Kuomba Msaada
Wimbo wa kwenda juu.
1 Katika dhiki yangu namwitaBwana,
naye hunijibu.
2 EeBwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo
na ndimi za udanganyifu.
3 Atakufanyia nini,
au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa,
kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki,
kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 Nimeishi muda mrefu mno
miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 Mimi ni mtu wa amani;
lakini ninaposema, wao wanataka vita.
—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/120-df46a67e829af36a3dad513361f137eb.mp3?version_id=1627—