Categories
Zaburi

Zaburi 43

Maombi Ya Mtu Aliyeko Uhamishoni Yanaendelea

1 Ee Mungu unihukumu,

nitetee dhidi ya taifa lisilomcha Mungu,

niokoe na watu wadanganyifu na waovu.

2 Wewe ni Mungu ngome yangu.

Kwa nini umenikataa?

Kwa nini niendelee kuomboleza,

nikiwa nimeonewa na adui?

3 Tuma hima nuru yako na kweli yako

na viniongoze;

vinilete mpaka mlima wako mtakatifu,

mpaka mahali unapoishi.

4 Ndipo nitakwenda madhabahuni pa Mungu,

kwa Mungu, furaha yangu na shangwe yangu.

Nitakusifu kwa kinubi,

Ee Mungu, Mungu wangu.

5 Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka?

Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?

Weka tumaini lako kwa Mungu,

kwa sababu bado nitamsifu

Mwokozi wangu na Mungu wangu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/43-73dc30c516be7542f8dd7374742d54b2.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *