Thawabu Ya Kumtii Bwana
Wimbo wa kwenda juu.
1 Heri ni wale wote wamchaoBwana,
waendao katika njia zake.
2 Utakula matunda ya kazi yako;
baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao
ndani ya nyumba yako;
wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni
kuizunguka meza yako.
4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa
mtu amchayeBwana.
5 Bwanana akubariki kutoka Sayuni
siku zote za maisha yako,
na uone mafanikio ya Yerusalemu,
6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako.
Amani iwe juu ya Israeli.
—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/128-42322bf991cd46273a32779b87cfd157.mp3?version_id=1627—