Categories
Zaburi

Zaburi Utangulizi

Utangulizi

Jina la kitabu hiki kwa Kiebrania ni “Sepher Tehillim,” maana yake “Nyimbo za Sifa.” Jina la Kiyunani ni “Psalmoi,” yaani “Nyimbo zinazoandamana na ala za uimbaji za nyuzi,” na ndiyo kiini cha kitabu hiki. Kila sura ya 150 za kitabu hiki ni ya kipekee tena imekamilika, isipokuwa chache tu.

Zaburi zinaleta hisia mbalimbali kama vile misisimko, hali na mivuto mikubwa tofauti. Kwa kuwa Zaburi zinatokana na uzoefu wa kibinafsi kutoka asili pana hivyo, bado zimekuwa na mvuto mkubwa ulimwenguni wote kwa miaka mingi hivi tangu ziandikwe.

Mara kwa mara Zaburi zimeainishwa kwa kufuata namna fulani za maelezeo au mafundisho. Baadhi ya mapendekezo ya aina zenyewe, na mifano yake ambayo inaweza kuwa msaada mkubwa katika kujifunza zaidi ni kama ifuatavyo:

Kawaida ya ibada na sala

120–130

Kuhusu Masiya

2

16

22

25

69

110

Kuomba toba

6

32

51

Kumkaribia Mungu binafsi

23

27

37

Historia

78

105–106

Kumsifu Mungu

95

100

146–150

Maombi ya mwenye haki

17

20

40

55

Kuna uwezekano mkubwa kwamba makusanyo ya awali yalifanywa na Daudi. Nyongeza nyingine na mpangilio inawezekana vilifanywa na Solomoni, Yehoshafati, Hezekia, Yosia na wengine.

Mwandishi

Daudi: 73, Asafu: 12, Wana wa Kora: 10, Mose: 1, Hemani: 1, Ethani: 1, Solomoni: 2, Hazijulikani: 50.

Kusudi

Kuelezea umuhimu wa mashairi katika sifa, kuabudu na kukiri dhambi mbele za Mungu.

Mahali

Palestina na Babeli.

Tarehe

Kati ya wakati wa Mose (1440 K.K.) na wakati wa utumwa wa Babeli (586 K.K.).

Wahusika Wakuu

Daudi, Asafu, Wana wa Kora, Mose, Hemani na Solomoni.

Wazo Kuu

Kusifu ni kutambua na kutangaza ukuu wa Mungu, kufurahia na kudhihirisha wema wake.

Mambo Muhimu

Zaburi zimeelezea ufunuo wa Mungu, uumbaji, hali ya mwanadamu, wokovu, dhambi na uovu, toba, haki na uadilifu, kuabudu na kusifu, maombi na hukumu.

Mgawanyo

Kitabu I:

1–41

Kitabu II:

42–72

Kitabu III:

73–89

Kitabu IV:

90–106

Kitabu V:

107–150

.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *