Categories
Zaburi

Zaburi 70

Kuomba Msaada

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Maombi.

1 Ee Mungu, ufanye haraka kuniokoa;

EeBwana, njoo hima unisaidie.

2 Wale wanaotafuta kuuondoa uhai wangu,

waaibishwe na kufadhaishwa;

wote wanaotamani kuangamizwa kwangu,

warudishwe nyuma kwa aibu.

3 Wale waniambiao, “Aha! Aha!”

warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao.

4 Lakini wote wakutafutao

washangilie na kukufurahia,

wale wapendao wokovu wako siku zote waseme,

“Mungu na atukuzwe!”

5 Lakini bado mimi ni maskini na mhitaji;

Ee Mungu, unijie haraka.

Wewe ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu;

EeBwana, usikawie.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/70-098f2b592afdfeb0c290fdafa03c8c88.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *