Categories
2 Timotheo

2 Timotheo Utangulizi

Utangulizi

Huu ulikuwa waraka wa mwisho kabisa wa Paulo. Baada ya kuandika waraka wa kwanza kwa Timotheo msaidizi wake, Paulo alikamatwa na kurudishwa gerezani huko Rumi. Katika waraka huu, Paulo alihisi fursa zake za kuhubiri Injili zilikuwa zikifikia kikomo. Alimkumbusha Timotheo kwamba hata kama maisha yake hapa duniani yangekoma, Mungu alikuwa amemwandalia maisha ya milele. Paulo pia alimkumbusha juu ya uaminifu wa Mungu ambaye alikuwa amemwongoza katika maisha yake yote. Aligusia nyakati za hatari ambazo zingekuja, na siku za taabu ambapo watu wangeiacha kweli na kupenda anasa kuliko kumpenda Mungu.

Alijitahidi kumtia moyo Timotheo na kumwimarisha kwa ajili ya kazi kubwa aliyokabidhiwa. Paulo alitamani kumwona Timotheo tena, akimwomba amletee vile vitabu alivyokuwa ameviacha Troa.

Mwandishi

Mtume Paulo.

Kusudi

Kumpa maelekezo ya mwisho, na kumtia moyo Timotheo, mchungaji wa kanisa la Efeso.

Mahali

Rumi.

Tarehe

Kati ya 66-67 B.K.

Wahusika Wakuu

Paulo, Timotheo, Luka, Marko.

Wazo Kuu

Barua hii inazungumzia uweza wa Mungu juu ya vitu vyote. Ingawa kuna mateso ambayo yataendelea kuongezeka, Mungu bado anatawala.

Mambo Muhimu

Kumwelekeza Timotheo ajitahidi kujionyesha kuwa amekubalika na Mungu, mtendakazi asiye na sababu ya kuona aibu, akilitumia kwa usahihi neno la kweli.

Mgawanyo

Shukrani za Paulo kwa ajili ya Timotheo (

1:1-5

)

Maagizo ya Paulo kwa Timotheo (

1:6–2:2

)

Sifa za mtumishi mwaminifu (

2:3-26

)

Mateso yajayo (

3:1-17

)

Maneno ya mwisho (

4:1-22

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *