Categories
Kumbukumbu

Kumbukumbu 23

Kutengwa Na Mkutano

1 Asiingie mtu yeyote aliyehasiwa kwa kupondwa makende au kwa kukatwa uume wake katika kusanyiko laBwana.

2 Mtu yeyote ambaye amezaliwa kwenye ndoa isiyo halali au wazao wake wasiingie kwenye kusanyiko laBwana, hata mpaka kizazi cha kumi.

3 Hapatakuwa na Mwamoni au Mmoabu au yeyote wa wazao wao atakayeruhusiwa kuingia katika kusanyiko laBwana, hata mpaka kizazi cha kumi.

4 Kwa kuwa hawakuja kuwalaki wakiwa na mkate na maji mlipokuwa njiani mlipotoka Misri, tena walimwajiri Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyoko Aramu-Naharaimuili kuwalaani ninyi.

5 Hata hivyo,BwanaMungu wenu hakumsikiliza Balaamu bali aligeuza laana kuwa baraka kwenu kwa sababuBwanaMungu wenu anawapenda.

6 Msitafute mapatano ya urafiki nao maisha yenu yote.

7 Usimchukie Mwedomu, kwa kuwa yeye ni ndugu yako. Usimchukie Mmisri, kwa sababu uliishi kama mgeni katika nchi yake.

8 Kizazi cha tatu cha watoto watakaozaliwa nao wanaweza kuingia katika kusanyiko laBwana.

Unajisi Katika Kambi

9 Unapokuwa umepiga kambi dhidi ya adui zako, jitenge na kitu chochote kisicho safi.

10 Ikiwa mtu amechafuka kwa sababu ya kutokwa na shahawa usiku, inampasa atoke nje ya kambi na kukaa huko.

11 Lakini jioni ikikaribia ataoga, na baada ya jua kuzama ataingia tena kambini.

12 Tengeni mahali nje ya kambi ambapo mnaweza kwenda kujisaidia.

13 Kama sehemu ya vifaa vyenu kuweni na kitu cha kulimia, nanyi mnapojisaidia, chimba shimo na kisha funika kile kikutokacho.

14 Kwa kuwaBwanaMungu wenu hutembea katika kambi yenu ili kuwalinda na kuwaweka adui zenu mikononi mwenu. Kambi yenu ni lazima iwe takatifu, ili asione kitu chochote miongoni mwenu kilicho kichafu akageuka na kuwaacha.

Sheria Mbalimbali

15 Ikiwa mtumwa amekimbilia kwako, usimrudishe kwa bwana wake.

16 Mwache aishi miongoni mwenu mahali popote anapopapenda na katika mji wowote anaochagua. Usimwonee.

17 Asiwepo Mwisraeli mwanamke kahaba au mwanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.

18 Kamwe usilete mapato ya ukahaba ikiwa ni ya mwanamke au ni ya mwanaume katika nyumba yaBwanaMungu wako kwa ajili ya nadhiri yoyote, kwa sababuBwanaMungu wako anachukizwa na yote mawili.

19 Usimtoze ndugu yako riba, iwe ni fedha ama chakula ama kitu kingine chochote ambacho waweza kupata riba juu yake.

20 Unaweza kumtoza mgeni riba, lakini siyo nduguyo Mwisraeli, ili kwambaBwanaMungu wako akubariki katika kila kitu unachoweka mkono katika nchi unayoingia kuimiliki.

21 Ukiweka nadhiri kwaBwanaMungu wako, usichelewe kuitimiza, kwa kuwaBwanaMungu wako atakudai, nawe utakuwa na hatia ya dhambi.

22 Lakini ukijizuia kuweka nadhiri, hutakuwa na hatia.

23 Chochote kitakachotamkwa kwa midomo yako ni lazima uhakikishe umekifanya, kwa sababu uliweka nadhiri yako kwa hiari mbele zaBwanaMungu wako kwa kinywa chako mwenyewe.

24 Kama ukiingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu kadiri utakavyo, lakini usiweke chochote kwenye kikapu chako.

25 Kama ukiingia katika shamba la nafaka la jirani yako, unaweza kukwanyua kwa mikono yako, lakini usikate kwa mundu nafaka iliyosimama.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/DEU/23-53383c563ac1f5e66e79b39871b3173e.mp3?version_id=1627—

Categories
Kumbukumbu

Kumbukumbu 24

Sheria Kuhusu Ndoa Na Talaka

1 Ikiwa mtu atamwoa mke na akamchukia kwa sababu ya kukosa adabu, naye akamwandikia hati ya talaka, akampa na kumfukuza kutoka nyumbani kwake,

2 ikiwa baada ya kuondoka nyumbani kwake atakuwa mke wa mtu mwingine,

3 ikiwa mume wake wa pili atachukizwa naye akamwandikia hati ya talaka, akampa na kumfukuza kutoka nyumbani kwake, au kama akifa,

4 basi yule mume wake wa kwanza, ambaye alimpa talaka, haruhusiwi kumwoa tena baada ya mwanamke huyo kuwa najisi. Hayo yatakuwa machukizo machoni paBwana. Usilete dhambi juu ya nchi ambayoBwanaMungu wako anakupa kama urithi.

5 Kama mtu ameoa karibuni, kamwe asipelekwe vitani au kupewa wajibu mwingine wowote. Kwa mwaka mmoja atakuwa huru kubaki nyumbani ili amfurahishe mke aliyemwoa.

6 Usitoe jozi ya mawe ya kusagia, hata ikiwa lile la juu, kuweka rehani kwa ajili ya deni, kwa sababu itakuwa ni kuweka uhai wa mtu kama dhamana.

7 Kama mtu akikamatwa akiiba yeyote miongoni mwa ndugu zake wa Waisraeli na kumtenda kama mtumwa au akimuuza, mwizi huyo ni lazima auawe. Nawe utaondoa uovu kutoka miongoni mwenu.

8 Pakitokea magonjwa ya ngozi ya kuambukiza, mwe waangalifu sana kufanya sawasawa na maagizo ya makuhani, ambao ni Walawi. Ni lazima mfuate kwa uangalifu yale niliyowaamuru.

9 Kumbukeni kileBwanaMungu wenu alichomfanyia Miriamu njiani baada ya ninyi kutoka Misri.

10 Unapomkopesha jirani yako chochote, usiingie nyumbani kwake kutwaa kile anachokitoa kama rehani.

11 Ukae nje na umwache huyo mtu uliyemkopesha akuletee hiyo rehani.

12 Ikiwa mtu huyo ni maskini, usiende kulala ukiwa na hiyo rehani yake katika milki yako.

13 Rudisha vazi lake kabla ya machweo ya jua ili apate kulilalia. Kisha atakushukuru na kitaonekana kama kitendo cha haki mbele zaBwanaMungu wako.

14 Usimwonee mtu maskini na mhitaji ambaye umemwajiri, akiwa ni nduguyo Mwisraeli au mgeni anayeishi katika mojawapo ya miji yenu.

15 Mlipe ujira wake kila siku kabla ya jua kutua, kwa sababu yeye ni maskini na anautegemea ujira huo. La sivyo, anaweza kumliliaBwanadhidi yako, nawe ukapata hatia ya dhambi.

16 Baba wasiuawe kwa ajili ya watoto wao, wala watoto wasiuawe kwa ajili ya baba zao; kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe.

17 Usipotoshe hukumu ya mgeni au yatima, au kuchukua vazi la mjane kama rehani.

18 Kumbukeni kwamba mlikuwa watumwa huko Misri, nayeBwanaMungu wenu akawakomboa kutoka huko. Hii ndiyo sababu ninawaamuru kutenda hili.

19 Unapovuna shamba lako na ukasahau mganda, usirudi kuuchukua. Acha kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane, iliBwanaMungu wako aweze kukubariki wewe katika kazi zote za mikono yako.

20 Unapovuna zeituni kutoka miti yako, usirudie matawi mara ya pili. Acha kilichobaki kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane.

21 Unapochuma zabibu katika shamba lako la mizabibu usirudie tena. Acha zinazobaki kwa ajili ya mgeni, yatima na mjane.

22 Kumbuka kwamba mlikuwa watumwa katika nchi ya Misri. Ndiyo sababu ninawaamuru kufanya hili.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/DEU/24-bae5375b07ac98e1f0ea5c5d90ebfdea.mp3?version_id=1627—

Categories
Kumbukumbu

Kumbukumbu 25

1 Watu wanapokuwa na ugomvi, wapeleke mahakamani na waamuzi wataamua shauri hilo; watawaachia wasio na kosa na kuwahukumu wenye hatia.

2 Kama mtu mwenye hatia anastahili kuchapwa, mwamuzi atamwamuru alale chini ili achapwe mbele yake idadi ya viboko kulingana na kosa lake,

3 lakini kamwe asichapwe zaidi ya viboko arobaini. Ikiwa atachapwa zaidi ya viboko arobaini, nduguyo atadhalilika machoni pako.

4 Usimfunge maksai kinywa anapopura nafaka.

5 Ikiwa ndugu wanaishi pamoja na mmoja wao akafa bila kuacha mwana, kamwe mjane wake asiolewe nje ya jamaa hiyo. Ndugu wa mumewe atamchukua, amwoe na kutimiza wajibu wa shemeji kwake.

6 Mwana wa kwanza atakayemzaa atapewa jina la ndugu aliyekufa ili jina lake lisifutike katika Israeli.

7 Hata hivyo, ikiwa ndugu huyo wa mume hataki kuoa huyo mke wa nduguye, mjane atawaendea wazee kwenye lango la mji na kusema, “Ndugu wa mume wangu anakataa kuendeleza jina la nduguye katika Israeli. Hataki kutimiza wajibu wa shemeji kwangu.”

8 Ndipo wazee wa mji wake watamwita na kuzungumza naye. Kama atashikilia kukataa akisema, “Sitaki kumwoa,”

9 mjane wa nduguye atamwendea mbele ya wazee, atamvua kiatu kimoja na kumtemea mate usoni, na kusema, “Hivi ndivyo ambavyo hufanywa kwa mtu ambaye atakataa kuendeleza jamaa ya ndugu yake.”

10 Jamaa ya mtu huyo itafahamika katika Israeli kama Jamaa ya Aliyevuliwa Kiatu.

11 Ikiwa watu wawili wanapigana na mke wa mmoja wao akaja kumwokoa mumewe na yule anayemshambulia, naye mke huyo akifika na kumkamata sehemu za siri,

12 huyo mwanamke utamkata mkono wake. Usimhurumie.

13 Usiwe na mawe ya kupimia ya aina mbili katika mkoba wako, moja zito na jingine jepesi.

14 Usiwe na vipimo viwili tofauti katika nyumba yako, kimoja kikubwa, kingine kidogo.

15 Ni lazima uwe na uzito na vipimo sahihi na vya haki, ili upate kuishi maisha marefu katika nchi anayokupaBwanaMungu wako.

16 Kwa maanaBwanaMungu wako humchukia yeyote ambaye hufanya mambo kama haya, yeyote anayetenda kwa udanganyifu.

17 Kumbuka kile Waamaleki walichowatendea mlipokuwa njiani mkitoka Misri.

18 Wakati mlipokuwa mmechoka na kuishiwa nguvu kwa safari yenu, wakawapiga wale wote waliokuja nyuma. Waamaleki hawakumwogopa Mungu.

19 BwanaMungu wako atakapokupa pumziko mbali na adui zako wote wanaokuzunguka katika nchi akupayo kuimiliki kuwa urithi, utafutilia mbali kumbukumbu lote la Waamaleki chini ya mbingu. Usisahau!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/DEU/25-a69a9ede5b6c28f1d8fb30b623580e89.mp3?version_id=1627—

Categories
Kumbukumbu

Kumbukumbu 26

Malimbuko Na Zaka

1 Mtakapokuwa mmeingia nchi ile ambayoBwanaMungu wenu anawapa kama urithi na mtakapokuwa mmeimiliki na kukaa ndani yake,

2 chukueni baadhi ya mavuno ya kwanza ya yale yote mtakayozalisha kutoka udongo wa nchi ambayoBwanaMungu wenu anawapa na mweke kwenye kapu. Kisha uende mahali ambapoBwanaMungu wako atapachagua kuwa makao kwa ajili ya Jina lake

3 na umwambie kuhani atakayekuwepo kwa wakati huo, “Ninatangaza leo kwaBwanaMungu wako kwamba nimekuja katika nchi ambayoBwanaaliwaapia baba zetu kwamba atatupa.”

4 Kuhani atapokea lile kapu mikononi mwako na kuliweka chini mbele ya madhabahu yaBwanaMungu wako.

5 Kisha utatangaza mbele zaBwanaMungu wako: “Baba yangu alikuwa Mwaramu aliyekuwa anatangatanga, akaenda Misri pamoja na watu wachache, akaishi huko hadi akawa taifa kubwa, lenye nguvu na watu wengi.

6 Lakini Wamisri walituonea na kututaabisha, wakitufanyisha kazi ngumu.

7 Kisha tulimliliaBwana, Mungu wa baba zetu, nayeBwanaakasikia sauti yetu na akaona huzuni yetu, taabu yetu na mateso yetu.

8 Kwa hiyoBwanaakatutoa nchi ya Misri kwa mkono wenye nguvu na ulionyooshwa, pamoja na utisho mkuu, ishara za miujiza na maajabu.

9 Akatuleta mahali hapa akatupa nchi hii, nchi inayotiririka maziwa na asali;

10 nami sasa ninaleta malimbuko ya ardhi ambayo wewe, EeBwana, umenipa.” Weka kapu mbele zaBwanaMungu wako na usujudu mbele zake.

11 Kisha wewe pamoja na Walawi na wageni wote walioko miongoni mwenu mtafurahi katika vitu vyote vizuri ambavyoBwanaMungu wenu amewapa pamoja na wa nyumbani mwenu.

12 Wakati utakapokuwa umeshatoa zaka zote za mazao yako katika mwaka wa tatu, ambao ni mwaka wa zaka, utampa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, ili waweze kula katika miji yenu na kushiba.

13 Kisha umwambieBwanaMungu wako: “Nimeondoa katika nyumba yangu ile sehemu iliyowekwa wakfu na nimempa Mlawi, mgeni, yatima na mjane, kulingana na yote uliyoamuru. Sijazihalifu amri zako wala kusahau hata mojawapo.

14 Sijala sehemu iliyowekwa wakfu wakati nilipokuwa nikiomboleza, wala sijaondoa mojawapo wakati nilipokuwa najisi, wala sijatoa sehemu yake yoyote kwa wafu. NimemtiiBwanaMungu wangu; nimefanya kila kitu ulichoniamuru.

15 Angalia chini kutoka mbinguni, maskani yako matakatifu, uwabariki watu wako Israeli pamoja na nchi uliyotupa kama ulivyoahidi kwa kiapo kwa baba zetu, nchi inayotiririka maziwa na asali.”

Fuata Maagizo Ya Bwana

16 BwanaMungu wako anakuagiza leo kufuata amri hizi na sheria; zishike kwa bidii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.

17 Umetangaza leo kwambaBwanandiye Mungu wako na kwamba utafuata njia zake, kwamba utayashika maagizo yake, amri zake na sheria zake nawe utamtii.

18 NayeBwanaametangaza leo kwamba ninyi ni taifa lake, hazina yake ya thamani kama alivyoahidi, ili kwamba mpate kuyashika maagizo yake yote.

19 Ametangaza kwamba atawaweka juu kuliko mataifa mengine aliyoyafanya katika sifa, kuwa fahari na heshima, na kwamba mtakuwa taifa takatifu kwaBwanaMungu wenu, kama alivyoahidi.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/DEU/26-beb6ce991e82a641bc01c2e5844202a8.mp3?version_id=1627—

Categories
Kumbukumbu

Kumbukumbu 27

Madhabahu Katika Mlima Ebali

1 Mose na wazee wa Israeli wakawaagiza watu: “Yashikeni maagizo haya yote ninayowaagiza leo.

2 Mtakapokuwa mmevuka Mto Yordani na kuingia katika nchi awapayoBwanaMungu wenu, msimamishe mawe makubwa na mkayatie lipu.

3 Andikeni juu yake maneno yote ya sheria hii wakati mtakapokuwa mmevuka na kuingia katika nchi awapayoBwanaMungu wenu, nchi itiririkayo maziwa na asali, kama vileBwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaahidi.

4 Mtakapokuwa mmevuka Yordani, simamisheni mawe haya juu ya Mlima Ebali, kama ninavyowaagiza leo, mkayatie lipu.

5 Huko mjengeeniBwanaMungu wenu madhabahu, madhabahu ya mawe. Msitumie kifaa chochote cha chuma juu yake.

6 Jengeni madhabahu yaBwanaMungu wenu kwa mawe ya shambani, na mtoe sadaka za kuteketezwa juu yake kwaBwanaMungu wenu.

7 Toeni sadaka za amani juu yake, mkizila na kufurahia mbele zaBwanaMungu wenu.

8 Nanyi mtaandika maneno yote ya sheria hii kwa wazi sana juu ya mawe haya ambayo mmesimamisha.”

Laana Kutoka Mlima Ebali

9 Kisha Mose na makuhani, ambao ni Walawi, wakawaambia Israeli wote, “Nyamaza ee Israeli, sikiliza! Sasa umekuwa taifa laBwanaMungu wako.

10 MtiiBwanaMungu wako, na kufuata amri zake na maagizo ninayokupa leo.”

11 Siku ile ile Mose akawaagiza watu:

12 Mtakapovuka Mto Yordani, makabila haya yatasimama juu ya Mlima Gerizimu kubariki watu: Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Yosefu na Benyamini.

13 Makabila haya yatasimama juu ya Mlima Ebali kwa kutamka laana: Reubeni, Gadi, Asheri, Zabuloni, Dani na Naftali.

14 Nao Walawi watawasomea watu wote wa Israeli kwa sauti kubwa:

15 “Alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga au mwenye kusubu sanamu, kitu ambacho ni chukizo kwaBwana, kazi ya mikono ya fundi stadi, na kuisimamisha kwa siri.”

Kisha watu wote watasema, “Amen!”

16 “Alaaniwe mtu amdharauye baba yake na mama yake.”

Kisha watu wote watasema, “Amen!”

17 “Alaaniwe mtu asogezaye jiwe la mpaka wa jirani yake.”

Kisha watu wote watasema, “Amen!”

18 “Alaaniwe mtu ampotoshaye kipofu njiani.”

Kisha watu wote watasema, “Amen!”

19 “Alaaniwe mtu apotoshaye haki ya mgeni, yatima au mjane.”

Kisha watu wote watasema, “Amen!”

20 “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mke wa baba yake, kwa maana anadharau malazi ya baba yake.”

Kisha watu wote watasema, “Amen!”

21 “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mnyama yeyote.”

Kisha watu wote watasema, “Amen!”

22 “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na dada yake, binti wa baba yake au binti wa mama yake.”

Kisha watu wote watasema, “Amen!”

23 “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mama mkwe wake.”

Kisha watu wote watasema, “Amen!”

24 “Alaaniwe mtu amuuaye jirani yake kwa siri.”

Kisha watu wote watasema, “Amen!”

25 “Alaaniwe mtu apokeaye rushwa ili kumuua mtu asiye na hatia.”

Kisha watu wote watasema, “Amen!”

26 “Alaaniwe mtu yule ambaye hatashikilia maneno ya sheria hii kwa kuyatekeleza.”

Kisha watu wote watasema, “Amen!”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/DEU/27-39b6836bc29112f6af7d77339696ec95.mp3?version_id=1627—

Categories
Kumbukumbu

Kumbukumbu 28

Baraka Za Utiifu

1 Kama ukimtiiBwanaMungu wako kwa bidii na kufuata amri zake zote ninazokupa leo kwa bidii,BwanaMungu wako atakuweka juu ya mataifa yote katika dunia.

2 Baraka hizi zote zitakuja juu yako na kukupata, kama ukimtiiBwanaMungu wako:

3 Utabarikiwa mjini na utabarikiwa mashambani.

4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na mazao ya nchi yako na wanyama wako wachanga wa kufugwa, yaani ndama wa makundi yako ya ngʼombe, na wana-kondoo wa makundi yako.

5 Kapu lako na vyombo vyako vya kukandia vitabarikiwa.

6 Utabarikiwa uingiapo na utabarikiwa utokapo.

7 Bwanaatasababisha adui wainukao dhidi yako kushindwa mbele yako. Watakujia kwa njia moja lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba.

8 Bwanaataagiza baraka juu ya ghala zako na juu ya kila kitu utakachogusa kwa mkono wako.BwanaMungu wako atakubariki katika nchi anayokupa.

9 Bwanaatakufanya kuwa taifa lake takatifu, kama alivyokuahidi kwa kiapo, kama ukishika maagizo yaBwanaMungu wako na kwenda katika njia zake.

10 Kisha mataifa yote ya dunia wataona kuwa unaitwa kwa jina laBwana, nao watakuogopa.

11 Bwanaatakupa kustawi kwa wingi, katika tunda la uzao wa tumbo lako, katika wanyama wachanga wa mifugo yako na katika mazao ya ardhi yako, katika nchi aliyowaapia baba zako kuwapa.

12 Bwanaatafungua mbingu, ghala zake za baraka, kukupa mvua kwa majira yake na kubariki kazi zako zote za mikono yako. Utakopesha mataifa mengi lakini hutakopa kwa yeyote.

13 Bwanaatakufanya kichwa, wala si mkia. Kama utazingatia maagizo yaBwanaMungu wako ninayokupa siku hii ya leo na kuyafuata kwa bidii, daima utakuwa juu, kamwe hutakuwa chini.

14 Usihalifu amri zangu zozote ninazokupa leo, kwa kwenda kuume au kushoto, kwa kufuata miungu mingine na kuitumikia.

Laana Kwa Kutokutii

15 Hata hivyo, kama hutamtiiBwanaMungu wako na kuzishika kwa bidii amri zake zote na maagizo ninayokupa leo, laana hizi zote zitakuja juu yako na kukupata:

16 Utalaaniwa mjini na utalaaniwa mashambani.

17 Kapu lako na chombo chako cha kukandia kitalaaniwa.

18 Uzao wa tumbo lako utalaaniwa, mazao ya ardhi yako, ndama wa makundi yako ya ngʼombe na wana-kondoo wa makundi yako.

19 Utalaaniwa uingiapo na utokapo.

20 Bwanaataleta laana juu yako, fadhaa na kukaripiwa katika kila kitu unachokigusa kwa mkono wako, mpaka uwe umeharibiwa na kuangamizwa ghafula kwa ajili ya maovu uliyoyafanya kwa kumwacha yeye.

21 Bwanaatakupiga kwa magonjwa mpaka akuangamize kutoka nchi unayoingia kuimiliki.

22 Bwanaatakupiga kwa magonjwa ya kudhoofisha, kwa homa na kuwashwa, hari na kwa ukame, kutu na kuwa na uchungu ambavyo vitakupiga mpaka uangamie.

23 Anga juu yako itakuwa shaba, na ardhi chini yako itakuwa chuma.

24 Bwanaatafanya mvua ya nchi yako kuwa mavumbi na mchanga; vitakujia kutoka angani mpaka uangamie.

25 Bwanaatakufanya ushindwe mbele ya adui zako. Utawajia kwa njia moja lakini utawakimbia mbele yao kwa njia saba, nawe utakuwa kitu cha kuchukiza kwa falme zote za dunia.

26 Mizoga yenu itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo mtu yeyote wa kuwafukuza.

27 Bwanaatakupiga kwa majipu ya Misri na kwa vidonda vitokavyo usaha na kuwashwa, ambako huwezi kuponywa.

28 Bwanaatakupiga kwa wazimu, upofu na kuchanganyikiwa kwa akili.

29 Wakati wa adhuhuri utapapasapapasa huku na huko kama mtu kipofu katika giza. Hutafanikiwa katika lolote ufanyalo; siku baada ya siku utaonewa na kunyangʼanywa, wala hakuna yeyote atakayekuokoa.

30 Utaposa mke, lakini mtu mwingine atakutana naye kimwili. Utajenga nyumba, lakini hutaishi ndani yake. Utapanda shamba la mizabibu, lakini hutakula matunda yake.

31 Ngʼombe wako atachinjwa mbele ya macho yako lakini hutakula nyama yake. Punda wako atachukuliwa kwa nguvu kutoka kwako wala hatarudishwa. Kondoo wako watapewa adui zako, wala hakuna mtu yeyote wa kuwaokoa.

32 Wanao na binti zako watatolewa kwa mataifa mengine, nawe utayachosha macho yako ukiwatazamia siku baada ya siku, hutakuwa na nguvu kuinua mkono.

33 Taifa usilolijua watakula mazao ya nchi yako na taabu ya kazi yako, hutakuwa na chochote, bali kuonewa kikatili siku zako zote.

34 Vitu utakavyoviona kwa macho yako vitakufanya wazimu.

35 Bwanaatayapiga magoti yako na miguu yako kwa majipu yenye maumivu makali yasiyoponyeka, yakienea kutoka nyayo za miguu yako hadi utosini.

36 Bwanaatakupeleka wewe na mfalme uliyemweka juu yako uende kwenye taifa ambalo hukulijua wewe wala baba zako. Huko utaabudu miungu mingine, miungu ya miti na mawe.

37 Utakuwa kitu cha kuchukiza, tena kitu cha kudharauliwa na kudhihakiwa kwa mataifa yote hukoBwanaatakakokupeleka.

38 Utapanda mbegu nyingi katika shamba lakini utavuna haba, kwa sababu nzige watazila.

39 Utapanda mashamba ya mizabibu na kuyapalilia, lakini hutakunywa divai yake wala hutakusanya zabibu, kwa sababu wadudu watazila.

40 Utakuwa na mizeituni katika nchi yako yote, lakini hutatumia hayo mafuta yake, kwa sababu zeituni zitapukutika.

41 Utakuwa na wana na binti lakini hawatakuwa nawe, kwa sababu watachukuliwa mateka.

42 Makundi ya nzige yatavamia miti yako yote na mazao ya nchi yako.

43 Mgeni anayeishi miongoni mwako atainuka juu zaidi na zaidi kuliko wewe, lakini wewe utashuka chini zaidi na zaidi.

44 Yeye atakukopesha, lakini wewe hutamkopesha. Yeye atakuwa kichwa, lakini wewe utakuwa mkia.

45 Laana hizi zote zitakuja juu yako. Zitakufuatia na kukupata mpaka uangamizwe, kwa sababu hukumtiiBwanaMungu wako, na kuzishika amri zake na maagizo yake aliyokupa.

46 Zitakuwa ishara na ajabu kwako na kwa wazao wako milele.

47 Kwa sababu hukumtumikiaBwanaMungu wako kwa furaha na kwa moyo wakati wa kufanikiwa kwako,

48 kwa hiyo katika njaa na kiu, katika uchi na umaskini wa kutisha, utawatumikia adui ambaoBwanaatawatuma dhidi yako. Yeye ataweka nira ya chuma shingoni mwako hadi amekwisha kukuangamiza.

49 Bwanaataleta taifa dhidi yako kutoka mbali, kutoka miisho ya dunia, kama tai ashukiavyo mawindo chini, taifa ambalo hutaijua lugha yake,

50 taifa lenye uso mkali lisilojali wazee wala kuwahurumia vijana.

51 Watakula wadogo wa mifugo yako na mazao ya nchi yako mpaka umeangamia. Hawatakuachia nafaka, divai mpya au mafuta, wala ndama wowote wa kundi lako au wana-kondoo wa kundi lako mpaka umekuwa magofu.

52 Nao wataizingira miji yote katika nchi yako mpaka kuta ndefu za ngome ambazo unazitegemea zimeanguka. Watazingira miji yote katika nchi ambayoBwanaMungu wako anakupa.

53 Utakula uzao wa tumbo lako, nyama ya wana wako na binti zako ambaoBwanaMungu wako amekupa, kwa sababu ya mateso yale adui zako watakayokuletea wakati wa kukuzingira.

54 Hata yule mtu muungwana sana na makini miongoni mwako hatakuwa na huruma kwa ndugu yake mwenyewe au kwa mke ampendaye au watoto wake waliosalia,

55 naye hatampa hata mmoja wao nyama ya watoto wake ambao anawala. Kwa kuwa hakuna kitu kingine kilichosalia kwake katika mazingirwa makali ambayo adui yako watakuletea kwa miji yako yote.

56 Mwanamke ambaye ni muungwana sana na makini miongoni mwako, yaani ambaye ni makini sana na muungwana kiasi kwamba asingethubutu kugusa ardhi kwa wayo wa mguu wake, yeye atakuwa mchoyo kwa mume ampendaye na mwanawe mwenyewe au binti yake,

57 kondoo wa nyuma kutoka kwenye tumbo lake na watoto anaowazaa. Kwa kuwa anakusudia kuwala kwa siri wakati wa kuzingirwa na katika taabu zile ambazo adui yako atazileta juu yako na miji yako.

58 Kama hutafuata kwa bidii maneno yote ya sheria hii, ambayo yameandikwa katika kitabu hiki na kama hutalicha hili jina la fahari na la kutisha, yaani laBwanaMungu wako,

59 Bwanaataleta mapigo ya kutisha juu yako na kwa wazao wako, maafa makali na ya kudumu, magonjwa mazito na ya kudumu.

60 Atakuletea juu yako magonjwa yote ya Misri yale uliyoyaogopa, nayo yataambatana nawe.

61 PiaBwanaatakuletea kila aina ya ugonjwa na maafa ambayo hayakuandikwa humu katika kitabu hiki cha sheria, mpaka utakapokuwa umeangamizwa.

62 Ninyi ambao mlikuwa wengi kama nyota za angani mtaachwa wachache tu, kwa sababu hamkumtiiBwanaMungu wenu.

63 Kama ilivyompendezaBwanakuwafanya ninyi mstawi na kuongezeka kwa idadi, ndivyo itakavyompendeza kuwaharibu na kuwaangamiza ninyi. Mtangʼolewa kutoka nchi mnayoiingia kuimiliki.

64 KishaBwanaatawatawanya miongoni mwa mataifa yote, kutoka mwisho mmoja wa dunia hadi mwingine. Huko mtaabudu miungu mingine, miungu ya miti na ya mawe, ambayo ninyi wala baba zenu hamkuijua.

65 Miongoni mwa mataifa hayo hamtapata raha wala mahali pa kupumzisha wayo wa mguu wenu. HukoBwanaatawapa mahangaiko ya mawazo, macho yaliyochoka kwa kungojea na moyo uliokata tamaa.

66 Utaishi katika mahangaiko siku zote, ukiwa umejaa hofu usiku na mchana, wala hutakuwa kamwe na uhakika wa maisha yako.

67 Wakati wa asubuhi utasema hivi, “Laiti ingekuwa jioni!” Jioni utasema, “Laiti ingekuwa asubuhi,” kwa sababu ya hofu ile itakayojaza moyo wako na vitu vile macho yako yatakavyoviona.

68 Bwanaatawarudisha tena Misri kwa meli, safari niliyosema kamwe hamngeenda tena. Huko mtajiuza ninyi wenyewe kwa adui zenu kama watumwa wa kiume na wa kike, lakini hakuna yeyote atakayewanunua.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/DEU/28-6fbea6aabb2e7d221f9ac2e45f31a268.mp3?version_id=1627—

Categories
Kumbukumbu

Kumbukumbu 29

Kufanya Upya Agano

1 Haya ndiyo maneno ya AganoBwanaaliyomwagiza Mose kufanya na Waisraeli huko Moabu, kuwa nyongeza ya Agano alilofanya nao huko Horebu.

2 Mose akawaita Waisraeli wote akawaambia:

Macho yenu yameona yale yoteBwanaaliyofanya kwa Mfalme Farao huko Misri, kwa maafisa wake wote na kwa nchi yake yote.

3 Kwa macho yenu wenyewe mliona yale majaribu makubwa, ishara zile za miujiza na maajabu makubwa.

4 Lakini mpaka leoBwanahajawapa akili ya kuelewa au macho yanayoona au masikio yanayosikia.

5 Kwa muda wa miaka arobaini niliyowaongoza jangwani, nguo zenu hazikuchakaa, wala viatu miguuni mwenu.

6 Hamkula mkate na hamkunywa divai wala kileo chochote. Nilifanya hivi ili mpate kujua kuwa mimi ndimiBwanaMungu wenu.

7 Wakati mlipofika mahali hapa, Sihoni mfalme wa Heshboni na Ogu mfalme wa Bashani walikuja kupigana dhidi yetu, lakini tuliwashinda.

8 Tuliichukua nchi yao na kuwapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase kama urithi wao.

9 Fuateni kwa bidii masharti ya Agano hili, ili kwamba mweze kustawi katika kila kitu mnachofanya.

10 Ninyi nyote leo mnasimama mbele zaBwanaMungu wenu; mkiwa viongozi na wakuu wenu, wazee na maafisa wenu, na wanaume wengine wote wa Israeli,

11 pamoja na watoto wenu, wake zenu na pia wageni waishio katika kambi zenu wanaowapasulia kuni na kuwachotea maji.

12 Mnasimama hapa ili kufanya Agano naBwanaMungu wenu, Agano ambalo Mungu analifanya nanyi siku hii ya leo na kulitia muhuri kwa kiapo,

13 kuwathibitisha ninyi siku hii ya leo kama taifa lake, ili aweze kuwa Mungu wenu kama alivyowaahidi na kama alivyowaapia baba zenu Abrahamu, Isaki na Yakobo.

14 Ninafanya Agano hili pamoja na kiapo chake, sio na ninyi tu

15 mnaosimama hapa na sisi leo mbele zaBwanaMungu wetu, bali pia pamoja na wale ambao hawapo hapa leo.

16 Ninyi wenyewe mnajua jinsi tulivyoishi nchini Misri na jinsi tulivyopita katikati ya nchi mpaka tukafika hapa.

17 Mliona miongoni mwao vinyago vyao vya kuchukiza na sanamu za miti na mawe, za fedha na dhahabu.

18 Hakikisheni kwamba hakuna mwanaume au mwanamke, ukoo au kabila miongoni mwenu leo ambalo moyo wake utamwachaBwanaMungu wetu, kwenda kuabudu miungu ya mataifa hayo. Hakikisheni hakuna mzizi miongoni mwenu unaotoa sumu chungu ya namna hii.

19 Wakati mtu wa namna hii asikiapo maneno ya kiapo hiki, hujibariki mwenyewe na kisha hufikiri, “Nitakuwa salama, hata kama nikiendelea kuifuata njia yangu mwenyewe.” Hili litaleta maafa juu ya nchi iliyonyeshewa sawasawa na nchi kame.

20 Bwanakamwe hatakuwa radhi kumsamehe, ghadhabu na wivu wa Mungu vitawaka dhidi ya mtu huyo. Laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki zitamwangukia naBwanaatafuta jina lake chini ya mbingu.

21 Bwanaatamtwaa peke yake kutoka makabila ya Israeli kwa maangamizo, kulingana na laana zote za Agano zilizoandikwa kwenye Kitabu hiki cha Sheria.

22 Watoto wako watakaofuata baada yako katika vizazi vya baadaye na wageni ambao watakuja kutoka nchi za mbali, wataona maafa, yaliyoipata nchi na magonjwa ambayoBwanaaliyaleta juu yake.

23 Nchi yote itakuwa jaa linaloungua la chumvi na kiberiti: hakutakuwa kilichopandwa, hakutakuwa kinachochipua, wala hakutakuwa mimea inayoota juu yake. Itakuwa kama maangamizo ya Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, ambazoBwanaaliangamiza kwa hasira kali.

24 Mataifa yote yatauliza: “Kwa niniBwanaamefanya hivi juu ya nchi hii? Kwa nini hasira hii kali ikawaka?”

25 Na jibu litakuwa: “Ni kwa sababu watu hawa waliacha Agano laBwana, Mungu wa baba zao, Agano alilofanya nao wakati alipowatoa katika nchi ya Misri.

26 Walienda zao na kuabudu miungu mingine na kuisujudia, miungu wasioijua, miungu ambayo Mungu hakuwapa.

27 Kwa hiyo hasira yaBwanaikawaka dhidi ya nchi hii, hivyo Mungu akaleta juu yake laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki.

28 Katika hasira kali na katika ghadhabu kuuBwanaaliwangʼoa kutoka nchi yao na kuwasukumia katika nchi nyingine, kama ilivyo sasa.”

29 Mambo ya siri ni yaBwanaMungu wetu, bali yaliyofunuliwa ni yetu na watoto wetu milele, ili tuweze kuyafanya maneno yote ya sheria hii.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/DEU/29-641d211a50d6b7fe9da4756f972f2499.mp3?version_id=1627—

Categories
Kumbukumbu

Kumbukumbu 30

Mafanikio Baada Ya Kumgeukia Bwana

1 Wakati baraka hizi zote pamoja na laana nilizoziweka mbele yako zitakapokujia, nawe ukazitafakari moyoni popoteBwanaMungu wako atakapokutawanya miongoni mwa mataifa,

2 hapo wewe na watoto wako mtakapomrudiaBwanaMungu wako, na kumtii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote kulingana na kila kitu ninachokuamuru leo,

3 ndipoBwanaMungu wako atakapokurudisha kutoka utumwani na kukuhurumia, naye atakukusanya tena kutoka mataifa yote kule alikutawanya.

4 Hata kama umefukuziwa katika nchi ya mbali kiasi gani chini ya mbingu, kutoka hukoBwanaMungu wako atakukusanya na kukurudisha.

5 YeyeBwanaatakurudisha katika nchi iliyokuwa mali ya baba zako, nawe utaimiliki. Naye atakufanya ufanikiwe sana na kukuzidisha kwa idadi kuliko baba zako.

6 BwanaMungu wako ataitahiri mioyo yenu na mioyo ya wazao wenu ili mweze kumpenda kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote ukaishi.

7 BwanaMungu wako ataweka laana hizi zote juu ya adui zako ambao wanakuchukia na kukutesa.

8 Utamtii tenaBwanana kuzishika amri zake zote ninazokupa leo.

9 NdipoBwanaMungu wako atakapokufanikisha sana katika kazi zote za mikono yako na katika uzao wa tumbo lako, wadogo wa mifugo yako na mazao ya nchi yako.Bwanaatakufurahia tena na kukufanikisha, kama alivyowafurahia baba zako,

10 kama ukimtiiBwanaMungu wako, na kuzishika amri zake na maagizo yake ambayo yameandikwa katika Kitabu hiki cha Sheria, na kumgeukiaBwanaMungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.

Uzima Na Mauti

11 Ninachokuagiza leo sio kigumu sana kwako au usichokiweza.

12 Hakiko juu mbinguni, ili uulize, “Ni nani atakayepanda mbinguni kukileta na kututangazia ili tuweze kutii?”

13 Wala hakiko ngʼambo ya bahari, ili uulize, “Ni nani atakayevuka bahari kwenda kukichukua na kututangazia ili tupate kutii?”

14 La hasha! Lile neno liko karibu sana nawe; liko kinywani mwako na ndani ya moyo wako ili uweze kulitii.

15 Tazama, naweka mbele yako leo uzima na mafanikio, mauti na maangamizo.

16 Ninakuamuru leo kwamba umpendeBwanaMungu wako, utembee katika njia zake, na kutunza maagizo yake, amri na sheria zake; ndipo utakapoishi na kuongezeka, nayeBwanaMungu wako atakubariki katika nchi unayoingia kuimiliki.

17 Lakini kama moyo wako ukigeukia mbali ukawa huna utii, kama umevutwa kuisujudia miungu mingine na kuiabudu,

18 nakutangazia leo hii kwamba hakika utaangamizwa. Hutaishi maisha marefu katika nchi unayovuka Yordani kuiingia na kuimiliki.

19 Leo ninaziita mbingu na nchi kama mashahidi dhidi yako kwamba nimeweka mbele yako uzima na mauti, baraka na laana. Basi sasa chagueni uzima, ili wewe na watoto wako mpate kuishi,

20 na ili upate kumpendaBwanaMungu wako, uisikilize sauti yake na kuambatana naye. Kwa kuwaBwanandiye uzima wako, na atakupa wingi wa siku ili upate kuishi katika nchi aliyoapa kuwapa baba zako Abrahamu, Isaki na Yakobo.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/DEU/30-7e4558bdab08c84d5d0739a04ab37b77.mp3?version_id=1627—

Categories
Kumbukumbu

Kumbukumbu 31

Yoshua Kutawala Baada Ya Mose

1 Kisha Mose akaenda akasema maneno haya kwa Waisraeli wote:

2 “Sasa nina miaka mia moja na ishirini nami siwezi tena kuwaongoza.Bwanaameniambia, ‘Hutavuka Yordani.’

3 BwanaMungu wenu, yeye mwenyewe atavuka mbele yenu. Ataangamiza mataifa haya mbele yenu, nanyi mtaimiliki nchi yao. Pia Yoshua atavuka mbele yenu, kamaBwanaalivyosema.

4 NayeBwanaatawafanyia watu hao kile alichowafanyia Sihoni na Ogu, wafalme wa Waamori, ambao aliwaangamiza pamoja na nchi yao.

5 Bwanaatawakabidhi kwenu, nanyi lazima mwatendee yale yote niliyowaamuru.

6 Kuweni imara na moyo wa ushujaa. Msiogope wala msifadhaike kwa sababu yao, kwa kuwaBwanaMungu wenu anakwenda pamoja nanyi; kamwe hatawaacha wala hatawatupa ninyi.”

7 Kisha Mose akamwita Yoshua na akamwambia mbele ya Israeli wote, “Uwe imara na moyo wa ushujaa, kwa kuwa ni lazima uende na watu hawa katika nchi ileBwanaaliyowaapia baba zao kuwapa, nawe ni lazima uwagawie kama urithi wao.

8 Bwanamwenyewe atakutangulia naye atakuwa pamoja nawe; kamwe hatakuacha wala hatakutupa. Usiogope, wala usifadhaike.”

Kusoma Sheria

9 Kwa hiyo Mose akaandika sheria hii na kuwapa makuhani, wana wa Lawi, waliochukua Sanduku la Agano laBwanana wazee wote wa Israeli.

10 Kisha Mose akawaamuru, akasema: “Mwishoni mwa kila miaka saba, katika mwaka wa kufuta madeni, wakati wa Sikukuu ya Vibanda,

11 Waisraeli wote wanapokuja mbele zaBwanaMungu wenu mahali atakapopachagua, utasoma sheria hii mbele yao masikioni mwao.

12 Kusanya watu wote, wanaume, wanawake, watoto na wageni wanaoishi katika miji yenu, ili waweze kusikia na kujifunza kumchaBwanaMungu wenu na kufuata kwa bidii maneno yote ya sheria hii.

13 Watoto wao, ambao hawaijui sheria hii, lazima waisikie na kujifunza kumchaBwanaMungu wenu kwa muda mtakaoishi katika nchi mnayovuka Yordani kuimiliki.”

Kuasi Kwa Waisraeli Kunatabiriwa

14 Bwanaakamwambia Mose, “Sasa siku ya kifo chako imekaribia. Mwite Yoshua, mkajihudhurishe katika Hema la Kukutania, mahali nitakapompa maagizo ya kazi.” Kwa hiyo Mose na Yoshua wakaja na kujihudhurisha kwenye Hema la Kukutania.

15 KishaBwanaakatokea katika Hema katika nguzo ya wingu, nalo wingu likasimama juu ya ingilio la Hema.

16 KishaBwanaakamwambia Mose: “Unakwenda kupumzika na baba zako, nao watu hawa hivi karibuni watazini na miungu migeni ya nchi wanayoingia. Wataniacha na kuvunja Agano nililofanya nao.

17 Siku hiyo nitawakasirikia na kuwaacha; nitawaficha uso wangu, nao wataangamizwa. Maafa mengi na shida nyingi zitakuja juu yao, nao siku hiyo watauliza, ‘Je, maafa haya hayakuja juu yetu kwa sababu Mungu wetu hayuko pamoja nasi?’

18 Nami hakika nitauficha uso wangu siku hiyo kwa sababu ya maovu yao yote kwa kugeukia miungu mingine.

19 “Sasa ujiandikie wimbo huu,uwafundishe Waisraeli na uwaamuru wauimbe, ili upate kuwa ushahidi wangu dhidi yao.

20 Nitakapokwisha kuwaingiza katika nchi itiririkayo maziwa na asali, nchi niliyowaahidi baba zao kwa kiapo, nao watakapokula wakashiba na kufanikiwa, watageukia miungu mingine na kuiabudu, wakinikataa mimi na kuvunja Agano langu.

21 Maafa na shida zitakapokuja juu yao, wimbo huu utashuhudia dhidi yao, kwa sababu hautasahauliwa na wazao wao. Ninajua lile wanaloandaa kufanya, hata kabla sijawaingiza katika nchi niliyowaahidi kwa kiapo.”

22 Hivyo Mose akaandika wimbo huu siku ile na akawafundisha Waisraeli.

23 Bwanaakampa Yoshua mwana wa Nuni agizo hili: “Uwe hodari na shujaa, kwa kuwa utawaleta Waisraeli katika nchi niliyowaahidi kwa kiapo, nami mwenyewe nitakuwa pamoja nawe.”

24 Baada ya Mose kumaliza kuandika kwenye kitabu maneno ya sheria hii kutoka mwanzo hadi mwisho,

25 akawapa Walawi wale waliolibeba Sanduku la Agano laBwanaagizo hili, akawaambia:

26 “Chukueni Kitabu hiki cha Sheria mkakiweke kando ya Sanduku la Agano laBwanaMungu wenu. Hapo ndipo kitakapokaa kama shahidi dhidi yenu.

27 Kwa kuwa ninajua jinsi mlivyo waasi na mlivyo na shingo ngumu. Kama mmekuwa mkiasi dhidi yaBwananikiwa bado niko hai na nikiwa pamoja nanyi, mtaasi mara ngapi baada ya kufa kwangu!

28 Kusanyeni mbele yangu wazee wote wa makabila yenu na maafisa wenu wote, ili nipate kusema maneno haya masikioni mwao na kuziita mbingu na nchi ili kushuhudia dhidi yao.

29 Kwa kuwa ninajua baada ya kifo changu hakika mtakuwa waovu kabisa na kugeuka kutoka njia niliyowaamuru ninyi. Katika siku zijazo, maafa yatawapata kwa sababu mtafanya maovu mbele ya macho yaBwana, na kuchochea hasira yake kwa yale mikono yenu itakayokuwa imefanya.”

Wimbo Wa Mose

30 Mose akayasoma maneno ya wimbo huu kutoka mwanzo hadi mwisho katika masikio ya kusanyiko lote la Israeli:

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/DEU/31-352d8c8e6fa80c4366c1ca104f0630c5.mp3?version_id=1627—

Categories
Kumbukumbu

Kumbukumbu 32

1 Sikilizeni, enyi mbingu, nami nitasema;

sikia, ee nchi, maneno ya kinywa changu.

2 Mafundisho yangu na yanyeshe kama mvua,

na maneno yangu na yashuke kama umande,

kama manyunyu juu ya majani mabichi,

kama mvua tele juu ya mimea myororo.

3 Nitalitangaza jina laBwana.

Naam, sifuni ukuu wa Mungu wetu!

4 Yeye ni Mwamba, kazi zake ni kamilifu,

njia zake zote ni haki.

Mungu mwaminifu ambaye hakosei,

yeye ni mnyofu na mwenye haki.

5 Wamefanya mambo ya upotovu mbele zake;

kwa aibu yao, wao si watoto wake tena,

lakini ni kizazi kilicho kiovu na kilichopotoka.

6 Je, hii ndiyo njia ya kumlipaBwana,

enyi watu wajinga na wasio na busara?

Je, yeye siye Baba yenu, Muumba wenu,

aliyewafanya ninyi na kuwaumba?

7 Kumbuka siku za kale;

tafakari vizazi vya zamani vilivyopita.

Uliza baba yako, naye atakuambia,

wazee wako, nao watakueleza.

8 Aliye Juu Sana alipowapa mataifa urithi wao,

alipogawanya wanadamu wote,

aliweka mipaka kwa ajili ya mataifa

sawasawa na hesabu ya wana wa Israeli.

9 Kwa kuwa fungu laBwanani watu wake,

Yakobo kura yake ya urithi.

10 Katika nchi ya jangwa alimkuta,

katika nyika tupu ivumayo upepo.

Alimhifadhi na kumtunza;

akamlinda kama mboni ya jicho lake,

11 kama tai avurugaye kiota chake,

na kurukaruka juu ya makinda yake,

ambaye hutanda mabawa yake kuwadaka,

na huwachukua kwenye mabawa yake.

12 Bwanapeke yake alimwongoza;

hakuwepo mungu mgeni pamoja naye.

13 Akamfanya apande sehemu zilizoinuka za nchi,

akamlisha kwa mavuno ya mashamba.

Akamlea kwa asali toka mwambani,

na kwa mafuta kutoka mwamba mgumu,

14 kwa jibini na maziwa kutoka makundi ya ngʼombe

na kutoka makundi ya mbuzi,

kwa mafuta ya wana-kondoo na mbuzi,

kwa kondoo dume wazuri wa Bashani,

na kwa ngano nzuri.

Ukanywa damu ya zabibu inayotoa povu.

15 Yeshurunialinenepa na kupiga teke;

alikuwa na chakula tele,

akawa mzito na akapendeza sana.

Akamwacha Mungu aliyemuumba,

na kumkataa Mwamba Mwokozi wake.

16 Wakamfanya Mungu kuwa na wivu kwa miungu yao migeni,

na kumkasirisha kwa sanamu zao

za machukizo.

17 Wakatoa dhabihu kwa pepo, ambao si Mungu:

miungu wasiyoijua,

miungu iliyojitokeza siku za karibuni,

miungu ambayo baba zenu hawakuiogopa.

18 Mkamwacha Mwamba, aliyewazaa ninyi;

mkamsahau Mungu aliyewazaa.

19 Bwanaakaona hili, akawakataa,

kwa sababu alikasirishwa

na wanawe na binti zake.

20 Akasema, “Nitawaficha uso wangu,

nami nione mwisho wao utakuwa nini,

kwa kuwa wao ni kizazi kilichopotoka,

watoto ambao si waaminifu.

21 Wamenifanya niwe na wivu

kwa kile ambacho si mungu,

na kunikasirisha kwa sanamu zao

zisizokuwa na thamani.

Nitawafanya wawaonee wivu wale ambao si taifa.

Nitawafanya wakasirishwe

na taifa lile lisilo na ufahamu.

22 Kwa maana moto umewashwa kwa hasira yangu,

ule uwakao hadi kwenye vina vya mauti.

Utateketeza dunia pamoja na mazao yake,

na kuwasha moto katika misingi ya milima.

23 “Nitalundika majanga juu yao

na kutumia mishale yangu dhidi yao.

24 Nitatuma njaa kali dhidi yao maradhi mabaya,

yateketezayo na tauni ya kufisha;

nitawapelekea meno makali ya wanyama mwitu,

na sumu ya nyoka wale watambaao mavumbini.

25 Barabarani upanga utawakosesha watoto;

nyumbani mwao hofu itatawala.

Vijana wao wa kiume na wa kike wataangamia,

pia watoto wachanga na wazee wenye mvi.

26 Nilisema ningewatawanya

na kufuta kumbukumbu lao

katika mwanadamu.

27 Lakini nilihofia dhihaka za adui,

adui asije akashindwa kuelewa,

na kusema, ‘Mikono yetu imeshinda;

Bwanahakufanya yote haya.’ ”

28 Wao ni taifa lisilo na akili,

hakuna busara ndani yao.

29 Laiti wangekuwa na hekima wangefahamu hili,

na kutambua mwisho wao utakuwa aje!

30 Mtu mmoja angewezaje kufukuza elfu moja,

au wawili kufukuza elfu kumi,

kama si kwamba Mwamba wao amewauza,

kama si kwambaBwanaamewaacha?

31 Kwa kuwa mwamba wao si kama Mwamba wetu,

sawasawa na vile adui zetu wanavyokiri.

32 Mzabibu wao unatoka kwenye mzabibu wa Sodoma,

na kutoka kwenye mashamba ya Gomora.

Zabibu zake zimejaa sumu,

na vishada vyake vimejaa uchungu.

33 Mvinyo wao ni sumu ya nyoka,

sumu yenye kufisha ya swila.

34 “Je, hili sikuliweka akiba

na kulifungia kwenye vyumba vyangu vya hazina?

35 Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza.

Wakati utakapowadia, mguu wao utateleza;

siku yao ya maafa ni karibu,

na maangamizo yao yanawajia haraka.”

36 Bwanaatawahukumu watu wake,

na kuwahurumia watumishi wake

atakapoona nguvu zao zimekwisha

wala hakuna yeyote aliyebaki,

mtumwa au aliye huru.

37 Atasema: “Sasa iko wapi miungu yao,

mwamba walioukimbilia,

38 miungu wale waliokula mafuta ya dhabihu zao

na kunywa mvinyo wa sadaka zao za vinywaji?

Wainuke basi, wawasaidie!

Wawapeni basi ulinzi!

39 “Tazama basi, Mimi mwenyewe, Mimi Ndiye!

Hakuna mungu mwingine ila Mimi.

Mimi ninaua na Mimi ninafufua,

Mimi nimejeruhi na Mimi nitaponya,

wala hakuna awezaye kuokoa kutoka mkononi mwangu.

40 Ninainua mkono wangu kuelekea mbinguni na kusema:

Hakika kama niishivyo milele,

41 wakati ninapounoa upanga wangu unaometameta

na mkono wangu unapoushika ili kutoa hukumu,

nitalipiza kisasi juu ya adui zangu

na kuwalipiza wale wanaonichukia.

42 Nitailevya mishale yangu kwa damu,

wakati upanga wangu ukitafuna nyama:

damu ya waliochinjwa pamoja na mateka,

vichwa vya viongozi wa adui.”

43 Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake,

kwa kuwa atailipiza damu ya watumishi wake,

atalipiza kisasi juu ya adui zake

na kufanya upatanisho

kwa ajili ya nchi na watu wake.

44 Mose na Yoshuamwana wa Nuni wakaja, wakanena maneno yote ya wimbo watu wakiwa wanasikia.

45 Mose alipomaliza kuyasoma maneno haya yote kwa Israeli wote,

46 akawaambia, “Yawekeni moyoni maneno yote ambayo nimewatangazia kwa makini siku hii ya leo, ili kwamba mpate kuwaagiza watoto wenu wayatii kwa bidii maneno yote ya sheria hii.

47 Siyo maneno matupu tu kwenu, bali ni uzima wenu. Kwa hayo mtaishi maisha marefu katika nchi mnayovuka Yordani kuimiliki.”

Mose Aelezwa Kuhusu Kifo Chake

48 Siku hiyo hiyoBwanaakamwambia Mose,

49 “Kwea katika mapangano ya Mlima Abarimu hadi kilima cha Nebo kilichoko Moabu, ngʼambo ya Yeriko, na uitazame Kanaani, nchi ninayowapa Waisraeli kama milki yao wenyewe.

50 Utafia kwenye mlima huo unaokwea na kukusanyika pamoja na watu wako, kama ndugu yako Aroni alivyofia juu ya Mlima Hori naye akakusanyika kwa watu wake.

51 Hii ni kwa sababu ninyi wawili mlivunja uaminifu nami mbele ya Waisraeli kwenye maji ya Meriba-Kadeshi katika Jangwa la Sini, na kwa sababu hamkuuinua utakatifu wangu miongoni mwa Waisraeli.

52 Kwa hiyo, utaiona tu nchi kwa mbali; wewe hutaingia nchi ninayowapa watu wa Israeli.”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/DEU/32-58ef675860feeb6b511494e672a545f8.mp3?version_id=1627—