Categories
Zaburi

Zaburi 29

Sauti Ya Bwana Wakati Wa Dhoruba

Zaburi ya Daudi.

1 MpeniBwana, enyi mashujaa,

mpeniBwanautukufu na nguvu.

2 MpeniBwanautukufu unaostahili jina lake;

mwabuduniBwanakatika uzuri wa utakatifu wake.

3 Sauti yaBwanaiko juu ya maji;

Mungu wa utukufu hupiga radi,

Bwanahupiga radi juu ya maji makuu.

4 Sauti yaBwanaina nguvu;

sauti yaBwanani tukufu.

5 Sauti yaBwanahuvunja mierezi;

Bwanahuvunja vipande vipande

mierezi ya Lebanoni.

6 Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama,

Sirioniurukaruke kama mwana nyati.

7 Sauti yaBwanahupiga kwa miali

ya umeme wa radi.

8 Sauti yaBwanahutikisa jangwa;

Bwanahutikisa Jangwa la Kadeshi.

9 Sauti yaBwanahuzalisha ayala,

na huuacha msitu wazi.

Hekaluni mwake wote wasema,

“Utukufu!”

10 Bwanahuketi akiwa ametawazwa juu ya gharika;

Bwanaametawazwa kuwa Mfalme milele.

11 Bwanahuwapa watu wake nguvu;

Bwanahuwabariki watu wake kwa kuwapa amani.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/29-a77bafb769001fb1643ac0ddcb064950.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *