Sifa Na Wema Wa Mungu
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka.
1 NitamtukuzaBwananyakati zote,
sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
2 Nafsi yangu itajisifu katikaBwana,
walioonewa watasikia na wafurahi.
3 MtukuzeniBwanapamoja nami,
naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
4 NilimtafutaBwananaye akanijibu,
akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5 Wale wamtazamao hutiwa nuru,
nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6 Maskini huyu alimwitaBwana, naye akamsikia,
akamwokoa katika taabu zake zote.
7 Malaika waBwanahufanya kituo
akiwazunguka wale wamchao,
naye huwaokoa.
8 Onjeni mwone kwambaBwanani mwema,
heri mtu yule anayemkimbilia.
9 McheniBwanaenyi watakatifu wake,
kwa maana wale wamchao
hawapungukiwi na chochote.
10 Wana simba wenye nguvu
hutindikiwa na kuona njaa,
bali wale wamtafutaoBwana
hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize,
nitawafundisha kumchaBwana.
12 Yeyote kati yenu anayependa uzima
na kutamani kuziona siku nyingi njema,
13 basi auzuie ulimi wake na mabaya,
na midomo yake kutokana na kusema uongo.
14 Aache uovu, atende mema,
aitafute amani na kuifuatilia.
15 Macho yaBwanahuwaelekea wenye haki,
na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
16 Uso waBwanauko kinyume na watendao maovu,
ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
17 Wenye haki hulia, nayeBwanahuwasikia,
huwaokoa katika taabu zao zote.
18 Bwanayu karibu na waliovunjika moyo,
na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Mwenye haki ana mateso mengi,
lakiniBwanahumwokoa nayo yote,
20 huhifadhi mifupa yake yote,
hata mmoja hautavunjika.
21 Ubaya utamuua mtu mwovu,
nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
22 Bwanahuwakomboa watumishi wake,
yeyote anayemkimbilia yeye
hatahukumiwa kamwe.
—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/34-ccb420443dc43577cc3db3894086b01d.mp3?version_id=1627—