Categories
Zaburi

Zaburi 125

Usalama Wa Watu Wa Mungu

Wimbo wa kwenda juu.

1 Wale wamtumainioBwanani kama mlima Sayuni,

ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.

2 Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,

ndivyoBwanaanavyowazunguka watu wake

sasa na hata milele.

3 Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi

waliopewa wenye haki,

ili wenye haki wasije wakatumia

mikono yao kutenda ubaya.

4 EeBwana, watendee mema walio wema,

wale walio wanyofu wa moyo.

5 Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka,

Bwanaatawafukuza pamoja na watenda mabaya.

Amani iwe juu ya Israeli.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/125-370cee1374973ac54166d030d902839e.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *