Categories
Zaburi

Zaburi 11

Kumtumaini Bwana

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 KwaBwananinakimbilia,

unawezaje basi kuniambia:

“Ruka kama ndege kwenye mlima wako.

2 Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao,

huweka mishale kwenye uzi wake,

wakiwa gizani ili kuwapiga

wale wanyofu wa moyo.

3 Wakati misingi imeharibiwa,

mwenye haki anaweza kufanya nini?”

4 Bwanayuko ndani ya Hekalu lake takatifu;

Bwanayuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni.

Huwaangalia wana wa watu,

macho yake yanawajaribu.

5 Bwanahuwajaribu wenye haki,

lakini waovu na wanaopenda jeuri,

nafsi yake huwachukia.

6 Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali

na kiberiti kinachowaka,

upepo wenye joto kali ndio fungu lao.

7 Kwa kuwaBwanani mwenye haki,

yeye hupenda haki.

Wanyofu watauona uso wake.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/11-5c07d8f7f91202ea2f0e5f2cfada8510.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *