Categories
Zaburi

Zaburi 138

Maombi Ya Shukrani

Zaburi ya Daudi.

1 Nitakusifu wewe, EeBwana, kwa moyo wangu wote,

mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.

2 Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu,

nami nitalisifu jina lako

kwa ajili ya upendo wako

na uaminifu,

kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako

juu ya vitu vyote.

3 Nilipoita, ulinijibu;

ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.

4 Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe EeBwana,

wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.

5 Wao na waimbe kuhusu njia zaBwana,

kwa maana utukufu waBwanani mkuu.

6 IngawaBwanayuko juu,

humwangalia mnyonge,

bali mwenye kiburi

yeye anamjua kutokea mbali.

7 Nijapopita katikati ya shida,

wewe unayahifadhi maisha yangu,

unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu,

kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.

8 Bwanaatatimiza kusudi lake kwangu,

EeBwana, upendo wako wadumu milele:

usiziache kazi za mikono yako.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/138-d40040723c8c708f47c1cf84d80d04cd.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *