Uovu Wa Wanadamu
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 Mpumbavu anasema moyoni mwake,
“Hakuna Mungu.”
Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa;
hakuna hata mmoja atendaye mema.
2 Bwanaanawachungulia wanadamu chini
kutoka mbinguni
aone kama wako wenye akili,
wowote wanaomtafuta Mungu.
3 Wote wamepotoka,
wameharibika wote pamoja,
hakuna atendaye mema.
Naam, hakuna hata mmoja!
4 Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza:
wale ambao huwala watu wangu
kama watu walavyo mkate,
hao ambao hawamwitiBwana?
5 Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu,
maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.
6 Ninyi watenda mabaya mnakwamisha mipango ya maskini,
baliBwanandiye kimbilio lao.
7 Laiti wokovu wa Israeli
ungalikuja kutoka Sayuni!
WakatiBwanaarejeshapo
wafungwa wa watu wake,
Yakobo na ashangilie,
Israeli na afurahi!
—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/14-dc78f06060b2adf0d54a4e409f70b76f.mp3?version_id=1627—