Kumsifu Bwana Kwa Wema Wake
1 MsifuniBwana.
Enyi watumishi waBwanamsifuni,
lisifuni jina laBwana.
2 Jina laBwanana lisifiwe,
sasa na hata milele.
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake,
jina laBwanalinapaswa kusifiwa.
4 Bwanaametukuka juu ya mataifa yote,
utukufu wake juu ya mbingu.
5 Ni nani aliye kamaBwanaMungu wetu,
Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 ambaye huinama atazame chini
aone mbingu na nchi?
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini,
na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 huwaketisha pamoja na wakuu,
pamoja na wakuu wa watu wake.
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake,
akiwa mama watoto mwenye furaha.
MsifuniBwana.
—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/113-53c3869e1e1a9355715e21b5247d5f73.mp3?version_id=1627—