Categories
Zaburi

Zaburi 64

Kuomba Ulinzi Dhidi Ya Maadui

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu,

uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.

2 Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu,

kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.

3 Wananoa ndimi zao kama panga

na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.

4 Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia,

humrushia ghafula bila woga.

5 Kila mmoja humtia moyo mwenzake

katika mipango mibaya;

huzungumza juu ya kuficha mitego yao,

nao husema, “Ni nani ataiona?”

6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema,

“Tumebuni mpango mkamilifu!”

Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.

7 Bali Mungu atawapiga kwa mishale,

nao ghafula wataangushwa.

8 Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao

na kuwaleta kwenye maangamizi;

wote wawaonao watatikisa vichwa vyao

kwa dharau.

9 Wanadamu wote wataogopa,

watatangaza kazi za Mungu

na kutafakari yale aliyoyatenda.

10 Wenye haki na wafurahi katikaBwana,

na wakimbilie kwake;

wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/64-0954e5e1243e91350d7b817e5d554bc1.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 65

Kusifu Na Kushukuru

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo.

1 Ee Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni;

kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa.

2 Ewe usikiaye maombi,

kwako wewe watu wote watakuja.

3 Tulipokuwa tumefunikwa kabisa na dhambi,

wewe ulisamehe makosa yetu.

4 Heri wale uliowachagua

na kuwaleta karibu ili waishi katika nyua zako!

Tunashibishwa kwa mema ya nyumba yako,

mema ya Hekalu lako takatifu.

5 Unatujibu kwa matendo ya kushangaza ya haki,

Ee Mungu Mwokozi wetu,

tumaini la miisho yote ya duniani

na la bahari zilizo mbali sana,

6 uliyeumba milima kwa uwezo wako,

ukiwa umejivika nguvu,

7 uliyenyamazisha dhoruba za bahari,

ngurumo za mawimbi yake,

na ghasia za mataifa.

8 Wale wanaoishi mbali sana

wanaogopa maajabu yako,

kule asubuhi ipambazukiapo

na kule jioni inakofifilia

umeziita nyimbo za furaha.

9 Waitunza nchi na kuinyeshea,

waitajirisha kwa wingi.

Vijito vya Mungu vimejaa maji

ili kuwapa watu nafaka,

kwa maana wewe umeviamuru.

10 Umeilowesha mifereji yake

na kusawazisha kingo zake;

umeilainisha kwa manyunyu

na kuibariki mimea yake.

11 Umeuvika mwaka taji ya baraka,

magari yako yanafurika kwa wingi.

12 Mbuga za majani za jangwani umezineemesha;

vilima vimevikwa furaha.

13 Penye nyanda za malisho pamejaa makundi ya wanyama,

na mabonde yamepambwa kwa mavuno;

vyote vinashangilia kwa furaha na kuimba.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/65-f12412d24536665e5d22b9fcfae35ba2.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 66

Kusifu Mungu Kwa Ajili Ya Wema Wake

Kwa mwimbishaji. Wimbo. Zaburi.

1 Mpigieni Mungu kelele za shangwe, dunia yote!

2 Imbeni utukufu wa jina lake;

mpeni sifa zake kwa utukufu!

3 Mwambieni Mungu, “Jinsi gani yalivyo ya kutisha matendo yako!

Uwezo wako ni mkuu mno kiasi kwamba

adui wananyenyekea mbele zako.

4 Dunia yote yakusujudia,

wanakuimbia wewe sifa,

wanaliimbia sifa jina lako.”

5 Njooni mwone yale Mungu aliyoyatenda,

mambo ya kutisha aliyoyatenda

miongoni mwa wanadamu!

6 Alifanya bahari kuwa nchi kavu,

wakapita kati ya maji kwa miguu,

njooni, tumshangilie.

7 Yeye hutawala kwa uwezo wake milele,

macho yake huangalia mataifa yote:

waasi wasithubutu kujiinua dhidi yake.

8 Enyi mataifa, msifuni Mungu wetu,

sauti ya sifa yake isikike,

9 ameyahifadhi maisha yetu

na kuizuia miguu yetu kuteleza.

10 Ee Mungu, wewe ulitujaribu,

ukatusafisha kama fedha.

11 Umetuingiza kwenye nyavu

na umetubebesha mizigo mizito

migongoni mwetu.

12 Uliwaruhusu watu watukalie vichwani,

tulipita kwenye moto na kwenye maji,

lakini ulituleta kwenye nchi

iliyojaa utajiri tele.

13 Nitakuja hekaluni mwako na sadaka za kuteketezwa

na kukutimizia nadhiri zangu:

14 nadhiri ambazo midomo yangu iliahidi

na nilizotamka kwa kinywa changu

nilipokuwa katika shida.

15 Nitakutolea dhabihu za wanyama wanono

na sadaka za kondoo dume,

nitakutolea mafahali na mbuzi.

16 Njooni msikilize ninyi nyote mnaomcha Mungu,

nami niwaambie aliyonitendea.

17 Nilimlilia kwa kinywa changu,

sifa zake zilikuwa katika ulimi wangu.

18 Kama ningekuwa nimeyaficha maovu moyoni mwangu,

Bwana asingekuwa amenisikiliza;

19 lakini hakika Mungu amenisikiliza

na amesikia sauti yangu katika maombi.

20 Sifa apewe Mungu,

ambaye hakulikataa ombi langu

wala kunizuilia upendo wake!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/66-70ae261997c556379da49c61557244d9.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 67

Mataifa Yahimizwa Kumsifu Mungu

Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za muziki. Zaburi. Wimbo.

1 Mungu aturehemu na kutubariki,

na kutuangazia nuru za uso wake,

2 ili njia zako zijulikane duniani,

wokovu wako katikati ya mataifa yote.

3 Ee Mungu, mataifa na wakusifu,

mataifa yote na wakusifu.

4 Mataifa yote wafurahi na kuimba kwa shangwe,

kwa kuwa unatawala watu kwa haki

na kuongoza mataifa ya dunia.

5 Ee Mungu, mataifa na wakusifu,

mataifa yote na wakusifu.

6 Ndipo nchi itatoa mazao yake,

naye Mungu, Mungu wetu, atatubariki.

7 Mungu atatubariki

na miisho yote ya dunia itamcha yeye.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/67-2c582af6264c83c4cba031743f9b97c6.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 68

Wimbo Wa Taifa Wa Shangwe Kwa Ushindi

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo.

1 Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike,

adui zake na wakimbie mbele zake.

2 Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo,

vivyo hivyo uwapeperushe mbali,

kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto,

vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.

3 Bali wenye haki na wafurahi,

washangilie mbele za Mungu,

wafurahi na kushangilia.

4 Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake,

mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu:

jina lake niBwana,

furahini mbele zake.

5 Baba wa yatima, mtetezi wa wajane,

ni Mungu katika makao yake matakatifu.

6 Mungu huwaweka wapweke katika jamaa,

huwaongoza wafungwa wakiimba,

bali waasi huishi katika nchi kame.

7 Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako,

ulipopita nyikani,

8 dunia ilitikisika,

mbingu zikanyesha mvua,

mbele za Mungu, Yule wa Sinai,

mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.

9 Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi

na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.

10 Ee Mungu, watu wako waliishi huko,

nawe kwa wingi wa utajiri wako

uliwapa maskini mahitaji yao.

11 Bwana alitangaza neno,

waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:

12 “Wafalme na majeshi walikimbia upesi,

watu waliobaki kambini waligawana nyara.

13 Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini,

mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha,

manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”

14 Wakati Mwenyezialipowatawanya wafalme katika nchi,

ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.

15 Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka,

milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.

16 Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka,

kwa nini mnakazia macho kwa wivu,

katika mlima Mungu anaochagua kutawala,

ambakoBwanamwenyewe ataishi milele?

17 Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu,

na maelfu ya maelfu;

Bwana amekuja kutoka Sinai

hadi katika patakatifu pake.

18 Ulipopanda juu, uliteka mateka,

ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu,

hata kutoka kwa wale walioasi,

ili wewe, EeBwanaMungu, upate kuishi huko.

19 Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu,

ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.

20 Mungu wetu ni Mungu aokoaye,

BwanaMwenyezi hutuokoa na kifo.

21 Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake,

vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.

22 Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani;

nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,

23 ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako,

huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”

24 Ee Mungu, maandamano yako yameonekana,

maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu,

yakielekea patakatifu pake.

25 Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda,

pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.

26 Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa,

msifuniBwanakatika kusanyiko la Israeli.

27 Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza,

wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda,

hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.

28 Ee Mungu, amuru uwezo wako,

Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako,

kama ulivyofanya hapo awali.

29 Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu

wafalme watakuletea zawadi.

30 Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi,

kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa.

Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea.

Tawanya mataifa yapendayo vita.

31 Wajumbe watakuja kutoka Misri,

Kushiatajisalimisha kwa Mungu.

32 Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia,

mwimbieni Bwana sifa,

33 mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu,

yeye angurumaye kwa sauti kuu.

34 Tangazeni uwezo wa Mungu,

ambaye fahari yake iko juu ya Israeli,

ambaye uwezo wake uko katika anga.

35 Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako,

Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu.

Mungu Asifiwe!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/68-d8dfb1c4c99c05a6b89a1af668daac70.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 69

Kilio Cha Kuomba Msaada Wakati Wa Dhiki

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi.” Zaburi ya Daudi.

1 Ee Mungu, niokoe,

kwa maana maji yamenifika shingoni.

2 Ninazama kwenye vilindi vya matope,

pasipo mahali pa kukanyaga,

Nimefika kwenye maji makuu,

mafuriko yamenigharikisha.

3 Nimechoka kwa kuomba msaada,

koo langu limekauka.

Macho yangu yanafifia,

nikimtafuta Mungu wangu.

4 Wale wanaonichukia bila sababu

ni wengi kuliko nywele za kichwa changu;

wengi ni adui kwangu bila sababu,

wale wanaotafuta kuniangamiza.

Ninalazimishwa kurudisha

kitu ambacho sikuiba.

5 Ee Mungu, wewe unajua upumbavu wangu,

wala hatia yangu haikufichika kwako.

6 Ee Bwana, eweBwanaMwenye Nguvu Zote,

wakutumainio wasiaibishwe

kwa ajili yangu;

wakutafutao wasifedheheshwe kwa ajili yangu,

Ee Mungu wa Israeli.

7 Kwa maana nimestahimili dharau kwa ajili yako,

aibu imefunika uso wangu.

8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu,

mgeni kwa wana wa mama yangu mwenyewe.

9 Kwa kuwa wivu wa nyumba yako unanila,

matukano ya wale wanaokutukana yameniangukia.

10 Ninapolia na kufunga,

lazima nivumilie matusi.

11 Ninapovaa nguo ya gunia,

watu hunidharau.

12 Wale wanaoketi mlangoni wananisimanga,

nimekuwa wimbo wa walevi.

13 Lakini EeBwana, ninakuomba,

kwa wakati ukupendezao;

katika upendo wako mkuu, Ee Mungu,

unijibu kwa wokovu wako wa hakika.

14 Uniokoe katika matope,

usiniache nizame;

niokoe na hao wanichukiao,

kutoka kwenye vilindi vya maji.

15 Usiache mafuriko yanigharikishe

au vilindi vinimeze,

au shimo lifumbe kinywa chake juu yangu.

16 EeBwana, unijibu, kwa wema wa upendo wako;

kwa huruma zako nyingi unigeukie.

17 Usimfiche mtumishi wako uso wako,

uharakishe kunijibu, kwa sababu niko katika shida.

18 Njoo karibu uniokoe,

nikomboe kwa sababu ya adui zangu.

19 Unajua jinsi ninavyodharauliwa,

kufedheheshwa na kuaibishwa,

adui zangu wote unawajua.

20 Dharau zimenivunja moyo

na nimekata tamaa,

nimetafuta wa kunihurumia, lakini sikumpata,

wa kunituliza, lakini sikumpata.

21 Waliweka nyongo katika chakula changu

na walinipa siki nilipokuwa na kiu.

22 Meza iliyoandaliwa mbele yao na iwe mtego,

nayo iwe upatilizo na tanzi.

23 Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona,

nayo migongo yao iinamishwe daima.

24 Uwamwagie ghadhabu yako,

hasira yako kali na iwapate.

25 Mahali pao na pawe ukiwa,

wala asiwepo yeyote atakayeishi katika mahema yao.

26 Kwa kuwa wanawatesa wale uliowajeruhi,

na kuzungumza juu ya maumivu ya wale uliowaumiza.

27 Walipize uovu juu ya uovu,

usiwaache washiriki katika wokovu wako.

28 Wafutwe kutoka kitabu cha uzima

na wasiorodheshwe pamoja na wenye haki.

29 Mimi niko katika maumivu na dhiki;

Ee Mungu, wokovu wako na unihifadhi.

30 Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo,

nami nitamtukuza kwa kumtolea shukrani.

31 Hili litampendezaBwanakuliko ngʼombe dume,

zaidi ya fahali akiwa na pembe na kwato zake.

32 Maskini wataona na kufurahi:

ninyi mnaomtafuta Mungu, mioyo yenu na iishi!

33 Bwanahuwasikia wahitaji

wala hadharau watu wake waliotekwa.

34 Mbingu na dunia zimsifu,

bahari na vyote viendavyo ndani yake,

35 kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni

na kuijenga tena miji ya Yuda.

Kisha watu watafanya makao yao humo na kuimiliki,

36 watoto wa watumishi wake watairithi

na wale wote walipendao jina lake

wataishi humo.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/69-14c7d602a9ec7a028a4fa2d12acf7a7d.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 70

Kuomba Msaada

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Maombi.

1 Ee Mungu, ufanye haraka kuniokoa;

EeBwana, njoo hima unisaidie.

2 Wale wanaotafuta kuuondoa uhai wangu,

waaibishwe na kufadhaishwa;

wote wanaotamani kuangamizwa kwangu,

warudishwe nyuma kwa aibu.

3 Wale waniambiao, “Aha! Aha!”

warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao.

4 Lakini wote wakutafutao

washangilie na kukufurahia,

wale wapendao wokovu wako siku zote waseme,

“Mungu na atukuzwe!”

5 Lakini bado mimi ni maskini na mhitaji;

Ee Mungu, unijie haraka.

Wewe ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu;

EeBwana, usikawie.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/70-098f2b592afdfeb0c290fdafa03c8c88.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 71

Kuomba Ulinzi Na Msaada Siku Zote Za Maisha

1 EeBwana, nimekukimbilia wewe,

usiache nikaaibika kamwe.

2 Kwa haki yako uniponye na kuniokoa,

unitegee sikio lako uniokoe.

3 Uwe kwangu mwamba wa kimbilio,

mahali nitakapokimbilia kila wakati;

toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe

ni mwamba wangu na ngome yangu.

4 Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu,

kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.

5 Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, EeBwanaMwenyezi,

tegemeo langu tangu ujana wangu.

6 Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe,

ulinitoa tumboni mwa mama yangu.

Nitakusifu wewe daima.

7 Nimekuwa kama kioja kwa wengi,

lakini wewe ni kimbilio langu imara.

8 Kinywa changu kimejazwa sifa zako,

nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.

9 Usinitupe wakati wa uzee,

wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.

10 Kwa maana adui zangu wananisengenya,

wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.

11 Wanasema, “Mungu amemwacha,

mkimbilieni mkamkamate,

kwani hakuna wa kumwokoa.”

12 Ee Mungu, usiwe mbali nami,

njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.

13 Washtaki wangu na waangamie kwa aibu,

wale wanaotaka kunidhuru

na wafunikwe kwa dharau na fedheha.

14 Lakini mimi, nitatumaini siku zote,

nitakusifu zaidi na zaidi.

15 Kinywa changu kitasimulia haki yako,

wokovu wako mchana kutwa,

ingawa sifahamu kipimo chake.

16 EeBwanaMwenyezi, nitakuja

na kutangaza matendo yako makuu,

nitatangaza haki yako, yako peke yako.

17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu,

hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.

18 Ee Mungu, usiniache,

hata niwapo mzee wa mvi,

mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho,

nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.

19 Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu,

wewe ambaye umefanya mambo makuu.

Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?

20 Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu,

utanihuisha tena,

kutoka vilindi vya dunia

utaniinua tena.

21 Utaongeza heshima yangu

na kunifariji tena.

22 Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi

kwa ajili ya uaminifu wako;

Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli,

nitakuimbia sifa kwa zeze.

23 Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha

ninapokuimbia sifa,

mimi, ambaye umenikomboa.

24 Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki

mchana kutwa,

kwa maana wale waliotaka kunidhuru,

wameaibishwa na kufadhaishwa.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/71-149ba03c6f364dd403de2bd6907a5c88.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 72

Maombi Kwa Ajili Ya Mfalme

Zaburi ya Solomoni.

1 Ee Mungu, mjalie mfalme aamue kwa haki yako,

mwana wa mfalme kwa haki yako.

2 Atawaamua watu wako kwa haki,

watu wako walioonewa kwa haki.

3 Milima italeta mafanikio kwa watu,

vilima tunda la haki.

4 Atawatetea walioonewa miongoni mwa watu

na atawaokoa watoto wa wahitaji,

ataponda mdhalimu.

5 Atadumu kama jua lidumuvyo, kama mwezi, vizazi vyote.

6 Atakuwa kama mvua inyeshayo juu ya shamba lililofyekwa,

kama manyunyu yanyeshayo ardhi.

7 Katika siku zake wenye haki watastawi;

mafanikio yatakuwepo mpaka mwezi utakapokoma.

8 Atatawala kutoka bahari hadi bahari

na kutoka Mtompaka miisho ya dunia.

9 Makabila ya jangwani watamsujudia,

na adui zake wataramba mavumbi.

10 Wafalme wa Tarshishi na wa pwani za mbali

watamletea kodi;

wafalme wa Sheba na Seba

watampa zawadi.

11 Wafalme wote watamsujudia

na mataifa yote yatamtumikia.

12 Kwa maana atamwokoa mhitaji anayemlilia,

aliyeonewa asiye na wa kumsaidia.

13 Atawahurumia wanyonge na wahitaji

na kuwaokoa wahitaji kutoka mauti.

14 Atawaokoa kutoka uonevu na ukatili,

kwani damu yao ni ya thamani machoni pake.

15 Aishi maisha marefu!

Na apewe dhahabu ya Sheba.

Watu wamwombee daima

na kumbariki mchana kutwa.

16 Nafaka ijae tele katika nchi yote,

juu ya vilele vya vilima na istawi.

Tunda lake na listawi kama Lebanoni,

listawi kama majani ya kondeni.

17 Jina lake na lidumu milele,

na lidumu kama jua.

Mataifa yote yatabarikiwa kupitia kwake,

nao watamwita aliyebarikiwa.

18 BwanaMungu, Mungu wa Israeli, apewe sifa,

yeye ambaye peke yake hutenda mambo ya ajabu.

19 Jina lake tukufu lisifiwe milele,

ulimwengu wote ujae utukufu wake.

Amen na Amen.

20 Huu ndio mwisho wa maombi ya Daudi mwana wa Yese.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/72-abe08fca07014b184f67512ba27e742f.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 73

Haki Ya Mungu

Zaburi ya Asafu.

1 Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli,

kwa wale ambao mioyo yao ni safi.

2 Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza;

nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.

3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna

nilipoona kufanikiwa kwa waovu.

4 Wao hawana taabu,

miili yao ina afya na nguvu.

5 Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine,

wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.

6 Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao,

wamejivika jeuri.

7 Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi,

majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.

8 Hudhihaki na kusema kwa ukorofi,

katika majivuno yao wanatishia kutesa.

9 Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu,

nazo ndimi zao humiliki duniani.

10 Kwa hiyo watu wao huwageukia

na kunywa maji tele.

11 Wanasema, “Mungu awezaje kujua?

Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”

12 Hivi ndivyo walivyo waovu:

siku zote hawajali,

wanaongezeka katika utajiri.

13 Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure,

ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.

14 Mchana kutwa nimetaabika,

nimeadhibiwa kila asubuhi.

15 Kama ningesema, “Nitasema hivi,”

ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.

16 Nilipojaribu kuelewa haya yote,

yalikuwa magumu kwangu kuelewa.

17 Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu,

ndipo nilipotambua mwisho wao.

18 Hakika unawaweka mahali pa utelezi,

unawaangusha chini kwa uharibifu.

19 Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula,

wanatoweshwa kabisa na vitisho!

20 Kama ndoto mtu aamkapo,

hivyo wakati uinukapo, EeBwana,

utawatowesha kama ndoto.

21 Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa,

na roho yangu ilipotiwa uchungu,

22 nilikuwa mpumbavu na mjinga,

nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.

23 Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote,

umenishika mkono wangu wa kuume.

24 Unaniongoza kwa shauri lako,

hatimaye utaniingiza katika utukufu.

25 Nani niliye naye mbinguni ila wewe?

Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.

26 Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa,

bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu

na fungu langu milele.

27 Wale walio mbali nawe wataangamia,

unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.

28 Lakini kwangu mimi,

ni vyema kuwa karibu na Mungu.

NimemfanyaBwanaMwenyezi kimbilio langu;

nami nitayasimulia matendo yako yote.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/73-ab948d2191334554d6a119482f5bea6c.mp3?version_id=1627—