Categories
Zaburi

Zaburi 24

Mfalme Mkuu

Zaburi ya Daudi.

1 Dunia ni mali yaBwana, na vyote vilivyomo ndani yake,

ulimwengu, na wote waishio ndani yake,

2 maana aliiwekea misingi yake baharini

na kuifanya imara juu ya maji.

3 Nani awezaye kuupanda mlima waBwana?

Ni nani awezaye kusimama patakatifu pake?

4 Ni yule mwenye mikono safi na moyo mweupe,

yule ambaye hakuinulia sanamu nafsi yake

au kuapa kwa kitu cha uongo.

5 Huyo atapokea baraka kutoka kwaBwana,

na hukumu ya haki kutoka kwa Mungu Mwokozi wake.

6 Hiki ndicho kizazi cha wale wamtafutao,

wale wautafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.

7 Inueni vichwa vyenu, enyi malango,

inukeni enyi milango ya kale,

ili mfalme wa utukufu apate kuingia.

8 Ni nani huyu Mfalme wa utukufu?

NiBwanaaliye na nguvu na uweza,

niBwanaaliye hodari katika vita.

9 Inueni vichwa vyenu, enyi malango,

viinueni juu enyi milango ya kale,

ili Mfalme wa utukufu apate kuingia.

10 Ni nani yeye, huyu Mfalme wa utukufu?

NiBwanaMwenye Nguvu Zote;

yeye ndiye Mfalme wa utukufu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/24-91c40c17d34778b02a40e9bd38202f5a.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 25

Kumwomba Mungu Uongozi Na Ulinzi

Zaburi ya Daudi.

1 Kwako wewe, EeBwana,

nainua nafsi yangu,

2 ni wewe ninayekutumainia,

Ee Mungu wangu.

Usiniache niaibike,

wala usiache adui zangu wakanishinda.

3 Kamwe hakuna hata mmoja anayekutegemea

atakayeaibishwa,

bali wataaibishwa

wafanyao hila bila sababu.

4 Nionyeshe njia zako, EeBwana,

nifundishe mapito yako,

5 niongoze katika kweli yako na kunifundisha,

kwa maana wewe ni Mungu Mwokozi wangu,

nalo tumaini langu liko kwako wakati wote.

6 Kumbuka, EeBwana, rehema zako kuu na upendo,

kwa maana zimekuwepo tangu zamani.

7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu

wala njia zangu za uasi,

sawasawa na upendo wako unikumbuke,

kwa maana wewe ni mwema, EeBwana.

8 Bwanani mwema na mwenye adili,

kwa hiyo huwafundisha wenye dhambi njia zake.

9 Huwaongoza wanyenyekevu katika haki,

naye huwafundisha njia yake.

10 Njia zote zaBwanani za upendo na uaminifu

kwa wale wanaoshika shuhuda za agano lake.

11 EeBwana, kwa ajili ya jina lako,

unisamehe uovu wangu, ijapokuwa ni mwingi.

12 Ni nani basi, mtu yule anayemchaBwana?

Atamfundisha katika njia

atakayoichagua kwa ajili yake.

13 Mtu huyo atafanikiwa maishani mwake,

nao wazao wake watairithi nchi.

14 Siri yaBwanaiko kwa wale wamchao,

yeye huwajulisha agano lake.

15 Macho yangu humwelekeaBwanadaima,

kwa kuwa yeye peke yake ndiye ataitoa

miguu yangu kutoka mtego.

16 Nigeukie na unihurumie,

kwa maana mimi ni mpweke na mwenye kuteseka.

17 Shida za moyo wangu zimeongezeka,

niokoe katika dhiki yangu.

18 Uangalie mateso na shida zangu

na uniondolee dhambi zangu zote.

19 Tazama adui zangu walivyo wengi,

pia uone jinsi wanavyonichukia vikali!

20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe,

usiniache niaibike,

kwa maana nimekukimbilia wewe.

21 Uadilifu na uaminifu vinilinde,

kwa sababu tumaini langu ni kwako.

22 Ee Mungu, wakomboe Israeli,

katika shida zao zote!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/25-d574a817dbd54a3e276411792368f1c6.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 26

Maombi Ya Mtu Mwema

Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, nithibitishe katika haki,

maana nimeishi maisha yasiyo na lawama;

nimemtumainiaBwana

bila kusitasita.

2 EeBwana, unijaribu, unipime,

uuchunguze moyo wangu

na mawazo yangu;

3 kwa maana upendo wako

uko mbele yangu daima,

nami natembea siku zote

katika kweli yako.

4 Siketi pamoja na watu wadanganyifu,

wala siandamani na wanafiki,

5 ninachukia kusanyiko la watenda mabaya

na ninakataa kuketi pamoja na waovu.

6 Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia,

naikaribia madhabahu yako, EeBwana,

7 nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa,

huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.

8 EeBwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi,

mahali ambapo utukufu wako hukaa.

9 Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi,

wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,

10 ambao mikononi mwao kuna mipango miovu,

ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.

11 Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama;

nikomboe na unihurumie.

12 Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare;

katika kusanyiko kuu nitamsifuBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/26-7419f63c65255b42ade02f98cd34b3ef.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 27

Sala Ya Kusifu

Zaburi ya Daudi.

1 Bwanani nuru yangu na wokovu wangu,

nimwogope nani?

Bwanani ngome ya uzima wangu,

nimhofu nani?

2 Waovu watakaposogea dhidi yangu

ili wanile nyama yangu,

adui zangu na watesi wangu watakaponishambulia,

watajikwaa na kuanguka.

3 Hata jeshi linizunguke pande zote,

moyo wangu hautaogopa;

hata vita vitokee dhidi yangu,

hata hapo nitakuwa na ujasiri.

4 Jambo moja ninamwombaBwana,

hili ndilo ninalolitafuta:

niweze kukaa nyumbani mwaBwana

siku zote za maisha yangu,

niutazame uzuri waBwana

na kumtafuta hekaluni mwake.

5 Kwa kuwa siku ya shida,

atanihifadhi salama katika maskani yake,

atanificha uvulini mwa hema yake

na kuniweka juu kwenye mwamba.

6 Kisha kichwa changu kitainuliwa

juu ya adui zangu wanaonizunguka.

Katika maskani yake nitatoa dhabihu kwa kelele za shangwe;

nitamwimbiaBwanana kumsifu.

7 Isikie sauti yangu nikuitapo, EeBwana,

unihurumie na unijibu.

8 Moyo wangu unasema kuhusu wewe,

“Utafute uso wake!”

Uso wako,Bwana“Nitautafuta.”

9 Usinifiche uso wako,

usimkatae mtumishi wako kwa hasira;

wewe umekuwa msaada wangu.

Usinikatae wala usiniache,

Ee Mungu Mwokozi wangu.

10 Hata kama baba yangu na mama wakiniacha,

Bwanaatanipokea.

11 Nifundishe njia yako, EeBwana,

niongoze katika njia iliyonyooka

kwa sababu ya watesi wangu.

12 Usiniachilie kwa nia za adui zangu,

kwa maana mashahidi wa uongo

wameinuka dhidi yangu,

wakipumua ujeuri.

13 Nami bado nina tumaini hili:

nitauona wema waBwana

katika nchi ya walio hai.

14 MngojeeBwana,

uwe hodari na mwenye moyo mkuu,

nawe, umngojeeBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/27-9152c2d2d9cc93af54e1c71054b93235.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 28

Kuomba Msaada

Zaburi ya Daudi.

1 Ninakuita wewe, EeBwana, Mwamba wangu;

usiwe kwangu kama kiziwi.

Kwa sababu ukinyamaza

nitafanana na walioshuka shimoni.

2 Sikia kilio changu unihurumie

ninapokuita kwa ajili ya msaada,

niinuapo mikono yangu kuelekea

Patakatifu pa Patakatifu pako.

3 Usiniburute pamoja na waovu,

pamoja na hao watendao mabaya,

ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri,

lakini mioyoni mwao wameficha chuki.

4 Walipe sawasawa na matendo yao,

sawasawa na matendo yao maovu;

walipe sawasawa na kazi za mikono yao,

uwalipe wanavyostahili.

5 Kwa kuwa hawaheshimu kazi zaBwana,

na yale ambayo mikono yake imetenda,

atawabomoa na kamwe

hatawajenga tena.

6 Bwanaasifiwe,

kwa maana amesikia kilio changu

nikimwomba anihurumie.

7 Bwanani nguvu zangu na ngao yangu,

moyo wangu umemtumaini yeye,

nami nimesaidiwa.

Moyo wangu unarukaruka kwa furaha

nami nitamshukuru kwa wimbo.

8 Bwanani nguvu ya watu wake,

ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.

9 Waokoe watu wako na uubariki urithi wako;

uwe mchungaji wao na uwabebe milele.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/28-ccdd4c1f15c10ab12f79c0f60d9b93a3.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 29

Sauti Ya Bwana Wakati Wa Dhoruba

Zaburi ya Daudi.

1 MpeniBwana, enyi mashujaa,

mpeniBwanautukufu na nguvu.

2 MpeniBwanautukufu unaostahili jina lake;

mwabuduniBwanakatika uzuri wa utakatifu wake.

3 Sauti yaBwanaiko juu ya maji;

Mungu wa utukufu hupiga radi,

Bwanahupiga radi juu ya maji makuu.

4 Sauti yaBwanaina nguvu;

sauti yaBwanani tukufu.

5 Sauti yaBwanahuvunja mierezi;

Bwanahuvunja vipande vipande

mierezi ya Lebanoni.

6 Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama,

Sirioniurukaruke kama mwana nyati.

7 Sauti yaBwanahupiga kwa miali

ya umeme wa radi.

8 Sauti yaBwanahutikisa jangwa;

Bwanahutikisa Jangwa la Kadeshi.

9 Sauti yaBwanahuzalisha ayala,

na huuacha msitu wazi.

Hekaluni mwake wote wasema,

“Utukufu!”

10 Bwanahuketi akiwa ametawazwa juu ya gharika;

Bwanaametawazwa kuwa Mfalme milele.

11 Bwanahuwapa watu wake nguvu;

Bwanahuwabariki watu wake kwa kuwapa amani.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/29-a77bafb769001fb1643ac0ddcb064950.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 30

Maombi Ya Shukrani

Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi.

1 Nitakutukuza wewe, EeBwana,

kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi,

na hukuacha adui zangu

washangilie juu yangu.

2 EeBwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie

na wewe umeniponya.

3 EeBwana, umenitoa Kuzimu,

umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti.

4 MwimbieniBwana, enyi watakatifu wake;

lisifuni jina lake takatifu.

5 Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi,

bali upendo wake hudumu siku zote.

Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha,

lakini asubuhi kukawa na furaha.

6 Nilipofanikiwa nilisema,

“Sitatikiswa kamwe.”

7 EeBwana, uliponijalia,

uliuimarisha mlima wangu,

lakini ulipouficha uso wako

nilifadhaika.

8 Kwako wewe, EeBwana, niliita,

kwa Bwana niliomba rehema:

9 “Kuna faida gani katika kuangamia kwangu?

Katika kushuka kwangu shimoni?

Je, mavumbi yatakusifu?

Je, yatatangaza uaminifu wako?

10 EeBwana, unisikie na kunihurumia,

EeBwana, uwe msaada wangu.”

11 Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza,

ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,

12 ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya.

EeBwanaMungu wangu, nitakushukuru milele.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/30-445301d403cecad780d7e1817451227b.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 31

Maombi Na Sifa Kwa Kuokolewa Kutoka Kwa Adui

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 EeBwana, nimekukimbilia wewe,

usiache nikaaibika kamwe,

kwa haki yako uniokoe.

2 Nitegee sikio lako,

uje uniokoe haraka;

uwe kwangu mwamba wa kimbilio,

ngome imara ya kuniokoa.

3 Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu,

uniongoze na kunilinda kwa ajili ya jina lako.

4 Uniepushe na mtego niliotegewa,

maana wewe ndiwe kimbilio langu.

5 Ninaikabidhi roho yangu mikononi mwako,

unikomboe EeBwana, uliye Mungu wa kweli.

6 Ninawachukia wale wanaongʼangʼania sanamu batili;

mimi ninamtumainiBwana.

7 Nitafurahia na kushangilia upendo wako,

kwa kuwa uliona mateso yangu

na ulijua maumivu ya nafsi yangu.

8 Hukunikabidhi kwa adui yangu

bali umeiweka miguu yangu mahali penye nafasi.

9 EeBwanaunihurumie, kwa kuwa niko kwenye shida;

macho yangu yanafifia kwa huzuni,

nafsi yangu na mwili wangu kwa sikitiko.

10 Maisha yangu yamedhoofika kwa majonzi,

naam, miaka yangu kwa kulia kwa maumivu makali;

nguvu zangu zinaisha kwa ajili ya mateso,

na mifupa yangu inachakaa.

11 Kwa sababu ya adui zangu wote,

nimedharauliwa kabisa na jirani zangu,

hata kwa rafiki zangu nimekuwa tisho,

wale wanionao barabarani hunikimbia.

12 Nimesahaulika miongoni mwao kama mtu aliyekufa,

nimekuwa kama chombo cha mfinyanzi kilichovunjika.

13 Kwa maana nimesikia maneno niliyosingiziwa na wengi;

vitisho viko pande zote;

kwa kuwa wamefanya mashauri dhidi yangu,

na kula njama kuniua.

14 Lakini mimi ninakutumaini wewe peke yako, EeBwana;

nimesema, “Wewe ndiwe Mungu wangu.”

15 Siku za maisha yangu ziko mikononi mwako,

uniokoe mikononi mwa adui zangu

na wale wanifuatiao.

16 Mwangazie mtumishi wako uso wako,

uniokoe kwa ajili ya upendo wako usiokoma.

17 Usiniache niaibike, EeBwana,

kwa maana nimekulilia wewe,

bali waovu waaibishwe

na kunyamazishwa Kuzimu.

18 Midomo yao isemayo uongo na inyamazishwe,

kwa maana kwa kiburi na dharau

wao husema kwa majivuno

dhidi ya wenye haki.

19 Tazama jinsi ulivyo mkuu wema wako,

uliowawekea akiba wakuchao,

ambao huwapa wale wakukimbiliao

machoni pa watu.

20 Unawahifadhi katika uvuli wa uwepo wako

kutokana na hila za wanadamu;

katika makao yako huwaweka salama

kutokana na ndimi za mashtaka.

21 AtukuzweBwana,

kwa kuwa amenionyesha upendo wake wa ajabu

nilipokuwa katika mji uliozingirwa.

22 Katika hofu yangu nilisema,

“Nimekatiliwa mbali na macho yako!”

Hata hivyo ulisikia kilio changu

ukanihurumia nilipokuita unisaidie.

23 MpendeniBwananinyi watakatifu wake wote!

Bwanahuwahifadhi waaminifu,

lakini wenye kiburi huwalipiza kikamilifu.

24 Kuweni hodari na mjipe moyo,

ninyi nyote mnaomtumainiBwana.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/31-5c2a77da4be1198712267b5c53c1fb47.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 32

Furaha Ya Msamaha

Zaburi ya Daudi. Funzo.

1 Heri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake,

ambaye dhambi zake zimefunikwa.

2 Heri mtu yule ambayeBwana

hamhesabii dhambi,

na ambaye rohoni mwake

hamna udanganyifu.

3 Niliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa

kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.

4 Usiku na mchana

mkono wako ulinilemea,

nguvu zangu zilinyonywa

kama vile katika joto la kiangazi.

5 Kisha nilikujulisha dhambi yangu

wala sikuficha uovu wangu.

Nilisema, “Nitaungama

makosa yangu kwaBwana.”

Ndipo uliponisamehe

hatia ya dhambi yangu.

6 Kwa hiyo kila mtu mcha Mungu akuombe

wakati unapopatikana,

hakika maji makuu yatakapofurika

hayatamfikia yeye.

7 Wewe ndiwe mahali pangu pa kujificha,

utaniepusha na taabu

na kunizunguka kwa nyimbo za wokovu.

8 Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea;

nitakushauri na kukuangalia.

9 Usiwe kama farasi au nyumbu

wasio na akili,

ambao ni lazima waongozwe kwa lijamu na hatamu

la sivyo hawatakukaribia.

10 Mtu mwovu ana taabu nyingi,

bali upendo usio na kikomo waBwana

unamzunguka mtu anayemtumaini.

11 Shangilieni katikaBwanana mfurahi, enyi wenye haki!

Imbeni, nyote mlio wanyofu wa moyo!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/32-6087b1c971c45e990043259d2e9cb7ac.mp3?version_id=1627—

Categories
Zaburi

Zaburi 33

Ukuu Na Wema Wa Mungu

1 MwimbieniBwanakwa furaha, enyi wenye haki;

kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.

2 MsifuniBwanakwa kinubi,

mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.

3 Mwimbieni wimbo mpya;

pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.

4 Maana neno laBwanani haki na kweli,

ni mwaminifu kwa yote atendayo.

5 Bwanahupenda uadilifu na haki;

dunia imejaa upendo wake usiokoma.

6 Kwa neno laBwanambingu ziliumbwa,

jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.

7 Ameyakusanya maji ya bahari

kama kwenye chungu;

vilindi vya bahari

ameviweka katika ghala.

8 Dunia yote na imwogopeBwana,

watu wote wa dunia wamche.

9 Kwa maana Mungu alisema, na ikawa,

aliamuru na ikasimama imara.

10 Bwanahuzuia mipango ya mataifa,

hupinga makusudi ya mataifa.

11 Lakini mipango yaBwanainasimama imara milele,

makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.

12 Heri taifa ambaloBwanani Mungu wao,

watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.

13 Kutoka mbinguniBwanahutazama chini

na kuwaona wanadamu wote;

14 kutoka maskani mwake huwaangalia

wote wakaao duniani:

15 yeye ambaye huumba mioyo yao wote,

ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.

16 Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake;

hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.

17 Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu,

licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.

18 Lakini macho yaBwanayako kwa wale wamchao,

kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,

19 ili awaokoe na mauti,

na kuwahifadhi wakati wa njaa.

20 Sisi tunamngojeaBwanakwa matumaini,

yeye ni msaada wetu na ngao yetu.

21 Mioyo yetu humshangilia,

kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.

22 Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, EeBwana,

tunapoliweka tumaini letu kwako.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/33-1fce9b791359e502eb1f99b6a9c33f07.mp3?version_id=1627—