Categories
Zaburi

Zaburi 123

Kuomba Rehema

Wimbo wa kwenda juu.

1 Ninayainua macho yangu kwako,

kwako wewe ambaye kiti chako cha enzi kiko mbinguni.

2 Kama vile macho ya watumwa

yatazamavyo mkono wa bwana wao,

kama vile macho ya mtumishi wa kike

yatazamavyo mkono wa bibi yake,

ndivyo macho yetu yamtazamavyoBwanaMungu wetu,

mpaka atakapotuhurumia.

3 Uturehemu, EeBwana, uturehemu,

kwa maana tumevumilia dharau nyingi.

4 Tumevumilia dhihaka nyingi kutoka kwa wenye kiburi,

dharau nyingi kutoka kwa wenye majivuno.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/123-731c2710bf4366fcd14b363a09c0ebe6.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *