Categories
Zaburi

Zaburi 96

Mungu Mfalme Mkuu

1 MwimbieniBwanawimbo mpya;

mwimbieniBwanadunia yote.

2 MwimbieniBwana, lisifuni jina lake;

tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.

3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa,

matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.

4 Kwa kuwaBwanani mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote;

yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.

5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu,

lakiniBwanaaliziumba mbingu.

6 Fahari na enzi viko mbele yake;

nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.

7 MpeniBwana, enyi jamaa za mataifa,

mpeniBwanautukufu na nguvu.

8 MpeniBwanautukufu unaostahili jina lake;

leteni sadaka na mje katika nyua zake.

9 MwabuduniBwanakatika uzuri wa utakatifu wake;

dunia yote na itetemeke mbele zake.

10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwanaanatawala.”

Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa;

atawahukumu watu kwa uadilifu.

11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi;

bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;

12 mashamba na yashangilie,

pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.

Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;

13 itaimba mbele zaBwanakwa maana anakuja,

anakuja kuihukumu dunia.

Ataihukumu dunia kwa haki,

na mataifa katika kweli yake.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/96-a54c28136746e51ea86d1c4f8707af2d.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *