Categories
Zaburi

Zaburi 15

Kitu Mungu Anachotaka

Zaburi ya Daudi.

1 Bwana, ni nani awezaye kukaa

katika Hekalu lako?

Nani awezaye kuishi

katika mlima wako mtakatifu?

2 Ni yule aendaye pasipo mawaa,

atendaye yaliyo haki,

asemaye kweli toka moyoni mwake,

3 na hana masingizio ulimini mwake,

asiyemtenda jirani yake vibaya,

na asiyemsingizia mwenzake,

4 ambaye humdharau mtu mbaya,

lakini huwaheshimu wale wamwogopaoBwana,

yule atunzaye kiapo chake

hata kama anaumia.

5 Yeye akopeshaye fedha yake bila riba,

na hapokei rushwa dhidi ya mtu asiye na hatia.

Mtu afanyaye haya

kamwe hatatikisika.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/15-12ac0bb687ff8678dd16cf5435ddfab1.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *