Categories
Zaburi

Zaburi 33

Ukuu Na Wema Wa Mungu

1 MwimbieniBwanakwa furaha, enyi wenye haki;

kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.

2 MsifuniBwanakwa kinubi,

mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.

3 Mwimbieni wimbo mpya;

pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.

4 Maana neno laBwanani haki na kweli,

ni mwaminifu kwa yote atendayo.

5 Bwanahupenda uadilifu na haki;

dunia imejaa upendo wake usiokoma.

6 Kwa neno laBwanambingu ziliumbwa,

jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.

7 Ameyakusanya maji ya bahari

kama kwenye chungu;

vilindi vya bahari

ameviweka katika ghala.

8 Dunia yote na imwogopeBwana,

watu wote wa dunia wamche.

9 Kwa maana Mungu alisema, na ikawa,

aliamuru na ikasimama imara.

10 Bwanahuzuia mipango ya mataifa,

hupinga makusudi ya mataifa.

11 Lakini mipango yaBwanainasimama imara milele,

makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.

12 Heri taifa ambaloBwanani Mungu wao,

watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.

13 Kutoka mbinguniBwanahutazama chini

na kuwaona wanadamu wote;

14 kutoka maskani mwake huwaangalia

wote wakaao duniani:

15 yeye ambaye huumba mioyo yao wote,

ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.

16 Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake;

hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.

17 Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu,

licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.

18 Lakini macho yaBwanayako kwa wale wamchao,

kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,

19 ili awaokoe na mauti,

na kuwahifadhi wakati wa njaa.

20 Sisi tunamngojeaBwanakwa matumaini,

yeye ni msaada wetu na ngao yetu.

21 Mioyo yetu humshangilia,

kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.

22 Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, EeBwana,

tunapoliweka tumaini letu kwako.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/33-1fce9b791359e502eb1f99b6a9c33f07.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *