Kuomba Ulinzi Wa Mungu Kutokana Na Adui
Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Wakati Wazifu walimwendea Sauli na kumjulisha, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu?”
1 Ee Mungu uniokoe kwa jina lako,
unifanyie hukumu kwa uwezo wako.
2 Ee Mungu, sikia maombi yangu,
usikilize maneno ya kinywa changu.
3 Wageni wananishambulia,
watu wakatili wanayatafuta maisha yangu,
watu wasiomjali Mungu.
4 Hakika Mungu ni msaada wangu,
Bwana ndiye anayenitegemeza.
5 Mabaya na yawarudie wale wanaonisingizia,
kwa uaminifu wako uwaangamize.
6 Nitakutolea dhabihu za hiari;
EeBwana, nitalisifu jina lako
kwa kuwa ni vyema.
7 Kwa maana ameniokoa katika shida zangu zote,
na macho yangu yamewatazama adui zangu kwa ushindi.
—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/54-d49c4c9ba5831ca660230c77e7a26ee4.mp3?version_id=1627—