Categories
Zaburi

Zaburi 130

Kuomba Msaada

Wimbo wa kwenda juu.

1 Kutoka vilindini ninakulilia, EeBwana.

2 EeBwana, sikia sauti yangu.

Masikio yako na yawe masikivu

kwa kilio changu unihurumie.

3 Kama wewe, EeBwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi,

Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?

4 Lakini kwako kuna msamaha,

kwa hiyo wewe unaogopwa.

5 NamngojeaBwana, nafsi yangu inangojea,

katika neno lake naweka tumaini langu.

6 Nafsi yangu inamngojea Bwana

kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi,

naam, kuliko walinzi

waingojeavyo asubuhi.

7 Ee Israeli, mtumainiBwana,

maana kwaBwanakuna upendo usiokoma,

na kwake kuna ukombozi kamili.

8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli

kutoka dhambi zao zote.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/130-0fa0927afafceabcb36aa675010cc524.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *