusanywa dhidi yao

ili kuwaweka katika vifungo

kwa ajili ya dhambi zao mbili.

11 Efraimu ni mtamba wa ngʼombe aliyefundishwa

ambaye hupenda kupura,

hivyo nitamfunga nira

juu ya shingo yake nzuri.

Nitamwendesha Efraimu,

Yuda lazima alime,

naye Yakobo lazima avunjavunje

mabonge ya udongo.

12 Jipandieni wenyewe haki,

vuneni matunda ya upendo usio na kikomo,

vunjeni ardhi yenu isiyolimwa;

kwa kuwa ni wakati wa kumtafutaBwana,

mpaka atakapokuja

na kuwanyeshea juu yenu haki.

13 Lakini mmepanda uovu,

mkavuna ubaya,

mmekula tunda la udanganyifu.

Kwa sababu mmetegemea nguvu zenu wenyewe

na wingi wa mashujaa wenu,

14 mngurumo wa vita utainuka dhidi ya watu wako,

ili kwamba ngome zako zote zitaharibiwa:

kama Shalmani alivyoharibu Beth-Arbeli katika siku ile ya vita,

wakati mama pamoja na watoto wao

walipotupwa kwa nguvu ardhini.

15 Ndivyo itakavyotokea kwako, ee Betheli,

kwa sababu uovu wako ni mkuu.

Siku ile itakapopambazuka,

mfalme wa Israeli ataharibiwa kabisa.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/10-8a3954d8315f85488382196086d379dc.mp3?version_id=1627—

Categories
Hosea

Hosea 11

Upendo Wa Mungu Kwa Israeli

1 “Wakati Israeli alipokuwa mtoto, nilimpenda,

nilimwita mwanangu kutoka Misri.

2 Lakini kadiri nilivyomwita Israeli,

ndivyo walivyokwenda mbali nami.

Walitoa dhabihu kwa Mabaali

na kufukiza uvumba kwa vinyago.

3 Mimi ndiye niliyemfundisha Efraimu kutembea,

nikiwashika mikono;

lakini hawakutambua

kuwa ni mimi niliyewaponya.

4 Niliwaongoza kwa kamba za huruma ya kibinadamu,

kwa vifungo vya upendo;

niliondoa nira shingoni mwao

nami nikainama kuwalisha.

5 “Je, hawatarudi Misri,

nayo Ashuru haitawatawala

kwa sababu wamekataa kutubu?

6 Panga zitametameta katika miji yao,

zitaharibu makomeo ya malango yao

na kukomesha mipango yao.

7 Watu wangu wamedhamiria kuniacha.

Hata kama wakimwita Yeye Aliye Juu Sana,

kwa vyovyote hatawainua.

8 “Efraimu, ninawezaje kukuacha?

Ee Israeli, ninawezaje kukutoa?

Nitawezaje kukutendea kama Adma?

Nitawezaje kukufanya kama Seboimu?

Moyo wangu umegeuka ndani yangu,

huruma zangu zote zimeamshwa.

9 Sitatimiza hasira yangu kali,

wala sitageuka na kumharibu Efraimu.

Kwa kuwa mimi ndimi Mungu,

wala si mwanadamu,

Aliye Mtakatifu miongoni mwenu.

Sitakuja kwa ghadhabu.

10 WatamfuataBwana;

atanguruma kama simba.

Wakati angurumapo,

watoto wake watakuja wakitetemeka

kutoka magharibi.

11 Watakuja wakitetemeka

kama ndege wakitoka Misri,

kama hua wakitoka Ashuru.

Nitawakalisha katika nyumba zao,”

asemaBwana.

Dhambi Ya Israeli

12 Efraimu amenizunguka kwa uongo,

nyumba ya Israeli kwa udanganyifu.

Naye Yuda ni mkaidi dhidi ya Mungu,

hata kinyume cha yule mwaminifu Aliye Mtakatifu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/11-000f60637bc045ab5428ac4196071c11.mp3?version_id=1627—

Categories
Hosea

Hosea 12

1 Efraimu anajilisha upepo;

hufukuzia upepo wa mashariki kutwa nzima

na kuzidisha uongo na jeuri.

Anafanya mkataba na Ashuru

na kutuma mafuta ya zeituni Misri.

2 Bwanaanalo shtaka dhidi ya Yuda,

atamwadhibu Yakobo kwa kadiri ya njia zake

na kumlipa kwa kadiri ya matendo yake.

3 Yakobo akiwa tumboni alishika kisigino cha kaka yake;

kama mwanadamu, alishindana na Mungu.

4 Alishindana na malaika na kumshinda;

alilia na kuomba upendeleo wake.

Alimkuta huko Betheli

na kuzungumza naye huko:

5 BwanaMungu Mwenye Nguvu Zote,

Bwanandilo jina lake!

6 Lakini ni lazima urudi kwa Mungu wako;

dumisha upendo na haki,

nawe umngojee Mungu wako siku zote.

7 Mfanyabiashara hutumia vipimo vya udanganyifu;

hupenda kupunja.

8 Efraimu hujisifu akisema,

“Mimi ni tajiri sana; nimetajirika.

Pamoja na utajiri wangu wote hawatakuta ndani yangu

uovu wowote au dhambi.”

9 “Mimi ndimiBwanaMungu wenu

niliyewaleta kutoka Misri;

nitawafanya mkae tena kwenye mahema,

kama vile katika siku

za sikukuu zenu zilizoamriwa.

10 Niliongea na manabii, nikawapa maono mengi

na kusema mifano kupitia wao.”

11 Je, Gileadi si mwovu?

Watu wake hawafai kitu!

Je, hawatoi dhabihu za mafahali huko Gilgali?

Madhabahu zao zitakuwa

kama malundo ya mawe

katika shamba lililolimwa.

12 Yakobo alikimbilia katika nchi ya Aramu;

Israeli alitumika ili apate mke,

ili aweze kulipa kwa ajili yake alichunga kondoo.

13 Bwanaalimtumia nabii

kumpandisha Israeli kutoka Misri,

kwa njia ya nabii alimtunza.

14 Lakini Efraimu amemchochea sana hasira;

Bwana wake ataleta juu yake

hatia yake ya kumwaga damu naye atamlipiza

kwa ajili ya dharau yake.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/12-78dc8f9269267ff93ed97af1852f50f0.mp3?version_id=1627—

Categories
Hosea

Hosea 13

Hasira Ya Bwana Dhidi Ya Israeli

1 Wakati Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka,

alikuwa ametukuzwa katika Israeli.

Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali

naye akafa.

2 Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi;

wanajitengenezea sanamu

kutokana na fedha yao,

vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari,

vyote kazi ya fundi stadi.

Inasemekana kuhusu hawa watu,

“Hutoa dhabihu za binadamu

na kubusu sanamu za ndama.”

3 Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi,

kama umande wa alfajiri utowekao,

kama makapi yapeperushwayo

kutoka sakafu ya kupuria nafaka,

kama moshi utorokao kupitia dirishani.

4 “Bali mimi ndimiBwanaMungu wenu,

niliyewaleta ninyi toka Misri.

Msimkubali Mungu mwingine ila mimi,

hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.

5 Niliwatunza huko jangwani,

katika nchi yenye joto liunguzalo.

6 Nilipowalisha, walishiba,

waliposhiba, wakajivuna,

kisha wakanisahau mimi.

7 Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba,

kama chui nitawavizia kando ya njia.

8 Kama dubu aliyenyangʼanywa watoto wake,

nitawashambulia na kurarua vifua vyenu.

Kama simba nitawala;

mnyama pori atawararua vipande vipande.

9 “Ee Israeli, umeangamizwa,

kwa sababu wewe u kinyume nami,

kinyume na msaidizi wako.

10 Yuko wapi mfalme wako,

ili apate kukuokoa?

Wako wapi watawala wako katika miji yako yote

ambao ulisema kuwahusu,

‘Nipe mfalme na wakuu’?

11 Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme

na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.

12 Kosa la Efraimu limehifadhiwa,

dhambi zake zimewekwa katika kumbukumbu.

13 Utungu kama wa mwanamke anayejifungua mtoto humjia,

lakini yeye ni mtoto asiyekuwa na hekima;

wakati utakapowadia hatatoka

katika tumbo la mama yake.

14 “Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi,

nitawakomboa kutoka mautini.

Yako wapi, ee mauti, mateso yako?

Uko wapi, ee kuzimu, uharibifu wako?

“Sitakuwa na huruma,

15 hata ingawa Efraimu atastawi

miongoni mwa ndugu zake.

Upepo wa mashariki kutoka kwaBwanautakuja,

ukivuma kutoka jangwani,

chemchemi yake haitatoa maji

na kisima chake kitakauka.

Ghala lake litatekwa

hazina zake zote.

16 Watu wa Samaria ni lazima wabebe hatia yao,

kwa sababu wameasi dhidi ya Mungu wao.

Wataanguka kwa upanga;

watoto wao wadogo watatupwa kwa nguvu ardhini,

wanawake wao walio na mimba watatumbuliwa.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/13-4d260f4230ffca6f074e731e55a03566.mp3?version_id=1627—

Categories
Hosea

Hosea 14

Toba Iletayo Baraka

1 Rudi, ee Israeli, kwaBwanaMungu wako.

Dhambi zako zimekuwa

ndilo anguko lako!

2 Chukueni maneno pamoja nanyi,

mkamrudieBwana.

Mwambieni:

“Samehe dhambi zetu zote

na utupokee kwa neema,

ili tuweze kutoa matunda yetu

kama sadaka za mafahali.

3 Ashuru hawezi kutuokoa,

hatutapanda farasi wa vita.

Kamwe hatutasema tena ‘Miungu yetu’

kwa kile ambacho mikono yetu wenyewe imetengeneza,

kwa kuwa kwako wewe yatima hupata huruma.”

4 “Nitaponya ukaidi wao

na kuwapenda kwa hiari yangu,

kwa kuwa hasira yangu imeondoka kwao.

5 Nitakuwa kama umande kwa Israeli;

atachanua kama yungiyungi.

Kama mwerezi wa Lebanoni

atashusha mizizi yake chini;

6 matawi yake yatatanda.

Fahari yake itakuwa kama mti wa mzeituni,

harufu yake nzuri kama mwerezi wa Lebanoni.

7 Watu wataishi tena kwenye kivuli chake.

Atastawi kama nafaka.

Atachanua kama mzabibu,

nao umaarufu wake utakuwa

kama divai itokayo Lebanoni.

8 Ee Efraimu, nina shughuli gani tena na sanamu?

Nitamjibu na kumtunza.

Mimi ni kama msunobari wenye majani mabichi;

kuzaa kwako matunda kunatoka kwangu.”

9 Ni nani mwenye hekima? Atayatambua mambo haya.

Ni nani mwenye ufahamu? Huyu atayaelewa.

Njia zaBwanani adili;

wenye haki huenda katika njia hizo,

lakini waasi watajikwaa ndani yake.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/14-521fc4943468d9e6135356aa63b8d720.mp3?version_id=1627—