Categories
Zaburi

Zaburi 4

Sala Ya Jioni Ya Kuomba Msaada

Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi.

1 Nijibu nikuitapo,

Ee Mungu wangu mwenye haki!

Nipumzishe katika shida zangu;

nirehemu, usikie ombi langu.

2 Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu

kuwa aibu mpaka lini?

Mtapenda udanganyifu

na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?

3 Fahamuni hakika kwambaBwanaamewatenga

wale wamchao kwa ajili yake;

Bwanaatanisikia nimwitapo.

4 Katika hasira yako, usitende dhambi.

Mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya

mkiichunguza mioyo yenu.

5 Toeni dhabihu zilizo haki;

mtegemeeniBwana.

6 Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye

kutuonyesha jema lolote?”

EeBwana, tuangazie nuru ya uso wako.

7 Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa

kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.

8 Nitajilaza chini na kulala kwa amani,

kwa kuwa wewe peke yako, EeBwana,

waniwezesha kukaa kwa salama.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/4-d29771b2637e4953932c84584e8c7c0e.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *