Categories
Zaburi

Zaburi 104

Kumsifu Muumba

1 Ee nafsi yangu, umhimidiBwana.

EeBwanaMungu wangu, wewe ni mkuu sana,

umejivika utukufu na enzi.

2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi,

amezitandaza mbingu kama hema

3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji.

Huyafanya mawingu kuwa gari lake,

na hupanda kwenye mbawa za upepo.

4 Huzifanya pepo kuwa wajumbewake,

miali ya moto watumishi wake.

5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake,

haiwezi kamwe kuondoshwa.

6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi,

maji yalisimama juu ya milima.

7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia,

kwa sauti ya radi yako yakatoroka,

8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni,

hadi mahali pale ulipoyakusudia.

9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka,

kamwe hayataifunika dunia tena.

10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni,

hutiririka kati ya milima.

11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni,

punda-mwitu huzima kiu yao.

12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji,

huimba katikati ya matawi.

13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake,

dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.

14 Huyafanya majani ya mifugo yaote,

na mimea kwa watu kulima,

wajipatie chakula kutoka ardhini:

15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu,

mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake,

na mkate wa kutia mwili nguvu.

16 Miti yaBwanainanyeshewa vizuri,

mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.

17 Humo ndege hufanya viota vyao,

korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.

18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu,

majabali ni kimbilio la pelele.

19 Mwezi hugawanya majira,

na jua hutambua wakati wake wa kutua.

20 Unaleta giza, kunakuwa usiku,

wanyama wote wa mwituni huzurura.

21 Simba hunguruma kwa mawindo yao,

na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.

22 Jua huchomoza, nao huondoka,

hurudi na kulala katika mapango yao.

23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake,

katika kazi yake mpaka jioni.

24 EeBwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi!

Kwa hekima ulizifanya zote,

dunia imejaa viumbe vyako.

25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele,

imejaa viumbe visivyo na idadi,

vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.

26 Huko meli huenda na kurudi,

pia Lewiathani,uliyemuumba acheze ndani yake.

27 Hawa wote wanakutazamia wewe,

uwape chakula chao kwa wakati wake.

28 Wakati unapowapa,

wanakikusanya,

unapofumbua mkono wako,

wao wanashibishwa mema.

29 Unapoficha uso wako,

wanapata hofu,

unapoondoa pumzi yao,

wanakufa na kurudi mavumbini.

30 Unapopeleka Roho wako,

wanaumbwa,

nawe huufanya upya uso wa dunia.

31 Utukufu waBwanana udumu milele,

Bwanana azifurahie kazi zake:

32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka,

aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.

33 NitamwimbiaBwanamaisha yangu yote;

nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.

34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye,

ninapofurahi katikaBwana.

35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia

na waovu wasiwepo tena.

Ee nafsi yangu, msifuBwana.

MsifuniBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/104-e585def5ed27db73babc7cf5c5653b5a.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 105

Uaminifu Wa Mungu Kwa Israeli

1 MshukuruniBwana, liitieni jina lake,

wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.

2 Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa,

waambieni matendo yake yote ya ajabu.

3 Lishangilieni jina lake takatifu,

mioyo ya wale wamtafutaoBwanana ifurahi.

4 MtafuteniBwanana nguvu zake,

utafuteni uso wake siku zote.

5 Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya,

miujiza yake na hukumu alizozitamka,

6 enyi wazao wa Abrahamu mtumishi wake,

enyi wana wa Yakobo, wateule wake.

7 Yeye ndiyeBwanaMungu wetu,

hukumu zake zimo duniani pote.

8 Hulikumbuka agano lake milele,

neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,

9 agano alilolifanya na Abrahamu,

kiapo alichomwapia Isaki.

10 Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri,

kwa Israeli liwe agano la milele:

11 “Nitakupa wewe nchi ya Kanaani

kuwa sehemu utakayoirithi.”

12 Walipokuwa wachache kwa idadi,

wachache sana na wageni ndani yake,

13 walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine,

kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.

14 Hakuruhusu mtu yeyote awaonee;

kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:

15 “Msiwaguse niliowatia mafuta;

msiwadhuru manabii wangu.”

16 Akaiita njaa juu ya nchi

na kuharibu chakula chao chote,

17 naye akatuma mtu mbele yao,

Yosefu, aliyeuzwa kama mtumwa.

18 Walichubua miguu yake kwa minyororo,

shingo yake ilifungwa kwa chuma,

19 hadi yale aliyotangulia kusema yalipotimia,

hadi neno laBwanalilipomthibitisha.

20 Mfalme alituma watu wakamfungua,

mtawala wa watu alimwachia huru.

21 Alimfanya mkuu wa nyumba yake,

mtawala juu ya vyote alivyokuwa navyo,

22 kuwaelekeza wakuu wa mfalme apendavyo

na kuwafundisha wazee wake hekima.

23 Kisha Israeli akaingia Misri,

Yakobo akaishi kama mgeni katika nchi ya Hamu.

24 Bwanaaliwafanya watu wake kuzaana sana,

akawafanya kuwa wengi sana kuliko adui zao,

25 ndiye aliigeuza mioyo yao iwachukie watu wake,

wakatenda hila dhidi ya watumishi wake.

26 Akamtuma Mose mtumishi wake,

pamoja na Aroni, aliyemchagua.

27 Walifanya ishara zake za ajabu miongoni mwao,

miujiza yake katika nchi ya Hamu.

28 Alituma giza na nchi ikajaa giza,

kwani si walikuwa wameyaasi maneno yake?

29 Aligeuza maji yao kuwa damu,

ikasababisha samaki wao kufa.

30 Nchi yao ilijaa vyura tele, ambao waliingia

hadi kwenye vyumba vya kulala vya watawala wao.

31 Alisema, yakaja makundi ya mainzi,

na viroboto katika nchi yao yote.

32 Alibadilisha mvua yao ikawa mvua ya mawe,

yenye umeme wa radi nchini yao yote,

33 akaharibu mizabibu yao na miti ya tini,

na akaangamiza miti ya nchi yao.

34 Alisema, nzige wakaja,

tunutu wasio na idadi,

35 wakala kila jani katika nchi yao,

wakala mazao ya ardhi yao.

36 Kisha akawaua wazaliwa wote wa kwanza katika nchi yao,

matunda ya kwanza ya ujana wao wote.

37 Akawatoa Israeli katika nchi

wakiwa na fedha na dhahabu nyingi,

wala hakuna hata mmoja

kutoka kabila zao aliyejikwaa.

38 Misri ilifurahi walipoondoka,

kwa sababu hofu ya Israeli ilikuwa imewaangukia.

39 Alitandaza wingu kama kifuniko,

na moto kuwamulikia usiku.

40 Waliomba, naye akawaletea kware,

akawashibisha kwa mkate wa mbinguni.

41 Alipasua mwamba, maji yakabubujika,

yakatiririka jangwani kama mto.

42 Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu,

aliyompa Abrahamu mtumishi wake.

43 Aliwatoa watu wake kwa furaha,

wateule wake kwa kelele za shangwe,

44 akawapa nchi za mataifa, wakawa warithi

wa mali wengine walikuwa wameitaabikia:

45 alifanya haya ili wayashike mausia yake

na kuzitii sheria zake.

MsifuniBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/105-11a17a0347b8487edfbd27bdbd14030f.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 106

Wema Wa Bwana Kwa Watu Wake

1 MsifuniBwana.

MshukuruniBwana, kwa kuwa ni mwema;

upendo wake wadumu milele.

2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu yaBwana

au kutangaza kikamilifu sifa zake?

3 Heri wale wanaodumisha haki,

ambao daima wanafanya yaliyo mema.

4 EeBwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako,

uwe msaada wangu unapowaokoa,

5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako,

niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako,

na kuungana na urithi wako katika kukusifu.

6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda,

tumekosa na tumetenda uovu.

7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri,

hawakuzingatia maajabu yako,

wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako,

bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.

8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake,

ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.

9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka,

akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.

10 Aliwaokoa mikononi mwa adui;

kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.

11 Maji yaliwafunika adui zao,

hakunusurika hata mmoja.

12 Ndipo walipoamini ahadi zake,

nao wakaimba sifa zake.

13 Lakini mara walisahau aliyowatendea,

wala hawakungojea shauri lake.

14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao,

walimjaribu Mungu nyikani.

15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba,

lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.

16 Kambini walimwonea wivu Mose,

na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwaBwana.

17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani,

ikawazika Abiramu na kundi lake.

18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao,

mwali wa moto uliwateketeza waovu.

19 Huko Horebu walitengeneza ndama,

na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.

20 Waliubadilisha Utukufu wao

kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.

21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa,

aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,

22 miujiza katika nchi ya Hamu

na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.

23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza:

kama Mose mteule wake,

asingesimama kati yao na Mungu

kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.

24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri,

hawakuiamini ahadi yake.

25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao,

wala hawakumtiiBwana.

26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa

kwamba atawafanya waanguke jangwani,

27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa,

na kuwatawanya katika nchi zote.

28 Walijifunga nira na Baali wa Peori,

wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.

29 Waliichochea hasira yaBwana,

wakamkasirisha kwa matendo yao maovu,

nayo tauni ikazuka katikati yao.

30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati,

nayo tauni ikazuiliwa.

31 Hili likahesabiwa kwake haki,

kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.

32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirishaBwana,

janga likampata Mose kwa sababu yao;

33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu,

na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.

34 Hawakuyaangamiza yale mataifa

kamaBwanaalivyowaagiza,

35 bali walijichanganya na mataifa

na wakazikubali desturi zao.

36 Waliabudu sanamu zao,

zikawa mtego kwao.

37 Wakawatoa wana wao

na binti zao dhabihu kwa mashetani.

38 Walimwaga damu isiyo na hatia,

damu za wana wao na binti zao,

ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani,

nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.

39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda;

kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.

40 Kwa hiyoBwanaakawakasirikia watu wake

na akauchukia sana urithi wake.

41 Akawakabidhi kwa mataifa

na adui zao wakawatawala.

42 Adui zao wakawaonea

na kuwatia chini ya mamlaka yao.

43 Mara nyingi aliwaokoa

lakini walikuwa wamezama kwenye uasi,

nao wakajiharibu katika dhambi zao.

44 Lakini akaangalia mateso yao

wakati aliposikia kilio chao;

45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake,

na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.

46 Akawafanya wahurumiwe

na wote waliowashikilia mateka.

47 EeBwanaMungu wetu, tuokoe.

Tukusanye tena kutoka kwa mataifa,

ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu,

na kushangilia katika sifa zako.

48 AtukuzweBwana, Mungu wa Israeli,

tangu milele na hata milele.

Watu wote na waseme, “Amen!”

MsifuniBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/106-e75590dd685bd20a7f4923c70dfa3630.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 107

Kumsifu Mungu Kwa Wema Wake

1 MshukuruniBwana, kwa kuwa yeye ni mwema,

upendo wake wadumu milele.

2 Waliokombolewa waBwanana waseme hivi,

wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,

3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali,

kutoka mashariki na magharibi,

kutoka kaskazini na kusini.

4 Baadhi yao walitangatanga jangwani,

hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.

5 Walikuwa na njaa na kiu,

nafsi zao zikadhoofika.

6 Ndipo walipomliliaBwanakatika shida yao,

naye akawaokoa kutoka taabu yao.

7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa

hadi mji ambao wangeweza kuishi.

8 Basi na wamshukuruBwanakwa upendo wake usiokoma,

na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,

9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu,

na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.

10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu,

wafungwa wakiteseka katika minyororo,

11 kwa sababu walikuwa wameasi

dhidi ya maneno ya Mungu

na kudharau shauri

la Aliye Juu Sana.

12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu;

walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.

13 Ndipo walipomliliaBwanakatika shida yao,

naye akawaokoa kutoka taabu yao.

14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu

na akavunja minyororo yao.

15 Basi na wamshukuruBwanakwa upendo wake usiokoma,

na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,

16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba

na kukata mapingo ya chuma.

17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao,

wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.

18 Wakachukia kabisa vyakula vyote,

wakakaribia malango ya mauti.

19 Ndipo walipomliliaBwanakatika shida yao,

naye akawaokoa kutoka taabu yao.

20 Akalituma neno lake na kuwaponya,

akawaokoa kutoka maangamizo yao.

21 Basi na wamshukuruBwanakwa upendo wake usiokoma,

na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.

22 Na watoe dhabihu za kushukuru,

na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.

23 Wengine walisafiri baharini kwa meli,

walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.

24 Waliziona kazi zaBwana,

matendo yake ya ajabu kilindini.

25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani

iliyoinua mawimbi juu.

26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini,

katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.

27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi,

ujanja wao ukafikia ukomo.

28 Ndipo walipomliliaBwanakatika shida yao,

naye akawatoa kwenye taabu yao.

29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono,

mawimbi ya bahari yakatulia.

30 Walifurahi ilipokuwa shwari,

naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.

31 Basi na wamshukuruBwanakwa upendo wake usiokoma,

na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.

32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu,

na wamsifu katika baraza la wazee.

33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa,

chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,

34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa,

kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.

35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji,

nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;

36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo,

nao wakajenga mji wangeweza kuishi.

37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu,

nayo ikazaa matunda mengi,

38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana,

wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.

39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa

kwa kuonewa, maafa na huzuni.

40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu,

aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.

41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao,

na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.

42 Wanyofu wataona na kufurahi,

lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.

43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya,

na atafakari upendo mkuu waBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/107-26377a1b5677ac9f51893a4d49503e03.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 108

Kuomba Msaada Dhidi Ya Adui

Wimbo. Zaburi ya Daudi.

1 Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti;

nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.

2 Amka, kinubi na zeze!

Nitayaamsha mapambazuko.

3 Nitakusifu wewe, EeBwana, katikati ya mataifa;

nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.

4 Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu;

uaminifu wako unazifikia anga.

5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,

utukufu wako na uenee duniani kote.

6 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume,

ili wale uwapendao wapate kuokolewa.

7 Mungu amenena kutoka patakatifu pake:

“Nitaigawa Shekemu kwa ushindi

na kulipima Bonde la Sukothi.

8 Gileadi ni yangu, Manase ni yangu,

Efraimu ni kofia yangu ya chuma,

nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.

9 Moabu ni sinia langu la kunawia,

juu ya Edomu natupa kiatu changu;

nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”

10 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome?

Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?

11 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi,

na hutoki tena na majeshi yetu?

12 Tuletee msaada dhidi ya adui,

kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.

13 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi,

naye atawaponda adui zetu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/108-39932af83d283fa9eb8ec3980fb18537.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 109

Lalamiko La Mtu Aliyeko Kwenye Shida

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 Ee Mungu, ambaye ninakusifu,

usiwe kimya,

2 kwa maana watu waovu na wadanganyifu

wamefungua vinywa vyao dhidi yangu;

wasema dhidi yangu

kwa ndimi za udanganyifu.

3 Wamenizunguka kwa maneno ya chuki,

wananishambulia bila sababu.

4 Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki,

lakini mimi ninawaombea.

5 Wananilipiza mabaya kwa mema,

chuki badala ya urafiki wangu.

6 Agiza mtu mwovu ampinge,

mshtakiasimame mkono wake wa kuume.

7 Anapohukumiwa, apatikane na hatia,

nayo maombi yake yamhukumu.

8 Siku zake za kuishi na ziwe chache,

nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.

9 Watoto wake na waachwe yatima,

mke wake na awe mjane.

10 Watoto wake na watangetange wakiomba,

na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.

11 Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo,

matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.

12 Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema

wala wa kuwahurumia yatima wake.

13 Uzao wake na ukatiliwe mbali,

majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.

14 Maovu ya baba zake na yakumbukwe

mbele zaBwana,

dhambi ya mama yake

isifutwe kamwe.

15 Dhambi zao na zibaki daima mbele zaBwana,

ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.

16 Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema,

bali alimfukuza mnyonge na mhitaji,

aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.

17 Alipenda kulaani,

nayo laana ikampata;

hakupenda kubariki,

kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.

18 Alivaa kulaani kama vazi lake,

nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji,

kwenye mifupa yake kama mafuta.

19 Na iwe kama joho alilozungushiwa,

kama mshipi aliofungiwa daima.

20 Haya na yawe malipo yaBwanakwa washtaki wangu,

kwa wale wanaoninenea mabaya.

21 Lakini wewe, EeBwanaMwenyezi,

unitendee wema kwa ajili ya jina lako,

uniokoe kwa wema wa pendo lako.

22 Maana mimi ni maskini na mhitaji,

moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.

23 Ninafifia kama kivuli cha jioni,

nimerushwa-rushwa kama nzige.

24 Magoti yangu yamelegea kwa kufunga,

mwili wangu umedhoofika na kukonda.

25 Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu,

wanionapo, hutikisa vichwa vyao.

26 EeBwana, Mungu wangu nisaidie,

niokoe sawasawa na upendo wako.

27 Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako,

kwamba wewe, EeBwana, umetenda hili.

28 Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki,

watakaposhambulia wataaibishwa,

lakini mtumishi wako atashangilia.

29 Washtaki wangu watavikwa fedheha,

na kufunikwa na aibu kama joho.

30 Kwa kinywa changu nitamtukuza sanaBwana,

katika umati mkubwa nitamsifu.

31 Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji,

kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/109-fd72b023db33f14ecb3b7e5a63785879.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 110

Bwana Na Mfalme Wake Mteule

Zaburi ya Daudi.

1 Bwanaamwambia Bwana wangu:

“Keti mkono wangu wa kuume,

mpaka nitakapowafanya adui zako

kuwa mahali pa kuweka miguu yako.”

2 Bwanaataeneza fimbo yako ya utawala yenye nguvu kutoka Sayuni;

utatawala katikati ya adui zako.

3 Askari wako watajitolea kwa hiari

katika siku yako ya vita.

Ukiwa umevikwa fahari takatifu,

kutoka tumbo la mapambazuko

utapokea umande wa ujana wako.

4 Bwanaameapa,

naye hatabadilisha mawazo yake:

“Wewe ni kuhani milele,

kwa mfano wa Melkizedeki.”

5 Bwana yuko mkono wako wa kuume,

atawaponda wafalme siku ya ghadhabu yake.

6 Atawahukumu mataifa, akilundika mizoga

na kuwaponda watawala wa dunia nzima.

7 Atakunywa maji katika kijito kando ya njia,

kwa hiyo atainua kichwa chake juu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/110-8f324b599490c012590b4eb9baf7390b.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 111

Sifa Za Bwana Kwa Matendo Ya Ajabu

1 MsifuniBwana.

NitamtukuzaBwanakwa moyo wangu wote,

katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.

2 Kazi zaBwanani kuu,

wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.

3 Kazi zake zimejaa fahari na utukufu,

haki yake hudumu daima.

4 Amefanya maajabu yake yakumbukwe,

Bwanani mwenye neema na huruma.

5 Huwapa chakula wale wanaomcha,

hulikumbuka agano lake milele.

6 Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake,

akiwapa nchi za mataifa mengine.

7 Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki,

mausia yake yote ni ya kuaminika.

8 Zinadumu milele na milele,

zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.

9 Aliwapa watu wake ukombozi,

aliamuru agano lake milele:

jina lake ni takatifu na la kuogopwa.

10 KumchaBwanandicho chanzo cha hekima,

wote wanaozifuata amri zake wana busara.

Sifa zake zadumu milele.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/111-fcbaf92f4ba0a7f3ecc7034f23b9cdb2.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 112

Baraka Za Mwenye Haki

1 MsifuniBwana.

Heri mtu yule amchayeBwana,

mtu yule apendezwaye sana na amri zake.

2 Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi,

kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.

3 Nyumbani mwake kuna mali na utajiri,

haki yake hudumu milele.

4 Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu,

yule mwenye rehema, huruma na haki.

5 Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba,

anayefanya mambo yake kwa haki.

6 Hakika hatatikisika kamwe,

mtu mwenye haki atakumbukwa milele.

7 Hataogopa habari mbaya,

moyo wake ni thabiti, ukimtegemeaBwana.

8 Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu,

mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.

9 Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini;

haki yake hudumu milele;

pembe yake itatukuzwa kwa heshima.

10 Mtu mwovu ataona na kuchukizwa,

atasaga meno yake na kutoweka,

kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/112-9a9d1bf374d655d84427efbeb9eed1f0.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 113

Kumsifu Bwana Kwa Wema Wake

1 MsifuniBwana.

Enyi watumishi waBwanamsifuni,

lisifuni jina laBwana.

2 Jina laBwanana lisifiwe,

sasa na hata milele.

3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake,

jina laBwanalinapaswa kusifiwa.

4 Bwanaametukuka juu ya mataifa yote,

utukufu wake juu ya mbingu.

5 Ni nani aliye kamaBwanaMungu wetu,

Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,

6 ambaye huinama atazame chini

aone mbingu na nchi?

7 Huwainua maskini kutoka mavumbini,

na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,

8 huwaketisha pamoja na wakuu,

pamoja na wakuu wa watu wake.

9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake,

akiwa mama watoto mwenye furaha.

MsifuniBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/113-53c3869e1e1a9355715e21b5247d5f73.mp3?version_id=1627—