Categories
Zaburi

Zaburi 34

Sifa Na Wema Wa Mungu

Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka.

1 NitamtukuzaBwananyakati zote,

sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.

2 Nafsi yangu itajisifu katikaBwana,

walioonewa watasikia na wafurahi.

3 MtukuzeniBwanapamoja nami,

naam, na tulitukuze jina lake pamoja.

4 NilimtafutaBwananaye akanijibu,

akaniokoa kwenye hofu zangu zote.

5 Wale wamtazamao hutiwa nuru,

nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.

6 Maskini huyu alimwitaBwana, naye akamsikia,

akamwokoa katika taabu zake zote.

7 Malaika waBwanahufanya kituo

akiwazunguka wale wamchao,

naye huwaokoa.

8 Onjeni mwone kwambaBwanani mwema,

heri mtu yule anayemkimbilia.

9 McheniBwanaenyi watakatifu wake,

kwa maana wale wamchao

hawapungukiwi na chochote.

10 Wana simba wenye nguvu

hutindikiwa na kuona njaa,

bali wale wamtafutaoBwana

hawatakosa kitu chochote kilicho chema.

11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize,

nitawafundisha kumchaBwana.

12 Yeyote kati yenu anayependa uzima

na kutamani kuziona siku nyingi njema,

13 basi auzuie ulimi wake na mabaya,

na midomo yake kutokana na kusema uongo.

14 Aache uovu, atende mema,

aitafute amani na kuifuatilia.

15 Macho yaBwanahuwaelekea wenye haki,

na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.

16 Uso waBwanauko kinyume na watendao maovu,

ili kufuta kumbukumbu lao duniani.

17 Wenye haki hulia, nayeBwanahuwasikia,

huwaokoa katika taabu zao zote.

18 Bwanayu karibu na waliovunjika moyo,

na huwaokoa waliopondeka roho.

19 Mwenye haki ana mateso mengi,

lakiniBwanahumwokoa nayo yote,

20 huhifadhi mifupa yake yote,

hata mmoja hautavunjika.

21 Ubaya utamuua mtu mwovu,

nao adui za mwenye haki watahukumiwa.

22 Bwanahuwakomboa watumishi wake,

yeyote anayemkimbilia yeye

hatahukumiwa kamwe.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/34-ccb420443dc43577cc3db3894086b01d.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *