Categories
Zaburi

Zaburi 134

Wito Wa Kumsifu Mungu

Wimbo wa kwenda juu.

1 MsifuniBwana, ninyi nyote watumishi waBwana,

ninyi mnaotumika usiku ndani ya nyumba yaBwana.

2 Inueni mikono yenu katika pale patakatifu

na kumsifuBwana.

3 NayeBwana, Muumba wa mbingu na dunia,

awabariki kutoka Sayuni.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/134-0ab0f077880d8b738f1866dcc6bb3977.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 135

Wimbo Wa Sifa Kwa Mungu

1 MsifuniBwana.

Lisifuni jina laBwana,

msifuni, enyi watumishi waBwana,

2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba yaBwana,

katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.

3 MsifuniBwana, kwa kuwaBwanani mwema,

liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.

4 Kwa maanaBwanaamemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe,

Israeli kuwa mali yake ya thamani.

5 Ninajua ya kuwaBwanani mkuu,

kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.

6 Bwanahufanya lolote apendalo,

mbinguni na duniani,

katika bahari na vilindi vyake vyote.

7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia;

hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua

na huleta upepo kutoka ghala zake.

8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri,

mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.

9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri,

dhidi ya Farao na watumishi wake wote.

10 Aliyapiga mataifa mengi,

na akaua wafalme wenye nguvu:

11 Mfalme Sihoni na Waamori,

Ogu mfalme wa Bashani

na wafalme wote wa Kanaani:

12 akatoa nchi yao kuwa urithi,

urithi kwa watu wake Israeli.

13 EeBwana, jina lako ladumu milele,

kumbukumbu za fahari zako, EeBwana, kwa vizazi vyote.

14 MaanaBwanaatawathibitisha watu wake,

na kuwahurumia watumishi wake.

15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu,

zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.

16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema,

zina macho, lakini haziwezi kuona;

17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia,

wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.

18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo,

vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.

19 Ee nyumba ya Israeli, msifuniBwana;

ee nyumba ya Aroni, msifuniBwana;

20 ee nyumba ya Lawi, msifuniBwana;

ninyi mnaomcha, msifuniBwana.

21 MsifuniBwanakutoka Sayuni,

msifuni yeye aishiye Yerusalemu.

MsifuniBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/135-b3cc2ae163386368ef8435e6ed41db87.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 136

Wimbo Wa Kumshukuru Mungu

1 MshukuruniBwana, kwa kuwa ni mwema.

Fadhili zake zadumu milele.

2 Mshukuruni Mungu wa miungu.

Fadhili zake zadumu milele.

3 Mshukuruni Bwana wa mabwana:

Fadhili zake zadumu milele.

4 Kwake yeye pekee atendaye maajabu makuu,

Fadhili zake zadumu milele.

5 Ambaye kwa ufahamu wake aliziumba mbingu,

Fadhili zake zadumu milele.

6 Ambaye aliitandaza dunia juu ya maji,

Fadhili zake zadumu milele.

7 Ambaye aliumba mianga mikubwa,

Fadhili zake zadumu milele.

8 Jua litawale mchana,

Fadhili zake zadumu milele.

9 Mwezi na nyota vitawale usiku,

Fadhili zake zadumu milele.

10 Kwake yeye aliyemuua mzaliwa wa kwanza wa Misri,

Fadhili zake zadumu milele.

11 Na kuwatoa Israeli katikati yao,

Fadhili zake zadumu milele.

12 Kwa mkono wenye nguvu ulionyooshwa,

Fadhili zake zadumu milele.

13 Kwake yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu,

Fadhili zake zadumu milele.

14 Na kuwapitisha Israeli katikati yake,

Fadhili zake zadumu milele.

15 Lakini alimfagia Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu,

Fadhili zake zadumu milele.

16 Kwake yeye aliyewaongoza watu wake katika jangwa,

Fadhili zake zadumu milele.

17 Ambaye aliwapiga wafalme wenye nguvu,

Fadhili zake zadumu milele.

18 Naye aliwaua wafalme wenye nguvu,

Fadhili zake zadumu milele.

19 Sihoni mfalme wa Waamori,

Fadhili zake zadumu milele.

20 Ogu mfalme wa Bashani,

Fadhili zake zadumu milele.

21 Akatoa nchi yao kuwa urithi,

Fadhili zake zadumu milele.

22 Urithi kwa Israeli mtumishi wake,

Fadhili zake zadumu milele.

23 Aliyetukumbuka katika unyonge wetu,

Fadhili zake zadumu milele.

24 Alituweka huru toka adui zetu,

Fadhili zake zadumu milele.

25 Ambaye humpa chakula kila kiumbe.

Fadhili zake zadumu milele.

26 Mshukuruni Mungu wa mbinguni,

Fadhili zake zadumu milele.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/136-97e5e5a1599c147afab74fa8bd390b95.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 137

Maombolezo Ya Israeli Uhamishoni

1 Kando ya mito ya Babeli tuliketi, tukaomboleza

tulipokumbuka Sayuni.

2 Kwenye miti ya huko

tulitundika vinubi vyetu,

3 kwa maana huko hao waliotuteka

walitaka tuwaimbie nyimbo,

watesi wetu walidai nyimbo za furaha;

walisema, “Tuimbieni wimbo mmoja kati ya nyimbo za Sayuni!”

4 Tutaimbaje nyimbo zaBwana,

tukiwa nchi ya kigeni?

5 Nikikusahau wewe, ee Yerusalemu,

basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.

6 Ulimi wangu ushikamane na kaakaa la kinywa changu

kama sitakukumbuka wewe,

kama nisipokufikiri Yerusalemu

kuwa furaha yangu kubwa.

7 Kumbuka, EeBwana, walichokifanya Waedomu,

siku ile Yerusalemu ilipoanguka.

Walisema, “Bomoa, Bomoa

mpaka kwenye misingi yake!”

8 Ee binti Babeli, uliyehukumiwa kuangamizwa,

heri yeye atakayekulipiza wewe

kwa yale uliyotutenda sisi:

9 yeye ambaye atawakamata watoto wako wachanga

na kuwaponda juu ya miamba.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/137-aa0e5e3e6f830102379a716d0b434f81.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 138

Maombi Ya Shukrani

Zaburi ya Daudi.

1 Nitakusifu wewe, EeBwana, kwa moyo wangu wote,

mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.

2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu,

nami nitalisifu jina lako

kwa ajili ya upendo wako

na uaminifu,

kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako

juu ya vitu vyote.

3 Nilipoita, ulinijibu;

ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.

4 Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe EeBwana,

wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.

5 Wao na waimbe kuhusu njia zaBwana,

kwa maana utukufu waBwanani mkuu.

6 IngawaBwanayuko juu,

humwangalia mnyonge,

bali mwenye kiburi

yeye anamjua kutokea mbali.

7 Nijapopita katikati ya shida,

wewe unayahifadhi maisha yangu,

unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu,

kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.

8 Bwanaatatimiza kusudi lake kwangu,

EeBwana, upendo wako wadumu milele:

usiziache kazi za mikono yako.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/138-d40040723c8c708f47c1cf84d80d04cd.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 139

Mungu Asiyeweza Kukwepwa

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, umenichunguza

na kunijua.

2 Unajua ninapoketi na ninapoinuka;

unatambua mawazo yangu tokea mbali.

3 Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu;

unaelewa njia zangu zote.

4 Kabla neno halijafika katika ulimi wangu,

wewe walijua kikamilifu, EeBwana.

5 Umenizunguka nyuma na mbele;

umeweka mkono wako juu yangu.

6 Maarifa haya ni ya ajabu mno kwangu,

ni ya juu sana kwangu kuyafikia.

7 Niende wapi nijiepushe na Roho yako?

Niende wapi niukimbie uso wako?

8 Kama nikienda juu mbinguni, wewe uko huko;

nikifanya vilindikuwa kitanda changu,

wewe uko huko.

9 Kama nikipanda juu ya mbawa za mapambazuko,

kama nikikaa pande za mbali za bahari,

10 hata huko mkono wako utaniongoza,

mkono wako wa kuume utanishika kwa uthabiti.

11 Kama nikisema, “Hakika giza litanificha

na nuru inayonizunguka iwe usiku,”

12 hata giza halitakuwa giza kwako,

usiku utangʼaa kama mchana,

kwa kuwa giza ni kama nuru kwako.

13 Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani;

uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.

14 Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa

kwa namna ya ajabu na ya kutisha;

kazi zako ni za ajabu,

ninajua hayo kikamilifu.

15 Umbile langu halikufichika kwako,

nilipoumbwa mahali pa siri.

Nilipoungwa pamoja kwa ustadi katika vilindi vya nchi,

16 macho yako yaliniona kabla mwili wangu haujakamilika.

Siku zangu zote ulizonipangia

ziliandikwa katika kitabu chako

kabla haijakuwepo hata moja.

17 Tazama jinsi yalivyo ya thamani mawazo yako kwangu, Ee Mungu!

Jinsi jumla yake ilivyo kubwa!

18 Kama ningezihesabu,

zingekuwa nyingi kuliko mchanga.

Niamkapo,

bado niko pamoja nawe.

19 Laiti ungewachinja waovu, Ee Mungu!

Ondokeni kwangu, ninyi wamwaga damu!

20 Wanazungumza juu yako wakiwa na kusudi baya,

adui zako wanatumia vibaya jina lako.

21 EeBwana, je, nisiwachukie wanaokuchukia?

Nisiwachukie sana wanaoinuka dhidi yako?

22 Sina kitu zaidi ya chuki dhidi yao,

ninawahesabu ni adui zangu.

23 Ee Mungu, nichunguze, uujue moyo wangu,

nijaribu na ujue mawazo yangu.

24 Uone kama kuna njia iletayo machukizo ndani yangu,

uniongoze katika njia ya milele.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/139-a92dc228fd3bdfb24c069e45c20f4d67.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 140

Kuomba Ulinzi Wa Mungu

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu;

nilinde na watu wenye jeuri,

2 ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao,

na kuchochea vita siku zote.

3 Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka,

sumu ya nyoka iko midomoni mwao.

4 EeBwana, niepushe na mikono ya waovu;

nilinde na watu wenye jeuri

wanaopanga kunikwaza miguu yangu.

5 Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa,

wametandaza kamba za wavu wao,

wametega mitego kwenye njia yangu.

6 EeBwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.”

EeBwana, usikie kilio changu na kunihurumia.

7 EeBwanaMwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu,

unikingaye kichwa changu siku ya vita:

8 EeBwana, usiwape waovu matakwa yao,

usiache mipango yao ikafanikiwa,

wasije wakajisifu.

9 Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe

na shida zinazosababishwa na midomo yao.

10 Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie!

Na watupwe motoni,

katika mashimo ya matope,

wasiinuke tena kamwe.

11 Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi;

maafa na yawawinde watu wenye jeuri.

12 Najua kwambaBwanahuwapatia maskini haki,

na kuitegemeza njia ya mhitaji.

13 Hakika wenye haki watalisifu jina lako,

na waadilifu wataishi mbele zako.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/140-c7abfd880fe0c293fccb9cebb7d5d1a7.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 141

Maombi Ya Kuhifadhiwa Dhidi Ya Uovu

Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima.

Sikia sauti yangu ninapokuita.

2 Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba;

kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.

3 EeBwana, weka mlinzi kinywani mwangu,

weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.

4 Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya,

nisije nikashiriki katika matendo maovu

pamoja na watu watendao mabaya,

wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.

5 Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma;

na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu.

Kichwa changu hakitalikataa.

Hata hivyo, maombi yangu daima

ni kinyume cha watenda mabaya,

6 watawala wao watatupwa chini

kutoka kwenye majabali,

waovu watajifunza kwamba maneno yangu

yalikuwa kweli.

7 Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi,

ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.”

8 Lakini nimekaza macho yangu kwako, EeBwanaMwenyezi,

ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.

9 Niepushe na mitego waliyonitegea,

kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya.

10 Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe,

wakati mimi ninapita salama.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/141-2e78f72da3c85efe3c132cabfafda772.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 142

Maombi Ya Kuokolewa Dhidi Ya Watesi

Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi.

1 NamliliaBwanakwa sauti,

nainua sauti yangu kwaBwanaanihurumie.

2 Namimina malalamiko yangu mbele zake,

mbele zake naeleza shida zangu.

3 Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu,

wewe ndiwe unajua njia zangu.

Katika njia ninayopita

watu wameniwekea mtego.

4 Tazama kuume kwangu na uone,

hakuna hata mmoja anayejihusisha nami.

Sina kimbilio,

hakuna anayejali maisha yangu.

5 EeBwana, nakulilia wewe,

nasema, “Wewe ni kimbilio langu,

fungu langu katika nchi ya walio hai.”

6 Sikiliza kilio changu,

kwa sababu mimi ni mhitaji sana;

niokoe na wale wanaonifuatilia,

kwa kuwa wamenizidi nguvu.

7 Nifungue kutoka kifungo changu,

ili niweze kulisifu jina lako.

Ndipo wenye haki watanizunguka,

kwa sababu ya wema wako kwangu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/142-016a7e0786320f3f02f0ea5ebd0aba8f.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 143

Maombi Ya Kuokolewa Dhidi Ya Adui

Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, sikia sala yangu,

sikiliza kilio changu unihurumie;

katika uaminifu na haki yako

njoo unisaidie.

2 Usimhukumu mtumishi wako,

kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako.

3 Adui hunifuatilia,

hunipondaponda chini;

hunifanya niishi gizani

kama wale waliokufa zamani.

4 Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu,

moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.

5 Nakumbuka siku za zamani;

natafakari juu ya kazi zako zote,

naangalia juu ya kazi

ambazo mikono yako imezifanya.

6 Nanyoosha mikono yangu kwako,

nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame.

7 EeBwana, unijibu haraka,

roho yangu inazimia.

Usinifiche uso wako,

ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni.

8 Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma,

kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako.

Nionyeshe njia nitakayoiendea,

kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.

9 EeBwana, uniokoe na adui zangu,

kwa kuwa nimejificha kwako.

10 Nifundishe kufanya mapenzi yako,

kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu,

Roho wako mwema na aniongoze

katika nchi tambarare.

11 EeBwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu,

kwa haki yako nitoe katika taabu.

12 Kwa upendo wako usiokoma,

nyamazisha adui zangu;

waangamize watesi wangu wote,

kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/143-cd2153934e693222771bbe87b6f52c43.mp3?version_id=1627—