Categories
Zaburi

Zaburi 124

Shukrani Kwa Ukombozi Wa Israeli

Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.

1 KamaBwanaasingalikuwa upande wetu;

Israeli na aseme sasa:

2 kamaBwanaasingalikuwa upande wetu,

wakati watu walipotushambulia,

3 wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu,

wangalitumeza tungali hai,

4 mafuriko yangalitugharikisha,

maji mengi yangalitufunika,

5 maji yaendayo kasi

yangalituchukua.

6 Bwanaasifiwe,

yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.

7 Tumeponyoka kama ndege

kutoka mtego wa mwindaji;

mtego umevunjika,

nasi tukaokoka.

8 Msaada wetu ni katika jina laBwana,

Muumba wa mbingu na dunia.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/124-9ccb6bbd9ae29a84ffb8315500236917.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 125

Usalama Wa Watu Wa Mungu

Wimbo wa kwenda juu.

1 Wale wamtumainioBwanani kama mlima Sayuni,

ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.

2 Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,

ndivyoBwanaanavyowazunguka watu wake

sasa na hata milele.

3 Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi

waliopewa wenye haki,

ili wenye haki wasije wakatumia

mikono yao kutenda ubaya.

4 EeBwana, watendee mema walio wema,

wale walio wanyofu wa moyo.

5 Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka,

Bwanaatawafukuza pamoja na watenda mabaya.

Amani iwe juu ya Israeli.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/125-370cee1374973ac54166d030d902839e.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 126

Kurejezwa Kutoka Utumwani

Wimbo wa kwenda juu.

1 Bwanaalipowarejeza mateka Sayuni,

tulikuwa kama watu walioota ndoto.

2 Vinywa vyetu vilijaa kicheko,

ndimi zetu zilijaa nyimbo za shangwe.

Ndipo iliposemwa miongoni mwa mataifa,

“Bwanaamewatendea mambo makuu.”

3 Bwanaametutendea mambo makuu,

nasi tumejaa furaha.

4 EeBwana, turejeshee watu wetu waliotekwa,

kama vijito katika Negebu.

5 Wapandao kwa machozi

watavuna kwa nyimbo za shangwe.

6 Yeye azichukuaye mbegu zake

kwenda kupanda, huku akilia,

atarudi kwa nyimbo za shangwe,

akichukua miganda ya mavuno yake.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/126-911e1a86f635da446023b7d1d66d0b5f.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 127

Bila Mungu, Kazi Ya Mwanadamu Haifai

Wimbo wa kwenda juu. Wa Solomoni.

1 Bwanaasipoijenga nyumba,

wajengao hufanya kazi bure.

Bwanaasipoulinda mji,

walinzi wakesha bure.

2 Mnajisumbua bure kuamka mapema

na kuchelewa kulala,

mkitaabikia chakula:

kwa maana yeye huwapa usingizi wapenzi wake.

3 Wana ni urithi utokao kwaBwana,

watoto ni zawadi kutoka kwake.

4 Kama mishale mikononi mwa shujaa

ndivyo walivyo wana awazaao mtu katika ujana wake.

5 Heri mtu ambaye podo lake

limejazwa nao.

Hawataaibishwa wanaposhindana

na adui zao langoni.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/127-3d0950ea8f485d2b1b38b93607d112ef.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 128

Thawabu Ya Kumtii Bwana

Wimbo wa kwenda juu.

1 Heri ni wale wote wamchaoBwana,

waendao katika njia zake.

2 Utakula matunda ya kazi yako;

baraka na mafanikio vitakuwa vyako.

3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao

ndani ya nyumba yako;

wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni

kuizunguka meza yako.

4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa

mtu amchayeBwana.

5 Bwanana akubariki kutoka Sayuni

siku zote za maisha yako,

na uone mafanikio ya Yerusalemu,

6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako.

Amani iwe juu ya Israeli.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/128-42322bf991cd46273a32779b87cfd157.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 129

Maombi Dhidi Ya Adui Za Israeli

Wimbo wa kwenda juu.

1 Wamenionea mno tangu ujana wangu;

Israeli na aseme sasa:

2 wamenionea mno tangu ujana wangu,

lakini bado hawajanishinda.

3 Wakulima wamelima mgongo wangu,

na kufanya mifereji yao mirefu.

4 LakiniBwanani mwenye haki;

amenifungua toka kamba za waovu.

5 Wale wote waichukiao Sayuni

na warudishwe nyuma kwa aibu.

6 Wawe kama majani juu ya paa,

ambayo hunyauka kabla hayajakua;

7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake,

wala akusanyaye kujaza mikono yake.

8 Wale wapitao karibu na wasiseme,

“Baraka yaBwanaiwe juu yako;

tunakubariki katika jina laBwana.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/129-9ffa949f38b7f78e6764c6dbb56706d0.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 130

Kuomba Msaada

Wimbo wa kwenda juu.

1 Kutoka vilindini ninakulilia, EeBwana.

2 EeBwana, sikia sauti yangu.

Masikio yako na yawe masikivu

kwa kilio changu unihurumie.

3 Kama wewe, EeBwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi,

Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?

4 Lakini kwako kuna msamaha,

kwa hiyo wewe unaogopwa.

5 NamngojeaBwana, nafsi yangu inangojea,

katika neno lake naweka tumaini langu.

6 Nafsi yangu inamngojea Bwana

kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi,

naam, kuliko walinzi

waingojeavyo asubuhi.

7 Ee Israeli, mtumainiBwana,

maana kwaBwanakuna upendo usiokoma,

na kwake kuna ukombozi kamili.

8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli

kutoka dhambi zao zote.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/130-0fa0927afafceabcb36aa675010cc524.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 131

Kumtegemea Mungu Kwa Unyenyekevu

Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.

1 Moyo wangu hauna kiburi, EeBwana,

macho yangu hayajivuni;

sijishughulishi na mambo makuu kunizidi

wala mambo ya ajabu mno kwangu.

2 Lakini nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu;

kama mtoto aliyeachishwa kunyonya na mama yake,

kama mtoto aliyeachishwa kunyonya

ndivyo ilivyo nafsi iliyoko ndani yangu.

3 Ee Israeli, mtumainiBwana

tangu sasa na hata milele.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/131-437d8757822eb8e3099c323a4841105e.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 132

Maskani Ya Mungu Ya Milele Katika Sayuni

Wimbo wa kwenda juu.

1 EeBwana, mkumbuke Daudi

na taabu zote alizozistahimili.

2 Aliapa kiapo kwaBwana

na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:

3 “Sitaingia nyumbani mwangu

au kwenda kitandani mwangu:

4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu,

wala kope zangu kusinzia,

5 mpaka nitakapompatiaBwanamahali,

makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”

6 Tulisikia habari hii huko Efrathi,

tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:

7 “Twendeni kwenye makao yake,

na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;

8 inuka, EeBwana, uje mahali pako pa kupumzikia,

wewe na Sanduku la nguvu zako.

9 Makuhani wako na wavikwe haki,

watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”

10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako,

usimkatae mpakwa mafuta wako.

11 Bwanaalimwapia Daudi kiapo,

kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua:

“Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe

katika kiti chako cha enzi,

12 kama wanao watashika Agano langu

na sheria ninazowafundisha,

ndipo wana wao watarithi

kiti chako cha enzi milele na milele.”

13 Kwa maanaBwanaameichagua Sayuni,

amepaonea shauku pawe maskani yake:

14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele;

hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:

15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele:

nitashibisha maskini wake kwa chakula.

16 Nitawavika makuhani wake wokovu,

nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.

17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe,

na kuweka taa kwa ajili ya masiyawangu.

18 Adui zake nitawavika aibu,

bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/132-f29cd9d9b7dc1d8d234191c8996384b2.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 133

Sifa Za Pendo La Undugu

Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.

1 Tazama jinsi ilivyo vyema na kupendeza

wakati ndugu wanapoishi pamoja katika umoja!

2 Ni kama mafuta ya thamani yaliyomiminwa kichwani,

yakitiririka kwenye ndevu,

yakitiririka kwenye ndevu za Aroni,

mpaka kwenye upindo wa mavazi yake.

3 Ni kama vile umande wa Hermoni

unavyoanguka juu ya Mlima Sayuni.

Kwa maana huko ndikoBwanaalikoamuru baraka yake,

naam, hata uzima milele.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/133-38ef0c4a3e3a0da405966e0ae173ef01.mp3?version_id=1627—