Sala Ya Kuomba Msaada
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 Mpaka lini, EeBwana? Je, utanisahau milele?
Utanificha uso wako mpaka lini?
2 Nitapambana na mawazo yangu mpaka lini,
na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu?
Adui zangu watanishinda mpaka lini?
3 Nitazame, unijibu, EeBwanaMungu wangu.
Yatie nuru macho yangu,
ama sivyo nitalala usingizi wa mauti.
4 Adui yangu atasema, “Nimemshinda,”
nao adui zangu watashangilia nitakapoanguka.
5 Lakini ninategemea upendo wako usiokoma;
moyo wangu unashangilia katika wokovu wako.
6 NitamwimbiaBwana,
kwa kuwa amekuwa mwema kwangu.
—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/13-e4324ab50d31ef0ba6d185a93f9159ae.mp3?version_id=1627—