Categories
Zaburi

Zaburi 14

Uovu Wa Wanadamu

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 Mpumbavu anasema moyoni mwake,

“Hakuna Mungu.”

Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa;

hakuna hata mmoja atendaye mema.

2 Bwanaanawachungulia wanadamu chini

kutoka mbinguni

aone kama wako wenye akili,

wowote wanaomtafuta Mungu.

3 Wote wamepotoka,

wameharibika wote pamoja,

hakuna atendaye mema.

Naam, hakuna hata mmoja!

4 Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza:

wale ambao huwala watu wangu

kama watu walavyo mkate,

hao ambao hawamwitiBwana?

5 Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu,

maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.

6 Ninyi watenda mabaya mnakwamisha mipango ya maskini,

baliBwanandiye kimbilio lao.

7 Laiti wokovu wa Israeli

ungalikuja kutoka Sayuni!

WakatiBwanaarejeshapo

wafungwa wa watu wake,

Yakobo na ashangilie,

Israeli na afurahi!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/14-dc78f06060b2adf0d54a4e409f70b76f.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *