Categories
Zaburi

Zaburi 120

Kuomba Msaada

Wimbo wa kwenda juu.

1 Katika dhiki yangu namwitaBwana,

naye hunijibu.

2 EeBwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo

na ndimi za udanganyifu.

3 Atakufanyia nini,

au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?

4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa,

kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.

5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki,

kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!

6 Nimeishi muda mrefu mno

miongoni mwa wale wanaochukia amani.

7 Mimi ni mtu wa amani;

lakini ninaposema, wao wanataka vita.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/120-df46a67e829af36a3dad513361f137eb.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *