Categories
Zaburi

Zaburi 112

Baraka Za Mwenye Haki

1 MsifuniBwana.

Heri mtu yule amchayeBwana,

mtu yule apendezwaye sana na amri zake.

2 Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi,

kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.

3 Nyumbani mwake kuna mali na utajiri,

haki yake hudumu milele.

4 Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu,

yule mwenye rehema, huruma na haki.

5 Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba,

anayefanya mambo yake kwa haki.

6 Hakika hatatikisika kamwe,

mtu mwenye haki atakumbukwa milele.

7 Hataogopa habari mbaya,

moyo wake ni thabiti, ukimtegemeaBwana.

8 Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu,

mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.

9 Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini;

haki yake hudumu milele;

pembe yake itatukuzwa kwa heshima.

10 Mtu mwovu ataona na kuchukizwa,

atasaga meno yake na kutoweka,

kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/112-9a9d1bf374d655d84427efbeb9eed1f0.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *