Usalama Wa Watu Wa Mungu
Wimbo wa kwenda juu.
1 Wale wamtumainioBwanani kama mlima Sayuni,
ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.
2 Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,
ndivyoBwanaanavyowazunguka watu wake
sasa na hata milele.
3 Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi
waliopewa wenye haki,
ili wenye haki wasije wakatumia
mikono yao kutenda ubaya.
4 EeBwana, watendee mema walio wema,
wale walio wanyofu wa moyo.
5 Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka,
Bwanaatawafukuza pamoja na watenda mabaya.
Amani iwe juu ya Israeli.
—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/125-370cee1374973ac54166d030d902839e.mp3?version_id=1627—