Categories
Zaburi

Zaburi 34

Sifa Na Wema Wa Mungu

Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka.

1 NitamtukuzaBwananyakati zote,

sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.

2 Nafsi yangu itajisifu katikaBwana,

walioonewa watasikia na wafurahi.

3 MtukuzeniBwanapamoja nami,

naam, na tulitukuze jina lake pamoja.

4 NilimtafutaBwananaye akanijibu,

akaniokoa kwenye hofu zangu zote.

5 Wale wamtazamao hutiwa nuru,

nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.

6 Maskini huyu alimwitaBwana, naye akamsikia,

akamwokoa katika taabu zake zote.

7 Malaika waBwanahufanya kituo

akiwazunguka wale wamchao,

naye huwaokoa.

8 Onjeni mwone kwambaBwanani mwema,

heri mtu yule anayemkimbilia.

9 McheniBwanaenyi watakatifu wake,

kwa maana wale wamchao

hawapungukiwi na chochote.

10 Wana simba wenye nguvu

hutindikiwa na kuona njaa,

bali wale wamtafutaoBwana

hawatakosa kitu chochote kilicho chema.

11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize,

nitawafundisha kumchaBwana.

12 Yeyote kati yenu anayependa uzima

na kutamani kuziona siku nyingi njema,

13 basi auzuie ulimi wake na mabaya,

na midomo yake kutokana na kusema uongo.

14 Aache uovu, atende mema,

aitafute amani na kuifuatilia.

15 Macho yaBwanahuwaelekea wenye haki,

na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.

16 Uso waBwanauko kinyume na watendao maovu,

ili kufuta kumbukumbu lao duniani.

17 Wenye haki hulia, nayeBwanahuwasikia,

huwaokoa katika taabu zao zote.

18 Bwanayu karibu na waliovunjika moyo,

na huwaokoa waliopondeka roho.

19 Mwenye haki ana mateso mengi,

lakiniBwanahumwokoa nayo yote,

20 huhifadhi mifupa yake yote,

hata mmoja hautavunjika.

21 Ubaya utamuua mtu mwovu,

nao adui za mwenye haki watahukumiwa.

22 Bwanahuwakomboa watumishi wake,

yeyote anayemkimbilia yeye

hatahukumiwa kamwe.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/34-ccb420443dc43577cc3db3894086b01d.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 35

Kuomba Msaada: Kuokolewa Kutokana Na Maadui

Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, pingana na wale wanaopingana nami,

upigane na hao wanaopigana nami.

2 Chukua ngao na kigao.

Inuka unisaidie.

3 Inua mkuki wako na fumolako

dhidi ya hao wanaonifuatia.

Iambie nafsi yangu,

“Mimi ni wokovu wako.”

4 Wafedheheshwe na waaibishwe

wale wanaotafuta uhai wangu.

Wanaofanya shauri kuniangamiza

warudishwe nyuma kwa hofu.

5 Wawe kama makapi yapeperushwayo na upepo,

malaika waBwanaakiwafukuza.

6 Njia yao na iwe giza na ya utelezi,

malaika waBwanaakiwafuatilia.

7 Kwa vile walinifichia wavu wao bila sababu,

na bila sababu wamenichimbia shimo,

8 maafa na yawapate ghafula:

wavu walionifichia na uwatege wenyewe,

na waanguke katika shimo hilo,

kwa maangamizo yao.

9 Ndipo nafsi yangu itashangilia katikaBwana

na kuufurahia wokovu wake.

10 Nitapaza sauti yangu nikisema,

“Ni nani aliye kama wewe, EeBwana?

Wewe huwaokoa maskini kutokana na wale walio na nguvu kuliko wao,

maskini na mhitaji kutokana na wanaowanyangʼanya!”

11 Mashahidi wakatili wanainuka,

wananiuliza mambo nisiyoyajua.

12 Wananilipa baya kwa jema

na kuiacha nafsi yangu ukiwa.

13 Lakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo ya gunia

na nikajinyenyekesha kwa kufunga.

Maombi yangu yaliponirudia bila kujibiwa,

14 niliendelea kuomboleza

kama vile wao ni rafiki au ndugu.

Niliinamisha kichwa chini kwa huzuni

kama ninayemwombolezea mama yangu.

15 Lakini nilipojikwaa,

walikusanyika kwa shangwe;

washambuliaji walijikusanya dhidi yangu

bila mimi kujua.

Walinisingizia pasipo kukoma.

16 Kama watu wasiomcha Mungu, wamenidhihaki,

wamenisagia meno.

17 EeBwana, utatazama mpaka lini?

Niokoe maisha yangu na maangamizi yao,

uhai wangu wa thamani

kutokana na simba hawa.

18 Nami nitakushukuru mbele ya kusanyiko kubwa,

nitakusifu katikati ya watu wengi.

19 Usiwaache wale wanaonisimanga,

wale ambao ni adui zangu bila sababu;

usiwaache wale ambao ni adui zangu bila sababu

wakonyeze jicho kwa hila.

20 Hawazungumzi kwa amani,

bali wanatunga mashtaka ya uongo

dhidi ya wale wanaoishi

kwa utulivu katika nchi.

21 Hunifumbulia vinywa vyao wakisema, “Aha! Aha!

Kwa macho yetu wenyewe tumeliona.”

22 EeBwana, umeona hili, usiwe kimya.

Usiwe mbali nami, EeBwana.

23 Amka, inuka unitetee!

Unipiganie Mungu wangu na Bwana wangu.

24 Nihukumu kwa haki yako, EeBwanaMungu wangu,

sawasawa na haki yako;

usiwaache wakusimange.

25 Usiwaache wafikiri, “Aha, hili ndilo tulilotaka!”

Au waseme, “Tumemmeza.”

26 Wote wanaofurahia dhiki yangu

waaibishwe na wachanganyikiwe;

hao wanaojiinua dhidi yangu

wavikwe aibu na dharau.

27 Wale wanaofurahia hukumu yangu ya haki

wapige kelele za shangwe na furaha;

hebu waseme siku zote, “Bwanaatukuzwe,

ambaye amefurahia mafanikio ya mtumishi wake.”

28 Ulimi wangu utanena haki yako

na sifa zako mchana kutwa.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/35-55cb7add9158b71d13574b9940749697.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 36

Uovu Wa Mwanadamu

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa

Bwana

.

1 Kuna neno moyoni mwangu

kuhusu hali ya dhambi ya mwovu.

Hakuna hofu ya Mungu

mbele ya macho yake.

2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno

hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.

3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu,

ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.

4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya,

hujitia katika njia ya dhambi

na hakatai lililo baya.

5 Upendo wako, EeBwana, unafika hadi mbinguni,

uaminifu wako hadi kwenye anga.

6 Haki yako ni kama milima mikubwa,

hukumu zako ni kama kilindi kikuu.

EeBwana, wewe huwahifadhi

mwanadamu na mnyama.

7 Upendo wako usiokoma

ni wa thamani mno!

Watu wakuu na wadogo

hujificha uvulini wa mbawa zako.

8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako,

nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.

9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima,

katika nuru yako twaona nuru.

10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe,

haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.

11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu,

wala mkono wa mwovu usinifukuze.

12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka:

wametupwa chini, hawawezi kuinuka!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/36-1a88171c243532a801b4f48713566e12.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 37

Mwisho Wa Mwovu Na Urithi Wa Mwenye Haki

Zaburi ya Daudi.

1 Usisumbuke kwa ajili ya watendao maovu,

wala usiwaonee wivu watendao mabaya,

2 kwa maana kama majani watanyauka mara,

kama mimea ya kijani watakufa mara.

3 MtumainiBwanana utende yaliyo mema;

Kaa katika nchi ukafurahie malisho salama.

4 Jifurahishe katikaBwana

naye atakupa haja za moyo wako.

5 MkabidhiBwananjia yako,

mtumaini yeye, naye atatenda hili:

6 Yeye atafanya haki yako ingʼae kama mapambazuko,

na hukumu ya shauri lako kama jua la adhuhuri.

7 Tulia mbele zaBwana

na umngojee kwa uvumilivu;

usisumbuke watu wanapofanikiwa katika njia zao,

wanapotekeleza mipango yao miovu.

8 Epuka hasira na uache ghadhabu,

usihangaike: itakuongoza tu kutenda uovu.

9 Kwa maana waovu watakatiliwa mbali,

bali wale wanaomtumainiBwanawatairithi nchi.

10 Bado kitambo kidogo, nao waovu hawataonekana,

ingawa utawatafuta, hawataonekana.

11 Bali wanyenyekevu watairithi nchi

na wafurahie amani tele.

12 Waovu hula njama dhidi ya wenye haki

na kuwasagia meno,

13 bali Bwana huwacheka waovu,

kwa sababu anajua siku yao inakuja.

14 Waovu huchomoa upanga

na kupinda upinde,

ili wawaangushe maskini na wahitaji,

kuwachinja wale ambao njia zao ni nyofu.

15 Lakini panga zao zitachoma mioyo yao wenyewe,

na pinde zao zitavunjwa.

16 Bora kidogo walicho nacho wenye haki

kuliko wingi wa mali wa waovu wengi;

17 kwa maana nguvu za waovu zitavunjwa,

lakiniBwanahumtegemeza mwenye haki.

18 Bwanaanazifahamu siku za wanyofu,

na urithi wao utadumu milele.

19 Siku za maafa hawatanyauka,

siku za njaa watafurahia wingi wa vitu.

20 Lakini waovu wataangamia:

Adui zaBwanawatakuwa

kama uzuri wa mashamba,

watatoweka,

watatoweka kama moshi.

21 Waovu hukopa na hawalipi,

bali wenye haki hutoa kwa ukarimu.

22 Wale wanaobarikiwa naBwanawatairithi nchi,

bali wale anaowalaani watakatiliwa mbali.

23 KamaBwanaakipendezwa na njia ya mtu,

yeye huimarisha hatua zake,

24 ajapojikwaa, hataanguka,

kwa maanaBwana

humtegemeza kwa mkono wake.

25 Nilikuwa kijana na sasa ni mzee,

lakini sijaona kamwe wenye haki wameachwa

au watoto wao wakiombaomba chakula.

26 Wakati wote ni wakarimu na hukopesha bila masharti.

Watoto wao watabarikiwa.

27 Acha ubaya na utende wema,

nawe utaishi katika nchi milele.

28 Kwa kuwaBwanahuwapenda wenye haki

naye hatawaacha waaminifu wake.

Watalindwa milele,

lakini uzao wa waovu utakatiliwa mbali.

29 Wenye haki watairithi nchi,

na kuishi humo milele.

30 Kinywa cha mwenye haki hutamka hekima,

nao ulimi wake huzungumza lililo haki.

31 Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake;

nyayo zake hazitelezi.

32 Watu waovu huvizia wenye haki,

wakitafuta kuwaua;

33 lakiniBwanahatawaacha mikononi mwao

wala hatawaacha wahukumiwe

kuwa wakosa wanaposhtakiwa.

34 MngojeeBwana,

na uishike njia yake.

Naye atakutukuza uirithi nchi,

waovu watakapokatiliwa mbali,

utaliona hilo.

35 Nimemwona mtu mwovu na mkatili akistawi

kama mwerezi wa Lebanoni,

36 lakini alitoweka mara na hakuonekana,

ingawa nilimtafuta, hakupatikana.

37 Watafakari watu wasio na hatia,

wachunguze watu wakamilifu,

kuna mafanikio kwa mtu apendaye amani.

38 Lakini watenda dhambi wote wataangamizwa,

mafanikio yao yatakatiliwa mbali.

39 Wokovu wa wenye haki hutoka kwaBwana,

yeye ni ngome yao wakati wa shida.

40 Bwanahuwasaidia na kuwaokoa,

huwaokoa kutoka kwa waovu na kuwahifadhi,

kwa maana wanamkimbilia.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/37-e0d9208b6fe305ab72a7084c51613c73.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 38

Maombi Ya Mtu Anayeteseka

Zaburi ya Daudi. Maombi.

1 EeBwana, usinikemee katika hasira yako,

wala kuniadhibu katika ghadhabu yako.

2 Kwa kuwa mishale yako imenichoma,

na mkono wako umenishukia.

3 Hakuna afya mwilini mwangu

kwa sababu ya ghadhabu yako,

mifupa yangu haina uzima

kwa sababu ya dhambi zangu.

4 Maovu yangu yamenifunika

kama mzigo usiochukulika.

5 Majeraha yangu yameoza na yananuka,

kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.

6 Nimeinamishwa chini na kushushwa sana,

mchana kutwa nazunguka nikiomboleza.

7 Viuno vyangu vimejaa maumivu yaunguzayo,

hakuna afya mwilini mwangu.

8 Nimedhoofika na kupondwa kabisa,

nasononeka kwa maumivu makuu ya moyoni.

9 EeBwana, yote ninayoyaonea shauku

yako wazi mbele zako,

kutamani kwangu sana

hakufichiki mbele zako.

10 Moyo wangu unapigapiga,

nguvu zangu zimeniishia;

hata macho yangu yametiwa giza.

11 Rafiki na wenzangu wananikwepa

kwa sababu ya majeraha yangu;

majirani zangu wanakaa mbali nami.

12 Wale wanaotafuta uhai wangu

wanatega mitego yao,

wale ambao wangetaka kunidhuru

huongea juu ya maangamizi yangu;

hufanya shauri la hila mchana kutwa.

13 Mimi ni kama mtu kiziwi, asiyeweza kusikia,

ni kama bubu, asiyeweza kufungua kinywa chake,

14 nimekuwa kama mtu asiyesikia,

ambaye kinywa chake hakiwezi kutoa jibu.

15 EeBwana, ninakungojea wewe,

Ee Bwana Mungu wangu, utajibu.

16 Kwa kuwa nilisema, “Usiwaache wafurahie,

wala wasijitukuze juu yangu

mguu wangu unapoteleza.”

17 Kwa maana ninakaribia kuanguka,

na maumivu yangu yananiandama siku zote.

18 Naungama uovu wangu,

ninataabishwa na dhambi yangu.

19 Wengi ni wale ambao ni adui zangu hodari,

wale wanaonichukia bila sababu ni wengi.

20 Wanaolipa maovu kwa wema wangu

hunisingizia ninapofuata lililo jema.

21 EeBwana, usiniache,

usiwe mbali nami, Ee Mungu wangu.

22 Ee Bwana Mwokozi wangu,

uje upesi kunisaidia.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/38-a4e5602d287546c89aef7971609df7bf.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 39

Maombi Ya Mtu Anayeteseka

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa Yeduthuni. Zaburi ya Daudi.

1 Nilisema, “Nitaziangalia njia zangu

na kuuzuia ulimi wangu usije ukatenda dhambi;

nitaweka lijamu kinywani mwangu

wakati wote waovu wanapokuwa karibu nami.”

2 Lakini niliponyamaza kimya na kutulia,

hata pasipo kusema lolote jema,

uchungu wangu uliongezeka.

3 Moyo wangu ulipata moto ndani yangu,

nilipotafakari, moto uliwaka,

ndipo nikasema kwa ulimi wangu:

4 “EeBwana, nijulishe mwisho wa maisha yangu

na hesabu ya siku zangu;

nijalie kujua jinsi maisha yangu

yanavyopita upesi.

5 Umefanya maisha yangu mafupi kama pumzi;

muda wangu wa kuishi ni kama

hauna thamani kwako.

Maisha ya kila mwanadamu

ni kama pumzi.

6 Hakika kila binadamu ni kama njozi

aendapo huku na huko:

hujishughulisha na mengi lakini ni ubatili;

anakusanya mali nyingi,

wala hajui ni nani atakayeifaidi.

7 “Lakini sasa Bwana, nitafute nini?

Tumaini langu ni kwako.

8 Niokoe kutoka kwenye makosa yangu yote,

usinifanye kuwa dhihaka ya wapumbavu.

9 Nilinyamaza kimya,

sikufumbua kinywa changu,

kwa sababu wewe ndiwe uliyetenda hili.

10 Niondolee mjeledi wako,

nimeshindwa kwa mapigo ya mkono wako.

11 Unakemea na kuadhibu wanadamu

kwa ajili ya dhambi zao;

unaharibu utajiri wao kama nondo aharibuvyo:

kila mwanadamu ni kama pumzi tu.

12 “EeBwana, usikie maombi yangu,

usikie kilio changu unisaidie,

usiwe kiziwi kwa kulia kwangu.

Kwani mimi ninaishi na wewe kama mgeni,

kama walivyokuwa baba zangu wote,

13 Tazama mbali nami, ili niweze kufurahi tena

kabla sijaondoka na nisiwepo tena.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/39-cf5301ce3fac771eada1f8c6a16dcd0c.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 40

Wimbo Wa Sifa

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 NilimngojaBwanakwa saburi,

naye akaniinamia, akasikia kilio changu.

2 Akanipandisha kutoka shimo la uharibifu,

kutoka matope na utelezi;

akaiweka miguu yangu juu ya mwamba

na kunipa mahali imara pa kusimama.

3 Akaweka wimbo mpya kinywani mwangu,

wimbo wa sifa kwa Mungu wetu.

Wengi wataona na kuogopa

na kuweka tumaini lao kwaBwana.

4 Heri mtu yule amfanyayeBwanakuwa tumaini lake,

asiyewategemea wenye kiburi,

wale wenye kugeukia miungu ya uongo.

5 EeBwanaMungu wangu,

umefanya mambo mengi ya ajabu.

Mambo uliyopanga kwa ajili yetu

hakuna awezaye kukuhesabia;

kama ningesema na kuyaelezea,

yangekuwa mengi mno kuyaelezea.

6 Dhabihu na sadaka hukuvitaka,

lakini umefungua masikio yangu;

sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi

hukuzihitaji.

7 Ndipo niliposema, “Mimi hapa, nimekuja:

imeandikwa kunihusu katika kitabu.

8 Ee Mungu wangu,

natamani kuyafanya mapenzi yako;

sheria yako iko ndani ya moyo wangu.”

9 Nimehubiri haki katika kusanyiko kubwa,

sikufunga mdomo wangu,

EeBwana, kama ujuavyo.

10 Sikuficha haki yako moyoni mwangu;

ninasema juu ya uaminifu wako na wokovu wako.

Sikuficha upendo wako na kweli yako

mbele ya kusanyiko kubwa.

11 EeBwana, usizuilie huruma zako,

upendo wako na kweli yako daima vinilinde.

12 Kwa maana taabu zisizo na hesabu zimenizunguka,

dhambi zangu zimenikamata, hata nisiweze kuona.

Zimekuwa nyingi kuliko nywele za kichwa changu,

nao moyo unazimia ndani yangu.

13 EeBwana, uwe radhi kuniokoa;

EeBwana, njoo hima unisaidie.

14 Wote wanaotafuta kuuondoa uhai wangu,

waaibishwe na kufadhaishwa;

wote wanaotamani kuangamizwa kwangu,

warudishwe nyuma kwa aibu.

15 Wale waniambiao, “Aha! Aha!”

wafadhaishwe na iwe aibu yao.

16 Lakini wote wakutafutao

washangilie na kukufurahia,

wale wapendao wokovu wako siku zote waseme,

“Bwanaatukuzwe!”

17 Lakini bado mimi ni maskini na mhitaji;

Bwana na anifikirie.

Wewe ndiwe msaada wangu na Mwokozi wangu;

Ee Mungu wangu, usikawie.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/40-6e5c826ea55f00171622d693cfba7ef5.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 41

Maombi Ya Mtu Mgonjwa

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 Heri mtu yule anayemjali mnyonge,

Bwanaatamwokoa wakati wa shida.

2 Bwanaatamlinda na kuyahifadhi maisha yake,

atambariki katika nchi

na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.

3 Bwanaatamtegemeza awapo mgonjwa kitandani,

atamwinua kutoka kitandani mwake.

4 Nilisema, “EeBwananihurumie,

niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”

5 Adui zangu wanasema kwa hila,

“Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”

6 Kila anapokuja mtu kunitazama,

huzungumza uongo,

huku moyo wake hukusanya masingizio;

kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.

7 Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu,

hao huniwazia mabaya sana, wakisema,

8 “Ugonjwa mbaya sana umempata,

kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”

9 Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini,

yule aliyekula chakula changu

ameniinulia kisigino chake.

10 Lakini wewe, EeBwana, nihurumie,

ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.

11 Najua kwamba wapendezwa nami,

kwa kuwa adui yangu hanishindi.

12 Katika uadilifu wangu unanitegemeza

na kuniweka kwenye uwepo wako milele.

13 MsifuniBwana, Mungu wa Israeli,

tangu milele na hata milele.

Amen na Amen.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/41-e49091db6bebff4e9f22e709b3efe730.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 42

Maombi Ya Mtu Aliye Uhamishoni

Kwa mwimbishaji. Utenzi wa wana wa Kora.

1 Kama vile ayala aoneavyo shauku vijito vya maji,

ndivyo nafsi yangu ikuoneavyo shauku, Ee Mungu.

2 Nafsi yangu inamwonea Mungu kiu, Mungu aliye hai.

Ni lini nitaweza kwenda kukutana na Mungu?

3 Machozi yangu yamekuwa chakula changu

usiku na mchana,

huku watu wakiniambia mchana kutwa,

“Yuko wapi Mungu wako?”

4 Mambo haya nayakumbuka

ninapoimimina nafsi yangu:

Jinsi nilivyokuwa nikienda na umati wa watu,

nikiongoza maandamano kuelekea kwenye nyumba ya Mungu,

kwa kelele za shangwe na za shukrani

katikati ya umati uliosherehekea.

5 Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka?

Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?

Weka tumaini lako kwa Mungu,

kwa sababu bado nitamsifu,

Mwokozi wangu na

6 Mungu wangu.

Nafsi yangu inasononeka ndani yangu;

kwa hiyo nitakukumbuka

kutoka nchi ya Yordani,

katika vilele vya Hermoni,

kutoka Mlima Mizari.

7 Kilindi huita kilindi,

katika ngurumo za maporomoko ya maji yako;

mawimbi yako yote pamoja na viwimbi

vimepita juu yangu.

8 MchanaBwanahuelekeza upendo wake,

usiku wimbo wake uko nami:

maombi kwa Mungu wa uzima wangu.

9 Ninamwambia Mungu Mwamba wangu,

“Kwa nini umenisahau?

Kwa nini niendelee kuomboleza,

nikiwa nimeonewa na adui?”

10 Mifupa yangu inateseka kwa maumivu makali

adui zangu wanaponidhihaki,

wakiniambia mchana kutwa,

“Yuko wapi Mungu wako?”

11 Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka?

Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?

Weka tumaini lako kwa Mungu,

kwa sababu bado nitamsifu,

Mwokozi wangu na Mungu wangu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/42-b22cac1a8003a7912ce1f01e13fe83ca.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 43

Maombi Ya Mtu Aliyeko Uhamishoni Yanaendelea

1 Ee Mungu unihukumu,

nitetee dhidi ya taifa lisilomcha Mungu,

niokoe na watu wadanganyifu na waovu.

2 Wewe ni Mungu ngome yangu.

Kwa nini umenikataa?

Kwa nini niendelee kuomboleza,

nikiwa nimeonewa na adui?

3 Tuma hima nuru yako na kweli yako

na viniongoze;

vinilete mpaka mlima wako mtakatifu,

mpaka mahali unapoishi.

4 Ndipo nitakwenda madhabahuni pa Mungu,

kwa Mungu, furaha yangu na shangwe yangu.

Nitakusifu kwa kinubi,

Ee Mungu, Mungu wangu.

5 Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka?

Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?

Weka tumaini lako kwa Mungu,

kwa sababu bado nitamsifu

Mwokozi wangu na Mungu wangu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/43-73dc30c516be7542f8dd7374742d54b2.mp3?version_id=1627—