Kuomba Msaada
Wimbo wa kwenda juu.
1 Kutoka vilindini ninakulilia, EeBwana.
2 EeBwana, sikia sauti yangu.
Masikio yako na yawe masikivu
kwa kilio changu unihurumie.
3 Kama wewe, EeBwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi,
Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
4 Lakini kwako kuna msamaha,
kwa hiyo wewe unaogopwa.
5 NamngojeaBwana, nafsi yangu inangojea,
katika neno lake naweka tumaini langu.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana
kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi,
naam, kuliko walinzi
waingojeavyo asubuhi.
7 Ee Israeli, mtumainiBwana,
maana kwaBwanakuna upendo usiokoma,
na kwake kuna ukombozi kamili.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli
kutoka dhambi zao zote.
—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/130-0fa0927afafceabcb36aa675010cc524.mp3?version_id=1627—