Categories
Zaburi

Zaburi 84

Kuionea Shauku Nyumba Ya Mungu

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora.

1 EeBwanaMwenye Nguvu Zote,

makao yako yapendeza kama nini!

2 Nafsi yangu inatamani sana,

naam, hata kuona shauku,

kwa ajili ya nyua zaBwana;

moyo wangu na mwili wangu

vinamlilia Mungu Aliye Hai.

3 Hata shomoro amejipatia makao,

mbayuwayu amejipatia kiota

mahali awezapo kuweka makinda yake:

mahali karibu na madhabahu yako,

EeBwanaMwenye Nguvu Zote,

Mfalme wangu na Mungu wangu.

4 Heri wale wanaokaa nyumbani mwako,

wanaokusifu wewe daima.

5 Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako,

na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.

6 Wanapopita katika Bonde la Baka,

hulifanya mahali pa chemchemi,

pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.

7 Huendelea toka nguvu hadi nguvu,

hadi kila mmoja afikapo

mbele za Mungu huko Sayuni.

8 EeBwanaMungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu;

nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.

9 Ee Mungu, uitazame ngao yetu,

mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.

10 Siku moja katika nyua zako ni bora

kuliko siku elfu mahali pengine;

afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu

kuliko kukaa katika mahema ya waovu.

11 Kwa kuwaBwanani jua na ngao,

Bwanahutoa wema na heshima;

hakuna kitu chema anachowanyima

wale ambao hawana hatia.

12 EeBwanaMwenye Nguvu Zote,

heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/84-de9fa6d217312710ae91c4f248286a9d.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 85

Maombi Kwa Ajili Ya Ustawi Wa Taifa

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora.

1 EeBwana, ulionyesha wema kwa nchi yako.

Ulimrejeshea Yakobo baraka zake.

2 Ulisamehe uovu wa watu wako,

na kufunika dhambi zao zote.

3 Uliweka kando ghadhabu yako yote

na umegeuka na kuiacha hasira yako kali.

4 Ee Mungu Mwokozi wetu, uturejeshe tena,

nawe uiondoe chuki yako juu yetu.

5 Je, utatukasirikia milele?

Utaendeleza hasira yako kwa vizazi vyote?

6 Je, hutatuhuisha tena,

ili watu wako wakufurahie?

7 Utuonyeshe upendo wako usiokoma, EeBwana,

utupe wokovu wako.

8 Nitasikiliza lile atakalosema Mungu aliyeBwana;

anaahidi amani kwa watu wake, watakatifu wake:

lakini nao wasirudie upumbavu.

9 Hakika wokovu wake uko karibu na wale wamchao,

ili utukufu wake udumu katika nchi yetu.

10 Upendo na uaminifu hukutana pamoja,

haki na amani hubusiana.

11 Uaminifu huchipua kutoka nchi,

haki hutazama chini kutoka mbinguni.

12 Naam, hakikaBwanaatatoa kilicho chema,

nayo nchi yetu itazaa mavuno yake.

13 Haki itatangulia mbele yake

na kutengeneza njia kwa ajili ya hatua zake.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/85-156429c1a93caa8c13cec7b5208a6cb1.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 86

Kuomba Msaada

Maombi ya Daudi.

1 EeBwana, sikia na unijibu,

kwa maana mimi ni maskini na mhitaji.

2 Linda maisha yangu, kwa maana nimejiweka kwako,

wewe ni Mungu wangu,

mwokoe mtumishi wako anayekutumaini.

3 EeBwana, nihurumie mimi,

kwa maana ninakuita mchana kutwa.

4 Mpe mtumishi wako furaha,

kwa kuwa kwako wewe, EeBwana,

ninainua nafsi yangu.

5 EeBwana, wewe ni mwema na mwenye kusamehe,

umejaa upendo kwa wote wakuitao.

6 EeBwana, sikia maombi yangu,

sikiliza kilio changu unihurumie.

7 Katika siku ya shida yangu nitakuita,

kwa maana wewe utanijibu.

8 EeBwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe,

hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.

9 EeBwana, mataifa yote uliyoyafanya

yatakuja na kuabudu mbele zako;

wataliletea utukufu jina lako.

10 Kwa maana wewe ni mkuu, na unafanya mambo ya ajabu;

wewe peke yako ndiwe Mungu.

11 EeBwana, nifundishe njia yako,

nami nitakwenda katika kweli yako;

nipe moyo usiositasita,

ili niweze kulicha jina lako.

12 EeBwanawangu, nitakusifu kwa moyo wote;

nitaliadhimisha jina lako milele.

13 Kwa maana upendo wako ni mkuu kwangu;

umeniokoa kutoka kwenye vilindi vya kaburi.

14 Ee Mungu, wenye majivuno wananishambulia;

kundi la watu wakatili linatafuta uhai wangu:

watu wasiokuheshimu wewe.

15 Lakini wewe, EeBwana, ni Mungu wa huruma na neema,

si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo na uaminifu.

16 Nigeukie na unihurumie;

mpe mtumishi wako nguvu zako,

mwokoe mwana wa mtumishi wako wa kike.

17 Nipe ishara ya wema wako,

ili adui zangu waione nao waaibishwe,

kwa kuwa wewe, EeBwana,

umenisaidia na kunifariji.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/86-374bffae46feebf1d5ca5d4a064fa2db.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 87

Sifa Za Yerusalemu

Zaburi ya wana wa Kora. Wimbo.

1 Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;

2 Bwanaanayapenda malango ya Sayuni

kuliko makao yote ya Yakobo.

3 Mambo matukufu yanasemwa juu yako,

ee mji wa Mungu:

4 “Nitaweka kumbukumbu ya Rahabuna Babeli

miongoni mwa wale wanaonikubali mimi:

Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi,

nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’ ”

5 Kuhusu Sayuni itasemwa hivi,

“Huyu na yule walizaliwa humo,

naye Aliye Juu Sana mwenyewe

atamwimarisha.”

6 Bwanaataandika katika orodha ya mataifa:

“Huyu alizaliwa Sayuni.”

7 Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba,

“Chemchemi zangu zote ziko kwako.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/87-b58571d086216174f2c1a99235746623.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 88

Kilio Kwa Ajili Ya Kuomba Msaada

Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi.

1 EeBwana, Mungu uniokoaye,

nimelia mbele zako usiku na mchana.

2 Maombi yangu yafike mbele zako,

utegee kilio changu sikio lako.

3 Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu,

na maisha yangu yanakaribia kaburi.

4 Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni,

niko kama mtu asiye na nguvu.

5 Nimetengwa pamoja na wafu,

kama waliochinjwa walalao kaburini,

ambao huwakumbuki tena,

ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.

6 Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana,

katika vina vya giza nene.

7 Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu,

umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.

8 Umenitenga na rafiki zangu wa karibu

na kunifanya chukizo kwao.

Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;

9 nuru ya macho yangu

imefifia kwa ajili ya huzuni.

EeBwana, ninakuita kila siku,

ninakunyooshea wewe mikono yangu.

10 Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako?

Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?

11 Je, upendo wako hutangazwa kaburini,

uaminifu wako katika Uharibifu?

12 Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza,

au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?

13 Lakini ninakulilia wewe, EeBwana, unisaidie;

asubuhi maombi yangu huja mbele zako.

14 EeBwana, kwa nini unanikataa

na kunificha uso wako?

15 Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo;

nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.

16 Ghadhabu yako imepita juu yangu;

hofu zako zimeniangamiza.

17 Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko;

zimenimeza kabisa.

18 Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu;

giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/88-cacc7906f9c2e752d914701be3488263.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 89

Wimbo Wakati Wa Taabu Ya Kitaifa

Utenzi wa Ethani Mwezrahi.

1 Nitaimba juu ya upendo mkuu waBwanamilele;

kwa kinywa changu nitajulisha uaminifu wako

ujulikane kwa vizazi vyote.

2 Nitatangaza kuwa upendo wako unasimama imara milele

na uaminifu wako umeuthibitisha mbinguni.

3 Ulisema, “Nimefanya agano na mteule wangu,

nimemwapia mtumishi wangu Daudi,

4 ‘Nitaimarisha uzao wako milele

na kudumisha ufalme wako kwa vizazi vyote.’ ”

5 EeBwana, mbingu zinayasifu maajabu yako,

uaminifu wako pia katika kusanyiko la watakatifu.

6 Kwa kuwa ni nani katika mbingu

anayeweza kulinganishwa naBwana?

Ni nani miongoni mwa viumbe vya mbinguni

aliye kamaBwana?

7 Katika kusanyiko la watakatifu, Mungu huogopwa sana,

anahofiwa kuliko wote wanaomzunguka.

8 EeBwanaMwenye Nguvu Zote,

ni nani aliye kama wewe?

EeBwana, wewe ni mwenye nguvu,

na uaminifu wako unakuzunguka.

9 Wewe unatawala bahari yenye msukosuko;

wakati mawimbi yake yanapoinuka, wewe unayatuliza.

10 Wewe ulimponda Rahabu

kama mmojawapo wa waliochinjwa;

kwa mkono wako wenye nguvu,

uliwatawanya adui zako.

11 Mbingu ni zako, nayo nchi pia ni yako,

uliuwekea ulimwengu msingi

pamoja na vyote vilivyomo.

12 Uliumba kaskazini na kusini;

Tabori na Hermoni wanaliimbia jina lako kwa furaha.

13 Mkono wako umejaa uwezo;

mkono wako una nguvu,

mkono wako wa kuume umetukuzwa.

14 Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako cha enzi;

upendo na uaminifu vinakutangulia.

15 Heri ni wale ambao wamejifunza kukusifu kwa shangwe,

wanaotembea katika mwanga

wa uwepo wako, EeBwana.

16 Wanashangilia katika jina lako mchana kutwa,

wanafurahi katika haki yako.

17 Kwa kuwa wewe ni utukufu na nguvu yao,

kwa wema wako unatukuza pembeyetu.

18 Naam, ngao yetu ni mali yaBwana,

na mfalme wetu mali ya Aliye Mtakatifu wa Israeli.

19 Ulizungumza wakati fulani katika maono,

kwa watu wako waaminifu, ukasema:

“Nimeweka nguvu kwa shujaa,

nimemwinua kijana miongoni mwa watu.

20 Nimemwona Daudi, mtumishi wangu,

na nimemtia mafuta yangu matakatifu.

21 Kitanga changu kitamtegemeza,

hakika mkono wangu utamtia nguvu.

22 Hakuna adui atakayemtoza ushuru,

hakuna mtu mwovu atakayemwonea.

23 Nitawaponda adui zake mbele zake

na kuwaangamiza watesi wake.

24 Upendo wangu mkamilifu utakuwa pamoja naye,

kwa Jina langu pembe yake itatukuzwa.

25 Nitauweka mkono wake juu ya bahari,

mkono wake wa kuume juu ya mito.

26 Naye ataniita kwa sauti, ‘Wewe ni Baba yangu,

Mungu wangu, Mwamba na Mwokozi wangu.’

27 Nitamteua pia awe mzaliwa wangu wa kwanza,

aliyetukuka kuliko wafalme wote wa dunia.

28 Nitadumisha upendo wangu kwake milele,

na agano langu naye litakuwa imara.

29 Nitaudumisha uzao wake milele,

kiti chake cha enzi kama mbingu zinavyodumu.

30 “Kama wanae wataacha amri yangu

na wasifuate sheria zangu,

31 kama wakihalifu maagizo yangu

na kutoshika amri zangu,

32 nitaadhibu dhambi yao kwa fimbo,

uovu wao kwa kuwapiga,

33 lakini sitauondoa upendo wangu kwake,

wala sitausaliti uaminifu wangu kamwe.

34 Mimi sitavunja agano langu

wala sitabadili lile ambalo midomo yangu imelitamka.

35 Mara moja na kwa milele, nimeapa kwa utakatifu wangu,

nami sitamdanganya Daudi:

36 kwamba uzao wake utaendelea milele,

na kiti chake cha enzi kitadumu mbele zangu kama jua;

37 kitaimarishwa milele kama mwezi,

shahidi mwaminifu angani.”

38 Lakini wewe umemkataa, umemdharau,

umemkasirikia sana mpakwa mafuta wako.

39 Umelikana agano lako na mtumishi wako,

na umeinajisi taji yake mavumbini.

40 Umebomoa kuta zake zote,

na ngome zake zote umezifanya kuwa magofu.

41 Wote wapitao karibu wamemnyangʼanya mali zake;

amekuwa dharau kwa jirani zake.

42 Umeutukuza mkono wa kuume wa adui zake,

umewafanya watesi wake wote washangilie.

43 Umegeuza makali ya upanga wake,

na hukumpa msaada katika vita.

44 Umeikomesha fahari yake,

na kukiangusha kiti chake cha enzi.

45 Umezifupisha siku za ujana wake,

umemfunika kwa vazi la aibu.

46 Hata lini, EeBwana? Utajificha milele?

Ghadhabu yako itawaka kama moto hata lini?

47 Kumbuka jinsi maisha yangu yanavyopita haraka.

Ni kwa ubatili kiasi gani umemuumba mwanadamu!

48 Ni mtu gani awezaye kuishi na asione kifo,

au kujiokoa mwenyewe kutoka nguvu za kaburi?

49 EeBwana, uko wapi upendo wako mkuu wa mwanzoni,

ambao katika uaminifu wako ulimwapia Daudi?

50 Bwana kumbuka jinsi mtumishi wako amesimangwa,

jinsi ninavyovumilia moyoni mwangu dhihaka za mataifa yote,

51 dhihaka ambazo kwazo adui zako

wamenisimanga, EeBwana,

ambazo kwazo wamesimanga

kila hatua ya mpakwa mafuta wako.

52 MsifuniBwanamilele!

Amen na Amen.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/89-837c39996f28e55d2ddacbac4029ab64.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 90

Umilele Wa Mungu Na Udhaifu Wa Mwanadamu

Maombi ya Mose, mtu wa Mungu.

1 Bwana, wewe umekuwa makao yetu

katika vizazi vyote.

2 Kabla ya kuzaliwa milima

au hujaumba dunia na ulimwengu,

wewe ni Mungu tangu milele hata milele.

3 Huwarudisha watu mavumbini,

ukisema, “Rudini mavumbini, enyi wanadamu.”

4 Kwa maana kwako miaka elfu

ni kama siku moja iliyokwisha pita,

au kama kesha la usiku.

5 Unawatowesha wanadamu katika usingizi wa kifo,

nao ni kama majani machanga ya asubuhi:

6 ingawa asubuhi yanachipua,

ifikapo jioni huwa yamenyauka na kukauka.

7 Tumeangamizwa kwa hasira yako

na tumetishwa kwa ghadhabu yako.

8 Umeyaweka maovu yetu mbele yako,

dhambi zetu za siri katika nuru ya uwepo wako.

9 Tumeishi siku zetu zote chini ya ghadhabu yako,

tunamaliza miaka yetu kwa kuomboleza.

10 Siku zetu za kuishi ni miaka sabini,

au miaka themanini ikiwa tuna nguvu,

lakini yote ni ya shida na taabu,

nazo zapita haraka, nasi twatoweka.

11 Ni nani ajuaye nguvu za hasira yako?

Kwa maana ghadhabu yako ni kubwa

kama hofu tunayopaswa kuwa nayo kwako.

12 Tufundishe kuzihesabu siku zetu vizuri,

ili tujipatie moyo wa hekima.

13 EeBwana, uwe na huruma! Utakawia hata lini?

Wahurumie watumishi wako.

14 Tushibishe asubuhi kwa upendo wako usiokoma,

ili tuweze kuimba kwa shangwe na kufurahi siku zetu zote.

15 Utufurahishe kulingana na siku ulizotuadhibu,

kulingana na miaka tuliyotaabika.

16 Matendo yako na yaonekane kwa watumishi wako,

utukufu wako kwa watoto wao.

17 Wema waBwanaMungu wetu uwe juu yetu;

uzithibitishe kazi za mikono yetu:

naam, uzithibitishe kazi za mikono yetu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/90-150d8cdc999650290c1142b4dce37179.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 91

Mungu Mlinzi Wetu

1 Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana,

atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.

2 Nitasema kumhusuBwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu,

Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”

3 Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji,

na maradhi ya kuambukiza ya kuua.

4 Atakufunika kwa manyoya yake,

chini ya mbawa zake utapata kimbilio,

uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.

5 Hutaogopa vitisho vya usiku,

wala mshale urukao mchana,

6 wala maradhi ya kuambukiza

yanayonyemelea gizani,

wala tauni iharibuyo adhuhuri.

7 Ijapo watu elfu wataangukia kando yako,

kumi elfu mkono wako wa kuume,

lakini haitakukaribia wewe.

8 Utatazama tu kwa macho yako

na kuona adhabu ya waovu.

9 Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako:

naam,Bwanaambaye ni kimbilio langu,

10 basi hakuna madhara yatakayokupata wewe,

hakuna maafa yataikaribia hema yako.

11 Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako,

wakulinde katika njia zako zote.

12 Mikononi mwao watakuinua,

ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.

13 Utawakanyaga simba na nyoka wakali,

simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.

14 Bwanaasema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa;

nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.

15 Ataniita, nami nitamjibu;

nitakuwa pamoja naye katika taabu,

nitamwokoa na kumheshimu.

16 Kwa siku nyingi nitamshibisha

na kumwonyesha wokovu wangu.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/91-1e8eb4d06957f2222bb9adcc5be6fad7.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 92

Wimbo Wa Kumsifu Mungu

Zaburi. Wimbo wa siku ya Sabato.

1 Ni vyema kumshukuruBwana

na kuliimbia jina lako, Ee Uliye Juu Sana,

2 kuutangaza upendo wako asubuhi,

na uaminifu wako wakati wa usiku,

3 kwa zeze yenye nyuzi kumi

na kwa sauti ya kinubi.

4 EeBwana, kwa kuwa matendo yako yamenifurahisha,

nitaziimba kwa shangwe kazi za mikono yako.

5 EeBwana, tazama jinsi yalivyo makuu matendo yako,

tazama jinsi yalivyo ya kina mawazo yako!

6 Mjinga hafahamu,

mpumbavu haelewi,

7 ingawa waovu huchipua kama majani

na wote watendao mabaya wanastawi,

wataangamizwa milele.

8 Bali wewe, EeBwana,

utatukuzwa milele.

9 EeBwana, hakika adui zako,

hakika adui zako wataangamia.

Wote watendao mabaya watatawanyika.

10 Umeitukuza pembeyangu kama ile ya nyati dume,

mafuta mazuri yamemiminwa juu yangu.

11 Macho yangu yamewaona adui zangu wakishindwa,

masikio yangu yamesikia maangamizi ya adui zangu waovu.

12 Wenye haki watastawi kama mtende,

watakuwa kama mwerezi wa Lebanoni,

13 waliopandwa katika nyumba yaBwana,

watastawi katika nyua za Mungu wetu.

14 Wakati wa uzee watakuwa bado wanazaa matunda,

watakuwa wabichi tena wamejaa nguvu,

15 wakitangaza, “Bwanani mkamilifu;

yeye ni Mwamba wangu,

na ndani yake hamna uovu.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/92-abcb2c0bcc4264747d396a7aa8baa9d6.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 93

Mungu Mfalme

1 Bwanaanatawala, amejivika utukufu;

Bwanaamejivika utukufu

tena amejivika nguvu.

Dunia imewekwa imara,

haitaondoshwa.

2 Kiti chako cha enzi kimekuwa thabiti tangu zamani;

wewe umekuwako tangu milele.

3 Bahari zimeinua, EeBwana,

bahari zimeinua sauti zake;

bahari zimeinua sauti za mawimbi yake.

4 Yeye ni mkuu kuliko ngurumo ya maji makuu,

ni mkuu kuliko mawimbi ya bahari:

Bwanaaishiye juu sana ni mkuu.

5 EeBwana, sheria zako ni imara;

utakatifu umepamba nyumba yako

pasipo mwisho.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/93-cf07080b63ce6141768c12b426ba7404.mp3?version_id=1627—