Categories
Zaburi

Zaburi 53

Uovu Wa Wanadamu

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi. Utenzi wa Daudi.

1 Mpumbavu anasema moyoni mwake,

“Hakuna Mungu.”

Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa,

hakuna hata mmoja atendaye mema.

2 Mungu anawachungulia wanadamu chini

kutoka mbinguni

aone kama wako wenye akili,

wowote wanaomtafuta Mungu.

3 Kila mmoja amegeukia mbali,

wameharibika wote pamoja,

hakuna atendaye mema.

Naam, hakuna hata mmoja!

4 Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza:

wale ambao huwala watu wangu

kama watu walavyo mkate,

hao ambao hawamwiti Mungu?

5 Hapo waliingiwa na hofu kuu,

ambapo hapakuwa cha kutetemesha.

Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia;

uliwaaibisha, kwa sababu Mungu aliwadharau.

6 Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni!

Wakati Mungu arejeshapo wafungwa wa watu wake,

Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/53-b53885ea57ed4462561650e8e252af99.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *