Mataifa Yahimizwa Kumsifu Mungu
Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za muziki. Zaburi. Wimbo.
1 Mungu aturehemu na kutubariki,
na kutuangazia nuru za uso wake,
2 ili njia zako zijulikane duniani,
wokovu wako katikati ya mataifa yote.
3 Ee Mungu, mataifa na wakusifu,
mataifa yote na wakusifu.
4 Mataifa yote wafurahi na kuimba kwa shangwe,
kwa kuwa unatawala watu kwa haki
na kuongoza mataifa ya dunia.
5 Ee Mungu, mataifa na wakusifu,
mataifa yote na wakusifu.
6 Ndipo nchi itatoa mazao yake,
naye Mungu, Mungu wetu, atatubariki.
7 Mungu atatubariki
na miisho yote ya dunia itamcha yeye.
—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/67-2c582af6264c83c4cba031743f9b97c6.mp3?version_id=1627—