Categories
Hosea

Hosea Utangulizi

Utangulizi

Hosea mwana wa Beeri alikuwa mzaliwa wa Ufalme wa Kaskazini, yaani, Israeli, ambao pia anauita Efraimu. Maana ya jina lake ni “Wokovu.” Inawezekana alianza huduma yake kabla ya kifo cha Mfalme Yeroboamu wa Pili mwaka wa 753 K.K. Huduma ya Hosea kwa Ufalme wa Kaskazini ilikaribiana sana na ile ya Amosi. Hawa wawili ndio manabii pekee wa Agano la Kale ambao vitabu vyao vilihusu Ufalme wa Kaskazini na maangamizi yake.

Hosea alipoanza huduma yake katika miaka ya baadaye ya utawala wa Yeroboamu wa Pili, Israeli ilikuwa inafurahia ustawi mkubwa wa kiuchumi na amani ya kisiasa iliyosababisha kuwepo kwa usalama pande zote. Mara baada ya kufa kwa Yeroboamu wa Pili mwaka 753 K.K., taifa lilianza kuharibika kwa haraka, na hatimaye likaangamia, nao Waisraeli wakapelekwa utumwani na Waashuru mwaka 722 K.K.

Mwandishi

Hosea mwana wa Beeri.

Kusudi

Kiini cha ujumbe wa Hosea ni kuonyesha upendo wa Mungu kwa watu wa Israeli waliogeuka na kumwacha Bwana.

Mahali

Ufalme wa Kaskazini (Israeli), ambao nabii anauita Efraimu.

Tarehe

715 K.K.

Wahusika Wakuu

Hosea, Gomeri, na watoto wao.

Wazo Kuu

Uhusiano wa Mungu na Israeli uliokuwa umefifia.

Mambo Muhimu

Hosea anaelezea hali ya taifa la Israeli akitumia hali iliyojitokeza katika maisha ya kila siku. Mungu anafananishwa na: mume, baba, simba, chui, dubu, umande, mvua, nondo, n.k. Israeli inafananishwa na: mke aliyekosa uaminifu kwa mumewe, mtu mgonjwa, mzabibu, mzeituni, mwanamke anayejifungua, jiko la kuokea, ukungu wa asubuhi, makapi, moshi, n.k.

Mgawanyo

Maisha ya Hosea katika familia (

1:1–3:5

)

Hali ya dhambi ya Israeli (

4:1–6:3

)

Adhabu kwa ajili ya Israeli (

6:4–10:15

)

Hukumu ya Mungu na rehema zake (

11:1–14:9

).

Categories
Hosea

Hosea 1

1 Neno laBwanalililomjia Hosea mwana wa Beeri wakati wa utawala wa Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na wakati wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi, mfalme wa Israeli.

Mke Wa Hosea Na Watoto

2 WakatiBwanaalipoanza kuzungumza kupitia Hosea,Bwanaalimwambia, “Nenda ukajitwalie mwanamke wa uzinzi na watoto wa uzinzi, kwa sababu nchi ina hatia ya uzinzi wa kupindukia kwa kumwachaBwana.”

3 Kwa hiyo alimwoa Gomeri binti Diblaimu, naye akachukua mimba na kumzalia Hosea mwana.

4 KishaBwanaakamwambia Hosea, “Mwite Yezreeli,kwa kuwa kitambo kidogo nitaiadhibu nyumba ya Yehu kwa ajili ya mauaji ya kule Yezreeli, nami nitaukomesha ufalme wa Israeli.

5 Katika siku ile nitavunja upinde wa Israeli katika Bonde la Yezreeli.”

6 Gomeri akachukua tena mimba akamzaa binti. KishaBwanaakamwambia Hosea, “Mwite Lo-Ruhama,kwa maana sitaonyesha tena upendo kwa nyumba ya Israeli, kwamba nisije kabisa nikawasamehe.

7 Hata hivyo nitaonyesha upendo kwa nyumba ya Yuda, nami nitawaokoa si kwa upinde, upanga au vita, wala kwa farasi na wapanda farasi, bali kwa njia yaBwanaMungu wao.”

8 Baada ya Gomeri kumwachisha Lo-Ruhama kunyonya, Gomeri alipata mwana mwingine.

9 KishaBwanaakasema, “Mwite Lo-Amikwa maana ninyi si watu wangu, nami si Mungu wenu.

10 “Hata hivyo Waisraeli watakuwa kama mchanga kando ya bahari, ambao hauwezi kupimika wala kuhesabiwa. Mahali pale walipoambiwa, ‘Ninyi si watu wangu,’ wao wataitwa ‘wana wa Mungu aliye hai.’

11 Watu wa Yuda na watu wa Israeli wataunganishwa tena, nao watamchagua kiongozi mmoja nao watakwea watoke katika nchi, kwa kuwa siku ya Yezreeli itakuwa kuu sana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/1-3c0b99c1b9b82448541b0fa16862dcd1.mp3?version_id=1627—

Categories
Hosea

Hosea 2

1 “Waambie ndugu zako, ‘Watu wangu,’ na pia waambie dada zako, ‘Wapendwa wangu.’

Israeli Aadhibiwa Na Kurudishwa

2 “Mkemeeni mama yenu, mkemeeni,

kwa maana yeye si mke wangu,

nami si mume wake.

Aondoe sura ya uzinzi katika uso wake

na uzinzi kati ya matiti yake.

3 Kama sivyo nitamvua nguo zake awe uchi

na kumwacha uchi kama siku ile aliyozaliwa.

Nitamfanya kama jangwa,

nitamgeuza awe nchi ya kiu,

nami nitamuua kwa kiu.

4 Sitaonyesha upendo wangu kwa watoto wake,

kwa sababu ni watoto wa uzinzi.

5 Mama yao amekosa uaminifu

na amewachukua mimba katika aibu.

Gomeri alisema, ‘Nitawaendea wapenzi wangu,

ambao hunipa chakula changu

na maji yangu,

sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu

na kinywaji changu.’

6 Kwa hiyo mimi Mungu nitaizuia njia yake

kwa vichaka vya miiba,

nitamjengea ukuta ili kwamba

asiweze kutoka.

7 Gomeri atawafuatia wapenzi wake lakini hatawapata;

atawatafuta lakini hatawapata.

Kisha atasema,

‘Nitarudi kwa mume wangu kama kwanza,

kwa maana nilikuwa na hali njema zaidi

kuliko sasa.’

8 Gomeri hajakubali kuwa mimi ndiye

niliyempa nafaka, divai mpya na mafuta,

niliyemwongezea fedha na dhahabu waliyoitumia

kwa kumtumikia Baali.

9 “Kwa hiyo nitachukua nafaka yangu wakati itakapokomaa

na divai yangu mpya wakati itakapokuwa tayari.

Nitamnyangʼanya sufu yangu na kitani yangu

iliyokusudiwa kufunika uchi wake.

10 Basi sasa nitaufunua ufisadi wake

mbele ya wapenzi wake;

hakuna yeyote atakayemtoa

mikononi mwangu.

11 Nitakomesha furaha na macheko yake yote:

sikukuu zake za mwaka,

sikukuu za Miandamo ya Mwezi,

siku zake za Sabato,

sikukuu zake zote zilizoamriwa.

12 Nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake,

ambayo alisema yalikuwa malipo yake

kutoka kwa wapenzi wake;

nitaifanya kuwa kichaka,

nao wanyama pori wataila.

13 Nitamwadhibu kwa ajili ya siku

alizowafukizia uvumba Mabaali;

alipojipamba kwa pete

na kwa vito vya thamani,

na kuwaendea wapenzi wake,

lakini mimi alinisahau,”

asemaBwana.

14 “Kwa hiyo sasa nitamshawishi;

nitamwongoza hadi jangwani

na kuzungumza naye kwa upole.

15 Huko nitamrudishia mashamba yake ya mizabibu,

nami nitalifanya Bonde la Akori

mlango wa matumaini.

Huko ataimba kama alivyofanya katika siku za ujana wake,

kama siku zile alizotoka Misri.

16 “Katika siku ile,” asemaBwana,

“utaniita mimi ‘Mume wangu’;

hutaniita tena mimi ‘Bwana wangu.’

17 Nitaondoa majina ya Mabaali kutoka midomoni mwake,

wala hataomba tena kwa majina yao.

18 Katika siku ile nitafanya Agano kwa ajili yao

na wanyama wa kondeni, na ndege wa angani,

na viumbe vile vitambaavyo ardhini.

Upinde, upanga na vita,

nitaondolea mbali katika nchi,

ili kwamba wote waweze kukaa salama.

19 Nitakuposa uwe wangu milele;

nitakuposa kwa uadilifu na haki,

kwa upendo na huruma.

20 Nitakuposa kwa uaminifu,

nawe utamkubaliBwana.

21 “Katika siku ile nitajibu,”

asemaBwana,

“nitajibu kwa anga,

nazo anga zitajibu kwa nchi;

22 nayo nchi itajibu kwa nafaka,

divai mpya na mafuta,

navyo vitajibu kwa Yezreeli.

23 Nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe;

nami nitaonyesha pendo langu kwake

yule ambaye nilimwita, ‘Si mpenzi wangu.’

Nitawaambia wale walioitwa, ‘Sio watu wangu,’

‘Ninyi ni watu wangu’;

nao watasema, ‘Wewe ndiwe Mungu wangu.’ ”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/2-e489fbb9dba03145b6b6ec8a3998dd22.mp3?version_id=1627—

Categories
Hosea

Hosea 3

Upatanisho Wa Hosea Na Mkewe

1 Bwanaakaniambia, “Nenda, ukaonyeshe upendo wako kwa mke wako tena, ingawa amependwa na mwingine naye ni mzinzi. Mpende kamaBwanaapendavyo Waisraeli, ingawa wanageukia miungu mingine na kupenda mikate mitamu ya zabibu kavu iliyowekwa wakfu.”

2 Basi nilimnunua huyo mwanamke kwa shekeli kumi na tanoza fedha, pia kwa kiasi kama cha homeri moja na nusuya shayiri.

3 Kisha nilimwambia, “Utaishi nami kwa siku nyingi, hupaswi kuwa kahaba au kuwa na uhusiano wa karibu na mtu yeyote, nami nitaishi na wewe.”

4 Kwa maana Waisraeli wataishi siku nyingi bila kuwa na mfalme wala mkuu, bila kuwa na dhabihu wala mawe matakatifu, bila kisibau wala sanamu.

5 Baadaye Waisraeli watarudi na kumtafutaBwanaMungu wao na Daudi mfalme wao. Watakuja wakitetemeka kwaBwanana kwa baraka zake katika siku za mwisho.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/3-cc76f9180eaa010cd7d5e3abe3bbc37a.mp3?version_id=1627—

Categories
Hosea

Hosea 4

Shtaka Dhidi Ya Israeli

1 Sikieni neno laBwana, enyi Waisraeli,

kwa sababuBwanaanalo shtaka

dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi:

“Hakuna uaminifu, hakuna upendo,

hakuna kumjua Mungu katika nchi.

2 Kuna kulaani tu, uongo na uuaji,

wizi na uzinzi,

bila kuwa na mipaka,

nao umwagaji damu mmoja

baada ya mwingine.

3 Kwa sababu hii nchi huomboleza,

wote waishio ndani mwake wanadhoofika,

wanyama wa kondeni, ndege wa angani

na samaki wa baharini wanakufa.

4 “Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka,

mtu yeyote na asimlaumu mwenzake,

kwa maana watu wako ni kama wale

waletao mashtaka dhidi ya kuhani.

5 Unajikwaa usiku na mchana,

nao manabii hujikwaa pamoja nawe.

Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:

6 watu wangu wanaangamizwa

kwa kukosa maarifa,

“Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa,

mimi nami nitakukataa wewe

usiwe kuhani kwangu mimi;

kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako

mimi nami sitawajali watoto wako.

7 Kadiri makuhani walivyoongezeka,

ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu,

walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.

8 Hujilisha dhambi za watu wangu

na kupendezwa na uovu wao.

9 Hata itakuwa: Kama walivyo watu,

ndivyo walivyo makuhani.

Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao

na kuwalipa kwa matendo yao.

10 “Watakula lakini hawatashiba;

watajiingiza katika ukahaba

lakini hawataongezeka,

kwa sababu wamemwachaBwana

na kujiingiza wenyewe

11 katika ukahaba,

divai ya zamani na divai mpya,

ambavyo huondoa ufahamu

12 wa watu wangu.

Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti

nao hujibiwa na fimbo ya mti.

Roho ya ukahaba imewapotosha,

hawana uaminifu kwa Mungu wao.

13 Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima

na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima,

chini ya mialoni, milibua na miela,

ambako kuna vivuli vizuri.

Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba

na wake za wana wenu uzinzi.

14 “Sitawaadhibu binti zenu wakati

wanapogeukia ukahaba,

wala wake za wana wenu

wanapofanya uzinzi,

kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya

na kutambikia pamoja na makahaba

wa mahali pa kuabudia miungu:

watu wasiokuwa na ufahamu

wataangamia!

15 “Ingawa umefanya uzinzi, ee Israeli,

Yuda naye asije akawa na hatia.

“Usiende Gilgali,

usipande kwenda Beth-Aveni

Wala usiape,

‘Hakika kamaBwanaaishivyo!’

16 Waisraeli ni wakaidi,

kama mtamba wa ngʼombe ambaye ni mkaidi.

Ni jinsi gani basiBwanaanaweza kuwachunga

kama wana-kondoo

katika shamba la majani?

17 Efraimu amejiunga na sanamu,

ondokana naye!

18 Hata wakati wamemaliza vileo vyao

wanaendelea na ukahaba wao,

watawala wao hupenda sana

njia za aibu.

19 Kisulisuli kitawafagilia mbali

na dhabihu zao zitawaletea aibu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/4-23797682a4891b06886ad1291db73701.mp3?version_id=1627—

Categories
Hosea

Hosea 5

Hukumu Dhidi Ya Israeli

1 “Sikieni hili, enyi makuhani!

Kuweni wasikivu, enyi Waisraeli!

Sikieni, ee nyumba ya mfalme!

Hukumu hii ni dhidi yenu:

Mmekuwa mtego huko Mispa,

wavu uliotandwa juu ya Tabori.

2 Waasi wamezidisha sana mauaji.

Mimi nitawatiisha wote.

3 Ninajua yote kuhusu Efraimu,

Israeli hukufichika kwangu.

Efraimu, sasa umegeukia ukahaba,

Israeli amenajisika.

4 “Matendo yao hayawaachii

kurudi kwa Mungu wao.

Roho ya ukahaba imo ndani ya mioyo yao,

hawamkubaliBwana.

5 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yao;

Waisraeli, hata Efraimu,

wanajikwaa katika dhambi zao;

pia Yuda atajikwaa pamoja nao.

6 Wakati wanapokwenda na makundi yao

ya kondoo na ngʼombe

kumtafutaBwana,

hawatampata;

yeye amejiondoa kutoka kwao.

7 Wao si waaminifu kwaBwana;

wamezaa watoto haramu.

Sasa sikukuu zao za Mwandamo wa Mwezi

zitawaangamiza wao

pamoja na mashamba yao.

8 “Pigeni tarumbeta huko Gibea,

baragumu huko Rama.

Paza kilio cha vita huko Beth-Aveni,

ongoza, ee Benyamini.

9 Efraimu ataachwa ukiwa

katika siku ya kuadhibiwa.

Miongoni mwa makabila ya Israeli

ninatangaza lile ambalo halina budi kutukia.

10 Viongozi wa Yuda ni kama wale

wanaosogeza mawe ya mpaka.

Nitamwaga ghadhabu yangu juu yao

kama mafuriko ya maji.

11 Efraimu ameonewa,

amekanyagwa katika hukumu

kwa kuwa amekusudia kufuatia sanamu.

12 Mimi ni kama nondo kwa Efraimu,

na kama uozo kwa watu wa Yuda.

13 “Wakati Efraimu alipoona ugonjwa wake,

naye Yuda vidonda vyake,

ndipo Efraimu alipogeukia Ashuru,

na kuomba msaada kwa mfalme mkuu.

Lakini hawezi kukuponya,

wala hawezi kukuponya vidonda vyako.

14 Kwa maana nitakuwa kama simba kwa Efraimu,

kama simba mkubwa kwa Yuda.

Nitawararua vipande vipande na kuondoka;

nitawachukua mbali,

na hakuna wa kuwaokoa.

15 Kisha nitarudi mahali pangu

mpaka watakapokubali kosa lao.

Nao watautafuta uso wangu;

katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/5-d57a757ea2b641d3a776cb16c5cfda6b.mp3?version_id=1627—

Categories
Hosea

Hosea 6

Israeli Asiye Na Toba

1 “Njooni, tumrudieBwana.

Ameturarua vipande vipande

lakini atatuponya;

ametujeruhi lakini

atatufunga majeraha yetu.

2 Baada ya siku mbili atatufufua;

katika siku ya tatu atatuinua,

ili tuweze kuishi mbele zake.

3 TumkubaliBwana,

tukaze kumkubali yeye.

Kutokea kwake ni hakika kama vile

kuchomoza kwa jua;

atatujia kama mvua za masika,

kama vile mvua za vuli

ziinyweshavyo nchi.”

4 “Nifanye nini nawe, Efraimu?

Nifanye nini nawe, Yuda?

Upendo wako ni kama ukungu wa asubuhi,

kama umande wa alfajiri utowekao.

5 Kwa hiyo ninawakata ninyi vipande vipande

kwa kutumia manabii wangu;

nimewaua ninyi kwa maneno ya kinywa changu,

hukumu zangu zinawaka

kama umeme juu yenu.

6 Kwa maana nataka rehema, wala si dhabihu,

kumkubali Mungu zaidi

kuliko sadaka za kuteketezwa.

7 Wamevunja Agano kama Adamu:

huko hawakuwa waaminifu kwangu.

8 Gileadi ni mji wenye watu waovu,

umetiwa madoa kwa nyayo za damu.

9 Kama wanyangʼanyi wamviziavyo mtu,

ndivyo magenge ya makuhani wafanyavyo;

wanaulia watu kwenye njia iendayo Shekemu,

wakifanya uhalifu wa aibu.

10 Nimeona jambo la kutisha

katika nyumba ya Israeli.

Huko Efraimu amejitolea kwa ukahaba

na Israeli amenajisika.

11 “Pia kwa ajili yako, Yuda,

mavuno yameamriwa.

“Wakati wowote ningerejesha neema ya watu wangu,

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/6-e4752a038858b2342f51514b281dc81f.mp3?version_id=1627—

Categories
Hosea

Hosea 7

1 kila mara nilipotaka kumponya Israeli,

dhambi za Efraimu zinafichuliwa

na maovu ya Samaria yanafunuliwa.

Wanafanya udanganyifu,

wevi huvunja nyumba,

maharamia hunyangʼanya barabarani,

2 lakini hawafahamu kwamba

ninakumbuka matendo yao yote mabaya.

Dhambi zao zimewameza,

ziko mbele zangu siku zote.

3 “Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao,

wakuu wao kwa uongo wao.

4 Wote ni wazinzi,

wanawaka kama tanuru

ambayo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea

kuanzia kukanda unga

hadi umekwisha kuumuka.

5 Katika sikukuu ya mfalme wetu

wakuu wanawaka kwa mvinyo,

naye anawaunga mkono wenye mizaha.

6 Mioyo yao ni kama tanuru,

wanamwendea kwa hila.

Hasira yao inafoka moshi usiku kucha,

wakati wa asubuhi inalipuka

kama miali ya moto.

7 Wote ni moto kama tanuru;

wanawaangamiza watawala wao.

Wafalme wake wote wanaanguka,

wala hakuna yeyote kati yao aniitaye mimi.

8 “Efraimu anajichanganya na mataifa;

Efraimu ni mkate ambao haukuiva.

9 Wageni wananyonya nguvu zake,

lakini hafahamu hilo.

Nywele zake zina mvi hapa na pale,

lakini hana habari.

10 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake,

lakini pamoja na haya yote

harudi kwaBwanaMungu wake

wala kumtafuta.

11 “Efraimu ni kama hua,

hudanganywa kwa urahisi na hana akili:

mara anaita Misri,

mara anageukia Ashuru.

12 Wakati watakapokwenda,

nitatupa wavu wangu juu yao;

nitawavuta chini waanguke

kama ndege wa angani.

Nitakaposikia wakikusanyika pamoja,

nitawanasa.

13 Ole wao, kwa sababu

wamepotoka kutoka kwangu!

Maangamizi ni yao

kwa sababu wameniasi!

Ninatamani kuwakomboa,

lakini wanasema uongo dhidi yangu.

14 Hawanililii mimi kutoka mioyoni mwao,

bali wanaomboleza vitandani mwao.

Hukusanyika pamoja kwa ajili ya nafaka na divai mpya,

lakini hugeukia mbali nami.

15 Niliwafundisha na kuwatia nguvu,

lakini wanapanga mabaya dhidi yangu.

16 Hawamgeukii Yeye Aliye Juu Sana,

wako kama upinde wenye kasoro.

Viongozi wao wataanguka kwa upanga

kwa sababu ya maneno yao ya jeuri.

Kwa ajili ya hili watadhihakiwa

katika nchi ya Misri.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/7-1347b2c0019372d404eccd33f43faa3f.mp3?version_id=1627—

Categories
Hosea

Hosea 8

Israeli Kuvuna Kisulisuli

1 “Wekeni tarumbeta midomoni mwenu!

Tai yuko juu ya nyumba yaBwana

kwa sababu watu wamevunja Agano langu,

wameasi dhidi ya sheria yangu.

2 Israeli ananililia,

‘Ee Mungu wetu, tunakukubali!’

3 Lakini Israeli amekataa lile lililo jema,

adui atamfuatia.

4 Wanaweka wafalme bila idhini yangu,

wamechagua wakuu bila kibali changu.

Kwa fedha zao na dhahabu

wamejitengenezea sanamu kwa ajili

ya maangamizi yao wenyewe.

5 Ee Samaria, tupilieni mbali sanamu yenu ya ndama!

Hasira yangu inawaka dhidi yao.

Watakuwa najisi mpaka lini?

6 Zimetoka katika Israeli!

Ndama huyu: ametengenezwa na fundi, si Mungu.

Atavunjwa vipande vipande,

yule ndama wa Samaria.

7 “Wanapanda upepo

na kuvuna upepo wa kisulisuli.

Bua halina suke,

halitatoa unga.

Kama lingetoa nafaka,

wageni wangeila yote.

8 Israeli amemezwa;

sasa yupo miongoni mwa mataifa

kama kitu kisicho na thamani.

9 Kwa kuwa wamepanda kwenda Ashuru

kama punda-mwitu anayetangatanga peke yake.

Efraimu amejiuza mwenyewe

kwa wapenzi.

10 Ingawa wamejiuza wenyewe miongoni mwa mataifa,

sasa nitawakusanya pamoja.

Wataanza kudhoofika chini ya uonevu

wa mfalme mwenye nguvu.

11 “Ingawa Efraimu alijenga madhabahu nyingi

kwa ajili ya sadaka za dhambi,

hizi zimekuwa madhabahu

za kufanyia dhambi.

12 Nimeandika kwa ajili yao mambo mengi

kuhusu sheria yangu,

lakini wameziangalia

kama kitu cha kigeni.

13 Wanatoa dhabihu nilizopewa mimi

nao wanakula hiyo nyama,

lakiniBwanahapendezwi nao.

Sasa ataukumbuka uovu wao

na kuadhibu dhambi zao:

Watarudi Misri.

14 Israeli amemsahau Muumba wake

na kujenga majumba ya kifalme,

Yuda amejengea miji mingi ngome.

Lakini nitatuma moto kwenye miji yao

utakaoteketeza ngome zao.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/8-1765a550030a08f098e3f8b63100e9f7.mp3?version_id=1627—

Categories
Hosea

Hosea 9

Adhabu Kwa Israeli

1 Usifurahie, ee Israeli;

usishangilie kama mataifa mengine.

Kwa kuwa hukuwa

mwaminifu kwa Mungu wako;

umependa ujira wa kahaba kwenye kila sakafu

ya kupuria nafaka.

2 Sakafu za kupuria nafaka na mashinikizo ya kukamulia divai

havitalisha watu,

divai mpya itawapungukia.

3 Hawataishi katika nchi yaBwana,

Efraimu atarudi Misri

na atakula chakula

kilicho najisi huko Ashuru.

4 HawatammiminiaBwanasadaka ya divai

wala dhabihu zao hazitampendeza.

Dhabihu kama hizo zitakuwa kwao

kama mkate wa waombolezaji;

nao wote wazilao watakuwa najisi.

Chakula hiki kitakuwa kwa ajili yao wenyewe;

kisije katika Hekalu laBwana.

5 Mtafanya nini katika siku ya sikukuu zenu zilizoamriwa,

katika siku za sikukuu zaBwana?

6 Hata ikiwa wataokoka maangamizi,

Misri atawakusanya,

nayo Memfisiitawazika.

Hazina zao za fedha zitasongwa na michongoma,

nayo miiba itafunika mahema yao.

7 Siku za adhabu zinakuja,

siku za malipo zimewadia.

Israeli na afahamu hili.

Kwa sababu dhambi zenu ni nyingi sana

na uadui wenu ni mkubwa sana,

nabii anadhaniwa ni mpumbavu,

mtu aliyeongozwa na Mungu

anaonekana mwendawazimu.

8 Nabii, pamoja na Mungu wangu,

ndiye mlinzi juu ya Efraimu,

hata hivyo mitego inamngojea

katika mapito yake yote,

na uadui katika nyumba ya Mungu wake.

9 Wamezama sana katika rushwa,

kama katika siku za Gibea.

Mungu atakumbuka uovu wao

na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.

10 “Nilipompata Israeli, ilikuwa kama

kupata zabibu jangwani;

nilipowaona baba zenu, ilikuwa kama kuona

matunda ya kwanza katika mtini.

Lakini walipofika Baal-Peori, walijiweka wakfu

kwa ile sanamu ya aibu,

nao wakawa najisi

kama kitu kile walichokipenda.

11 Utukufu wa Efraimu utaruka kama ndege:

hakuna kuzaa, hakuna kuchukua mimba,

hakuna kutunga mimba.

12 Hata wakilea watoto,

nitamuua kila mmoja.

Ole wao

nitakapowapiga kisogo!

13 Nimemwona Efraimu, kama Tiro,

aliyeoteshwa mahali pazuri.

Lakini Efraimu wataleta

watoto wao kwa mchinjaji.”

14 Wape, EeBwana,

je, utawapa nini?

Wape matumbo ya kuharibu mimba

na matiti yaliyokauka.

15 “Kwa sababu ya uovu wao wote huko Gilgali,

niliwachukia huko.

Kwa sababu ya matendo yao ya dhambi,

nitawafukuza katika nyumba yangu.

Sitawapenda tena,

viongozi wao wote ni waasi.

16 Efraimu ameharibiwa,

mzizi wao umenyauka,

hawazai tunda.

Hata kama watazaa watoto,

nitawachinja watoto wao

waliotunzwa vizuri.”

17 Mungu wangu atawakataa

kwa sababu hawakumtii;

watakuwa watu wa kutangatanga

miongoni mwa mataifa.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/HOS/9-cf5284957e19d6f9703ac09c90732ebf.mp3?version_id=1627—