Categories
Zaburi

Zaburi 64

Kuomba Ulinzi Dhidi Ya Maadui

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu,

uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.

2 Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu,

kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.

3 Wananoa ndimi zao kama panga

na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.

4 Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia,

humrushia ghafula bila woga.

5 Kila mmoja humtia moyo mwenzake

katika mipango mibaya;

huzungumza juu ya kuficha mitego yao,

nao husema, “Ni nani ataiona?”

6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema,

“Tumebuni mpango mkamilifu!”

Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.

7 Bali Mungu atawapiga kwa mishale,

nao ghafula wataangushwa.

8 Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao

na kuwaleta kwenye maangamizi;

wote wawaonao watatikisa vichwa vyao

kwa dharau.

9 Wanadamu wote wataogopa,

watatangaza kazi za Mungu

na kutafakari yale aliyoyatenda.

10 Wenye haki na wafurahi katikaBwana,

na wakimbilie kwake;

wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/64-0954e5e1243e91350d7b817e5d554bc1.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *