Categories
Yoshua

Yoshua 18

Mgawanyo Wa Nchi Iliyobaki

1 Kusanyiko lote la Waisraeli likakusanyika huko Shilo na kusimamisha Hema la Kukutania. Nchi ikawa chini ya utawala wao,

2 lakini palikuwa bado makabila saba ya Israeli ambayo yalikuwa hayajapokea urithi wao.

3 Hivyo Yoshua akawaambia Waisraeli, “Je, mtasubiri hata lini ili kuingia kumiliki nchi ambayoBwana, Mungu wa baba zenu, amewapa?

4 Chagueni watu watatu kutoka kwenye kila kabila. Nitawatuma hao watu kukagua hiyo nchi na kuniandikia mapendekezo ya mgawanyo wa urithi wa kila kabila. Nao watanirudia.

5 Mtaigawanya hiyo nchi katika sehemu saba. Yuda atabaki katika eneo lake upande wa kusini na nyumba ya Yosefu katika nchi yake upande wa kaskazini.

6 Baada ya kuandika maelezo ya hizo sehemu saba za nchi, yaleteni kwangu, nami nitawapigia kura kwa kura mbele zaBwanaMungu wetu.

7 Hata hivyo, Walawi hawatakuwa na sehemu miongoni mwenu, kwa maana huduma ya ukuhani kwaBwanandio urithi wao. Nao Gadi, Reubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapata urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, ambako Mose mtumishi waBwanaaliwapa.”

8 Watu hao walipokuwa wanaondoka kwenda kuandika vizuri kuhusu hiyo nchi, Yoshua akawaagiza, “Nendeni mkakague hiyo nchi na mwandike maelezo kuihusu. Kisha mrudi kwangu, nami nitawapigia kura hapa Shilo mbele zaBwana.”

9 Ndipo hao watu walipoondoka na kupita katika ile nchi. Wakaandika maelezo yake kwenye kitabu, mji kwa mji, katika sehemu saba na kurudisha taarifa kwa Yoshua huko kambini Shilo.

10 Basi Yoshua akawapigia kura huko Shilo mbele zaBwana, na hapo akagawanya ile nchi kwa Waisraeli kufuatana na mgawanyo wa kabila zao.

Mgawo Kwa Benyamini

11 Kura iliangukia kabila la Benyamini, ukoo kwa ukoo. Eneo lao walilogawiwa lilikuwa kati ya kabila la Yuda na la Yosefu.

12 Upande wa kaskazini mpaka wao ulianzia pale Yordani, kupitia kaskazini ya mteremko wa Yeriko na kuendelea magharibi kuingia katika nchi ya vilima, ukitokea kwenye jangwa la Beth-Aveni.

13 Kutoka hapo ulikatiza kwenye mteremko wa kusini mwa Luzu (yaani Betheli) na kushuka hadi Ataroth-Adari katika kilima kusini mwa Beth-Horoni ya Chini.

14 Kutoka kilima kinachotazamana na Beth-Horoni upande wa kusini mpaka ule ukazunguka kusini kufuatia upande wa magharibi, na ukatokezea Kiriath-Baali (yaani Kiriath-Yearimu), mji wa watu wa Yuda. Huu ndio uliokuwa upande wa magharibi.

15 Upande wa kusini mpaka ulianzia kwenye viunga vya Kiriath-Yearimu kwa upande wa magharibi, nao ukatokeza kwenye chemchemi ya maji ya Neftoa.

16 Mpaka ukateremka hadi shefela inayotazamana na Bonde la Ben-Hinomu, kaskazini mwa Bonde la Refaimu. Ukaendelea chini kwenye Bonde la Hinomu sambamba na mteremko wa kusini mwa mji mkubwa wa Wayebusi na kisha hadi En-Rogeli.

17 Kisha ukapinda kuelekea kaskazini, ukaenda hadi En-Shemeshi na kuendelea mpaka Gelilothi, inayotazamana na Njia ya Adumimu, ukateremka hadi kwenye Jiwe la Bohani mwana wa Reubeni.

18 Ukaendelea upande wa mteremko wa kaskazini wa Beth-Araba ukateremka hadi Araba.

19 Kisha ukaenda mpaka kwenye mteremko wa kaskazini wa Beth-Hogla na kujitokeza kwenye ghuba ya kaskazini ya Bahari ya Chumvi, kwenye maingilio ya Yordani upande wa kusini. Huo ulikuwa mpaka wa kusini.

20 Nayo Yordani ikawa ndio mpaka wa upande wa mashariki.

Hii ilikuwa ndiyo mipaka iliyoonyesha urithi wa koo za Benyamini pande zote.

21 Kabila ya Benyamini, ukoo kwa ukoo, ilikuwa na miji mikubwa ifuatayo:

Yeriko, Beth-Hogla, Emeki-Kesisi,

22 Beth-Araba, Semaraimu, Betheli,

23 Avimu, Para na Ofra,

24 Kefar-Amoni, Ofni, na Geba; miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.

25 Gibeoni, Rama na Beerothi,

26 Mispa, Kefira, Moza,

27 Rekemu, Irpeeli, Tarala,

28 Zela, Elefu, mji wa Wayebusi (yaani Yerusalemu), Gibea na Kiriathi; miji kumi na minne pamoja na vijiji vyake.

Huu ndio uliokuwa urithi wa Benyamini kwa ajili ya koo zake.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOS/18-ea1dcbd53a72ff19fa7387ac9f8880e1.mp3?version_id=1627—

Categories
Yoshua

Yoshua 19

Mgawo Kwa Simeoni

1 Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.

2 Ulijumuisha:

Beer-Sheba (au Sheba), Molada,

3 Hasar-Shuali, Bala, Esemu,

4 Eltoladi, Bethuli, Horma,

5 Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,

6 Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.

7 Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,

8 pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu).

Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.

9 Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.

Mgawo Kwa Zabuloni

10 Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo:

Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.

11 Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.

12 Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.

13 Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.

14 Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.

15 Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.

16 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.

Mgawo Kwa Isakari

17 Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.

18 Eneo lao lilijumuisha:

Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,

19 Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,

20 Rabithi, Kishioni, Ebesi,

21 Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.

22 Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.

23 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.

Mgawo Kwa Asheri

24 Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.

25 Eneo lao lilijumuisha:

Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,

26 Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.

27 Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.

28 Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.

29 Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,

30 Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.

31 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.

Mgawo Kwa Naftali

32 Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:

33 Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.

34 Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.

35 Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,

36 Adama, Rama, Hazori,

37 Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,

38 Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.

39 Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.

Mgawo Kwa Dani

40 Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.

41 Eneo la urithi wao lilijumuisha:

Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,

42 Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,

43 Eloni, Timna, Ekroni,

44 Elteke, Gibethoni, Baalathi,

45 Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,

46 Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.

47 (Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)

48 Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.

Mgawo Kwa Yoshua

49 Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,

50 kama vileBwanaalivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Seraulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.

51 Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele zaBwanapenye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOS/19-a382a1f74d5d00631596cca7fbf30244.mp3?version_id=1627—

Categories
Yoshua

Yoshua 20

Miji Ya Makimbilio

1 NdipoBwanaakamwambia Yoshua,

2 “Waambie Waisraeli, watenge miji mikubwa ya kukimbilia, kama nilivyokuagiza kupitia Mose,

3 ili mtu yeyote atakayemuua mtu kwa bahati mbaya na pasipo kukusudia aweze kukimbilia huko na kujiepusha na mlipiza kisasi wa damu.

4 “Anapokimbilia mojawapo ya hii miji mikubwa atasimama kwenye maingilio ya lango la mji mkuu na kueleza wazee wa mji kuhusu shauri lake. Kisha watampokea katika mji wao na kumpa mahali pa kuishi nao.

5 Kama mlipiza kisasi wa damu akimfuatilia, wasimkabidhi yule mshtakiwa, kwa sababu alimuua jirani yake bila kukusudia, na bila kuwa na nia ya kudhuru.

6 Huyu aliyeua atakaa kwenye mji mkubwa huo mpaka awe amesimama kukabili mashtaka yake mbele ya kusanyiko na mpaka kuhani mkuu anayehudumu kwa wakati huo atakapokufa. Ndipo atakapoweza kurudi nyumbani kwake katika mji ambao aliukimbia.”

7 Basi wakatenga Kedeshi katika Galilaya kwenye nchi ya vilima ya Naftali, Shekemu katika nchi ya vilima ya Efraimu, na Kiriath-Arba (yaani Hebroni) kwenye nchi ya vilima ya Yuda.

8 Katika upande wa mashariki mwa Yordani ya Yeriko wakatenga Bezeri katika jangwa katika uwanda wa juu katika kabila la Reubeni, Ramothi katika Gileadi katika kabila la Gadi, na Golani huko Bashani katika kabila la Manase.

9 Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote aishiye miongoni mwao aliyemuua mtu kwa bahati mbaya, angeweza kukimbilia katika miji mikubwa hiyo iliyotengwa na asiuawe na mlipiza kisasi wa damu kabla hajasimama kukabili mashtaka mbele ya kusanyiko.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOS/20-c7cceb20f5e46f9c32b9499b2e677e89.mp3?version_id=1627—

Categories
Yoshua

Yoshua 21

Miji Kwa Walawi

1 Basi viongozi wa jamaa ya Walawi, wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa jamaa nyingine za makabila ya Israeli

2 huko Shilo katika Kanaani na kuwaambia, “Bwanaaliamuru kupitia Mose kuwa mtupe miji ya kuishi yenye sehemu za malisho kwa mifugo yetu.”

3 Hivyo kama vileBwanaalivyoamuru, Waisraeli wakawapa Walawi miji ifuatayo pamoja na sehemu zake za malisho kutoka urithi wao wenyewe.

4 Kura ya kwanza ikaangukia Wakohathi, ukoo kwa ukoo. Walawi waliokuwa wazao wa kuhani Aroni walipewa miji kumi na mitatu kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini.

5 Wazao wengine waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za makabila ya Efraimu, Dani na nusu ya Manase.

6 Wazao wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kutoka koo za makabila ya Isakari, Asheri, Naftali na nusu ya Manase huko Bashani.

7 Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.

8 Kwa hiyo Waisraeli wakawapa Walawi miji hii pamoja na sehemu zake za malisho, kama vileBwanaalivyokuwa ameamuru kupitia kwa Mose.

9 Kutoka makabila ya Yuda na Simeoni waligawa miji ifuatayo kwa majina

10 (miji hii walipewa wazao wa Aroni ambao walitokana na koo za Wakohathi wa Walawi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):

11 Waliwapa Kiriath-Arba (yaani Hebroni), pamoja na sehemu zake za malisho zilizoizunguka, katika nchi ya vilima ya Yuda. (Arba alikuwa baba wa Anaki.)

12 Lakini mashamba na vijiji vilivyozunguka mji mkubwa walikuwa wamempa Kalebu mwana wa Yefune kuwa milki yake.

13 Kwa hiyo wazao wa kuhani Aroni wakapewa Hebroni (mji mkuu wa makimbilio kwa ajili ya yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji), Libna,

14 Yatiri, Eshtemoa,

15 Holoni, Debiri,

16 Aini, Yuta na Beth-Shemeshi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji tisa kutoka kwa makabila haya mawili.

17 Kutoka kabila la Benyamini wakawapa Gibeoni, Geba,

18 Anathothi na Almoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.

19 Miji yote waliyopewa makuhani, wazao wa Aroni, ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.

20 Koo nyingine za Wakohathi, ambao pia ni Walawi, walipewa miji kutoka kabila la Efraimu:

21 Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji mkubwa wa makimbilio kwa yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji) na Gezeri,

22 Kibsaimu na Beth-Horoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.

23 Pia kutoka kabila la Dani wakapokea Elteke, Gibethoni,

24 Aiyaloni na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne

25 Kutoka nusu ya kabila la Manase, wakapokea Taanaki na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili.

26 Miji yote hii kumi pamoja na sehemu zake za malisho ilipewa koo za Wakohathi zilizobaki.

27 Koo za Walawi za Wagershoni walipewa:

kutoka nusu ya kabila la Manase,

Golani katika Bashani (mji mkuu wa makimbilio kwa yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji) na Beeshtera, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili;

28 kutoka kabila la Isakari walipewa,

Kishioni, Daberathi,

29 Yarmuthi na En-Ganimu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne

30 kutoka kabila la Asheri walipewa,

Mishali, Abdoni,

31 Helkathi na Rehobu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.

32 Kutoka kabila la Naftali walipewa,

Kedeshi katika Galilaya (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji), Hamoth-Dori na Kartani, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji mitano.

33 Miji yote ya koo za Wagershoni ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.

34 Koo za Wamerari (Walawi waliobaki) walipewa:

kutoka kabila la Zabuloni,

Yokneamu, Karta,

35 Dimna na Nahalali, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;

36 kutoka kabila la Reubeni walipewa

Bezeri, Yahasa,

37 Kedemothi na Mefaathi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;

38 kutoka kabila la Gadi walipewa,

Ramothi katika Gileadi (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa ajili ya mauaji), Mahanaimu,

39 Heshboni na Yazeri, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.

40 Miji yote waliyopewa koo za Wamerari, waliokuwa mabaki ya Walawi, ilikuwa ni kumi na miwili.

41 Miji yote ya Walawi katika eneo lililoshikwa na Waisraeli lilikuwa arobaini na minane, pamoja na sehemu zake za malisho.

42 Kila mmoja wa miji hii ulikuwa na sehemu ya malisho kuuzunguka; ndivyo ilivyokuwa kwa miji hii yote.

43 Kwa hiyoBwanaakawapa Israeli nchi yote aliyokuwa ameapa kuwapa baba zao, nao wakaimiliki na kukaa humo.

44 Bwanaakawapa pumziko kila upande, kama vile alivyokuwa amewaapia baba zao, hakuna hata mmoja wa adui zao aliyeweza kusimama mbele yao,Bwanaakawatia adui zao wote mikononi mwao.

45 Hakuna hata mojawapo ya ahadi nzuri yaBwanakwa nyumba ya Israeli ambayo haikutimia; kila moja ilitimia.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOS/21-3289d313f3c32f8264ff0432930a553c.mp3?version_id=1627—

Categories
Yoshua

Yoshua 22

Makabila Ya Mashariki Yarudi Nyumbani

1 Ndipo Yoshua akawaita Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase,

2 naye akawaambia, “Mmeshafanya yale yote Mose mtumishi waBwanaaliyowaamuru, nanyi mmenitii kwa kila jambo nililowaamuru.

3 Kwa muda mrefu sasa, hadi siku hii ya leo, hamkuwaacha ndugu zenu, bali ninyi mmetimiza ile kaziBwanaMungu wenu aliyowapa.

4 Sasa kwa kuwaBwanaMungu wenu amewapa ndugu zenu pumziko kama alivyoahidi, rudini nyumbani mwenu katika nchi ile ambayo Mose mtumishi waBwanaaliwapa ngʼambo ya Yordani.

5 Lakini mwe waangalifu sana kushika amri na sheria zile Mose mtumishi waBwanaalizowapa: yaani kumpendaBwanaMungu wenu na kuenenda katika njia zake zote, kutii amri zake, kushikamana naye kwa uthabiti na kumtumikia kwa moyo wenu wote na roho yenu yote.”

6 Ndipo Yoshua akawabariki na kuwaaga waende zao, nao wakaenda nyumbani mwao.

7 (Kwa nusu ya kabila la Manase Mose alikuwa amewapa eneo katika Bashani na ile nusu nyingine ya hilo kabila Yoshua aliwapa eneo upande wa magharibi ya Yordani pamoja na ndugu zao). Yoshua alipowaaga waende zao nyumbani, aliwabariki,

8 akisema, “Rudini nyumbani mwenu na utajiri wenu mwingi, yaani makundi makubwa ya mifugo, mkiwa na fedha, dhahabu, shaba na chuma, pia wingi wa nguo, nanyi mkagawane na ndugu zenu hizo nyara zilizotoka kwa adui zenu.”

9 Kwa hiyo Wareubeni, Wagadi na hiyo nusu ya kabila la Manase wakawaacha Waisraeli huko Shilo katika nchi ya Kanaani ili kurudi Gileadi, nchi yao wenyewe waliyoipata sawasawa na agizo laBwanakupitia Mose.

10 Walipofika Gelilothi karibu na Yordani, katika nchi ya Kanaani, Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakajenga madhabahu ya fahari kubwa huko kando ya Yordani.

11 Waisraeli wengine waliposikia kwamba Wareubeni, Wagadi na ile nusu ya kabila la Manase walikuwa wamejenga madhabahu kwenye mpaka wa Kanaani huko Gelilothi karibu na Yordani kwenye upande wa Israeli,

12 kusanyiko lote la Israeli wakakusanyika huko Shilo ili wakapigane vita dhidi yao.

13 Kwa hiyo Waisraeli wengine wakamtuma Finehasi mwana wa kuhani Eleazari katika nchi ya Gileadi, kwa Wareubeni, Wagadi na hiyo nusu ya kabila la Manase.

14 Wakatuma pamoja naye watu kumi ambao ni viongozi, mmoja kwa kila kabila la Israeli, kila mmoja aliyekuwa kiongozi katika mgawanyiko wa jamaa miongoni mwa koo za Israeli.

15 Walipofika Gileadi, kwa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, wakawaambia:

16 “Kusanyiko lote laBwanalasema: ‘Je, mmewezaje kuacha kumwamini Mungu wa Israeli jinsi hii? Mmewezaje kumwachaBwanana kujijengea madhabahu dhidi yake na kumwasi?

17 Je, dhambi ya Peori haikutosha? Hata ingawa kulikuja tauni juu ya kusanyiko laBwana, mpaka leo hii hatujatakasika kutokana na dhambi hiyo!

18 Je, sasa ndiyo mnamwachaBwana?

“ ‘Kama mkimwasiBwanaleo, kesho atalikasirikia kusanyiko lote la Israeli.

19 Kama nchi mnayomiliki imenajisika, vukeni mje katika nchi yaBwana, mahali Maskani yaBwanailipo, nanyi mkajitwalie sehemu miongoni mwetu, lakini msije mkaasi dhidi yaBwanawala dhidi yetu sisi kwa kujijengea madhabahu, zaidi ya madhabahu yaBwanaMungu wetu.

20 Wakati Akani mwana wa Zera alipokosa uaminifu kwa vitu vilivyowekwa wakfu, je, ghadhabu haikulipata kusanyiko lote la Israeli? Hakuwa yeye peke yake aliyekufa kwa ajili ya dhambi yake.’ ”

21 Ndipo Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walipowajibu viongozi wa koo za Israeli, wakisema:

22 “Yeye Mwenye Nguvu, Mungu,Bwana! Yeye Mwenye Nguvu, Mungu,Bwana! Yeye anajua! Israeli na wajue! Kama huu umekuwa ni uasi au kukosa utii kwaBwana, msituache hai siku hii ya leo.

23 Kama tumejijengea madhabahu yetu wenyewe ili kumwachaBwanana kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka, au kutoa sadaka za amani juu yake,Bwanamwenyewe na atupatilize leo.

24 “Sivyo! Tulifanya hivyo kwa hofu kwamba siku zijazo wazao wenu wanaweza wakawaambia wazao wetu, ‘Mna uhusiano gani naBwana, Mungu wa Israeli?

25 Bwanaameifanya Yordani kuwa mpaka kati yetu na ninyi, ninyi Wareubeni na Wagadi! Hamna fungu kwaBwana.’ Kwa hiyo wazao wenu wanaweza wakawasababisha wazao wetu wakaacha kumchaBwana.

26 “Hii ndiyo sababu tulisema, ‘Tujiweke tayari na tujenge madhabahu, lakini si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa au dhabihu.’

27 Badala yake, itakuwa ni ushahidi kati yetu na ninyi na vizazi vijavyo, kwamba tutamwabuduBwanakatika mahali patakatifu pake pamoja na sadaka zetu za kuteketezwa, dhabihu na sadaka za amani. Ndipo katika siku zijazo, wazao wenu hawataweza kuwaambia wazao wetu, ‘Ninyi hamna fungu katikaBwana.’

28 “Nasi tulisema, ‘Ikiwa wakati wowote watatuambia hilo, au kuwaambia uzao wetu, tutawajibu hivi: Angalieni nakala hii ya madhabahu yaBwana, ambayo baba zetu waliijenga, si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu, bali kama ushahidi kati yetu na ninyi.’

29 “Hili jambo la kumwasiBwanana kumwacha siku hii ya leo kwa kujenga madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na dhabihu, zaidi ya madhabahu yaBwanaMungu wetu iliyo mbele ya maskani yake na liwe mbali nasi.”

30 Wakati kuhani Finehasi na viongozi wa kusanyiko na wakuu wa koo za Israeli, waliposikia hayo waliyosema Wareubeni, Wagadi na Manase, wakaridhika.

31 Naye Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, akawaambia Wareubeni, Wagadi na Manase, “Leo tunajua kwambaBwanayuko pamoja nasi, kwa sababu hamkukosa uaminifu kwaBwanakatika jambo hili. Sasa mmewaokoa Waisraeli na mkono waBwana.”

32 Ndipo Finehasi, mwana wa kuhani Eleazari na viongozi wakarudi Kanaani kutoka kwenye kukutana kwao na Wareubeni na Wagadi huko Gileadi nao wakatoa taarifa kwa Waisraeli.

33 Walifurahi kusikia taarifa hiyo, na wakamhimidi Mungu. Wala hawakuzungumza tena habari za kupigana vita dhidi yao ili kuharibu nchi ambayo Wareubeni na Wagadi waliishi.

34 Nao Wareubeni na Wagadi wakayaita yale madhabahu Edi, yaani Shahidi: kwa kuwa itakuwa shahidi kati yetu na ninyi kwambaBwanandiye Mungu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOS/22-28b4efe4dc43b505ff70d12f79c11a8d.mp3?version_id=1627—

Categories
Yoshua

Yoshua 23

Yoshua Anawaaga Viongozi

1 Baada ya muda mrefu kupita, nayeBwanaakawa amewapa Israeli pumziko mbele ya adui zao wote waliowazunguka, Yoshua, wakati huo akiwa mzee na umri ukiwa umeendelea sana,

2 akawaita Israeli wote, wazee wao, viongozi, waamuzi na maafisa Yoshua akawaambia: “Mimi ni mzee na umri wangu umeendelea sana.

3 Ninyi wenyewe mmeona kila kituBwanaMungu wenu, alichowatendea mataifa haya yote kwa ajili yenu. Ilikuwa niBwanaMungu wenu aliyewapigania.

4 Kumbukeni jinsi nilivyowagawia kama urithi kwa makabila yenu yote nchi ya mataifa yaliyobaki, yaani mataifa niliyowashinda, kati ya Mto Yordani na Bahari kuu upande wa magharibi.

5 BwanaMungu wenu mwenyewe atawaondoa watoke mbele yenu. Atawafukuza mbele yenu, nanyi mtamiliki nchi yao, kama vileBwanaMungu wenu alivyowaahidi.

6 “Kuweni hodari sana, kuweni waangalifu kutii yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Sheria ya Mose, pasipo kugeuka upande wa kuume au kushoto.

7 Msishirikiane na mataifa yaliyobakia katikati yenu, wala msiombe kwa majina ya miungu yao au kuapa kwayo. Msiitumikie wala kuisujudia.

8 Bali mtashikamana kwa uthabiti naBwana, Mungu wenu, kama vile ambavyo mmefanya mpaka sasa.

9 “Bwanaamewafukuza mbele yenu mataifa makubwa na yenye nguvu, mpaka siku ya leo hakuna yeyote aliyeweza kusimama mbele yenu.

10 Mtu mmoja miongoni mwenu anafukuza watu elfu, kwa kuwaBwanaMungu wenu anawapigania, kama alivyoahidi.

11 Kwa hiyo kuweni waangalifu sana kumpendaBwanaMungu wenu.

12 “Lakini ikiwa mtageuka na kushikamana na mabaki ya mataifa haya yaliyosalia katikati yenu na kama mtaoana na kushirikiana nao,

13 basi mwe na hakika kuwaBwanaMungu wenu hatawafukuza tena mataifa hayo mbele yenu. Badala yake, watakuwa tanzi na mitego kwenu, mijeledi migongoni mwenu, na miiba machoni mwenu, mpaka mwangamie kutoka nchi hii nzuri, ambayoBwanaMungu wenu amewapa.

14 “Sasa mimi ninakaribia kwenda katika njia ya watu wote wa dunia. Mnajua kwa mioyo yenu na roho zenu kwamba hakuna ahadi zozote njemaBwanaMungu wenu alizowaahidia, ambazo hazikutimia. Kila ahadi imetimizwa, hakuna hata moja ambayo haikutimia.

15 Lakini kama vile kila ahadi njema yaBwanaMungu wenu imekuwa kweli, vivyo hivyoBwanaataleta maovu yote kama alivyo onya, mpaka awe amewaangamiza kutoka nchi hii nzuri aliyowapa.

16 Kama mkilivunja agano laBwanaMungu wenu, ambalo aliwaamuru ninyi, mkaenda na kuitumikia miungu mingine na kuisujudia, hasira yaBwanaitawaka dhidi yenu, nanyi mtaangamia kutoka nchi nzuri aliyowapa ninyi.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOS/23-66bad3d200ae96492b40ac9253ae7665.mp3?version_id=1627—

Categories
Yoshua

Yoshua 24

Agano Lafanywa Upya Huko Shekemu

1 Ndipo Yoshua akaita pamoja makabila yote ya Israeli huko Shekemu. Akawaita wazee, viongozi, waamuzi na maafisa wa Israeli, nao wakaja mbele za Mungu.

2 Yoshua akawaambia watu wote, “Hili ndiloBwana, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Hapo zamani baba zenu, pamoja na Tera baba yake Abrahamu na Nahori, waliishi ngʼambo ya Mto nao waliiabudu miungu mingine.

3 Lakini nilimwondoa baba yenu Abrahamu kutoka nchi hiyo ngʼambo ya Mto, nami nikamwongoza katika nchi yote ya Kanaani, nikampa wazao wengi. Nikampa Isaki,

4 naye Isaki nikampa Yakobo na Esau. Esau nikampa nchi ya vilima ya Seiri, lakini Yakobo pamoja na wanawe wakashuka Misri.

5 “ ‘Kisha nikawatuma Mose na Aroni, nami nikawapiga Wamisri kwa kile nilichokitenda huko, tena nikawatoa ninyi huko.

6 Nilipowatoa baba zenu Misri, mlifika kwenye bahari, nao Wamisri wakawafuatia baba zenu kwa magari na wapanda farasi mpaka kwenye Bahari ya Shamu.

7 Lakini wakamliliaBwanawakitaka msaada, naye akaweka giza kati yenu na Wamisri, akaileta bahari juu yao ikawafunika. Ninyi mliona kwa macho yenu wenyewe kile nilichowatendea Wamisri. Kisha mliishi jangwani kwa muda mrefu.

8 “ ‘Nikawaleta katika nchi ya Waamori ambao waliishi mashariki mwa Yordani. Wakapigana nanyi, lakini nikawatia mikononi mwenu. Nikawaangamiza mbele yenu nanyi mkaimiliki nchi yao.

9 Wakati Balaki mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu, alipojiandaa kupigana dhidi ya Israeli, alimwita Balaamu mwana wa Beori apate kuwalaani.

10 Lakini sikumkubali Balaamu, kwa hiyo aliwabariki tena na tena, nami niliwaokoa toka mkononi mwake.

11 “ ‘Ndipo mlipovuka Yordani mkafika Yeriko. Raiya wa Yeriko wakapigana nanyi, kama walivyofanya Waamori, Waperizi, Wakanaani, Wahiti, Wagirgashi, Wahivi na Wayebusi, lakini niliwatia mikononi mwenu.

12 Nikatuma manyigu mbele yenu, ambao pia waliwafukuza mbele yenu, hao wafalme wawili wa Waamori. Siyo upanga au upinde wenu wenyewe vilivyowapatia ushindi.

13 Hivyo nikawapa ninyi nchi ambayo hamkuitaabikia na miji ambayo hamkuijenga na mnaishi ndani yake na kula toka kwa mashamba ya mizabibu na mizeituni msiyoipanda.’

14 “Sasa basi mcheniBwanana kumtumikia kwa uaminifu wote. Itupeni mbali miungu ambayo baba zenu waliiabudu huko ngʼambo ya Mto Frati na huko Misri, nanyi mtumikieniBwana.

15 Lakini msipoona vyema kumtumikiaBwana, chagueni hivi leo mtakayemtumikia, kama ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ngʼambo Frati, au miungu ya Waamori, ambao mnakaa katika nchi yao. Lakini mimi na nyumba yangu, tutamtumikiaBwana.”

16 Ndipo hao watu wakajibu, “Hili jambo liwe mbali nasi la kumsahauBwanana kuitumikia miungu mingine!

17 BwanaMungu wetu mwenyewe ndiye alitutoa sisi na baba zetu akatupandisha kutoka Misri, kutoka nchi ile ya utumwa, na kutenda zile ishara kubwa mbele ya macho yetu. Ndiye aliyetulinda katika safari yetu yote na kutokana na mataifa yote ambayo tulipita katikati yao.

18 Bwanaakayafukuza mbele yetu mataifa yote pamoja na Waamori, walioishi katika nchi hii. Hivyo sisi nasi tutamtumikiaBwanakwa kuwa yeye ndiye Mungu wetu.”

19 Yoshua akawaambia watu, “Hamwezi kumtumikiaBwana. Yeye ni Mungu Mtakatifu, ni Mungu mwenye wivu. Hatasamehe uasi wenu na dhambi zenu.

20 Ikiwa mkimwachaBwanana kuitumikia miungu migeni, atageuka na kuwaleteeni maafa na kuwaangamiza, baada ya kuwa mwema kwenu.”

21 Lakini watu wakamwambia Yoshua, “Sivyo! Sisi tutamtumikiaBwana.”

22 Ndipo Yoshua akawaambia, “Ninyi mmekuwa mashahidi juu yenu wenyewe kuwa mmechagua kumtumikiaBwana.”

Nao wakajibu, “Ndiyo, tu mashahidi.”

23 Yoshua akawaambia, “Sasa basi, itupeni mbali hiyo miungu migeni iliyo katikati yenu, nanyi mtoleeniBwana, Mungu wa Israeli, mioyo yenu.”

24 Nao watu wakamwambia Yoshua, “TutamtumikiaBwanaMungu wetu na kumtii yeye.”

25 Siku ile Yoshua akafanya agano kwa ajili ya watu na hapo Shekemu ndipo alipowaandikia amri na sheria.

26 Naye Yoshua akayaandika mambo haya katika Kitabu cha Sheria ya Mungu. Ndipo akalitwaa jiwe kubwa, akalisimamisha huko chini ya mwaloni, karibu na mahali patakatifu paBwana.

27 Yoshua akawaambia watu wote, “Angalieni! Jiwe hili litakuwa shahidi juu yetu. Limesikia maneno yoteBwanaaliyotuambia. Litakuwa shahidi juu yenu kama mtakuwa waongo kwa Mungu wenu.”

Kuzikwa Katika Nchi Ya Ahadi

28 Basi Yoshua akawatuma watu kila mmoja aende katika urithi wake mwenyewe.

29 Baada ya mambo haya, Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi waBwanaakafa akiwa na umri wa miaka mia moja na kumi.

30 Nao wakamzika katika nchi ya urithi wake, huko Timnath-Serakatika nchi ya vilima ya Efraimu, kaskazini ya Mlima wa Gaashi.

31 Israeli wakamtumikiaBwanasiku zote za maisha ya Yoshua, na za hao wazee walioishi baada ya Yoshua kufa, ambao waliona kila kituBwanaalichowatendea Israeli.

32 Nayo ile mifupa ya Yosefu, ambayo Waisraeli waliipandisha kutoka huko Misri, wakaizika huko Shekemu kwenye eneo, ambalo Yakobo alilinunua kwa wana wa Hamori baba yake Shekemu, kwa vipande mia vya fedha. Eneo hili likawa ni urithi wa uzao wa Yosefu.

33 Naye Eleazari mwana wa Aroni akafariki akazikwa huko Gibea, mlima aliokuwa amepewa mtoto wake Finehasi, kwenye nchi ya vilima ya Efraimu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JOS/24-60870f2732749295a19fb15578d5f092.mp3?version_id=1627—

Categories
Waamuzi

Waamuzi Utangulizi

Utangulizi

Jina la kitabu hiki limetokana na viongozi waliojulikana kama Waamuzi ambao Mungu aliwainua kuongoza nchi ya Israeli. Hii ilitokana na kupotoka kwingi na kurudi nyuma kwa wana wa Israeli baada ya kifo cha Yoshua. Kwa sababu yeye alikuwa amewachagua kuwa watu wake, ambao kupitia kwao watu wote wangeweza kujua upendo wa Mungu, basi Mungu asingewaacha waanguke kabisa chini ya uonevu wa adui zao. Kitabu hiki kinaelezea habari za Waisraeli kwa kipindi kati ya kifo cha Yoshua na huduma ya Samweli.

Mungu alikuwa amewasaidia Waisraeli kuishinda na kuiteka Kanaani, ambako ndani yake yaliishi mataifa mengi maovu. Lakini walikuwa katika hatari ya kuipoteza hii Nchi ya Ahadi kwa sababu walianza kumwasi Mungu. Walipomrudia Mungu, naye Mungu aliwainulia Waamuzi wa kuwaokoa kutoka mikononi mwa adui zao, na kuwarudisha tena katika njia na kusudi lake, na kuwaongoza. Hivyo kipindi hiki kilijulikana kwa mashujaa walioitwa Waamuzi ambao ndio walioongoza makabila ya Israeli. Jumla ya waamuzi kumi na wanne wameorodheshwa kuwa waliiongoza Israeli katika kitabu hiki. Waliojulikana zaidi walikuwa Yefta, Debora, Gideoni na Samsoni.

Mataifa yaliyowaonea Waisraeli wakati wa kipindi hiki cha Waamuzi yalikuwa: Wakaldayo, Wamoabu, Wakanaani, Wamidiani, Waamoni na Wafilisti. Kipindi hiki cha Waamuzi kilidumu kwa miaka 410 kikitazamwa na vile matukio yalivyofuatana.

Mwandishi

Mwandishi wa kitabu hiki hajulikani ni nani, lakini mapokeo ya Kiyahudi yanasema ni Samweli.

Kusudi

Ni kuonyesha kwamba hukumu ya Mungu juu ya dhambi ni lazima, na pia kuwasamahe na kuwarudisha waliotubu katika uhusiano wake ni lazima.

Mahali

Nchi ya Kanaani ambayo baadaye iliitwa Israeli.

Tarehe

Wakati kitabu hiki kiliandikwa haujulikani.

Wahusika Wakuu

Othnieli, Ehudi, Debora, Gideoni, Abimeleki, Yefta, Samsoni na Delila.

Wazo Kuu

Baada ya Yoshua kufariki, Waisraeli walikuwa wakiinuka walipompata kiongozi na baada ya kiongozi huyo kufariki walipotoka na kuangukia mikononi mwa maadui zao. Walipomlilia Mungu aliwainulia mwamuzi, ambaye aliwaongoza na kuwapa ushindi.

Mambo Muhimu

Mambo mawili muhimu katika kitabu cha Waamuzi ni vile Waisraeli waligandamizwa na mataifa jirani kwa sababu ya kumwasi Mungu, na vile Mungu aliwakomboa kutoka kwa watesi wao baada ya kutubu na kumrudia.

Mgawanyo

Waisraeli kushindwa kuyafukuza kabisa mataifa yaliyokuwa nchi ya Kanaani (

1:1–3:6

)

Waamuzi kuwakomboa Waisraeli (

3:7–16:31

)

Waisraeli kuanguka kiroho, kimaadili na kisiasa (

17:1–21:25

).

Categories
Waamuzi

Waamuzi 1

Israeli Wapigana Na Wakanaani Waliobaki

1 Baada ya kifo cha Yoshua, Waisraeli wakamuulizaBwana, “Ni nani atakayetangulia kupanda mbele yetu kwa ajili ya kupigana na Wakanaani?”

2 Bwanaakajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia; nimewapa hiyo nchi mikononi mwao.”

3 Ndipo watu wa Yuda wakawaambia Wasimeoni ndugu zao, “Pandeni pamoja nasi katika nchi tuliyopewa, ili tupate kupigana na Wakanaani. Sisi pia tutakwenda pamoja nanyi katika sehemu yenu mliyopewa.” Basi Wasimeoni wakaenda pamoja nao.

4 Yuda aliposhambulia,Bwanaakawatia Wakanaani na Waperizi mikononi mwao, nao wakawaua watu 10,000 huko Bezeki.

5 Huko ndiko walipomkuta huyo Adoni-Bezeki, nao wakapigana naye na kuwafanya Wakanaani na Waperizi wakimbie.

6 Adoni-Bezeki pia alikimbia, nao wakamfuata na kumkamata, wakamkata vidole vyake gumba vya mikono na vya miguu.

7 Ndipo Adoni-Bezeki akasema, “Nimewatendea wafalme sabini kama nilivyotendewa na kuwalisha makombo ya chakula chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa haya, kama yale niliyowatendea.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.

8 Watu wa Yuda wakashambulia pia Yerusalemu na kuiteka. Wakaupiga mji kwa upanga na kuuchoma kwa moto.

9 Baada ya hayo, watu wa Yuda wakateremka kupigana na Wakanaani walioishi katika nchi ya vilima, yaani, Negebu na nchi chini ya vilima vya magharibi.

10 Yuda wakakabiliana na Wakanaani walioishi Hebroni (ambayo hapo kwanza iliitwa Kiriath-Arba) na kuwashinda Sheshai, Ahimani na Talmai.

11 Kutoka huko wakasonga mbele kukabiliana na watu walioishi Debiri (ambao hapo kwanza uliitwa Kiriath-Seferi.)

12 Kalebu akasema, “Nitamwoza binti yangu Aksa kwa mtu atakayeweza kupigana na kuteka Kiriath-Seferi.”

13 Basi Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa huyo Kalebu, akawashinda, kwa hiyo Kalebu akamtoa binti yake Aksa akaolewa naye.

14 Siku moja Aksa alipokuja kwa Othnieli, alimsihi Othnieli amwombe baba yake, Kalebu, shamba. Aksa aliposhuka kutoka juu ya punda wake, Kalebu akamuuliza, “Je, wataka nikufanyie nini?”

15 Akamjibu, “Naomba unifanyie jambo moja la hisani. Kwa kuwa umenipa ardhi huko Negebu, nipe pia chemchemi za maji.” Ndipo Kalebu akampa chemchemi za juu na za chini.

16 Wazao wa yule Mkeni, baba mkwe wa Mose, wakapanda pamoja na watu wa Yuda kutoka Mji wa Mitende,wakaenda kuishi miongoni mwa watu wa jangwa ya Yuda huko Negebu karibu na mji wa Aradi.

17 Basi watu wa Yuda wakaenda na Wasimeoni ndugu zao kushambulia Wakanaani waishio Sefathi, nao wakauangamiza huo mji kabisa. Kwa hiyo huo mji ukaitwa Horma

18 Watu wa Yuda wakatwaa pia Gaza, Ashkeloni na Ekroni, kila mji na vijiji vyake vinavyouzunguka.

19 Bwanaalikuwa pamoja na watu wa Yuda. Wakaimiliki nchi ya vilima, lakini hawakuweza kuwafukuza watu waliokaa katika hiyo tambarare, kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.

20 Kama vile Mose alivyoahidi, Kalebu alipewa Hebroni, naye akawafukuza wana watatu wa Anaki.

21 Hata hivyo, Wabenyamini walishindwa kuwafukuza Wayebusi, waliokuwa wanaishi Yerusalemu; hivyo hadi leo Wayebusi huishi humo pamoja na Wabenyamini.

22 Basi nyumba ya Yosefu wakashambulia Betheli, nayeBwanaalikuwa pamoja nao.

23 Walipotuma watu kwenda kupeleleza Betheli (ambao hapo kwanza uliitwa Luzu),

24 wale wapelelezi wakaona mtu anatoka mjini, nao wakamwambia, “Tuonyeshe jinsi ya kuingia mjini nasi tutakutendea wema.”

25 Hivyo akawaonyesha, nao wakaupiga mji kwa upanga lakini wakamhifadhi hai yule mtu na jamaa yake yote.

26 Yule mtu akaenda hadi nchi ya Wahiti, ambapo aliujenga mji na kuuita Luzu, ambao ndio jina lake hadi leo.

27 Lakini Manase hawakuwafukuza watu wa Beth-Shani na vijiji vyake, au watu wa Taanaki na vijiji vyake, au watu wa Dori na vijiji vyake, au watu wa Ibleamu na vijiji vyake, au watu wa Megido na vijiji vyake, lakini Wakanaani waliazimu kuishi katika nchi ile.

28 Israeli walipopata nguvu, wakawatia Wakanaani katika kazi ya kulazimishwa, lakini kamwe hawakuwafukuza watoke kabisa.

29 Wala Efraimu hawakuwafukuza kabisa Wakanaani walioishi Gezeri, bali Wakanaani waliendelea kuishi humo miongoni mwao.

30 Vivyo hivyo Zabuloni hawakuwafukuza Wakanaani walioishi huko Kitroni, wala walioishi Nahaloli, ambao walibaki miongoni mwao; bali waliwatia katika kazi ya kulazimishwa.

31 Wala Asheri hawakuwafukuza wale walioishi huko Ako, Sidoni, Alabu, Akzibu, Helba, Afeki wala Rehobu

32 na kwa sababu ya jambo hili Waasheri wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi.

33 Wala Naftali hawakuwafukuza wale walioishi Beth-Shemeshi wala wale walioishi Beth-Anathi; lakini Naftali nao pia wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi, nao wale walioishi Beth-Shemeshi na Beth-Anathi wakawa watumishi wao katika kazi ya kulazimishwa.

34 Waamori wakawazuilia Wadani kwenye nchi ya vilima, kwa maana hawakuwaacha washuke kuingia kwenye sehemu tambarare.

35 Waamori pia wakaendelea kukaa katika Mlima Heresi, katika Aiyaloni na Shaalbimu, lakini mkono wa nyumba ya Yosefu ukawalemea, nao wakashindwa hata wakalazimika kuingia katika kazi ya kulazimishwa.

36 Mpaka wa Waamori ulikuwa kuanzia Genge la Akrabimu, kuendelea hadi Sela na kuelekea juu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JDG/1-22c681990a665b316a7d299bf06d47a5.mp3?version_id=1627—

Categories
Waamuzi

Waamuzi 2

Malaika Wa Bwana Huko Bokimu

1 Malaika waBwanaakakwea kutoka Gilgali hadi Bokimu, naye akasema, “Niliwapandisha kutoka Misri na kuwaingiza katika nchi niliyoapa kuwapa baba zenu. Nikasema, ‘Kamwe sitalivunja Agano langu nanyi.

2 Nanyi msifanye agano na watu wa nchi hii, bali mtazibomoa madhabahu yao.’ Lakini ninyi hamkunitii mimi. Kwa nini mmefanya jambo hili?

3 Sasa basi ninawaambia kuwa sitawafukuza watoke katikati yenu ila watakuwa miiba kwenu, nao miungu yao itakuwa tanzi kwenu.”

4 Malaika waBwanaalipomaliza kusema mambo haya kwa Waisraeli wote, watu wakalia kwa sauti kuu.

5 Wakapaita mahali pale Bokimu. Nao wakamtoleaBwanasadaka.

Kifo Cha Yoshua

6 Baada ya Yoshua kuwapa watu ruhusa waende zao, Waisraeli wakaenda kwenye urithi wao wenyewe ili kumiliki nchi yao.

7 Watu wakamtumikiaBwanasiku zote za maisha ya Yoshua, na za hao wazee walioishi baada ya Yoshua kufa, waliokuwa wameona mambo makuu ambayoBwanaalikuwa ametenda kwa ajili ya Israeli.

8 Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi waBwana, akafa akiwa na umri wa miaka 110.

9 Wakamzika katika nchi ya urithi wake, huko Timnath-Heresikatika nchi ya vilima ya Efraimu, kaskazini ya Mlima Gaashi.

10 Baada ya kizazi kile chote kukusanywa pamoja na baba zao, kikainuka kizazi kingine baada yao ambacho hakikumjuaBwana, wala matendo yale aliyokuwa ametenda kwa ajili ya Waisraeli.

11 Kwa hiyo Waisraeli wakatenda maovu machoni paBwanana kuwatumikia Mabaali.

12 WakamwachaBwana, Mungu wa baba zao, aliyekuwa amewatoa katika nchi ya Misri. Wakaifuata na kuiabudu miungu mbalimbali ya mataifa yanayowazunguka. WakamkasirishaBwana,

13 kwa sababu walimwacha na kutumikia Baali na Maashtorethi.

14 Hivyo hasira yaBwanaikawaka juu ya Israeli, naye akawatia mikononi mwa wavamizi waliowateka nyara. Akawauza katika mikono ya adui zao pande zote, hivyo hawakuweza tena kuwazuia adui zao.

15 Popote Israeli walipotoka kwenda kupigana, mkono waBwanaulikuwa kinyume nao ili kuwashinda, kama vile alivyokuwa amewaapia. Nao wakawa katika taabu kubwa.

16 NdipoBwanaakawainua waamuzi, ambao waliwaokoa katika mikono ya hao watu waliowashambulia.

17 Lakini hawakuwasikiliza hata waamuzi wao, bali walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine na kuiabudu. Waligeuka mara na kuiacha njia ambayo baba zao waliiendea, yaani, njia ya kutii amri zaBwana.

18 Kila maraBwanaalipowainulia mwamuzi,Bwanaalikuwa pamoja na huyo mwamuzi, naye aliwaokoa kutoka mikononi mwa adui zao kwa kipindi chote alichoishi yule mwamuzi. Kwa kuwaBwanaaliwahurumia kwa sababu ya kilio chao cha huzuni kwa ajili ya wale waliokuwa wakiwatesa na kuwataabisha.

19 Lakini kila mara mwamuzi alipofariki, watu walirudia katika hali mbaya ya uovu zaidi kuliko baba zao, wakiifuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu. Walikataa kuacha matendo yao maovu na njia zao za ukaidi.

20 Kwa hiyoBwanaakawakasirikia sana Israeli na kusema, “Kwa kuwa taifa hili limevunja Agano lile nililofanya na baba zao na hawakunisikiliza,

21 mimi nami sitafukuza taifa lolote ambalo Yoshua aliliacha alipofariki.

22 Nitayatumia ili nipate kuwapima Israeli na kuona kama wataishika njia yaBwanana kuenenda katika hiyo kama njia baba zao walivyofanya.”

23 Bwanaalikuwa ameyaacha hayo mataifa yabaki; hakuyaondoa mara moja kwa kuyatia mikononi mwa Yoshua.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JDG/2-2c8fb430d3a9cedf1d755d1cac3f4efe.mp3?version_id=1627—