Sala Ya Jioni Ya Kuomba Msaada
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi.
1 Nijibu nikuitapo,
Ee Mungu wangu mwenye haki!
Nipumzishe katika shida zangu;
nirehemu, usikie ombi langu.
2 Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu
kuwa aibu mpaka lini?
Mtapenda udanganyifu
na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?
3 Fahamuni hakika kwambaBwanaamewatenga
wale wamchao kwa ajili yake;
Bwanaatanisikia nimwitapo.
4 Katika hasira yako, usitende dhambi.
Mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya
mkiichunguza mioyo yenu.
5 Toeni dhabihu zilizo haki;
mtegemeeniBwana.
6 Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye
kutuonyesha jema lolote?”
EeBwana, tuangazie nuru ya uso wako.
7 Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa
kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.
8 Nitajilaza chini na kulala kwa amani,
kwa kuwa wewe peke yako, EeBwana,
waniwezesha kukaa kwa salama.
—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/4-d29771b2637e4953932c84584e8c7c0e.mp3?version_id=1627—